Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 1 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 8...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...
Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Wito wa Hekima
1 Taz Meth 1:20-21 Sikilizeni! Hekima anaita!
Busara anapaza sauti yake!
2Juu penye mwinuko karibu na njia,
katika njia panda ndipo alipojiweka.
3Karibu na malango ya kuingilia mjini,
mahali wanapoingia watu anaita kwa sauti:
4“Enyi watu wote, nawaita nyinyi!
Wito wangu ni kwa ajili ya binadamu.
5Enyi wajinga, jifunzeni kuwa na akili;
sikilizeni kwa makini enyi wapumbavu.
6Sikilizeni maana nitakachosema ni jambo muhimu;
midomoni mwangu mtatoka mambo ya adili.
7Kinywa changu kitatamka kweli tupu;
uovu ni chukizo midomoni mwangu.
8Kinywa changu kitatamka maneno ya kweli,
udanganyifu ni haramu midomoni mwangu.
9Kwa mtu mwelewa kila kitu ni wazi,
kwa mwenye maarifa yote ni sawa.
10Chagua mafundisho yangu badala ya fedha;
na maarifa badala ya dhahabu safi.
11“Mimi Hekima nina thamani kuliko johari;
chochote unachotamani hakiwezi kulingana nami.
12Mimi Hekima ninao ujuzi;
ninayo maarifa na busara.
13Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu.
Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya;
nachukia na lugha mbaya.
14Nina uwezo wa kushauri na nina hekima.
Ninao ujuzi na nina nguvu.
15Kwa msaada wangu wafalme hutawala,
watawala huamua yaliyo ya haki.
16Kwa msaada wangu viongozi hutawala,
wakuu na watawala halali.8:16 tafsiri nyingine: Wakuu, mahakimu wa dunia.
17Nawapenda wale wanaonipenda;
wanaonitafuta kwa bidii hunipata.
18Utajiri na heshima viko kwangu,
mali ya kudumu na fanaka.
19Matunda yangu ni mazuri kuliko dhahabu safi,
faida yangu yashinda ile ya fedha bora.
20Natembea katika njia ya uadilifu;
ninafuata njia za haki.
21Mimi huwatajirisha wanaonipenda,
huzijaza tele hazina zao wanipendao.
22 Taz Ufu 3:14 “Mwenyezi-Mungu aliniumba mwanzoni mwa kazi yake,8:22 kazi yake: Makala ya Kiebrania: Njia yake.
zama za zama kabla ya kuwako kitu chochote.
23Nilifanywa mwanzoni mwa nyakati,
nilikuwako kabla ya dunia kuanza.
24Nilizaliwa kabla ya vilindi vya bahari,
kabla ya chemchemi zibubujikazo maji.
25Kabla ya milima haijaumbwa,
na vilima kusimamishwa mahali pake,
mimi nilikuwako tayari.
26Kabla Mungu hajaumba dunia na mashamba yake,
wala chembe za kwanza za mavumbi ya dunia.
27Nilikuwako wakati alipoziweka mbingu,
wakati alipopiga duara juu ya bahari;
28wakati alipoimarisha mawingu mbinguni,
alipozifanya imara chemchemi za bahari;
29wakati alipoiwekea bahari mpaka wake,
maji yake yasije yakavunja amri yake;
wakati alipoiweka misingi ya dunia.
30Nilikuwa pamoja naye kama fundi stadi,8:30 fundi stadi: Au Mtoto mdogo.
nilikuwa furaha yake kila siku,
nikishangilia mbele yake daima,
31nikifurahia dunia na wakazi wake,
na kupendezwa kuwa pamoja na wanadamu.
32“Sasa basi wanangu, nisikilizeni:
Heri wale wanaofuata njia zangu.
33Sikilizeni mafunzo mpate hekima,
wala msiyakatae.
34Heri mtu anayenisikiliza,
anayekaa kila siku mlangoni pangu,
anayekesha karibu na milango yangu.
35Anayenipata mimi amepata uhai,
amepata upendeleo kwa Mwenyezi-Mungu.
36Asiyenipata anajidhuru mwenyewe;
wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Methali8;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: