Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 18 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 21...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika kuungana na Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya. Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni. Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe. Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Injili. Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Moyo wa mfalme ni kama maji yanayotiririka;
Mwenyezi-Mungu, huuongoza popote apendapo.
2Matendo yote ya mtu ni sawa machoni pake,
lakini Mwenyezi-Mungu hupima mioyo.
3Kutenda mambo mema na ya haki,
humpendeza Mwenyezi-Mungu kuliko tambiko.
4Macho ya kiburi na moyo wa majivuno
huonesha wazi dhambi ya waovu.
5Mipango ya mtu wa bidii huleta mali kwa wingi,
lakini kila aliye na pupa huishia patupu.
6Mali ipatikanayo kwa udanganyifu,
ni mvuke upitao na mtego wa kifo.
7Ukatili wa wakatili utawafutilia mbali,
maana wanakataa kutenda yaliyo ya haki.
8Njia ya mtu mwenye hatia imepotoka,
lakini mwenendo wa mnyofu umenyooka.
9Afadhali kuishi pembeni juu ya paa,
kuliko kuishi nyumbani na mwanamke mgomvi.
10Anachopania kutenda mtu mbaya ni uovu;
hata kwa jirani yake hana huruma.
11Ukimwadhibu mwenye dhihaka, mjinga hupata hekima;
ukimfundisha mwenye hekima, unampatia maarifa.
12Mungu Mwadilifu21:12 Mungu Mwadilifu:Mungu. anajua wanayotenda waovu nyumbani kwao;
naye atawaangusha na kuwaangamiza.
13Anayekataa kusikiliza kilio cha maskini,
naye pia hatasikilizwa atakapolilia msaada.
14Hasira hutulizwa kwa zawadi ya siri;
tunu apewayo mtu imefichwa hupooza ghadhabu.
15Haki ikitekelezwa watu wema hufurahi,
lakini watu waovu hufadhaishwa.
16Anayetangatanga mbali na njia ya busara,
atajikuta ametua miongoni mwa wafu.
17Anayependa anasa atakuwa maskini;
anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.
18Mwovu atapata pigo ambalo halitampata mtu mwema,
mkosefu ataadhibiwa badala ya mnyofu.
19Afadhali kuishi jangwani,
kuliko kukaa na mwanamke mgomvi na msumbufu.
20Nyumbani kwa mwenye busara mna hazina za thamani,
lakini mpumbavu huponda mali yake yote.
21Anayepania uadilifu na huruma,
ataishi maisha marefu na kuheshimiwa.
22Mwenye hekima aweza kuteka mji wa wenye nguvu,
na kuziporomosha ngome wanazozitegemea.
23Achungaye mdomo wake na ulimi wake,
hujiepusha na matatizo.
24Mwenye majivuno na kiburi jina lake ni “Madharau;”
matendo yake yamejaa majivuno ya ufidhuli wake.
25Mvivu hufa kwa kutotimizwa tamaa zake,
maana mikono yake milegevu haitaki kufanya kazi.
26Mchana kutwa mwovu hutamani kupata kitu,
lakini mwadilifu hutoa, tena kwa ukarimu.
27Tambiko ya mwovu ni kitu cha kuchukiza,
huchukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.
28Shahidi mwongo ataangamia,
lakini msikivu hawezi kunyamazishwa.
29Mtu mwovu hujionesha kuwa jasiri,
lakini mwadilifu huhakikisha ametenda sawa.
30Hakuna hekima, maarifa, wala mawaidha yoyote ya mtu,
yawezayo kumshinda Mwenyezi-Mungu.
31Farasi hutayarishwa kwa vita,
lakini ushindi wamtegemea Mwenyezi-Mungu.

Methali21;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: