Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 10 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 15...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yohane alikuwa kama taa iliyokuwa ikiwaka na kuangaza, nanyi mlikuwa tayari kufurahia mwanga huo kwa kitambo. Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Nyinyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake, na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma. Nyinyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uhai wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia! Hata hivyo, nyinyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uhai.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

“Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu. Lakini nawajua nyinyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu. Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea. Mwawezaje kuamini, hali nyinyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu nyinyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu? Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye nyinyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki. Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia, maana Mose aliandika juu yangu. Lakini hamyaamini yale aliyoandika; mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Kujibu kwa upole hutuliza hasira,
lakini neno kali huchochea hasira.
2Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa,
lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.
3Macho ya Mwenyezi-Mungu huona kila kitu,
humchunguza mtu mwema na mtu mbaya.
4Ulimi mpole ni chanzo cha uhai,
lakini uovu wake huvunja moyo.
5Mpumbavu hudharau mafundisho ya baba yake,
lakini anayekubali maonyo ana busara.
6Nyumbani mwa mwadilifu mna wingi wa mali,
lakini mapato ya waovu huishia na balaa.
7Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa,
lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
8Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini sala ya wanyofu humfurahisha Mungu.
9Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini Mungu huwapenda wale wafuatao mambo adili.
10Adhabu kali ipo kwa wanaoacha mwenendo mwema;
yeyote achukiaye kuonywa atakufa.
11Ikiwa Mwenyezi-Mungu ajua yaliyo Kuzimu na Abadoni,
mawazo ya binadamu yatawezaje kujificha mbele yake?
12Mwenye madharau hapendi kuonywa,
hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.
13Moyo wa furaha hungarisha uso,
lakini uchungu huvunja moyo.
14Mwenye busara hutafuta maarifa,
lakini wapumbavu hujilisha upuuzi.
15Kwa mnyonge kila siku ni mbaya,
lakini kwa mwenye moyo mchangamfu ni sikukuu.
16Afadhali kuwa na kidogo na kumcha Mwenyezi-Mungu,
kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.
17Afadhali mlo wa jioni wa mchicha na upendo,
kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.
18Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi,
lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.
19Njia ya mvivu imesambaa miiba,
njia ya mwaminifu ni wazi kama barabara kuu.
20Mtoto mwenye hekima humfurahisha baba yake,
lakini mpumbavu humdharau mama yake.
21Upumbavu ni furaha kwa mtu asiye na akili,
lakini mwenye busara huchagua njia iliyo sawa.
22Mipango huharibika kwa kukosa shauri,
lakini kwa washauri wengi, hufaulu.
23Kutoa jibu sahihi hufurahisha;
neno lifaalo kwa wakati wake ni jema mno!
24Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,
ili aepe kuingia chini kuzimu.
25Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,
lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.
26Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
bali maneno mema humfurahisha.
27Anayetamani faida ya ulanguzi
anaitaabisha jamaa yake,
lakini achukiaye hongo ataishi.
28Moyo wa mwadilifu hufikiri kabla ya kujibu,
lakini kinywa cha mwovu hububujika uovu.
29Mwenyezi-Mungu yuko mbali na watu waovu,
lakini yu karibu na watu wema kuwasikiliza.
30Macho ya huruma hufurahisha moyo,
habari njema huuburudisha mwili.
31Mtu ambaye husikiliza maonyo mema,
anayo nafasi yake miongoni mwa wenye hekima.
32Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe,
bali anayekubali maonyo hupata busara.
33Kumcha Mwenyezi-Mungu ni shule ya hekima;
kabla ya kuheshimika ni lazima kuwa mnyenyekevu.

Methali15;1-33

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: