Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 5 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 12...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Baba ampenda Mwana, na humwonesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uhai, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uhai wale anaopenda.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Apendaye nidhamu hupenda maarifa,
bali asiyependa kuonywa ni mjinga.
2Mtu mwema hufadhiliwa na Mwenyezi-Mungu,
lakini mwenye nia mbaya hulaaniwa na Mungu.
3Mtu hawi imara kwa kutenda maovu,
lakini hakuna kiwezacho kumngoa mtu mwadilifu.
4Mke mwema ni taji ya fahari kwa mumewe;
amwaibishaye mumewe ni kama kidonda mifupani mwake.
5Mawazo ya mwadilifu ni ya haki;
mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.
6Maneno ya waovu lengo lake ni kuua,
lakini maneno ya waadilifu huwaokoa wanaotishwa.
7Waovu huangamizwa na kutoweka kabisa,
lakini jamaa ya waadilifu hudumishwa.
8Mtu husifiwa kadiri ya hekima yake,
lakini mtu wa fikira mbaya hudharauliwa.
9Afadhali mtu wa chini anayejitegemea,
kuliko ajitakiaye makuu na kukosa chakula.
10Mtu mwadilifu huwajali wanyama wake,
lakini huruma ya mwovu ni ukatili.
11Mkulima mwenye bidii ana chakula tele,
lakini afuataye mambo yasiyofaa hana akili.
12Waovu hutamani faida isiyo halali,
lakini mtu mwadilifu husimama imara.12:12 aya ya 12 makala ya Kiebrania si dhahiri na tafsiri yake si hakika.
13Mtu mwovu hunaswa kwa uongo wake mwenyewe,
lakini mwadilifu hutoka katika taabu.
14Mtu hufanikiwa kutokana na maneno yake
kama apatavyo matokeo ya kazi za mikono yake.
15Mpumbavu huiona njia yake kuwa sawa,
lakini mwenye hekima husikiliza shauri.
16Udhia wa mpumbavu hujulikana mara,
lakini mwerevu huyapuuza matukano.
17Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli,
lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.
18Maneno ya ovyo hujeruhi kama upanga,
lakini asemayo mwenye hekima huponesha kidonda.
19Ukweli hudumu milele,
lakini uongo ni wa kitambo tu.
20Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni,
lakini wanaonuia mema hupata furaha.
21Waadilifu hawapatwi na jambo lolote baya,
lakini waovu wamejaa dhiki.
22Midomo isemayo uongo ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini watu waaminifu ni furaha yake.
23Mwenye busara huficha maarifa yake,
lakini wapumbavu hutangaza upumbavu wao.
24Kuwa na bidii kutampa mtu cheo,
lakini uvivu utamfanya mtumwa.
25Wasiwasi moyoni humkosesha mtu raha,
lakini neno jema humchangamsha.
26Mtu mwadilifu huuepa uovu,12:26 Mtu mwadilifu … uovu: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
lakini njia ya waovu huwapotosha wenyewe.
27Mwindaji mvivu hatapata anachowinda,
lakini mwenye bidii atafanikiwa.12:27 aya ya 27, makala ya Kiebrania si dhahiri.
28Uadilifu ni njia ya uhai,
lakini uovu huongoza katika mauti.


Methali12;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: