Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 29 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 28...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Waambie watu wa Israeli hivi: Mtu yeyote akitoa sadaka ya amani, atampa Mwenyezi-Mungu sehemu ya sadaka hiyo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Atamletea kwa mikono yake mwenyewe kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Ataleta mafuta yake pamoja na kidari ambacho atafanya nacho ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kuhani atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe makuhani. Mguu wa kulia wa nyuma wa mnyama wa sadaka zenu za amani mtampa kuhani. Mguu huo utakuwa mali ya kuhani aliye mzawa wa Aroni anayetoa damu ya sadaka za amani na mafuta yake.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

1Waovu hukimbia japo hawafukuzwi na mtu,
lakini waadilifu ni hodari kama simba.
2Taifa la fujo huzusha viongozi wengi,
lakini kwa kiongozi mmoja mwenye akili na maarifa huwa na utengemano
3Mtu mhitaji anayewadhulumu maskini,
amefanana na mvua kubwa inayoharibu mimea.
4Watu wanaovunja sheria huwasifu waovu,
lakini wanaoishika sheria hupingana nao.
5Waovu hawajui maana ya haki,
lakini wamchao Mwenyezi-Mungu wanaielewa kabisa.
6Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,
kuliko tajiri aishiye kwa upotovu.
7Mtoto ashikaye sheria ni mwenye hekima,
lakini rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8Aongezaye mali yake kwa riba na kutoza faida
anamkusanyia mwingine mwenye kuwahurumia maskini.
9Anayekataa kuisikia sheria,
huyo hata sala yake ni chukizo kwa Mungu.
10Anayemshawishi mtu mwema kutenda mabaya,
ataanguka katika shimo lake mwenyewe.
Wasio na hatia wamewekewa mema yao.
11Tajiri hujiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,
lakini maskini mwenye busara atamfichua.
12Watu wema wakipata madaraka maisha hufana,
lakini waovu wakitawala watu hujificha.
13Afichaye makosa yake hatafanikiwa;
lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema.
14Heri mtu amchaye Mwenyezi-Mungu daima;
lakini mkaidi wa moyo ataangukia maafa.
15Mtawala mwovu anayewatawala maskini,
ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.
16Mtawala asiye na akili ni mdhalimu mkatili;
lakini achukiaye mali ya udanganyifu atatawala muda mrefu.
17Mtu anayelemewa na hatia ya kuua mtu,
atakuwa mkimbizi mpaka kaburini;
mtu yeyote na asijaribu kumzuia.
18Aishiye kwa unyofu atasalimishwa,
lakini mdanganyifu ataanguka kabisa.
19Anayelima shamba lake atapata chakula kingi,
bali anayefuata yasiyofaa atapata umaskini tele.
20Mtu mwaminifu atapata baraka tele,
lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepa adhabu.
21Si vizuri kumbagua mtu;
watu hufanya mabaya hata kwa kipande cha mkate.
22Mtu bahili hukimbilia mali,
wala hajui kwamba ufukara utamjia.
23Amwonyaye mwenzake hatimaye hupata mema zaidi,
kuliko yule anayembembeleza kwa maneno matamu.
24 Taz lawi 5:1 Anayeiba mali ya baba yake au mama yake, akasema si kosa,
hana tofauti yoyote na wezi wengine.
25Mchoyo huchochea ugomvi,
lakini anayemtegemea Mwenyezi-Mungu atafanikiwa.
26Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mpumbavu;
lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.
27Aliye mkarimu kwa maskini hatatindikiwa kitu,
lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.
28Waovu wakitawala watu hujificha,
lakini wakiangamia, waadilifu huongezeka.


Methali28;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: