Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 4 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 11...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, Yesu akawaambia, “Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumuua Yesu; si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini matumizi ya kipimo halali ni furaha kwake.
2Kiburi huandamana na fedheha,
lakini kwa watu wanyenyekevu mna hekima.
3Unyofu wa watu wema huwaongoza,
upotovu wa wenye hila huwaangamiza.
4Utajiri haufai kitu siku ya ghadhabu,
lakini uadilifu huokoa kutoka kifo.
5Uadilifu wa watu wanyofu huinyosha njia yao,
lakini waovu huanguka kwa uovu wao wenyewe.
6Uadilifu wa wanyofu huwaokoa na hatari,
lakini wafitini hunaswa kwa tamaa zao wenyewe.
7Mwovu akifa tumaini lake nalo hutoweka;
tazamio la asiyemcha Mungu huishia patupu.
8Mtu mnyofu huokolewa katika shida,
na mwovu huingia humo badala yake.
9Asiyemcha Mungu huangamiza wengine kwa mdomo wake,
lakini mwadilifu huokolewa kwa maarifa yake.
10Waadilifu wakipata fanaka mji hushangilia,
na waovu wakiangamia watu hupiga vigelegele.
11Mji hufanikishwa kwa baraka za wanyofu,
lakini huangamizwa kwa mdomo wa waovu.
12Anayemdharau jirani yake hana akili,
mtu mwenye busara hukaa kimya.
13Apitapitaye akichongea hutoa siri,
lakini anayeaminika rohoni huficha siri.
14Pasipo na uongozi taifa huanguka,
penye washauri wengi pana usalama.
15Anayemdhamini mgeni atakuja juta,
lakini anayechukia mambo ya dhamana yu salama.
16Mwanamke mwema huheshimiwa,
mwanamume mwenye bidii hutajirika.
17Mtu mkarimu hufaidika yeye mwenyewe,
lakini mtu mkatili hujiumiza mwenyewe.
18Faida anayopata mwovu ni ya uongo,
lakini atendaye mema hakika atapata faida ya kweli.
19Mtu anayepania kuwa mwadilifu ataishi,
lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.
20Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini wenye mwenendo mwema ni furaha yake.
21Hakika mwovu hataepa kuadhibiwa,
lakini waadilifu wataokolewa.
22Mwanamke mzuri asiye na akili,
ni kama pete ya dhahabu puani mwa nguruwe.
23Matazamio ya waadilifu yana matokeo mema;
tamaa za waovu huishia katika ghadhabu.
24Atoaye kwa ukarimu huzidi kutajirika;
lakini bahili huzidi kudidimia katika umaskini.
25Mtu mkarimu atafanikishwa,
amnyweshaye mwingine maji naye atanyweshwa.
26Watu humlaani afichaye nafaka,11:26 Hapa yahusu wanaoficha nafaka kungojea waiuze kwa bei kubwa wakati wa shida.
lakini humtakia baraka mwenye kuiuza.
27Atafutaye kutenda mema hupata fadhili,
lakini atafutaye kutenda maovu atapatwa na maovu.
28Anayetegemea mali zake ataanguka,
lakini mwadilifu atastawi kama jani bichi.
29Anayeivunja nyumba yake ataambua upepo.
Mpumbavu atakuwa mtumwa wa wenye hekima.
30Matendo ya mwadilifu huleta uhai,
lakini uhalifu huuondoa uhai.
31 Taz 1Pet 4:18 Ikiwa mwadilifu hupata tuzo hapa duniani,
hakika mwovu na mwenye dhambi atapatilizwa.


Methali11;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: