Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 28 December 2011

MKESHA MKUBWA WA KULIOMBEA TAIFA LA TANZANIA KUFANYIKA UWANJA WA TAIFA DESEMBA 31 MWAKA HUU, SERIKALI YAPONGEZWA KUKATAA USHOGA.


Umoja wa makanisa ya Kikiristo Tanzania (Tanzania ChristianFellowship of Churches) umeandaa mkesha mkubwa kwa ajili ya dua maalum kwa taifa kwa lengo la kumshukuru Mungu kwa kulivusha taifa katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na kuanza kipindi kingine ambapo mgeni rasmi katika mkesha huo atakuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Mkesha mkuu kutoka Tanzania Christian Fellowship of Chrches Askofu Godfrey Emmmanuel Malasi amesema watanzania wanapaswa kujua Mungu anakusudi gani na taifa la Tanzania katika kipindi hiki ambacho Taifa limetimiza miaka 50 ya uhuru na kuanza kipindi kingine na kutoa wito kwa kila mtanzania kufanya kazi kwa bidii na kushiriki katika uchumi wa taifa.
Amesema serikali inazo sera nzuri za kuweza kuwamilikisha wananchi rasilimali ziliizopo nchini ili waweze kuishi maisha bora na kuongeza kuwa wananchi wanapaswa kutambua majira na wakati uliopo sasa wakati taifa linapoanza miaka 50 mingine ya uhuru kwa kuzitumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo.
“Kila mmoja anapaswa kushiriki na kushirikishwa kikamilifu katika uchumi wa taifa letu ambalo sasa limemaliza miaka 50 ya uhuru, kila mtu anapaswa kutambua nafasi yake, tusikae kwa kubweteka, tusikae kwa kulalamika kila mtu ajue ni wakati wa kumiki na kurithishwa rasilimali zilizopo katika taifa hili”
Amesema mwaka huu dua maalum kwa taifa litafanyika katika mikoa 14 ya Tanzania ikiwemo Dar es salaam, Arusha, Mwanza,Kilimanjaro, Singida Iringa, Mbeya ,Iringa, Kagera, Dodoma, Ruvuma, Tabora,Tanga na visiwa vya Zanzbar na Pemba.
Amefafanua kuwa katika mkesha huo viongozi mbalimbali wa taifa ,vyama vya siasa na balozi mbalimbali zipatazo 37 zilizopo nchini zimearikwa kushiriki mkesha huo na kuongeza kuwa tayari baadhi ya balozi zimethibitisha kushiriki mkesha huo.
Kuhusu maadalizi ya mkesha huo askofu Godfrey Malasi amesema yanaendelea vizuri na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika dua hiyo maalum na kuongeza kuwa mkesha huo utaambatana na tukio maalum la watoto 50 kusimama uwanjani na kutamka maneno ya kupokea miaka 50 ijayo ikiwa ni ishara ya kupokea kizazi huru cha watanzania.
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa kamati ya mkesha mkuu wa Taifa Askofu Keneth Damas ameipongeza serikali kwa kuwa na msimamo wa kupinga suala la ndoa za jinsia moja (ushoga) katika mikutano ya kimataifa iliyofanyika hivi karibuni na kuuita uamuzi huo kuwa ni ushindi mkubwa kwa taifa la Tanzania na watu wake katika kuheshimu utu na utamaduni wa taifa na uukataaji wa vitendo vya udhalilishaji na kuongeza kuwa wao kama viongozi wa dini wataendelea kuonya na kufundisha watu wajue athari za dhambi hiyo.
“Sisi kama viongozi wa makanisa katika nchi hii tunapinga kwa nguzu zote vitendo vya ushoga ndani ya taifa letu, vitendo vya ushoga ndivyo vilivyosababisha Sodoma na Gomora kuchomwa moto kwa kuwa vilimchukiza sana Mungu, Sisi kama viongozi wa dini katika kizazi chetu na vizazi vijavyo hatutaki kufikia hapo na kuona taifa letu likichomwa moto”

Sunday 25 December 2011

Jikoni Leo na Xmas,Wazee wa kazi hawataki ulalamishi!!!!!!!

                                Kaka Asulwisye hapa anageuza!!
                        Hapa zamu ya kaka Hamza kugeuza.


Haya wapendwa mambo ya Xmas hayo,kaka zangu leo wameniambia,unafikiri wewe kutokuwepo watu hatuli?Wameingia wenyewe!!!!hii ndiyo hali halisi ya kwetu kwenye swala la kupika hakuna JINSIA.
Nami nawaunga mkono naona kitu si chakawaida hicho,mimi mwenyewe hapa mate yananitoka!!!


Mpendwa nawe Xmas yako imekwenda/inakwendaje? maana masaa yanatofautiana.
Wengine wameshakula na Wengine wanaandaa.


Tushirikishe basi!!!!Karibuni sana wapendwa.





Nawatakia Kheri, Baraka na Xmas Njema!!!!!!!!

Wednesday 21 December 2011

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akihojiwa na TBC1 juu ya Mafuriko jijini ...

SHINDANO: MCH. MWASAPILE (BABU WA LOLIONDO) NA GODBLES LEMA MBUNGE WA ARUSHA MJINI NANI ZAIDI MWAKA 2011?


 Godbles Lema Mbunge wa Arusha Mjini.
Mch. Mwasapile (Babu wa Loliondo)

Kutokana na maombi ya wengi kutaka kuwashindanisha watu ambao wamefanya mambo ambayo yameigusa jamii ya kitanzania kwa mwaka wa 2011 Blog yenu kwa mtazamo wa haraka kwa mwaka huu imeona iwashindanishe Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Godbles Lema na Mch. Mwasapile (Babu wa Loliondo).

Blog yenu baada ya kuwaingiza hao kwenye kinyang'anyiro hicho inapenda kuwaelezea kila mmoja kwa kifupi ni kwa nini ameingia. 
Tukianzia na Mh. Lema ni Mbunge kijana ambaye amekutana na mikiki mingi ya kisiasa ukizingatia yeye ni mara yake ya kwanza kuingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ameweza kupambana na majaribu mbali mbali ya kisiasa mpaka kumpelekea kugoma kupata dhamana ya kesi mojawapo katika kesi zinazomkabili na kuamua kwenda rumande ili ujumbe wake ufike, na vile vile kutokana na kura ambazo zilikuwa zinapigwa kutoka Blog ya Mjengwa akishindanishwa na wanasiasa mbali mbali ambao wengi wao ni vijana wenzie nakuweza kushinda katika kinyang'anyiro hicho.

Tukirudi kwa Mch. Mwasapile almaarufu kama Babu wa Loliondo au Babu Ambi, yeye ameingia kwenye kinyang'anyiro hiki kutokana na yeye kuwateka watanzania watoto, vijana na wazee katika nafasi zao mbali mbali kwa staili yake ya kugawa tiba ya asili kwa kutumia kikombe maarufu kama kikombe cha babu.
Mchungaji huyu alianza kutoa huduma hii mwanzoni mwa mwaka huu na kujizolea umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania kutokana na watu wengi kuamini dawa anayotoa kwa kutumia kikombe hicho inatibu magonjwa yote sugu yakiwemo Ukimwi, kisukari, TB na mengine mengi, kutokana na tukio hili kuwahusisha watu mbali mbali, ata wale wenye nyadhifa za juu tumeona Babu huyu anafaa kuingia kwenye mtanange huu.

TAFADHALI PIGA KURA YAKO KWA KUTUMIA UJUMBE WA MAANDISHI KWENDA NAMBA +255 714945143

UKIWA KWENYE ENEO LA KUANDIKA UJUMBE KWENYE SIMU YAKO UTAANDIKA:
"2011 WINNER BABU" AU
"2011 WINNER LEMA"
TUMA KWENYE NAMBA HIYO HAPO JUU, MWISHO SAA 5.59 USIKU WA TAR. 31/12/2011.

MAJIBU YATATOLEWA TAR. 1/01/2012

Nimetuwa na KapingaZ Blog
Ahsante sana.


Monday 19 December 2011

Mtoto huyu Auwawa!!!!!!!

Habari hii inasikitisha sana,Pole sana wazazi/walezi , ndugu,jamaa na marafiki, kwa Msiba huu mzito kweni,Mungu awape Nguvu na Uvumilivu katika wakati huu mgumu kwenu.
               Habari na picha zaidi utazipata kwa MASHUGHULI BLOG.Ahsante.

Wednesday 14 December 2011

Jikoni Leo ni Halwaa!!!!!!

Haya wapendwa leo ni kitu Halwaa kwa Kahawa,kuna inayochanganywa na Ufuta,pia kuna ya Karanga, hizi ndizo nilizowahi kula, kama kuna nyingine wewe unajua Tufahamishane!Vipi lakini Kitu Halwaa na Kahawa Vinapanda/Unapenda? au Hujafanikiwa kuonja?
Karibuni sana Waungwana!!!

Monday 12 December 2011

Watoto wa Kiume na Mitindo!!!!!!

                                        Kaka Mohamed kapozi
                                  hapa na Tabasam
                                              hapa katulia.
Wapendwa Watoto wa kiume na Mitindo yao!!Nakumbuka zamani kulikuwa na Kaunda Suti,Ngwabi,Mchelemchele,Jinzi za Chatu/kujikunjakunja hivi,Mashati ya drafti na nyingine nyingiii,pia watoto wengi walikuwa wanashonewa hizo Suti kwa Fundi tena SareSare,Viatu Moro shoes,Vimokasini,Raba Mtoni, Ndopa/Lakupanda.Pia kulikuwa na viatu vya Bora sijui kama bado lipo hili duka.Pia naona kama mitindo inajirudia .

Wewe unakumbuka nini/kuvutiwa na nini vya wakati ule na Wakati wa sasa jee?

Karibuni sana Waungwana!!!!!

Friday 9 December 2011

Kheri ya Miaka 50 yaUhuru,Na Siku kama ya Leo da'Halima Kiwinga Alizaliwa!!!

Nawatakia Kheri ya  Miaka 50 ya Uhuru!Pia Siku kama ya Leo Familia ya M.S.Kiwinga wa Ilala,Sharifu/Shamba,  Ilipata Mtoto wa kike na Wakamwita HALIMA!!!Leo ametimiza miaka 50!!!!!Hongera sana dada yetu mpendwa,Mungu akubariki sana katika yote,Sisi wadogo zako Tunakupenda,kukujali,kukuthamini na Tunajidai kuwa na dada kama wewe .Da'HALIMA Uwe na Wakati mzuri  Leo na siku zote za Maisha yako.MUNGU NI PENDO.Kwaniaba ya Familia ya Marehemu Mzee Kiwinga ni mimi Rachel-Siwa.

SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU JIJINI DAR PART - 2

SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU JIJINI DAR LEO PART-1

Thursday 8 December 2011

Chaguo la Mswahili Leo ;Les Wanyika : Paulina!!!!

Siku kama ya leo kaka Henry Mwana wa Kapinga Alizaliwa!!!!!!



MPIGANAJI SASA ATIMIZA MIAKA KADHAA!!!

Mpiganaji wenu Henry Kapinga wa Blog yenu ya KAPINGAZ Blog leo Tarehe 8/12 ndio siku aliyozaliwa.
Nawashukuru wale wote walionipa Hongera kwa kuukaribia uzee, sasa sijui kama ni wote mnaupenda uzee, manake fainali yake ni shughuli.
ASANTENI SANA!
Nasi Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililojema katika maisha yako.

Monday 5 December 2011

Comment ya kaka Manyanya kwenye post ya Peter Kapinga!!!!!!

Delete
Blogger Goodman Manyanya Phiri said...
Asante Rachel Mdogo wangu kwa habari hizo.

Kwa wengine wasiejuwa jeshi, taarifa yangu ni kwamba wastani wapo aina tatu wa askari popote pale duniani.


1. WAPIGANAJI (THE MEN/TROOPS---"seamen" kama ni wa baharini, "airmen", wenye kutumia ndege). Ngazi ya chini kuliko zote. Hao ndio waliezagaa katika mambo ya filamu pale panomwagika damu. Kama anajina lake kama "fulani", Wazungu watamtambua kama "PRIVATE FULANI". Nchi nyingi watamchukua kijana yoyote yule mwenye nia kupata mafunzo katika ngazi hii.


2. WARRANT OFFICERS (au "sergeant majors"). Shughuli zao hao ni kuchunga nidhamu ya jeshi. Wapiganaji (MEN/TROOPS) hua wanawaogopa sana hawa warrant officers na ukiwa mwanajeshi na umemridhisha WARRANT OFFICER wako basi wewe unayo nidhamu ya hali ya juu. Hua wanapewa mamlaka wao na Waziri wa ulinzi katika mataifa mengi duniani, na kibali wanachopewa na Waziri kinaitwa "A WARRANT" na ndio maana wanaitwa WARRANT OFFICERS. (Kufika wa WARRANT OFFICER utakuwa wastani umepitia uKoporali, Sajenti, Staff Sajenti na kadhalika na unahitaji sana elimu kabla ya kuchaguliwa!)


3. MAAFISA WA KAMISHENI, COMMISSIONED OFFICERS (kama mhusika hapa) nao wanapewa wadhifa na Raisi wa nchi pekee! Kazi zao za msingi jeshini sio kupigana lakini NIKUIMARISHA JESHI KIMAWAZO NA KUTOA MBINU ZA KUPIGANA KWA MAFANIKIO. WANATAKIWA WAWE MFANO WA KUIGWA NA JESHI LOTE PIA NA WANANCHI WOTE! (Kwa kuwa unahitaji elimu ya juu kuwa afisa wa aina hii, nchi nyingi hutachaguliwa kama hujamaliza angalau kidato cha mwisho/Fomu 6 ya Tanzania. Baadhi ya ngazi za kupitia hapo ni CANDIDATE OFFICER, LUTENI, KAPTENI, MEJA, LUTENI KANALI, KANALI, BRIGADIER NA KADHALIKA KATIKA NYADHIFA SASA ZA UJENERALI au "u-admirali" ukiwa jeshini la maji au baharini)



Sasa tuje kwa Bw. Kapinga:


Huyu bwana usimuonee wivu KWANI ANAKAZI KWELI SASA.

Mifano:

1. Popote asipokuwepo Raisi, YEYE ANACHUKUA MAJUKUMU YA RAISI IKISTAHILI. Kwa mfano: mwiko kuumia kwa mwananchi ikiwa afisa yupo karibu na angemuokoa lakini eti afisa hakujisumbua hata kidogo!


2. Awe amevaa sare ya kijeshi au hakuvaa anatakiwa awe muungwana (GENTLEMAN) kuliko Mtanzania yoyote yule mwingine nchini !

(Hii inamaana akiwa D'salaam huyu bwana daima atakuwa amesimama kwa miguu katika usafiri wa daladala kwani si uungwana kuketi wakati mwanamama amesimama!)


3. Asije akaonekana amelewa pombe hata akiwa nyumbani kwake na ANAWEZA KUTIWA MBARONI kwani hastahili AFISA kuwa mlevi! Pia hamna ugomvi au makelele alipokuwepo yeye!


4. Hata katika mifarakano au hatari ya aina gani ya umma yeye asionekane muoga wa kijingajinga , wala asikimbie na kama anataka kujiepusha na hatari hiyo ASIJE AKAONEKANA ANAKIMBIA....huenda anaweza akatia pupa (PANIC) kwa wengine!

5. Yeye ndie wa mwisho kula jeshini na kama chakula ni kidogo watakula wanajeshi wote (TROOPS AND WARRANT OFFICERS) YEYE NDIE MWENYE KUKAA KWA NJAA!

...YOTE HAYA KUTOKANA NA KWAMBA YEYE NI AFISA , AJITOE MHANGA DAIMA!!!!! Na ukitaka kuona mfano mzuri wa afisa tena wa kuigwa: ni Kanali Gaddafi wa huko Libya yeye aliekataa katakata kukimbia mpaka kufa!




Luteni Peter Kapinga, mimi kama luteni kanali wa jeshi la hapa Afrika nakukaribisha sana katika wadhifa wa uafisa. Ninayo ndoto moja tu kwamba kabla sijaenda kaburini jeshi laTanzania, Msumbiji, Malawi, Uganda, Congo, Angola, Namibia, Swaziland, Botswana, Afrika Kusini, Lesotho na nchi zingine LITAKUWA JESHI MOJA TU LA NCHI MOJA LABDA NAWE UTAKUWA JEMEDALI AU FIELD MARSHAL WAKE!

Kazi ipo, Ndugu yangu; lakini siri kukupa mimi ziko mbili

1. Chunga afya yako
2. Chunga dhamira yako)
4 December 2011 14:57

Sunday 4 December 2011

Nawatakia j'pili Njema!!Pata kibao hiki-wakati wakuomba!!!

PETER KAPINGA SIKU ALIPOTUNUKIWA KAMISHENI NA RAIS DR JAKAYA KIKWETE.


Luteni Peter Kapinga

Tarehe 26/11/2011 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kama Amiri Jeshi Mkuu aliwatunuku Kamisheni wanachuo wa Chuo cha kijeshi cha Monduli Mkoani Arusha.

Peter akiwa mmoja wa wahitimu hao anapenda kuwashukuru wote ambao walioshiriki katika kumsaidia kwa namna moja na nyingine mpaka amefikia hapo alipofikia, zaidi anapenda kumshukuru Dada ake Esther Mbapila pamoja na Mr Mbapila kwa kushiriki katika mchakato wote mpaka akafanikisha kupata alichokihitaji.
ASANTENI
Nasi Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililojema katika Yote.

Friday 2 December 2011

OMARY MJENGA NA SHEREHE YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI NCHINI SIERA LEONE.



Mwakilishi Mkazi wa UNOPS nchini Sierra Leone Bw Omary Mjenga akiwa na Mwakilishi Mkazi wa UNAIDS Bi. Mulunesh, raia wa Ethiopia, kwenye sherehe hizo, ambazo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Sierra Leone Mh Ernest Koroma. Bi Mulunesh aliwahi kuwa Mwakilishi Mkazi wa UNAIDS nchini Tanzania mwaka 1996 hadi 2000.


Thursday 1 December 2011

Jikoni Leo ni Dagaa!!pata na Burudani; Usiniseme-Ali kiba!!!!!!!

           Kitu Dagaa kipo Jikoni
Mimi Napenda zaidi na Ugali,Dagaa kila mtu anaupikaji wake, Mimi wa Chukuchuku,Mafuta Poa tuu,Lakini wa kuungwa/kuwekwa Nazi au Mawese wamenishinda!!Je wewe Mpendwa unapenda Dagaa? Unapikaje na Unapenda Kula na nini na kushushia na kinywaji gani?Karibuni sana Waungwana!!!USINISEME KAMA NAPENDA KULA!!!

Monday 28 November 2011

Wanawake na Urembo!!!!!!!!

                        Huyu kapaka sijui manjano.......
                        Huyu kawa wa pinki
                        Huyu na manyonyo
                                               Huyu kakaba shingo
                                                Huyu kachora .
Haya Wapendwa Wanawake na Urembo,kila siku yanazuka mapya,Pia ya Zamani yanarudi kama si kukumbukwa.Nao zamani kulikuwa na yao mengi tuu,Zazuu,Kuchoma nywele,Kusukia Rafya[sijui kama nimepatia]na Mengine Meeeeeeengi.

Wasasa kuna wanaopenda Maziwa makubwa mpaka kuyaongeza,Kujichubua/Mkorogo,Kujichora kwa sasa si hina tuu kuna Tattoo tena mpaka kwenye Nyusi, Wananyoa na kuweka tattoo ili wasipate shida ya kupaka Wanja.Kuna wanaoongeza Kope,Kunakuweka Vidubwasha ndani ya macho  na kubadili Lenzi kuwa kama ya Wadhungu. Na Mengine meeengi labda sikuweza kuyaandika au Siyajui Yote hayo kwa SABABU YA UREMBO!
Haya sasa  Mwanamke wewe;Katika hayo yote wewe unapenda nini ili uwe Mrembo au unaweza kuongezea ambayo hayapo hapo nasi Tufunguke,Pia unachukia kipi?

Wewe Mwanaume jee unapenda Mkeo,Mchumba,Rafiki yako wa Kike atoke vipi katika hayo na Unaweza kutujuza ambayo hayapo ili awe Mrembo na Unachukia kipi?

Duuhh Lakini Urembo mwingine unataka Moyo!!
Karibuni sana Wapendwa  kwa Mawazo/Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo!!!!!




Friday 25 November 2011

CITE- NA MIAKA 50 ya UHURU WA TANZANIA!!!!

Watanzania waishio Uingereza Kufanya Maombi ya Kumshukuru Mungu Kwa MIAKA 50 ya UHURU.

Waandaaji wa maombi ya ya Miaka 50 ya Uhuru chini Uingereza ”Association of Tanzanian Christians in Europe(CITE)” Wakiwa na Mwl Christopher Mwakasege wakati wa Summer Confference 2009.
Mithali 14:34 Biblia inasema Haki ya Mungu huinua Taifa na huu ndio mstari wa kusimamia katika Maombi hayo yanayowajumuisha watanzania wote waishio nchini Uingereza Hususani katika jiji la London. Kwa Mujibu Wa Mchungaji Emmanuel Chatawe ambaye ni mmoja wa waratibu wa Maombi hayo maombi hayo yatahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali.

Pamoja na Maombi hayo pia kutakuwepo na vikundi mbalimbali vya kusifu na kuabudu.Maombi hayo yameandaliwa na Umoja wa wakristo watanzania waishio bara la Ulaya(CITE).

TAREHE:10 Dec 2011

VENUE: Vision Gospel Ministry International 68 Wallis ROAD Hackney Wick London E9 5LH

TIME :13:00 – 18:00 HRS



Wakati Watumishi wa Mungu Kutoka  Tanzania  waishio nchini Uingereza wakijipanga kwa Maombi hayo, Kwa Upande wa Wakristo wa Watanzania Waishio Nchini Marekani wao wanatarajia kufanya Maombi hayo Tarehe 10 Dec 2011 .Kwa Maelezo zaidi juu ya Kusanyiko la Maombi ya Uhuru wa miaka 50 nchini Marekani Fuata LINK hapa chini.


http://hosannainc.blogspot.com/search/label/Watanzania%20Wahudumuo%20Nje


Thursday 24 November 2011

Miaka 50 ya Uhuru - Kijitonyama Evangelical Choir!!!!!

Wanakwambia Tujibweteke aaa,Turudi Nyuma mmm,Tusonge Mbele namnamnam,
Haya wapendwa mmejiaandaje na miaka 50 ya Uhuru? Mablogger nao sijui watatoka vipi/wameandaa nini?
kwani  nimeona Vyama, Vikundi vya ngoma,Muziki,Kwaya na mengine mengi kuhusu Miaka 50 ya UHURU. Uwe Huru na mwenye Amani na kila lililo jema!!!Usisite kutujuza Nasi Umejiaandaje au Unalipi kuhusu MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA. NA VISIWANI TUUNGANE PAMOJA!!

Tuesday 22 November 2011

Siku kama ya Leo dada Akhram wa Billy Alizaliwa!!!!

Siku kama ya leo Familia ya Bibi na Bwana Billy, Walipata mtoto wa kike na wakamwita Akhram!!
dada huyu ni mtu wakucheka wakati wote mpole na mwenye heshima,Si muoengeaji sana mpaka akuzoee sana,Nakuongea kwake uwe na muda ili mmalize hayo maongezi kwani ni taratibu mnoo,Ukiona kafunga mdomo bila tabasamu ujue NJAAA Kwenye sekta ya msosi ahaaa hana Tabu kabisa!!!Usikivu,samahani na kufanya vyema darasani kwake ni maisha  ya kawaida.
Mungu awabari wazazi na awape hekima katika Malezi yenu.


Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililo jema mwanakwetu!!!!

Thursday 17 November 2011

SHUKRANI KUTOKA KWA FAMILIA YA JUMA PENZA[JP]!!!


Marehemu JUMA PENZA enzi za uhai wake.
Familia ya Juma Penza ya Gongo la Mboto Dar es Salaam inapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki walioshirikiana  nasi katika kufanikisha shughuli za msiba wa baba yetu mpendwa, aliyefariki dunia tarehe 12/10/2011 katika hospitali ya Hindu Mandal na kuzikwa tarehe 13/11/2011 katika makaburi ya Kisutu. 



Tunatoa shukrani za pekee kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. J.M. Kikwete, CCM Makao Makuu, ndugu, jamaa, majirani na marafiki kwa misaada yenu ya hali na mali na kwa namna mlivyoshiriki katika shughuli zote za mazishi.  Shukrani za pekee ziwaendee Dr. Macha Ocean Road, wauguzi na madaktari  wa Hindu Mandal.


Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru  kila mtu kipekee, tunaomba shukrani hizi  mzipokee  wote kwa mikono miwili  kutokana na jinsi mlivyohusika kwa njia moja ama nyingine katika kufanikisha  shughuli nzima ya msiba wa baba yetu mpendwa Mzee JP.


Tunawashukuru kwa jinsi mlivyokuwa karibu  nasi  kwa dua  na maombi wakati wote  hadi tulipompumzisha baba yetu kipenzi .


Vilevile  tunapenda  kuwakaribisha  katika  mkesha  wa dua  itakayofanyika  Ijumaa usiku  Novemba 18 kuamkia siku ya Jumamosi Novemba 19 ambapo khitma  itasomwa  nyumbani kwa marehemu  Gongo la Mboto Dar es es Salaam wote mnakaribishwa .


Tunawakaribisha wote kwenye Arobaini ya marehemu. Mkesha na kisomo utafanyika siku ya Ijumaa tarehe 18/11/2011 na kufuatiwa na  Khitma itakayosomwa Jumamosi tarehe 19/11/2011 kuanzia saa 5:00 asubuhi nyumbani kwa marehemu Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam.Inna lilah Wainna Ilaih Rajiun

Wednesday 16 November 2011

Kuna Siku za Furaha na Siku za Vilio,Yote ni MaishaTusikate Tamaa!!!

                 Siku Ndugu zangu walipokuwa na Furaha.
                                        Mshumaa ulio Zimika.
                                            Mshumaa ulioZimika

Mungu awatie Nguvu katika wakati huu Mgumu na Sikuzote,Zaidi tudumishe Upendo,Umoja,Ushirikiano na Tusikate Tamaa,Wakati kama huu ndiyo utamjua Rafiki,Ndugu wa Kweli na Mengi Mema kwa Mabaya unaweza kuyasikia.Na niwakati kwa Waliopoteza Wazazi/Wapendwa wao Kuwakumbuka na Kulia tena,Nimeamini wanaosema Kilio hakiishi Utalia kila unapokumbuka.Nilitamani niwe nanyi lakini Mungu aliye nanyi ni Zaidi yetu sisi Tuliyo mbali.Mungu awalaze Mahali Pema Peponi Nduguzangu na Rafiki zangu,Jirani zangu na Wote waliotangulia.Sina Mengi ya Kusema bali nasema Asante Mungu.Wenu MWANAPENZA.

Monday 14 November 2011

Wanawake Waswahili wa Coventry wanakutakia,Kila la kheri da'May!!!!!!!!

                                        Mwenyewe da'May.
                                           Kekiiiii
                                               Kata mwanangu kataaa Keki
             May akilishwa na dada yake Esther,dada huyu ndiyo chanzo cha shughuli hii
                       May akimlisha dada yake kwa Furaha
             Da'May baada ya kumlisha dada yake wakaangaliana,May akasema Asante dada yangu
                   May na Mswahili wa Congo
                Mama mwenye nyumbaaa alilishwa pia
                    dada akisogea kutoa Nasaha zake mambo ya Tanga hayo
                           Heheheheee da'Stellah Akitoa Nasaha zake
                   Weshuuu!! da'Tina akitoa Nasaha zake
                           Wamama wakifuatilia Nasaha mbalimbali
                        Waswahili kutoka Milton nao walikuwepo
                          Da'Edna alikuwa MC siku hiyo, Yupo sambamba na mwali
                           Da'Asha mwenye furaha akifuatilia mapango mzima wa Nasaha
                              Wamama hawa wameguswa na Nasaha
                          Da'Bai yupo makini na kamera yake,lakini sikio lipowazi Kusikiliza Nasaha
                     Da'Sarah,Mamie na Stellah,Shughuli ilikamalika
                                 Da'Tinna alikuwepo
                        Dadazzzz walikuwepo,Neema,Maggie na Vick
                           Penye Wanawake Waswahili hakukosi Mila babuu Mtu kwako yakheeee
                         Haya funga Vibwebwe jamaniiiii!!!!Twende sasa!!
                                Hahhahahha Mwali kakuaaaaaaaaaaa,Swahili na Waswahili Wapendwaaaa


                         Nyanyuka sasa Mdogo wangu ya Coventry yameisha Subiri ya Dar na  Tangaaa

                    Mpango mzima wa muziki na Ngoma ulisababishwa na da'Chikuuuu huyo wa Mwisho


Shughuli hii ndogo ya Kumtakia Ndoa Njema dada May,Iliandaliwa na da'Esther,yeye ni dada wa bi Arusi mtarajiwa, Wanawake Waswahili wa Coventry U.K,[WWCU]Walikuwa bega kwa bega na da'Esther kufanikisha jambo hili.
Wanawake Coventry mpo juu na Mungu awabariki sana!!!


Dada May anatarajia kufunga Ndoa hivi karibuni,Ndoa hiyo itakuwa Nyumbani Tanzania[Bongo].
Kwaniaba ya Wanawake wenzangu;Da'May Tunakutakia Safari njema,Ndoa njema yenye baraka na Mungu akutangulie kwa kila jambo wewe na Mume wako Mtarajiwa pamoja na Familia na Wote watakaofanikisha.
Mengi yalishasemwa  pale kwenye sherehe,Hatuna la zaidi sisi TUNAKUPENDA SANA!!!!!!!