Umoja
wa makanisa ya Kikiristo Tanzania (Tanzania ChristianFellowship of
Churches) umeandaa mkesha mkubwa kwa ajili ya dua maalum kwa taifa kwa
lengo la kumshukuru Mungu kwa kulivusha taifa katika kipindi cha miaka
50 ya uhuru na kuanza kipindi kingine ambapo mgeni rasmi katika mkesha
huo atakuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa kamati
ya maandalizi ya Mkesha mkuu kutoka Tanzania Christian Fellowship of
Chrches Askofu Godfrey Emmmanuel Malasi amesema watanzania wanapaswa
kujua Mungu anakusudi gani na taifa la Tanzania katika kipindi hiki
ambacho Taifa limetimiza miaka 50 ya uhuru na kuanza kipindi kingine na
kutoa wito kwa kila mtanzania kufanya kazi kwa bidii na kushiriki
katika uchumi wa taifa.
Amesema
serikali inazo sera nzuri za kuweza kuwamilikisha wananchi rasilimali
ziliizopo nchini ili waweze kuishi maisha bora na kuongeza kuwa
wananchi wanapaswa kutambua majira na wakati uliopo sasa wakati taifa
linapoanza miaka 50 mingine ya uhuru kwa kuzitumia fursa zilizopo
kujiletea maendeleo.
“Kila
mmoja anapaswa kushiriki na kushirikishwa kikamilifu katika uchumi wa
taifa letu ambalo sasa limemaliza miaka 50 ya uhuru, kila mtu anapaswa
kutambua nafasi yake, tusikae kwa kubweteka, tusikae kwa kulalamika
kila mtu ajue ni wakati wa kumiki na kurithishwa rasilimali zilizopo
katika taifa hili”
Amesema
mwaka huu dua maalum kwa taifa litafanyika katika mikoa 14 ya Tanzania
ikiwemo Dar es salaam, Arusha, Mwanza,Kilimanjaro, Singida Iringa,
Mbeya ,Iringa, Kagera, Dodoma, Ruvuma, Tabora,Tanga na visiwa vya
Zanzbar na Pemba.
Amefafanua
kuwa katika mkesha huo viongozi mbalimbali wa taifa ,vyama vya siasa
na balozi mbalimbali zipatazo 37 zilizopo nchini zimearikwa kushiriki
mkesha huo na kuongeza kuwa tayari baadhi ya balozi zimethibitisha
kushiriki mkesha huo.
Kuhusu
maadalizi ya mkesha huo askofu Godfrey Malasi amesema yanaendelea
vizuri na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika dua hiyo
maalum na kuongeza kuwa mkesha huo utaambatana na tukio maalum la
watoto 50 kusimama uwanjani na kutamka maneno ya kupokea miaka 50 ijayo
ikiwa ni ishara ya kupokea kizazi huru cha watanzania.
Kwa
upande wake makamu mwenyekiti wa kamati ya mkesha mkuu wa Taifa Askofu
Keneth Damas ameipongeza serikali kwa kuwa na msimamo wa kupinga suala
la ndoa za jinsia moja (ushoga) katika mikutano ya kimataifa
iliyofanyika hivi karibuni na kuuita uamuzi huo kuwa ni ushindi mkubwa
kwa taifa la Tanzania na watu wake katika kuheshimu utu na utamaduni wa
taifa na uukataaji wa vitendo vya udhalilishaji na kuongeza kuwa wao
kama viongozi wa dini wataendelea kuonya na kufundisha watu wajue
athari za dhambi hiyo.
“Sisi
kama viongozi wa makanisa katika nchi hii tunapinga kwa nguzu zote
vitendo vya ushoga ndani ya taifa letu, vitendo vya ushoga ndivyo
vilivyosababisha Sodoma na Gomora kuchomwa moto kwa kuwa vilimchukiza
sana Mungu, Sisi kama viongozi wa dini katika kizazi chetu na vizazi
vijavyo hatutaki kufikia hapo na kuona taifa letu likichomwa moto”
Kwa wengine wasiejuwa jeshi, taarifa yangu ni kwamba wastani wapo aina tatu wa askari popote pale duniani.
1. WAPIGANAJI (THE MEN/TROOPS---"seamen" kama ni wa baharini, "airmen", wenye kutumia ndege). Ngazi ya chini kuliko zote. Hao ndio waliezagaa katika mambo ya filamu pale panomwagika damu. Kama anajina lake kama "fulani", Wazungu watamtambua kama "PRIVATE FULANI". Nchi nyingi watamchukua kijana yoyote yule mwenye nia kupata mafunzo katika ngazi hii.
2. WARRANT OFFICERS (au "sergeant majors"). Shughuli zao hao ni kuchunga nidhamu ya jeshi. Wapiganaji (MEN/TROOPS) hua wanawaogopa sana hawa warrant officers na ukiwa mwanajeshi na umemridhisha WARRANT OFFICER wako basi wewe unayo nidhamu ya hali ya juu. Hua wanapewa mamlaka wao na Waziri wa ulinzi katika mataifa mengi duniani, na kibali wanachopewa na Waziri kinaitwa "A WARRANT" na ndio maana wanaitwa WARRANT OFFICERS. (Kufika wa WARRANT OFFICER utakuwa wastani umepitia uKoporali, Sajenti, Staff Sajenti na kadhalika na unahitaji sana elimu kabla ya kuchaguliwa!)
3. MAAFISA WA KAMISHENI, COMMISSIONED OFFICERS (kama mhusika hapa) nao wanapewa wadhifa na Raisi wa nchi pekee! Kazi zao za msingi jeshini sio kupigana lakini NIKUIMARISHA JESHI KIMAWAZO NA KUTOA MBINU ZA KUPIGANA KWA MAFANIKIO. WANATAKIWA WAWE MFANO WA KUIGWA NA JESHI LOTE PIA NA WANANCHI WOTE! (Kwa kuwa unahitaji elimu ya juu kuwa afisa wa aina hii, nchi nyingi hutachaguliwa kama hujamaliza angalau kidato cha mwisho/Fomu 6 ya Tanzania. Baadhi ya ngazi za kupitia hapo ni CANDIDATE OFFICER, LUTENI, KAPTENI, MEJA, LUTENI KANALI, KANALI, BRIGADIER NA KADHALIKA KATIKA NYADHIFA SASA ZA UJENERALI au "u-admirali" ukiwa jeshini la maji au baharini)
Sasa tuje kwa Bw. Kapinga:
Huyu bwana usimuonee wivu KWANI ANAKAZI KWELI SASA.
Mifano:
1. Popote asipokuwepo Raisi, YEYE ANACHUKUA MAJUKUMU YA RAISI IKISTAHILI. Kwa mfano: mwiko kuumia kwa mwananchi ikiwa afisa yupo karibu na angemuokoa lakini eti afisa hakujisumbua hata kidogo!
2. Awe amevaa sare ya kijeshi au hakuvaa anatakiwa awe muungwana (GENTLEMAN) kuliko Mtanzania yoyote yule mwingine nchini !
(Hii inamaana akiwa D'salaam huyu bwana daima atakuwa amesimama kwa miguu katika usafiri wa daladala kwani si uungwana kuketi wakati mwanamama amesimama!)
3. Asije akaonekana amelewa pombe hata akiwa nyumbani kwake na ANAWEZA KUTIWA MBARONI kwani hastahili AFISA kuwa mlevi! Pia hamna ugomvi au makelele alipokuwepo yeye!
4. Hata katika mifarakano au hatari ya aina gani ya umma yeye asionekane muoga wa kijingajinga , wala asikimbie na kama anataka kujiepusha na hatari hiyo ASIJE AKAONEKANA ANAKIMBIA....huenda anaweza akatia pupa (PANIC) kwa wengine!
5. Yeye ndie wa mwisho kula jeshini na kama chakula ni kidogo watakula wanajeshi wote (TROOPS AND WARRANT OFFICERS) YEYE NDIE MWENYE KUKAA KWA NJAA!
...YOTE HAYA KUTOKANA NA KWAMBA YEYE NI AFISA , AJITOE MHANGA DAIMA!!!!! Na ukitaka kuona mfano mzuri wa afisa tena wa kuigwa: ni Kanali Gaddafi wa huko Libya yeye aliekataa katakata kukimbia mpaka kufa!
Luteni Peter Kapinga, mimi kama luteni kanali wa jeshi la hapa Afrika nakukaribisha sana katika wadhifa wa uafisa. Ninayo ndoto moja tu kwamba kabla sijaenda kaburini jeshi laTanzania, Msumbiji, Malawi, Uganda, Congo, Angola, Namibia, Swaziland, Botswana, Afrika Kusini, Lesotho na nchi zingine LITAKUWA JESHI MOJA TU LA NCHI MOJA LABDA NAWE UTAKUWA JEMEDALI AU FIELD MARSHAL WAKE!
Kazi ipo, Ndugu yangu; lakini siri kukupa mimi ziko mbili
1. Chunga afya yako
2. Chunga dhamira yako)