Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 24 December 2011

Nawatakia Machozi ya Furaha katika mwaka Ujao!!!

4 comments:

Goodman Manyanya Phiri said...

Tatizo kubwa kwa upande wangu sina kisima.....

kisima kama Alexandra Burke wa X-Factor mwenye wimbo mtamu "Hallelujah".

Sina kabisa kisima cha machozi ya furaha, lakini furaha ninayo daima tu!


Mwanadada mwenye blogu hii... sikiliza tafadhali...

Naomba niseme nimefurahi kuja kukufahamu mtandaoni hapa. Nakushukuru wewe binafsi pamoja na wasomaji wa blogu yako kwa kunisaidia kufanikisha ujumbe wangu mtandaoni hapa. Bila wewe, bila Da'Yasinta na bila ndugu wengine kibao (kama tishio la mtandaoni hapa lenye jina "Simon Kitururu" na abarikiwe naye daima na Mungu), nisingekuja kujulikana mtandaoni hapa kiasi cha kupewa mashtaka mepya ya kublogu kama nilivyopata kazini tarehe 12 mwezi huu (12 Desemba 2011).

Inamaana mumenifanya nyinyi nami niwe tishio kwa wabaguzi wa kikabila nchini mwetu. Mimi naona kama ni baraka kubwa mulienipa. Na najuwa tu Mungu wangu ameniwekea mazuri tu ulimwenguni hapa au maishani ya ng'ambo kwa kaburi BAADA YA MATESO YAO. Mimi siogopi kutetea haki ya umoja wa Mswahili.

Naomba niwataje Professor Mbele, Kamala Lutabasibwa, Bi. Edna, Raymond Mkandawili, "Mwanasosholojia", Yusuph Mcharia, "Mzee Wachangamoto", Hansom Omari, Ray Njau, Mzamera, "Chib", Bw. Bwaya, Tembe Mwana...

Na wengine wenye majina niliesahau!


Nawatakieni wanablogu wenzangu pamoja na wasomaji wenu, sherehe zenye baraka na usalama leo, kesho hadi mwaka mpya 2012!

Mwaka mpya usiwe X-factor kwenu, bali IN-factor. Mubarikiwe sana!!!

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Noeli njema kwako pamoja na familia na wapendwa wako. Hebu mwaka mpya na ukawe na heri tele!!!

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Heri ya Noeli na mwaka mpya nawe pia. Blessings !!!

Rachel Siwa said...

Kaka Manyanya ahsante sana, Kwa niaba ya Mablogger,Wapenzi/wasomaji wa blog hii sote Tunakutakia kila lililo jema Maishani mwako. Mungu awe nawe daima kila Iitwapo leo.

Kaka yangu Matondo ahsante sana na Mungu awe nawe pamoja na familia pia,uwe na wakati mwema leo na sikuzote,UBARIKIWE KAKA.AMEN.