Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 12 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 9....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Sisi tulipanda meli tukatangulia kwenda Aso ambako tungemchukua Paulo. Ndivyo alivyopanga; maana alitaka kufika huko kwa kupitia nchi kavu. Basi, alitukuta kule Aso, tukampandisha melini, tukaenda Mitulene.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kutoka huko tulisafiri tukafika Kio kesho yake. Siku ya pili, tulitia nanga Samo na kesho yake tukafika Mileto.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Paulo alikuwa amekusudia kuendelea na safari kwa meli bila kupitia Efeso ili asikawie zaidi huko Asia. Alikuwa na haraka ya kufika Yerusalemu kwa sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Laiti kichwa changu kingekuwa kisima cha maji,
na macho yangekuwa chemchemi ya machozi
ili nipate kulia mchana na usiku,
kwa ajili ya watu wangu waliouawa!
2Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa jangwani,
ambamo ningewaacha watu wangu na kwenda zangu.”
Mwenyezi-Mungu asema:
“Wote ni watu wazinzi,
ni genge la watu wahaini.
3Hupinda maneno yao kama pinde;
wameimarika kwa uongo na si kwa haki.
Huendelea kutoka uovu hata uovu,
wala hawanitambui mimi.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
4Kila mmoja ajihadhari na jirani yake!
Hata ndugu yeyote haaminiki,
kila ndugu ni mdanganyifu,
na kila jirani ni msengenyaji.
5Kila mmoja humdanganya jirani yake,
hakuna hata mmoja asemaye ukweli.
Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo;
hutenda uovu kiasi cha kushindwa kabisa kutubu.
6Wanarundika dhuluma juu ya dhuluma,
na udanganyifu juu ya udanganyifu.
Wanakataa kunitambua mimi.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
7Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nasema:
Tazama, nitawayeyusha na kuwajaribu!
Au, nifanye nini zaidi na watu wangu waovu?
8Ndimi zao ni kama mishale yenye sumu,
daima haziishi kudanganya;
kila mmoja huongea vema na jirani yake,
lakini moyoni mwake hupanga kumshambulia.
9Je, nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya?
Je, nisilipe kisasi kwa taifa kama hili?
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Nyakati za kulia na kuomboleza
10Nitaililia na kuiomboleza milima;
nitayaombolezea malisho nyikani,
kwa sababu yamekauka kabisa,
hakuna mtu apitaye mahali hapo.
Hakusikiki tena sauti za ng'ombe;
ndege na wanyama wamekimbia na kutoweka.
11Mwenyezi-Mungu asema:
“Nitaifanya Yerusalemu magofu matupu,
naam, nitaifanya kuwa pango la mbweha;
na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa,
mahali pasipokaliwa na mtu yeyote.”
12Nami nikauliza, “Je kuna mtu mwenye hekima kiasi cha kuweza kueleza mambo haya? Mwenyezi-Mungu aliongea na nani hata huyo aweze kutangaza kitu hicho? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mtu apitaye humo?”
13Mwenyezi-Mungu akajibu: “Kwa kuwa wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata matakwa yake. 14Badala yake wamefuata kwa ukaidi fikira za mioyo yao, wakaenda kuyaabudu Mabaali kama walivyofundishwa na wazee wao. 15Basi, mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Tazama nitawalisha watu hawa uchungu na kuwapa maji yenye sumu wanywe. 16Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wenyewe wala wazee wao hawakupata kuyajua; nitawafanya waandamwe na vita mpaka hapo nitakapowaangamiza wote.”
Watu wa Yerusalemu walilia msaada
17Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Fikirini na kuwaita wanawake waomboleze;
naam, waiteni wanawake hodari wa kuomboleza.
18Waambieni: ‘Njoni hima mkaomboleze juu yetu,
macho yetu yapate kuchuruzika machozi,
na kope zetu zibubujike machozi kama maji.’”
(Yeremia)
19Kilio kinasikika Siyoni:
“Tumeangamia kabisa!
Tumeaibishwa kabisa!
Lazima tuiache nchi yetu,
maana nyumba zetu zimebomolewa!
20Enyi wanawake, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu!
Tegeni masikio msikie jambo analosema.
Wafundisheni binti zenu kuomboleza,
na jirani zenu wimbo wa maziko:
21‘Kifo kimepenya madirisha yetu,
kimeingia ndani ya majumba yetu;
kimewakatilia mbali watoto wetu barabarani,
vijana wetu katika viwanja vya mji.
22Maiti za watu zimetapakaa kila mahali
kama marundo ya mavi mashambani,
kama masuke yaliyoachwa na mvunaji,
wala hakuna atakayeyakusanya.’
Ndivyo alivyoniambia Mwenyezi-Mungu niseme.”
23Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mwenye hekima asijivunie nguvu zake,
wala tajiri asijivunie utajiri wake.
24Anayetaka kujivuna na ajivunie jambo hili:
Kwamba ananifahamu
kwamba anajua Mwenyezi-Mungu hutenda mema,
hufanya mambo ya haki na uadilifu duniani.
Watu wa namna hiyo ndio wanipendezao.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
25Mwenyezi-Mungu asema: “Siku zaja ambapo nitawaadhibu wote waliotahiriwa mwilini tu: 26Wamisri, Wayuda, Waedomu, Waamoni, Wamoabu na wakazi wote wa jangwani wanaonyoa denge.9:26 wanaonyoa denge: Watu hao walinyoa denge kwa heshima ya mungu wao, desturi ambayo Waisraeli walikatazwa Maana watu hawa wote na Waisraeli wote hawakutahiriwa moyoni.”


Yeremia9;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: