Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 27 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 20....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Mafarisayo waliwasikia watu wakinongona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma. Mtanitafuta lakini hamtaniona, na pale nitakapokuwa nyinyi hamwezi kufika.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki? Ana maana gani anaposema: ‘Mtanitafuta lakini hamtanipata, na pale nitakapokuwa nyinyi hamwezi kufika?’”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Ugomvi kati ya Yeremia na Pashuri
1Kuhani Pashuri mwana wa Imeri, ambaye alikuwa ofisa mkuu wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu, alimsikia Yeremia akitoa unabii huo. 2Basi, Pashuri akampiga nabii Yeremia na kumtia kifungoni upande wa lango la juu la Benyamini, katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu. 3Kesho yake asubuhi, Pashuri alipomtoa Yeremia katika mkatale huo, Yeremia alimwambia hivi: “Mwenyezi-Mungu hakuiti tena Pashuri, bali ‘Kitisho Pande Zote’. 4Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi: ‘Tazama, nitakufanya uwe kitisho kwako wewe mwenyewe na kwa rafiki zako wote. Wao watauawa vitani kwa upanga wa maadui zao huku ukiangalia. Nitawatia watu wote wa Yuda mikononi mwa mfalme wa Babuloni, naye atawachukua mateka hadi Babuloni na kuwaua kwa upanga. 5Zaidi ya hayo, utajiri wote wa mji, mapato yake yote, vitu vyake vyote vya thamani pamoja na hazina zote za wafalme wa Yuda, nitazitia mikononi mwa maadui zao ambao watazipora na kuchukua kila kitu hadi Babuloni. 6Na kwa upande wako wewe Pashuri, pamoja na nyumba yako yote, mtapelekwa utumwani; hakika mtakwenda Babuloni. Huko ndiko utakakofia na kuzikwa, kadhalika na rafiki zako wote ambao uliwatabiria uongo.’”
Yeremia anamlalamikia Mungu
7Ee Mwenyezi-Mungu, wewe umenidanganya,
nami kweli nikadanganyika;
wewe una nguvu kuliko mimi,
nawe umeshinda.
Kutwa nzima nimekuwa mtu wa kuchekwa,
kila mtu ananidhihaki.
8Kila ninaposema kitu, nalalamika,
napaza sauti, “Ukatili na uharibifu!”
Maana kwangu kutangaza neno la Mwenyezi-Mungu
kwanifanya nishutumiwe na kudhihakiwa kutwa nzima.
9Lakini nikisema, “Sitamtaja Mwenyezi-Mungu,
wala sitasema tena kwa jina lake,”
moyoni mwangu huwa na kitu kama moto uwakao,
uliofungiwa ndani ya mifupa yangu.
Najaribu sana kuuzuia humo,
lakini ninashindwa.
10Nasikia wengi wakinongona juu yangu.
Wananipanga jina: “Kitisho kila upande!”
Wengine wanasema:
“Nendeni mkamshtaki! Na tumshtaki!”
Hata rafiki zangu wote wapenzi wanangojea tu nianguke!
Wanasema “Labda atadanganyika, nasi tutalipiza kisasi.”
11Lakini wewe Mwenyezi-Mungu u pamoja nami
kwangu wewe ni kama shujaa wa kutisha;
kwa hiyo watesi wangu watajikwaa,
na hawataweza kunishinda.
Wataaibika kupindukia,
maana hawatafaulu.
Fedheha yao itakuwa ya daima;
kamwe haitasahaulika.
12Ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
wewe humthibiti mtu mwadilifu,
huona yaliyo moyoni na akilini mwa watu,
unijalie kuona ukiwalipiza kisasi,
maana kwako nimekiweka kisa changu.
13Mwimbieni Mwenyezi-Mungu;
msifuni Mwenyezi-Mungu,
kwani ameyaokoa maisha ya mhitaji,
kutoka mikononi mwa watu waovu.
14Na ilaaniwe siku niliyozaliwa!
Siku hiyo mama aliponizaa,
isitakiwe baraka!
15Na alaaniwe aliyempelekea baba ujumbe:
“Umepata mtoto wa kiume”,
akamfanya ajae furaha.
16Mtu huyo na awe kama miji
aliyoiangusha Mwenyezi-Mungu bila huruma.
Mtu huyo na asikie kilio asubuhi,
na mchana kelele za vita,
17kwani hakuniua tumboni mwa mama yangu;
mama yangu angekuwa kaburi langu,
tumbo lake lingebaki kubwa daima.
18Kwa nini nilitoka tumboni mwa mama yangu?
Je, nilitoka ili nipate taabu na huzuni
na kuishi maisha ya aibu?


Yeremia20;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: