Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 15 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 103...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme, aliwahutubia watu. Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, “Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu.” Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa. Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza huduma yao, walitoka tena Yerusalemu, wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Sala kuu ya shukrani
(Zaburi ya Daudi)
1Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu;
nafsi yangu yote ilisifu jina lake takatifu!
2Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu!
Usisahau kamwe wema wake wote.
3Ndiye anayenisamehe uovu wangu wote,
na kuniponya magonjwa yote.
4Ndiye aniokoaye kutoka kifoni,
na kunijalia rehema na fadhili zake.
5Ndiye anayeniridhisha mema maisha yangu yote,
hata nabaki kijana mwenye nguvu kama tai.
6Mwenyezi-Mungu huhukumu kwa haki;
huwajalia wanaodhulumiwa haki zao.
7Alimjulisha Mose mwongozo wake,
aliwaonesha watu wa Israeli matendo yake.
8Mwenyezi-Mungu ni mwenye rehema na huruma;
ni mvumilivu na mwingi wa fadhili.
9Hatukemeikemei daima,
wala hasira yake haidumu milele.
10Yeye hatuadhibu kama tunavyostahili;
hatulipizi kadiri ya uovu wetu.
11Kama vile anga lilivyo juu mbali na dunia,
ndivyo ulivyo mwingi wema wake kwa watu wanaomcha.
12Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi,
ndivyo azitengavyo dhambi zetu mbali nasi.
13Kama vile baba amhurumiavyo mwanawe,
ndivyo Mwenyezi-Mungu awahurumiavyo wote wamchao.
14Mungu ajua mfumo wa nafsi zetu;
ajua kwamba sisi ni mavumbi.
15Walakini binadamu, maisha yake ni kama nyasi tu;
huchanua kama ua shambani:
16Upepo huvuma juu yake nalo latoweka;
na mahali lilipokuwa hapaonekani tena.
17Lakini fadhili za Mwenyezi-Mungu hudumu milele,
kwa wale wote wanaomheshimu;
na wema wake wadumu vizazi vyote,
18kwa wote wanaozingatia agano lake,
wanaokumbuka kutii amri zake.
19Mwenyezi-Mungu ameweka kiti chake cha enzi mbinguni;
yeye anatawala juu ya vitu vyote.
20Enyi malaika wakuu, msifuni Mwenyezi-Mungu;
mnaotimiza amri zake na kutekeleza neno lake!
21Enyi jeshi lote la mbinguni, msifuni Mwenyezi-Mungu;
enyi watumishi wake mnaotekeleza matakwa yake!
22Msifuni Mwenyezi-Mungu enyi viumbe vyake vyote;
msifuni popote mlipo katika milki yake.
Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu!


Zaburi103;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: