Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 18 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 106...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu. Mungu anataka nyinyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa. Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima, na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....
Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo. Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu. Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali anamdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Jehovah ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu kila mmoja na mahitaji yake...
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao....
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele....
Amina..!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Wema wa Mungu kwa watu wake
1 Taz Zab 11:5; 107:1; 118:1; 136:1 Haleluya! Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!
2Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu?
Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?
3Heri wale wanaotekeleza haki,
wanaotenda daima mambo yaliyo sawa.
4Unikumbuke ee Mwenyezi-Mungu unapowafadhili watu wako;
unisaidie wakati unapowaokoa;
5ili niweze kuona fanaka ya wateule wako,
nipate kufurahia furaha ya taifa lako,
na kuona fahari pamoja na watu wako.
6Tumetenda dhambi sisi na wazee wetu;
tumetenda maovu, tumefanya mabaya.
7Wazee wetu walipokuwa Misri,
hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu;
hawakukumbuka wingi wa fadhili zake,
bali walimwasi kando ya bahari ya Shamu.
8Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi,
ili aoneshe nguvu yake kuu.
9Aliikemea bahari ya Shamu ikakauka;
akawapitisha humo kama katika nchi kavu.
10Aliwaokoa mikononi mwa waliowachukia;
aliwaokoa kutoka kwa nguvu za maadui zao.
11Maji ya bahari yaliwafunika maadui zao;
wala hakusalia hata mmoja wao.
12Hapo watu wake wakaamini maneno yake,
wakamwimbia tenzi za sifa yake.
13Lakini mara walisahau matendo yake,
wakaacha kutegemea shauri lake.
14Walijawa na tamaa kubwa kule jangwani,
wakamjaribu Mungu kule nyikani.
15Naye akawapa kile walichoomba,
lakini akapeleka maradhi mabaya kati yao.
16Kule kambini walimwonea wivu Mose,
na Aroni mtumishi mtakatifu wa Mwenyezi-Mungu.
17Ndipo ardhi ikafunguka ikammeza Dathani,
na kumzika Abiramu na kundi lake lote;
18moto ukawatokea wafuasi wao,
ukawateketeza watu hao waovu.
19Walitengeneza ndama wa dhahabu kule Horebu,
wakaiabudu sanamu hiyo ya kusubu;
20waliubadilisha utukufu wa Mungu,
kwa sanamu ya mnyama ambaye hula nyasi.
21Walimsahau Mungu aliyewaokoa,
aliyetenda mambo makuu nchini Misri,
22maajabu katika nchi hiyo ya Hamu,
na mambo ya kutisha katika bahari ya Shamu.
23Mungu alisema atawaangamiza watu wake,
ila tu Mose mteule wake aliingilia kati,
akaizuia hasira yake isiwaangamize.
24Kisha wakaidharau nchi ile ya kupendeza,
kwa sababu hawakuwa na imani na ahadi ya Mungu.
25Walinungunika mahemani mwao,
wala hawakumsikiliza Mwenyezi-Mungu.
26Hivyo Mungu akainua mkono akaapa
kwamba atawaangamizia jangwani;
27atawatawanya wazawa wao kati ya watu,
na kuwasambaza duniani kote.
28Kisha wakajiunga kumwabudu Baali kule Peori,
wakala tambiko zilizotambikiwa mizimu.
29Waliichochea hasira ya Mwenyezi-Mungu kwa matendo yao,
maradhi mabaya yakazuka kati yao.
30Lakini Finehasi akasimama kufanya malipizi,
na yale maradhi yakakoma.
31Jambo hilo lakumbukwa kwa heshima yake,
tangu wakati huo na nyakati zote.
32Walimkasirisha Mungu penye maji ya Meriba,
Mose akapata taabu kwa ajili yao.
33Walimtia Mose uchungu rohoni,
hata akasema maneno bila kufikiri.
34Hawakuwaua watu wa mataifa mengine
kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru.
35Bali walijumuika na watu wa mataifa,
wakajifunza kutenda mambo yao.
36Waliabudu sanamu za miungu yao,
nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza.
37Waliwaua watoto wao wa kiume na wa kike,
wakawatoa tambiko kwa pepo.
38Walimwaga damu ya wasio na hatia,
damu ya watoto wao wa kiume na wa kike
ambao waliwatoa tambiko kwa sanamu za Kanaani,
nayo nchi ikatiwa unajisi kwa mauaji hayo.
39Hivyo wakafanywa najisi kwa matendo yao,
2wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazinzi.
40Hasira ya Mwenyezi-Mungu ikawawakia watu wake,
akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.
41Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa,
hao wenye kuwachukia wakawatawala.
42Maadui zao waliwakandamiza,
wakawatumikisha kwa nguvu.
43Mara nyingi Mungu aliwaokoa watu wake,
lakini wao wakachagua kumwasi,
wakazidi kuzama katika uovu wao.
44Hata hivyo Mungu alizijali taabu zao,
wakati aliposikia kilio chao;
45kwa ajili yao alilikumbuka agano lake,
akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.
46Aliwafanya waliowakandamiza wawaonee huruma.
47Utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa,
tupate kulisifu jina lako takatifu,
na kuona fahari juu ya sifa zako.
48Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele!
Na watu wote waseme: “Amina!”
Asifiwe Mwenyezi-Mungu!


Zaburi106;1-48

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: