Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 1 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 28...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii


Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu. Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao. Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: Vipofu, viwete na waliopooza. [Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe, maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona





Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane. Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo na kujua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, “Je, wataka kupona?” Naye akajibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.” Yesu akamwambia, “Inuka, chukua mkeka wako utembee.” Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako.” Lakini yeye akawaambia, “Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: ‘Chukua mkeka wako, utembee.’” Nao wakamwuliza, “Huyo mtu aliyekuambia: ‘Chukua mkeka wako, utembee,’ ni nani?” Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu. Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa hekaluni, akamwambia, “Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi.” Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.






Sifa za hekima

1“Hakika kuna machimbo ya fedha,
na mahali ambako dhahabu husafishwa.
2Watu huchimba chuma ardhini,
huyeyusha shaba kutoka mawe ya madini.
3Wachimba migodi huleta taa gizani,
huchunguza vina vya ardhi
na kuchimbua mawe yenye madini gizani.
4Binadamu huchimba mashimo mbali na makazi ya watu,
mbali na watu mahali kusipofikika,
wachimba madini huninginia wamefungwa kamba.
5Kutoka udongoni chakula hupatikana,
lakini chini yake kila kitu huvurugwa kwa moto.
6Katika mawe yake ndimo vilimo vito vya rangi ya samawati
na udongo wake una vumbi la dhahabu.
7“Njia za kwenda kwenye migodi hiyo
hakuna ndege mla nyama azijuaye;
na wala jicho la tai halijaiona.
8Wanyama waendao kwa madaha hawajazikanyaga
wala simba hawajawahi kuzipitia.
9Binadamu huchimbua miamba migumu kabisa,
huichimbua milima na kuiondolea mbali.
10Hupasua mifereji kati ya majabali,
na jicho lake huona vito vya thamani.
11Huziba chemchemi zisitiririke,
na kufichua vitu vilivyofichika.
12 Taz Sir 1:6; Bar 3:15 “Lakini hekima itapatikana wapi?
Ni mahali gani panapopatikana maarifa?
13 Taz Bar 3:29-31 Hakuna mtu ajuaye thamani ya hekima,
wala hekima haipatikani nchini mwa walio hai.
14Vilindi vyasema, ‘Hekima haimo kwetu,’
na bahari yasema, ‘Haiko kwangu.’
15Hekima haiwezi kupatikana kwa dhahabu,
wala kwa kupima kiasi kingi cha fedha.
16Haiwezi kupimwa kwa dhahabu ya Ofiri,
wala kwa vito vya Sardoniki au vya rangi ya samawati,
17dhahabu au kioo havilingani nayo,
wala haiwezi kubadilishwa na vito vya dhahabu safi.
18Hekima ina thamani kuliko matumbawe na marijani,
thamani yake yashinda thamani ya lulu.
19Topazi ya Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,
wala haiwezi kupewa bei ya dhahabu safi.
20“Basi, hekima yatoka wapi?
Ni wapi panapopatikana maarifa?
21Imefichika machoni pa viumbe vyote hai,
na ndege wa angani hawawezi kuiona.
22Abadoni na Kifo wasema,
‘Tumesikia uvumi wake kwa masikio yetu.’
23 Taz Bar 3:35-37 “Mungu aijua njia ya hekima,
anajua mahali inapopatikana.
24Maana yeye huona mpaka upeo wa dunia,
huona kila kitu chini ya mbingu.
25Alipoupa upepo uzito wake,
na kuyapimia maji mipaka yake;
26alipoamua mvua inyeshe wapi,
umeme na radi vipite wapi;
27 Taz Sira 1:9,19 hapo ndipo alipoiona hekima na kuitangaza,
aliisimika na kuichunguza.”
28 Taz Zab 111:10; Meth 1:7; 9:10 Kisha Mungu akamwambia mwanadamu:
“Tazama! Kumcha Bwana ndio hekima;
na kujitenga na uovu ndio maarifa.”



Yobu28;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: