Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 19 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 40...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua
na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani. Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.” Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani, akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamhudumia.

Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema, “Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu. Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya nyinyi kuwa wavuvi wa watu.” Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


1Mwenyezi-Mungu akaendelea kumwambia Yobu:
2“Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu?
Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”
3Kisha Yobu akamjibu Mwenyezi-Mungu:
4“Mimi sifai kitu nitakujibu nini?
Naufunga mdomo wangu.
5Nilithubutu kusema na sitasema tena.
Nilisisitiza lakini sitaendelea kusema zaidi.”
6Hapo Mwenyezi-Mungu akamjibu kutoka kimbunga:
7“Jikaze kama mwanamume.
Nitakuuliza, nawe utanijibu.
8Je, unataka kweli kubatilisha hukumu yangu,
kuniona nina hatia ili wewe usiwe na hatia?
9Je, una nguvu kama mimi Mungu?
Waweza kunguruma kwa sauti kama yangu?
10“Basi, jioneshe kuwa na fahari na ukuu,
ujipambe kwa utukufu na fahari.
11Wamwagie watu hasira yako kuu;
mwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.
12Mwangalie kila mwenye kiburi na kumporomosha,
uwakanyage waovu mahali walipo.
13Wazike wote pamoja ardhini;
mfunge kila mmoja kwa kifungo cha kifo.
14Hapo nitakutambua,
kwamba nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.
15“Liangalie lile dude Behemothi,40:15 Behemothi: Mnyama huyo huenda ni kiboko.
nililoliumba kama nilivyokuumba wewe.
Hilo hula nyasi kama ng'ombe,
16lakini mwilini lina nguvu ajabu,
na misuli ya tumbo lake ni imara.
17Huufanya mkia wake mgumu kama mwerezi,
mishipa ya mapaja yake imeshonwa pamoja.
18Mifupa yake ni mabomba ya shaba,
viungo vyake ni kama pao za chuma.
19“Hilo ni la kwanza la ajabu kati ya viumbe vyangu!40:19 Hilo … vyangu: Au hilo ndilo tunda la kwanza la kazi ya Mungu.
Ni mimi Muumba wake niwezaye kulishinda.
20Milima wanamocheza wanyama wote wa porini
hutoa chakula chake.
21Hujilaza chini ya vichaka vya miiba,
na kujificha kati ya matete mabwawani.
22Hujisitiri katika vivuli vya vichaka vya miiba
na vya miti iotayo kando ya vijito.
23Mto ukifurika haliogopi,
halitishiki hata mto Yordani ukilifurikia kinywani.
24Nani awezaye kuliziba macho na kuliteka?
Nani awezaye kulitoboa pua kwa mtego?
25 Taz Zab 74:14; 104:26; Isa 27:1 40:25 Kufuatana na Biblia ya Kiebrania; baadhi ya tafsiri ni 41:1 Je, waweza kuvua dude Lewiyathani40:25 Lewiyathani: Au Mamba. kwa ndoana,
au kuufunga ulimi wake kwa kamba?
26Je, unaweza kulitia kamba puani mwake,
au kulitoboa taya kwa kulabu?
27Je, wadhani litakusihi uliachilie?
Je, litazungumza nawe kwa upole?
28Je, litafanya mapatano nawe,
ulichukue kuwa mtumishi wako milele?
29Je, utacheza nalo kama ndege,
au kulifunga kamba licheze na wajakazi wako?
30Wadhani wavuvi watashindania bei yake?
Je, wafanyabiashara watathubutu kulikata na kugawana?
31Je, waweza kuichoma ngozi yake kwa mikuki,
au kichwa chake kwa mfumo wa kuvua samaki?
32Jaribu tu kuligusa, uone cha mtema kuni;
Kamwe hutarudia tena kufanya hivyo!


Yobu40;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: