Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 15 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 38...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii


Yesu aliuita tena ule umati wa watu, akawaambia, “Nisikilizeni nyote, mkaelewe. Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mtu kutoka nje kinachoweza kumtia mtu unajisi. Lakini kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia mtu unajisi.” Mwenye masikio na asikie! Alipouacha umati wa watu na kuingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza maana ya huo mfano. Naye akawaambia, “Je, hata nyinyi hamwelewi? Je, hamwelewi kwamba kitu kinachomwingia mtu kutoka nje, hakiwezi kumtia unajisi, kwa maana hakimwingii moyoni, ila tumboni, na baadaye hutolewa nje chooni?” (Kwa kusema hivyo, Yesu alihalalisha vyakula vyote.) Akaendelea kusema, “Kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia unajisi. Maana kutoka ndani, moyoni mwa mtu, hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, uchoyo, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi na upumbavu. Maovu hayo yote yatoka ndani ya mtu, nayo humtia mtu unajisi.”

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona



Yesu aliondoka hapo, akaenda wilaya ya Tiro. Huko aliingia katika nyumba moja na hakutaka mtu ajue; lakini hakuweza kujificha. Hapo mwanamke mmoja ambaye binti yake alikuwa na pepo, alisikia habari za Yesu. Basi, akaja akajitupa chini mbele ya miguu yake. Mama huyo alikuwa Mgiriki, mwenyeji wa Sirofoinike. Basi, akamwomba Yesu amtoe binti yake pepo mchafu. Yesu akamwambia, “Kwanza watoto washibe; kwa maana si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.” Lakini huyo mama akasema, “Ni kweli, Bwana; lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto.” Yesu akamwambia, “Kwa sababu ya neno hilo, nenda. Pepo amemtoka binti yako!” Basi, akaenda nyumbani kwake, akamkuta mtoto amelala kitandani, na pepo amekwisha mtoka.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kisha Yesu aliondoka wilaya ya Tiro, akapitia Sidoni, akafika ziwa Galilaya kwa kupitia nchi ya Dekapoli. Basi, wakamletea bubu kiziwi, wakamwomba amwekee mikono. Yesu akamtenga na umati wa watu, akamtia vidole masikioni, akatema mate na kumgusa ulimi. Kisha akatazama juu mbinguni, akapiga kite, akamwambia, “Efatha,” maana yake “Funguka.” Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukafunguliwa, akaanza kusema sawasawa. Yesu akawaamuru wasimwambie mtu juu ya jambo hilo. Lakini kadiri alivyowakataza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari hiyo. Watu walishangaa sana, wakasema, “Amefanya yote vyema: Amewajalia viziwi kusikia, na mabubu kusema!”

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Mungu anamjibu Yobu

1Hapo Mwenyezi-Mungu alimjibu Yobu kutoka dhoruba:
2“Nani wewe unayevuruga mashauri yangu
kwa maneno yasiyo na akili?
3Jikaze kama mwanamume,
nami nitakuuliza nawe utanijibu.
4“Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya dunia?
Niambie, kama una maarifa.
5Ni nani aliyeweka vipimo vyake, wajua bila shaka!
Au nani aliyelaza kamba juu yake kuipima?
6Je, nguzo za dunia zimesimikwa juu ya nini,
au nani aliyeliweka jiwe lake la msingi,
7 Taz Bar 3:34 nyota za asubuhi zilipokuwa zikiimba pamoja,
na wana wa Mungu wakapaza sauti za shangwe?
8 Taz Yer 5:22 Ni nani aliyeyafunga mafuriko ya bahari
wakati yalipozuka na kuvuma kutoka vilindini?
9Mimi ndiye niliyeifunika bahari kwa mawingu
na kuiviringishia giza nene.
10Niliiwekea bahari mipaka,
nikaizuia kwa makomeo na milango,
11nikaiambia: ‘Mwisho wako ni hapa, si zaidi!
Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!’
12“Yobu, tangu uzaliwe umewahi kuamuru kupambazuke?
na kulifanya pambazuko lijue mahali pake,
13ili lipate kuikamata dunia kwa pembe zake
na kuwatimulia mbali waovu waliomo?
14Dunia hugeuka na kupata rangi kama vazi;
kama udongo wa mfinyanzi unavyogeuzwa na mhuri.
15Lakini waovu watanyimwa mwanga wao,
mkono wanaonyosha kupiga watu utavunjwa.
16“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?
au kutembea juu ya sakafu ya kilindi cha bahari?
17Je, umewahi kuoneshwa malango ya kifo,
au kuyaona malango ya makazi ya giza nene?
18Je, wajua ukubwa wa dunia?
Niambie kama unajua haya yote.
19“Je, makao ya mwanga yako wapi?
Nyumbani kwa giza ni wapi,
20ili upate kulipeleka kwenye makao yake,
na kuifahamu njia ya kwenda huko kwake.
21Wewe unapaswa kujua,
wewe ambaye umekwisha ishi miaka mingi!
22“Je, umewahi kuingia katika bohari za theluji,
au kuona bohari za mvua ya mawe
23ambavyo nimevihifadhi kwa ajili ya wakati wa fujo,
kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?
24Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,
au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?
25“Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?
Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,
26ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtu
na jangwani ambako hakuna mtu,
27ili kuiburudisha nchi kavu na kame
na kuifanya iote nyasi?
28“Je, mvua ina baba?
Au nani ameyazaa matone ya umande?
29Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani?
Nani aliyeizaa theluji?
30Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,
na uso wa bahari ukaganda.
31 Taz Yobu 9:9; Amo 5:8 “Angalia makundi ya nyota:
Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia,
au kuvilegeza vifungo vya Orioni?
32Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake,
au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake?
33Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;
Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?
34“Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawingu
yakufunike kwa mtiririko wa mvua?
35Je, wewe ukiamuru umeme umulike,
utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’
36Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Nili
au aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?38:36 aya hii si dhahiri. Ilifikiriwa zamani kwamba ndege kwarara na jogoo walikuwa wanaweza kujua majira fulani.
37Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,
au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?
38ili vumbi duniani igandamane
na udongo ushikamane na kuwa matope?
39“Je, waweza kumwindia simba mawindo yake
au kuishibisha hamu ya wana simba;
40wanapojificha mapangoni mwao,
au kulala mafichoni wakiotea?
41Ni nani awapaye kunguru chakula chao,
makinda yao yanaponililia mimi Mungu,
na kurukaruka huku na huko kwa njaa?



Yobu38;1-41

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: