Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 9 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 34...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

Daudi alikuwa mtoto wa Yese, Mwefrathi kutoka Bethlehemu katika Yuda. Yese alikuwa na watoto wanane wa kiume. Wakati Shauli alipokuwa mfalme, yeye alikuwa tayari mzee, mtu mwenye umri mkubwa. Wana wakubwa watatu wa Yese, Eliabu mzaliwa wa kwanza, Abinadabu aliyefuata na Shama wa tatu, walikuwa wamekwenda pamoja na Shauli vitani. Daudi alikuwa ndiye mdogo wa wote. Wale watoto watatu wakubwa walikuwa wamekwenda na Shauli. Ingawa Daudi mara kwa mara alikwenda kwa Shauli, alirudi nyumbani Bethlehemu kuchunga kondoo wa baba yake.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...

Kwa muda wa siku arubaini, asubuhi na jioni, yule Mfilisti Goliathi alijitokeza hadharani, akasimama na kuwakejeli wanajeshi wa Israeli. Siku moja, Yese alimwambia mwanawe Daudi, “Wapelekee kaka zako bisi kilo kumi na mikate kumi. Wapelekee haraka huko kambini. Na yule kamanda wao wa kikosi cha wanajeshi elfu mpelekee jibini hizi kumi. Kawaangalie kaka zako kama wanaendelea vizuri na kisha uniletee habari zao.” Wakati huo mfalme Shauli, kaka zake Daudi na wanajeshi wote wa Israeli walikuwa kwenye bonde la Ela, wanapigana na Wafilisti.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kesho yake, Daudi aliamka asubuhi na mapema, na kondoo akamwachia mchungaji. Alichukua chakula na kwenda kama alivyoagizwa na baba yake Yese. Alipofika kwenye kambi ya Waisraeli, aliwakuta wanajipanga kwenye sehemu yao ya vita na wanapiga kelele za vita. Majeshi ya Waisraeli na ya Wafilisti walijipanga tayari kupigana vita, majeshi yakiwa yanakabiliana ana kwa ana. Daudi alimkabidhi chakula mtu aliyetunza mizigo, akawakimbilia wanajeshi, akaenda kwa kaka zake na kuwasalimia. Alipokuwa anaongea nao, Goliathi yule shujaa wa Wafilisti kutoka Gathi alijitokeza mbele ya wanajeshi wa Israeli kama alivyozoea. Naye Daudi alimsikiliza vizuri sana. Waisraeli walipomwona Goliathi, walimkimbia, na kumwogopa sana. Waliambiana, “Je, mmemwona yule mtu aliyejitokeza? Ama kweli, amejitokeza kuwakejeli Waisraeli. Mfalme Shauli atampa mtu yeyote atakayemuua mtu huyo utajiri mwingi. Zaidi ya yote, atamwoza binti yake. Tena, watu wa jamaa ya baba yake watakuwa huru, hawatalipa kodi.”

Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.


1Kisha Elihu akaendelea kusema:
2“Sikilizeni maneno yangu enyi wenye hekima,
nitegeeni masikio yenu, nyinyi wenye ujuzi.
3 Taz Yobu 12:11 Sikio huyapima maneno,
kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4Basi, na tuchague lililo sawa,
tuamue miongoni mwetu lililo jema.
5Basi, Yobu ametamka: ‘Mimi Yobu sina hatia,
Mungu ameniondolea haki yangu.
6Ingawa sina hatia naonekana kuwa mwongo;
kidonda changu hakiponyeki ingawa sina kosa.’
7Ni nani aliye kama Yobu
ambaye kwake ubaradhuli ni kama kunywa maji?
8Huandamana na watenda maovu
hutembea na watu waovu.
9Maana amesema, ‘Mtu hapati faida yoyote,
kujisumbua kumpendeza Mungu.’
10“Kwa hiyo nisikilizeni, enyi wenye ujuzi.
Mungu kamwe hawezi kufanya uovu;
Mungu Mwenye Nguvu hawezi kufanya kosa.
11 Taz Zab 62:12 Mungu atamlipa mtu kadiri ya matendo yake,
atamlipiza kulingana na mwenendo wake.
12Ni ukweli mtupu: Mungu hafanyi ovu;
Mungu Mwenye Nguvu kamwe hapotoshi haki.
13Je, kuna aliyemkabidhi mamlaka juu ya dunia?
Uwezo wake juu ya ulimwengu ni wake peke yake.
14Kama Mungu angejifikiria tu yeye mwenyewe,
akiondoa pumzi yake ya uhai duniani,
15viumbe vyote vingeangamia kabisa,
naye binadamu angerudi mavumbini.
16“Kama una akili sikiliza;
sikiliza ninachokuambia.
17Je, anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki?
Je, utathubutu kumhukumu mwadilifu na mwenye nguvu?
18Amwambiaye mfalme, ‘Wewe ni takataka!’
Na watu mashuhuri, ‘Nyinyi ni waovu!’
19Yeye hawapendelei wakuu,
wala kuwajali matajiri kuliko maskini,
maana wote hao ni kazi ya mikono yake.
20Kufumba na kufumbua hao wamekufa;
hutikiswa usiku na kuaga dunia;
nao wenye nguvu hufutiliwa mbali bila kutumia nguvu za mtu.
21“Macho ya Mungu huchunguza mienendo ya watu;
yeye huziona hatua zao zote.
22Hakuna weusi wala giza nene
ambamo watenda maovu waweza kujificha.
23Mungu hahitaji kumjulisha mtu
wakati wa kumleta mbele ya mahakama yake.
24Huwaangamiza wenye nguvu bila uchunguzi,
na kuwaweka wengine mahali pao.
25Kwa kuwa anayajua matendo yao yote,
huwaporomosha usiku wakaangamia.
26Huwachapa hadharani kwa ajili ya uovu wao,
27kwa sababu wameacha kumfuata yeye,
wakazipuuza njia zake zote.
28Hata wakasababisha kilio cha maskini kimfikie Mungu,
Mungu akasikiliza kilio chao hao walioteswa.
29Kama Mungu akinyamaza, nani awezaye kumlaumu?
Kama akificha uso wake, nani awezaye kumwona,
30liwe ni taifa au mtu mmojammoja?
Hufanya hivyo, mtu mbaya asitawale,34:30 hati nyingine za kale: Lakini aweza kuyawekea mataifa na watu mtu mbaya kuwa mfalme, mdhalimu.
au wale wahatarishao maisha ya watu.
31“Tuseme mtu amemwambia Mungu,
‘Nimekosa, sitatenda dhambi tena.
32Nioneshe makosa nisiyoweza kuyaona
kama nimetenda mabaya sitayarudia tena.’
33Je, Mungu atapaswa kumwadhibu kama uonavyo wewe?
Wewe ndiwe unayeamua, sio mimi.
Basi, sema unachofikiri wewe.
34Mtu yeyote mwenye akili,
na kila mwenye hekima anayenisikiliza atasema:
35‘Yobu anaongea bila kutumia akili,
maneno yake hayana maana.’
36Laiti Yobu angechunguzwa mpaka mwisho,
kwa maana anajibu kama watu waovu.
37Huongeza uasi juu ya dhambi zake;
anaeneza mashaka kati yetu,
na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

Yobu34;1-37

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: