Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 31 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 27...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana
Tumshukuru Mungu wetu kila wakati
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao. Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.

Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni
Uabudiwe Jehovah,Uhimidiwe Yahweh,Matendo yako ni makuu mno,
Matendo yako ni ya ajabu,Matendo yako yanatisha
Hakuna kama wewe ee Mungu wetu..

Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni...!!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua  njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu. Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi. Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.

Baba wa Mbinguni tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu
wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee  kama inavyokupendeza wewe
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
sawasawa na mapenzi yake....

Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo 
wa Mungu Baba ukae nanyi daima....


Nawapenda.



1Yobu akaendelea kutoa hoja yake, akasema:
2“Naapa kwa Mungu aliye hai,
aliyeniondolea haki yangu,
Mungu Mwenye Nguvu aliyeifanya nafsi yangu iwe na uchungu!
3Naapa kuwa kadiri ninavyoweza kupumua,
roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu;
4midomo yangu kamwe haitatamka uongo,
wala ulimi wangu kusema udanganyifu.
5Siwezi kabisa kusema kuwa nyinyi mnasema ukweli
mpaka kufa kwangu nasema sina hatia.
6Nashikilia unyofu wangu, wala sitauacha;
katika dhamiri yangu sina cha kunihukumu maishani mwangu.
7“Adui yangu na apate adhabu ya mwovu,
anayeinuka kunilaumu aadhibiwe kama mbaya.
8Asiyemcha Mungu ana tumaini gani,
Mungu anapomkatilia mbali,
anapomwondolea uhai wake?
9Je, atakapokumbwa na taabu,
Mungu atasikia kilio chake?
10Mwovu hawezi kufurahi mbele ya Mungu Mwenye Nguvu;
hataweza kudumu akimwomba Mungu.
11Nitawafundisheni kitendo cha Mungu kilivyo,
sitawaficheni mipango yake Mungu Mwenye Nguvu.
12Lakini nyinyi mnajua jambo hilo vizuri sana!
Mbona, basi mnaongea upuuzi?
13“Hiki ndicho Mungu alichomwekea mtu mwovu,
alichopangiwa mdhalimu kupata ni hiki:
14Watoto wake hata wawe wengi watauawa kwa upanga;
wazawa wake hawatakuwa na chakula cha kutosha.
15Wale watakaopona watakufa kwa maradhi mabaya,
na wajane wao hawatawaombolezea.
16Hata akirundika fedha kama mavumbi,
na mavazi kama udongo wa mfinyanzi,
17na arundike tu, lakini mnyofu ndiye atakayeyavaa,
na fedha yake watagawana watu wasio na hatia.
18Nyumba ajengayo mwovu ni kama utando wa buibui,27:18 kama utando wa buibui makala ya Kiebrania ina: “Kama nondo”.
ni kama kibanda cha mlinzi shambani.
19Huenda kulala tajiri, lakini ni mara ya mwisho;
atafungua macho yake, na utajiri wake umetoweka!
20Vitisho humvamia kama mafuriko;
usiku hukumbwa na kimbunga.
21Upepo wa mashariki humpeperusha akatoweka;
humfagilia mbali kutoka makao yake.
22Upepo huo humvamia bila huruma;
atajaribu kuukimbia lakini mbio za bure.
23Upepo humzomea akimbiapo,
na kumfyonya toka mahali pake.




Yobu27;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: