Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 11 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 13...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?


Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe ee Mungu wetu....!!




Lakini nyinyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo. Waliwaambieni: “Siku za mwisho, watatokea watu watakaowadhihaki nyinyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.” Hao ndio wanaosababisha mafarakano, watu wa fikira za kidunia, wasio na Roho wa Mungu.

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti 

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona



Lakini nyinyi, wapenzi wangu, jijengeni wenyewe juu ya imani yenu takatifu kabisa. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, na kudumu katika upendo wa Mungu, mkimngojea Bwana wetu Yesu Kristo ambaye, kwa huruma yake, atawajalieni uhai wa milele. Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka; waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni. Lakini kwa wengine muwe na huruma pamoja na tahadhari, mkichukia hata mavazi yao yenye madoa ya tamaa zao mbaya.


Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...




Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta nyinyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake, kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina.

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Jibu la Yobu laendelea

1“Tazama, hayo yote nimeyaona kwa macho yangu;
nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.
2Yote mnayoyajua, mimi pia nayajua.
Mimi si mtu duni kuliko nyinyi.
3Lakini ningependa kusema na Mungu mwenye nguvu,
natamani kujitetea mbele zake Mungu.
4Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa;
nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.
5Laiti mngekaa kimya kabisa,
ikafikiriwa kwamba mna hekima!
6Sikilizeni basi hoja yangu,
nisikilizeni ninapojitetea.
7Je, mnadhani mwamtumikia Mungu kwa kusema uongo?
Mnafikiri kusema kwa hila kunamfaa yeye?
8Je, mnajaribu kumpendelea Mungu?
Je, mtamtetea Mungu mahakamani?
9Je, akiwakagua nyinyi mtapona?
Au mnadhani mnaweza kumdanganya Mungu kama watu?
10Hakika yeye atawakemea
kama mkionesha upendeleo kwa siri.
11Je, fahari yake haiwatishi?
Je, hampatwi na hofu juu yake?
12Misemo yenu ni methali za majivu,
hoja zenu ni ngome za udongo.
13“Nyamazeni, nami niongee.
Yanipate yatakayonipata.
14Niko tayari hata kuhatarisha
maisha yangu;13:14 kadiri ya tafsiri ya kale ya Kigiriki yaani Septuaginta. Kiebrania aya yaanza na “Kwa nini…?” Na msemo “Kushika nyama yangu katikati ya meno yangu” haupatikani penginepo na maana yake si dhahiri – lakini kutokana na aya hiyo maana yake ni sawa na kuhatarisha maisha.
15Mungu aniue akitaka, sina la kupoteza,
hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.
16Kama nikifaulu hapo nitakuwa nimeshinda,
maana mtu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
17Sikilizeni kwa makini maneno yangu,
maelezo yangu na yatue masikioni mwenu.
18Kesi yangu nimeiandaa vilivyo,
nina hakika mimi sina hatia.
19“Nani atakayeipinga hoja yangu?
Niko tayari kunyamaza na kufa.
20Mungu wangu, nijalie tu haya mawili,
nami sitajificha mbali na wewe:
21Kwanza uniondolee mkono wako unaonipiga,
na usiniangamize kwa kitisho chako.
22“Uanze kutoa hoja yako nami nikujibu.
Au mimi nianze, nawe unijibu.
23Makosa na dhambi zangu ni ngapi?
Nijulishe hatia na dhambi yangu.
24“Mbona unaugeuza uso wako mbali nami?
Kwa nini unanitendea kama adui yako?
25Je, utalitisha jani linalopeperushwa,
au kuyakimbiza makapi?
26Wewe umetoa mashtaka makali dhidi yangu,
na kunibebesha dhambi za ujana wangu.
27 Taz Yobu 33:11 Wanifunga minyororo miguuni,
wazichungulia hatua zangu zote,
na nyayo zangu umeziwekea kikomo.
28Nami naishia kama mti uliooza,
mithili ya vazi lililoliwa na nondo.


Yobu13;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: