Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 17 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 4....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Naye akawaambia, “Nyinyi mmejaliwa kujua siri ya ufalme wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


ili, ‘Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.’”
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Yerusalemu baada ya kuangamia
1Jinsi gani dhahabu yetu ilivyochujuka,
dhahabu safi kabisa ilivyobadilika!
Mawe ya thamani yametawanywa
yamesambaa barabarani kote.
2Watoto wa Siyoni waliosifika sana,
waliothaminiwa kama dhahabu safi,
jinsi gani sasa wamekuwa kama vyombo vya udongo,
kazi ya mikono ya mfinyanzi!
3Hata mbwamwitu huwa na hisia za mama
na kuwanyonyesha watoto wao;
lakini watu wangu wamekuwa wakatili,
hufanya kama mbuni nyikani.
4Midomo ya watoto wachanga imekauka kwa kiu,
watoto wanaomba chakula lakini hakuna anayewapa.
5Watu waliojilisha vyakula vinono
sasa wanakufa njaa barabarani.
Waliolelewa na kuvikwa kifalme
sasa wanafukua kwa mikono kwenye majaa.
6 Taz Mwa 19:24 Watu wangu wamepata adhabu kubwa
kuliko watu wa mji wa Sodoma
mji ambao uliteketezwa ghafla
bila kuwa na muda wa kunyosha mkono.
7Vijana wa Siyoni walikuwa safi kuliko theluji,
walikuwa weupe kuliko maziwa.
Miili yao ilikuwa myekundu kama matumbawe,
uzuri wa viwiliwili vyao kama johari ya rangi ya samawati.
8Sasa sura zao ni nyeusi kuliko makaa,
wanapita barabarani bila kujulikana;
ngozi yao imegandamana na mifupa yao
imekauka, imekuwa kama kuni.
9Afadhali waliouawa kwa upanga
kuliko waliokufa kwa njaa,
ambao walikufa polepole
kwa kukosa chakula.
10 Taz Kumb 38:57; Eze 5:10 Kina mama ambao huwa na huruma kuu
waliwapika watoto wao wenyewe,
wakawafanya kuwa chakula chao
wakati watu wangu walipoangamizwa.
11Mwenyezi-Mungu alionesha uzito wa ghadhabu yake,
aliimimina hasira yake kali;
aliwasha moto huko mjini Siyoni
ambao uliteketeza misingi yake.
12Wafalme duniani hawakuamini
wala wakazi wowote wa ulimwenguni,
kwamba mvamizi au adui
angeweza kuingia malango ya Yerusalemu.
13Hayo yalisababishwa na dhambi za manabii wake,
yalitukia kwa sababu ya uovu wa makuhani wake
ambao walimwaga damu ya waadilifu mjini kwake.
14Walitangatanga barabarani kama vipofu,
walikuwa wamekuwa najisi kwa damu,
hata asiwepo mtu yeyote wa kuwagusa.
15Watu waliwapigia kelele wakisema:
“Tokeni, nendeni zenu enyi mlio najisi!
Tokeni, tokeni, msiguse chochote.”
Hivyo wakawa wakimbizi na kutangatanga;
watu wa mataifa walitamka:
“Hawa hawatakaribishwa kukaa kwetu!”
16Mwenyezi-Mungu mwenyewe aliwatawanya,
wala hatawajali tena.
Makuhani hawatapata tena heshima,
wazee hawatapendelewa tena.
17Tulichoka kukaa macho kungojea msaada;
tulikesha na kungojea kwa hamu
taifa ambalo halikuweza kutuokoa.
18Watu walifuatilia hatua zetu,
tukashindwa kupita katika barabara zetu.
Siku zetu zikawa zimetimia;
mwisho wetu ukawa umefika.
19Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai,
walitukimbiza milimani,
walituvizia huko nyikani.
20Walimnasa yule ambaye maisha yetu yalimtegemea,
yule mfalme aliyewekwa wakfu wa Mwenyezi-Mungu,
yule ambaye tulisema: “Chini ya ulinzi wake
tutaishi miongoni mwa mataifa.”
21Wakazi wa Edomu, mwaweza kushangilia kwa sasa,
mwaweza kwa sasa kufurahi enyi wakazi wa Uzi;
lakini kikombe hiki cha adhabu kitawajia pia,
nanyi pia mtakinywa na kulewa,
hata mtayavua mavazi yenu!
22Adhabu ya uovu wako ewe Siyoni imekamilika;
Mwenyezi-Mungu hatawaacha zaidi uhamishoni.
Lakini nyinyi Waedomu atawaadhibu kwa uovu wenu,
atazifichua dhambi zenu.



Maombolezo4;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: