Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 13 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 2....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Saba na visamaki vichache.” Basi, Yesu akawaamuru watu wakae chini.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi, nao wakawagawia watu. Wote wakala, wakashiba. Kisha wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu saba.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Hao waliokula walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto. Basi, Yesu akawaaga watu, akapanda mashua, akaenda katika eneo la Magadani.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Adhabu ya Yerusalemu
1Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yake,
amewaweka watu wa Siyoni gizani.
Fahari ya Israeli ameibwaga chini.
Siku ya hasira yake
alilitupilia mbali hata hekalu lake.
2Mwenyezi-Mungu ameharibu bila huruma
makazi yote ya wazawa wa Yakobo.
Kwa ghadhabu yake amezibomoa ngome za watu wa Yuda.
Ufalme wao na watawala wake
ameuporomosha chini kwa aibu.
3Nguvu yote ya Israeli ameivunja kwa hasira.
Hakunyosha mkono kuwasaidia
walipokutana na adui;
amewawakia watu wa Yakobo kama moto,
akateketeza kila kitu.
4Amevuta upinde wake kama adui,
na kuuweka mkono wake wa kulia tayari,
amewaua wote tuliowaonea fahari
katika maskani yetu watu wa Siyoni.
Ametumiminia hasira yake kama moto.
5Mwenyezi-Mungu amekuwa kama adui,
ameangamiza watu wa Israeli;
majumba yake yote ameyaharibu,
ngome zake amezibomoa.
Amewazidishia watu wa Yuda
matanga na maombolezo.
6Hekalu lake amelibomoa kama kitalu bustanini,
maskani yake ameiharibu.
Amefutilia mbali sikukuu na Sabato huko Siyoni,
kwa hasira yake kuu amewakataa mfalme na makuhani.
7Mwenyezi-Mungu ameipuuza madhabahu yake
na hekalu lake amelikataa.
Kuta za majumba mjini amewaachia maadui wazibomoe,
wakapiga kelele humo nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu
kama kelele za wakati wa sikukuu.
8Mwenyezi-Mungu alipania kuubomoa ukuta wa mji wa Siyoni;
aliupima na kuhakikisha kila kitu kimeharibiwa;
minara na kuta za nje ya mji akazifanya ukiwa,
zote kwa pamoja zikaangamia.
9Malango yake yameanguka chini,
makomeo yake ameyaharibu na kuyavunjavunja.
Mfalme na wakuu wake wako uhamishoni kati ya mataifa.
Mwongozo wa sheria umetoweka kabisa,
manabii wake hawapati tena maono
kutoka kwake Mwenyezi-Mungu.
10Wazee wa Siyoni wameketi chini kimya,
wamejitia mavumbi vichwani
na kuvaa mavazi ya gunia.
Wasichana wa Yerusalemu wameinamisha vichwa.
11Macho yangu yamevimba kwa kulia,
roho yangu imechafuka.
Moyo wangu una huzuni nyingi
kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu
kwa sababu watoto wachanga wanazirai katika barabara za mji.
12Wanawalilia mama zao:
“Wapi chakula, wapi kinywaji?”
Huku wanazirai kama majeruhi
katika barabara za mjini,
na kukata roho mikononi mwa mama zao.
13Nikuambie nini ee Yerusalemu?
Nikulinganishe na nini?
Nikufananishe na kitu gani
ili niweze kukufariji,
ee Siyoni uliye mzuri?
Maafa yako ni mengi kama bahari.
Ni nani awezaye kukuponya?
14Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu,
hawakufichua wazi uovu wako
ili wapate kukurekebisha,
bali walikuonea kauli ya uongo na ya kupotosha.
15Wapita njia wote wanakudhihaki;
wanakuzomea, ee Yerusalemu,
wakitikisa vichwa vyao kwa dharau na kusema:
“Je, huu ndio ule mji uliofikia upeo wa uzuri,
mji uliokuwa furaha ya dunia nzima?”
16Maadui zako wote wanakuzomea,
wanakufyonya na kukusagia meno,
huku wakisema, “Tumemwangamiza!
Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu
sasa imefika na tumeiona!”
17Mwenyezi-Mungu amefanya yale aliyokusudia,
ametekeleza yale aliyotishia;
kama alivyopanga tangu kale
ameangamiza bila huruma yoyote;
amewafanya maadui wafurahie adhabu yako,
amewakuza mashujaa wa maadui zako.
18Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu!
Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku!
Lia na kuomboleza bila kupumzika!
19Usiku kucha uamkeamke ukalie.
Mfungulie Mwenyezi-Mungu yaliyo moyoni mwako.
Mwinulie mikono yako kuwaombea watoto wako,
watoto wanaozirai kwa njaa popote barabarani.
20Tazama ee Mwenyezi-Mungu uone!
Je, kuna yeyote uliyemtendea ulivyotutendea sisi?
Je, hata kina mama wawale watoto wao?
Je, nao makuhani wauawe hekaluni mwako?
21Maiti za vijana na wazee zimelala vumbini barabarani,
wasichana na wavulana wangu wameuawa kwa upanga;
umewaua bila huruma siku ya hasira yako.
22Umewaalika kama kwenye sikukuu
maadui zangu walionitisha kila upande.
Katika siku ya hasira yako ee Mwenyezi-Mungu,
hakuna aliyetoroka au kunusurika.
Wale niliowazaa na kuwalea
adui zangu wamewaangamiza.


Maombolezo2;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: