Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 25 January 2020

Kisa/Hadithi Na Mswahili-Yusuph Mbuguni...

Imeandikwa na Yusuph Mbuguni




"Nakumbuka zamani za udogo wangu,zamani za utoto huko...Mtu mmoja alimpatia babu Yangu Box la nguo chakavu za mitumba kama zawadi,Na katika zile nguo kuukuu nyingi zilikuwa ndogo ndogo,Babu yangu alichukua vipande vya nguo akaviunga akanitengenezea koti kwa kuwa sikuwa na koti kipindi cha baridi,hivyo ni koti ambalo nilijivunia sana,Babu aliniambia Hadithi Ya Yusuph kwenye biblia na koti lake ambalo alikuwa akilivaa,hivyo aliniambia ni kwa namna gani anaamini jinsi koti hilo litakavyoweza kuniletea bahati nzuri katika maisha na kunifanya niwe na furaha,Nikienda kucheza na watoto wenzangu walikuwa wakinicheka nakuona ni kwa namna gani koti langu ni kituko,lakini nilikuwa najaribu kuwaelezea uzuri wa koti langu na kwa namna gani koti langu ni la thamani sana kuliko nguo zao wote japo walikuwa hawanielewi kabisa,japo tulikuwa hatuna kipato lakini nilikuwa najiona tajiri sana na wa maana sana kuliko wote kutokana na koti langu.
wise man yusuph mbuguni

......FUNZO usiangalie wengine wanazungumza nini kuhusu hali yako na Maisha yako wewe ndio unaweza itengeneza furaha yako mwenyewe hata kipindi cha huzuni,Unaweza kujitengenezea hisia za utajiri ukiwa masikini chagua kuwa na furaha na sio huzuni wewe ni Nahodha wa nafsi yako vile unavyotaka.

wise man yusuph mbuguni


No comments: