Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 11 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 9....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena. Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mmegundua kwamba Bwana ni mwema.” Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule na la thamani kubwa.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea tambiko za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mtoto amezaliwa kwetu
1 9:1 Taz Mat 4:15 
Lakini nchi ile iliyokuwa imekumbwa na huzuni haitabaki daima katika giza hilo kuu. Hapo awali Mungu alizifedhehesha nchi za Zebuluni na Naftali, lakini siku za usoni ataifanikisha sehemu hii ya baharini na nchi iliyo ngambo ya Yordani na hata Galilaya wanamoishi watu wa mataifa.
2 9:2 Taz Mat 4:16; Luka 1:79 Watu waliotembea gizani
wameona mwanga mkubwa.
Watu walioishi katika nchi ya giza kuu,
sasa mwanga umewaangazia.
3Wewe, ee Mungu, umelikuza taifa,
umeiongeza furaha yake.
Watu wanafurahi mbele yako,
wana furaha kama wakati wa mavuno,
kama wafurahivyo wanaogawana nyara.
4Maana nira nzito walizobeba,
nira walizokuwa wamefungwa,
na fimbo ya wanyapara wao,
umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.
5Viatu vyote vya washambulizi vitani
na mavazi yote yenye madoa ya damu
yatateketezwa kama kuni za kuwasha moto.
6Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu,
tumepewa mtoto wa kiume.
Naye atapewa mamlaka ya kutawala.
Ataitwa: “Mshauri wa Ajabu”.
“Mungu Mwenye Nguvu”,
“Baba wa Milele”,
“Mfalme wa Amani”.
7 9:7 Taz Luka 1:32-33 Utawala wake utastawi daima,
amani ya ufalme wake haitakoma.
Atachukua wadhifa wa mfalme Daudi
na kutawala juu ya ufalme wake;
ataustawisha na kuuimarisha,
kwa haki na uadilifu,
tangu sasa na hata milele.
Hayo atayafanya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

Adhabu ya Waisraeli
8Mwenyezi-Mungu ametoa tamko dhidi ya Yakobo
nalo litampata Israeli.
9Watu wote watatambua,
ukoo wote wa Efraimu
na wakazi wa Samaria.
Kwa kiburi na majivuno wanasema:
10“Kuta za matofali zimeanguka
lakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa!
Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwa
lakini mahali pake tutajenga za mierezi.”
11Basi, Mwenyezi-Mungu atawaletea wapinzani
na kuwachochea maadui zao.
12Waaramu upande wa mashariki,
Wafilisti upande wa magharibi,
wamepanua vinywa vyao kuimeza Israeli.
Hata hivyo, hasira yake haijatulia,
bado ameunyosha mkono wake.
13Ingawa aliwaadhibu watu,
hawakumrudia Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
14Basi kwa muda wa siku moja tu,
Mwenyezi-Mungu atakata katika Israeli vichwa na mikia,
tawi la mtende na nyasi:
15Vichwa ndio wazee na waheshimiwa,
mikia ndio manabii wafundishao uongo.
16Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha,
na hao wanaoongozwa nao wamepotoka.9:16 wamepotoka: Au wamemezwa.
17Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu hawahurumii9:17 hawahurumii: Kufuatana na hati moja ya kale. Kiebrania: Hapendezwi. vijana wao,
hana huruma juu ya yatima na wajane wao;
kwani hakuna hata mmoja amchaye Mungu,
kila mtu husema uongo.
Hata hivyo, hasira yake haijatulia,
bado ameunyosha mkono wake.
18Uovu huwaka kama moto
uteketezao mbigili na miiba;
huwaka kama moto msituni,
na kutoa moshi mzito upandao angani juu.
19Kwa ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi
nchi imechomwa moto,
na watu ni kama kuni za kuuwasha.
Hakuna mtu anayemhurumia ndugu yake;
20wananyanganya upande mmoja na hawatosheki;
wanakula upande mwingine lakini hawashibi.
Kila mmoja anamshambulia mwenzake.9:20 anamshambulia mwenzake: Kiebrania: Anakula nyama ya mwenzake.
21Manase dhidi ya Efraimu,
Efraimu dhidi ya Manase
na wote wawili dhidi ya Yuda.
Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,
bado ameunyosha mkono wake.

Isaya9;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: