Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 2 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 2....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Hivyo, ee mfalme Dario, utoe amri hiyo na kuitia hati sahihi yako ili isibadilishwe. Nayo itakuwa sheria ya Wamedi na Wapersi, sheria ambayo haibatilishwi.” Hivyo, mfalme Dario akaitia sahihi hati ya sheria hiyo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Danieli alipojua kuwa ile hati imetiwa sahihi, alirudi nyumbani kwake ghorofani katika chumba chake kilichokuwa na madirisha yaliyofunguka kuelekea Yerusalemu. Humo, Danieli, kama ilivyokuwa kawaida yake, alipiga magoti mara tatu kila siku akamwomba na kumshukuru Mungu wake.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Watu wale waliofanya mpango dhidi ya Danieli waliingia ndani, wakamkuta Danieli akiomba dua na kumsihi Mungu wake.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Amani ya kudumu
(Mika 4:1-3)
1Neno alilopewa Isaya, mwana wa Amozi, kuhusu Yuda na Yerusalemu.
2Siku zijazo mlima wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu
utaimarishwa kupita milima yote,
utainuliwa juu ya vilima vyote.
Mataifa yote yatamiminika huko,
3watu wengi wataujia na kusema,
“Njoni tupande mlima wa Mwenyezi-Mungu,
twende nyumbani kwa Mungu wa Yakobo,
apate kutufundisha njia zake,
nasi tuishi kadiri ya mwongozo wake.
Maana sheria itakuja kutoka Siyoni;
neno la Mwenyezi-Mungu kutoka Yerusalemu.”
4 2:4 Taz Yoe 3:10 Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa
atakata mashauri ya watu wengi.
Watu watafua panga za vita kuwa majembe
na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.
Taifa halitapigana na taifa lingine
wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
5Sasa, enyi wazawa wa Yakobo, njoni,
tutembee katika mwanga wa Mwenyezi-Mungu.

Kiburi kitaondolewa
6Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazawa wa Yakobo.
Maana kweli wachawi wa mashariki wamejaa kati yao,
wapo na wapiga ramli kama kwa Wafilisti.
Wanashirikiana na watu wageni.
7Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,
hazina yao ni kubwa kupindukia.
Nchi yao imejaa farasi,
magari yao ya kukokotwa hayana idadi.
8Nchi yao imejaa vinyago vya miungu,
huabudu kazi ya mikono yao,
vitu walivyotengeneza wao wenyewe.
9Kwa hiyo, kila mtu ataaibishwa na kufedheheshwa.
Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!
10 2:10 Taz Ufu 6:15; 2Thes 1:9 Ingieni katika mwamba,
mkajifiche mavumbini,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake.
11Siku yaja ambapo kiburi cha watu kitashushwa,
majivuno ya kila mtu yatavunjwa;
na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
12Naam, yaja siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi
dhidi ya wenye kiburi na majivuno,
dhidi ya wote wanaojikweza;
13dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni,
ambayo ni mirefu na mizuri,
dhidi ya mialoni yote nchini Bashani;
14dhidi ya milima yote mirefu,
dhidi ya vilima vyote vya juu;
15dhidi ya minara yote mirefu,
dhidi ya kuta zote za ngome;
16dhidi ya meli zote za Tarshishi,
na dhidi ya meli zote nzuri.
17Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,
majivuno ya kila mtu yatavunjwa.
Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
18Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.
19Ingieni katika mapango miambani,
katika mashimo ardhini,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake,
atakapokuja kuitia hofu dunia.
20Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo
vinyago vyao vya fedha na dhahabu
walivyojitengenezea ili kuviabudu.
21Nao wataingia katika mapango miambani
na kwenye nyufa za miamba,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake,
atakapokuja kuitia hofu dunia.
22Usimwamini binadamu,
uhai wake haudumu kama pumzi.
Yeye anafaa kitu gani?

Isaya2;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: