Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 17 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 13....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Enyi watumishi wa nyumbani, watiini wakuu wenu kwa heshima yote, wawe wema na wapole au wenye kuchukiza. Maana kama mnavumilia maumivu ya mateso msiyostahili kwa sababu mwajua kwamba Mungu anataka hivyo, basi Mungu atawafadhili. Maana, mtapata tuzo gani mkivumilia mapigo mnayostahili kwa sababu ya makosa yenu? Lakini kama mnavumilia mateso hata ingawa mmetenda mema, Mungu atawapeni baraka kwa ajili hiyo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hayo ndiyo mliyoitiwa; maana Kristo mwenyewe aliteseka kwa ajili yenu, akawaachieni mfano, ili mfuate mwenendo wake. Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake. Alipotukanwa yeye hakujibu kwa tukano; alipoteseka yeye hakutoa vitisho, bali aliyaweka matumaini yake kwa Mungu, hakimu mwenye haki.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake juu ya msalaba, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake, nyinyi mmeponywa. Nyinyi mlikuwa kama kondoo waliokuwa wamepotea; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu ataiadhibu Babuloni
1 13:1--14:23 Taz Isa 47:1-15; Yer 50:1--51:64 
Kauli ya Mungu dhidi ya Babuloni ambayo Isaya, mwana wa Amozi, alipewa katika maono:
2Mungu asema:
“Twekeni bendera juu ya mlima usio na miti.
Wapaazieni sauti askari
wapungieni watu mkono
waingie malango ya mji wa wakuu.
3Mimi nimewaamuru wateule wangu,
nimewaita mashujaa wangu,
hao wenye kunitukuza wakishangilia,
waje kutekeleza lengo la hasira yangu.”
4Sikilizeni kelele milimani
kama za kundi kubwa la watu!
Sikilizeni kelele za falme,
na mataifa yanayokusanyika!
Mwenyezi-Mungu wa majeshi
analikagua jeshi linalokwenda vitani.
5Wanakuja kutoka nchi za mbali,
wanatoka hata miisho ya dunia:
Mwenyezi-Mungu na silaha za hasira yake
anakuja kuiangamiza dunia.
6 13:6 Taz Yoe 1:15 Lieni maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia;
inakuja kama maafa kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.
7Kwa hiyo mikono ya kila mtu italegea,
kila mtu atakufa moyo.
8Watu watafadhaika,
watashikwa na hofu na maumivu,
watakuwa na uchungu kama mama anayejifungua.
Watatazamana kwa mashaka,
nyuso zao zitawaiva kwa haya.
9Siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja,
siku kali, ya ghadhabu na hasira kali.
Itaifanya nchi kuwa uharibifu,
itawaangamiza wenye dhambi wake.
10 13:10 Taz Eze 32:7; Mat 24:29; Marko 13:24-25; Luka 21:25; Ufu 6:12-13 Nyota na vilimia vyake angani hazitaangaza;
jua linapochomoza litakuwa giza,
na mwezi hautatoa mwanga wake.
11Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nitauadhibu ulimwengu kwa uovu wake,
waovu kwa sababu ya makosa yao.
Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno,
na kuporomosha ubaradhuli wa watu katili.
12Nitawafanya watu kuwa wachache kuliko dhahabu safi;
binadamu watakuwa wachache kuliko dhahabu ya Ofiri.
13Nitazitetemesha mbingu
nayo nchi itatikisika katika misingi yake
kwa sababu ya ghadhabu yangu Mwenyezi-Mungu
siku ile ya hasira yangu kali.
14“Kama swala anayewindwa,
kama kondoo wasio na mchungaji,
kila mmoja atajiunga na watu wake
kila mtu atakimbilia nchini mwake.
15Yeyote atakayeonekana atatumbuliwa,
atakayekamatwa atauawa kwa upanga.
16Watoto wao wachanga watapondwapondwa mbele yao,
watanyanganywa nyumba zao,
na wake zao watanajisiwa.
17“Ninawachochea Wamedi dhidi yao;
watu ambao hawajali fedha
wala hawavutiwi na dhahabu.
18Mishale yao itawaua vijana,
hawatakuwa na huruma kwa watoto,
wala kuwahurumia watoto wachanga.
19 13:19 Taz Mwa 19:24 Babuloni johari ya falme zote
na umaarufu wa kiburi cha Wakaldayo
utakuwa kama Sodoma na Gomora,
wakati Mungu alipoiangamiza.
20Kamwe hautakaliwa tena na watu,
watu hawataishi humo katika vizazi vyote.
Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake humo,
wala mchungaji atakayechunga wanyama wake humo.
21 13:21 Taz Isa 34:14; Sef 2:14; Ufu 18:2 Badala yake watakuwamo wanyama wakali wa porini,
bundi watajaa katika nyumba zake.
Mbuni13:21 Mbuni: Au pepo wabaya. wataishi humo,
na majini13:21 majini: Au Ibilisi; namna ya pepo wa hadithi za Babuloni. yatachezea humo.
22Mbwamwitu watalia ndani ya ngome zake,
mbweha wataonekana ndani ya nyumba zao za anasa.
Wakati wa Babuloni umekaribia,
wala siku zake hazitaongezwa.”

Isaya13;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: