Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 18 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 14....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika mahali pamoja. Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikaijaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani. Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Kurudi kutoka uhamishoni
1Mwenyezi-Mungu atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawateua tena Waisraeli. Atawarudisha katika nchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo. 2Watu wa mataifa watawasaidia Waisraeli kurudi katika nchi waliyopewa na Mwenyezi-Mungu. Na hapo watawatumikia Waisraeli kama watumwa. Wale waliowateka sasa watatekwa na Waisraeli, na watawatawala wale waliowadhulumu.
Mfalme wa Babuloni miongoni mwa wafu
3Ewe Israeli, wakati Mwenyezi-Mungu atakapokufariji baada ya mateso, misukosuko na utumwa uliofanyiwa, 4utaimba utenzi huu wa kumdhihaki mfalme wa Babuloni:
“Jinsi gani mdhalimu alivyokomeshwa!
Ujeuri wake umekomeshwa!
5Mwenyezi-Mungu amelivunja gongo la waovu,
ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,
6ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma,
na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.
7Sasa dunia yote ina utulivu na amani,
kila mtu anaimba kwa furaha.
8Misonobari inafurahia kuanguka kwako,
nayo mierezi ya Lebanoni pamoja yasema:
‘Kwa vile sasa umeangushwa,
hakuna mkata miti atakayekuja dhidi yetu!’
9“Kuzimu nako kumechangamka,
ili kukulaki wakati utakapokuja.
Kunaiamsha mizimu ije kukusalimu
na wote waliokuwa wakuu wa dunia;
huwaamsha kutoka viti vyao vya enzi
wote waliokuwa wafalme wa mataifa.
10Wote kwa pamoja watakuambia:
‘Nawe pia umedhoofika kama sisi!
Umekuwa kama sisi wenyewe!
11Fahari yako imeteremshwa kuzimu
pamoja na muziki wa vinubi vyako.
Chini mabuu ndio kitanda chako,
na wadudu ndio blanketi lako!’
12 “Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni,
wewe uliyekuwa nyota angavu ya alfajiri.
Jinsi gani ulivyoangushwa chini,
wewe uliyeyashinda mataifa!
13Wewe ulijisemea moyoni mwako:
‘Nitapanda mpaka mbinguni;
nitaweka kiti changu juu ya nyota za Mungu,
nitaketi juu ya mlima wakutanapo miungu,
huko mbali pande za kaskazini.
14Nitapanda vilele vya mawingu
nitajifanya kuwa sawa na Mungu Mkuu.’
15Lakini umeporomoshwa hadi kuzimu;
umeshushwa chini kabisa shimoni.
16“Watakaokuona watakukodolea macho,
watakushangaa wakisema:
‘Je, huyu ndiye aliyetetemesha dunia
na kuzitikisa falme,
17aliyegeuza dunia kuwa kama jangwa,
akaangamiza miji yake,
na kuwanyima wafungwa wake kurudi kwao?’
18Wafalme wote wa mataifa wamezikwa kwa heshima
kila mmoja ndani ya kaburi lake.
19Lakini wewe umetupwa nje ya kaburi lako;
kama mtoto wa kuchukiza aliyezaliwa mfu
maiti yako imekanyagwakanyagwa,
umerundikiwa maiti za waliouawa kwa upanga,
waliotupwa mashimoni penye mawe.
20Lakini wewe hutaunganishwa nao katika mazishi,
maana uliiharibu nchi yako,
wewe uliwaua watu wako.
Wazawa wa waovu na wasahaulike kabisa!
21Kaeni tayari kuwachinja watoto wake
kwa sababu ya makosa ya baba zao,
wasije wakaamka na kuimiliki nchi,
na kuijaza dunia yote miji yao.”
Mungu ataangamiza Babuloni
22Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Nitaushambulia mji wa Babuloni na kuuangamiza kabisa. Nitaharibu kila kitu, mji wote, watoto na yeyote aliyebaki hai. Mimi Mwenyezi-Mungu nimenena. 23Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa madimbwi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimenena.”
Mwisho wa udhalimu wote
24Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameapa:
“Kama nilivyopanga,
ndivyo itakavyokuwa;
kama nilivyokusudia,
ndivyo itakavyokamilika.
25Nitauvunja uwezo wa Waashuru nchini mwangu;
nitawakanyagakanyaga katika milima yangu.
Nitawaondolea watu wangu nira ya dhuluma yao,
na mzigo wa mateso yao.”
26Huu ndio uamuzi wake Mwenyezi-Mungu
kuhusu dunia yote;
hii ndiyo adhabu atakayotoa
juu ya mataifa yote.
27Kama Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameamua,
nani atakayeweza kubatilisha uamuzi wake?
Kama amepania kutoa adhabu,
ni nani atakayempinga?
Mungu atawaangamiza Wafilisti
28Mwaka alipofariki mfalme Ahazi, Mungu alitoa kauli hii:
29“Msishangilie enyi Wafilisti wote,
kwamba Ashuru, fimbo iliyowapiga, imevunjika;
maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu,
na nyoka mwenye sumu atazaa joka lirukalo.
30Wazaliwa wa kwanza wa maskini watashiba,
na fukara watakaa kwa usalama.
Lakini chipukizi wenu nitawaua kwa njaa;
na yeyote wenu atakayebaki nitamuua.
31Piga yowe ewe lango; lia ewe mji;
yeyuka kwa hofu ewe nchi yote ya Filistia.
Maana moshi wa askari waja kutoka kaskazini,
wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.”
32Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo?
Wataambiwa: Mwenyezi-Mungu ameijenga imara Siyoni,
na maskini wa watu wake watakimbilia usalama huko.

Isaya14;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: