Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 30 January 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 50...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Tajiri mmoja alikuwa na karani wake. Huyu karani alichongewa kwamba alitumia ovyo mali ya tajiri wake. Yule tajiri akamwita, akamwambia: ‘Ni mambo gani haya ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya mapato na matumizi ya mali yangu, kwa maana huwezi kuwa karani tena.’

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....



Yule karani akafikiri: ‘Bwana wangu amenifukuza kazi ya ukarani; nitafanya nini? Kwenda kulima siwezi; kwenda kuombaomba kama maskini ni aibu. Naam, najua la kufanya, ili nitakapofukuzwa kazi, watu waweze kunikaribisha nyumbani kwao.’

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....


Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Basi, akawaita wadeni wa bwana wake, mmojammoja, akamwambia yule wa kwanza: ‘Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?’ Yeye akamjibu: ‘Mapipa 100 ya mafuta ya zeituni.’ Yule karani akamwambia: ‘Chukua hati yako ya deni, keti haraka, andika hamsini.’ Kisha akamwuliza mdeni mwingine: ‘Wewe unadaiwa kiasi gani?’ Yeye akamjibu: ‘Magunia 100 ya ngano.’ Yule karani akamwambia: ‘Chukua hati yako ya deni, andika themanini.’ “Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga.”

Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...

Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Ibada ya kweli
(Zaburi ya Asafu)
1Mungu wa nguvu50:1 Mungu wa nguvu: Hivyo, kadiri ya makala ya Kiebrania; au Mungu Mkuu. Mwenyezi-Mungu, amenena,
amewaita wakazi wa dunia,
tokea mawio ya jua hadi machweo yake.
2Kutoka Siyoni, mji mzuri mno,
Mungu anajitokeza, akiangaza.
3Mungu wetu anakuja, na sio kimyakimya:
Moto uunguzao wamtangulia,
na dhoruba kali yamzunguka.
4Kutoka juu anaziita mbingu na dunia;
zishuhudie akiwahukumu watu wake:
5“Nikusanyieni waaminifu wangu,
waliofanya agano nami kwa tambiko!”
6Mbingu zatangaza uadilifu wa Mungu;
kwamba Mungu mwenyewe ni hakimu.
7“Sikilizeni watu wangu, ninachosema!
Israeli, natoa ushahidi dhidi yako.
Mimi ni Mungu! Mimi ni Mungu wako!
8Sikukaripii kwa sababu ya tambiko zako;
hujaacha kunitolea tambiko za kuteketeza.
9Kwa kweli sina haja na fahali wa zizi lako,
wala beberu wa mifugo yako;
10maana wanyama wote porini ni mali yangu,
na maelfu ya wanyama milimani ni wangu.
11Ndege wote wa mwitu ni mali yangu,
na viumbe vyote hai mashambani ni vyangu.
12Kama ningeona njaa singekuambia wewe,
maana ulimwengu na vyote vilivyomo ni vyangu.
13Je, wadhani nala nyama ya fahali,
au Kunywa damu ya mbuzi?
14Shukrani iwe ndio tambiko yako kwa Mungu
mtimizie Mungu Aliye Juu ahadi zako.
15Uniite wakati wa taabu,
nami nitakuokoa, nawe utaniheshimu.”
16Lakini Mungu amwambia mtu mwovu:
“Ya nini kuzitajataja tu sheria zangu?
Kwa nini unasemasema juu ya agano langu?
17Wewe wachukia kuwa na nidhamu,
na maneno yangu hupendi kuyafuata.
18Ukimwona mwizi unaandamana naye,
na wazinzi unashirikiana nao.
19Uko tayari daima kunena mabaya;
kazi ya ulimi wako ni kutunga uongo.
20Wakaa kitako kumsengenya binadamu mwenzako,
naam, kumchongea ndugu yako mwenyewe.
21Umefanya hayo yote nami nimenyamaa.
Je, wadhani kweli mimi ni kama wewe?
Lakini sasa ninakukaripia,
ninakugombeza waziwazi.
22“Fikirini vizuri jambo hili, enyi msionijali,
la sivyo nitawaangamizeni,
wala hapatakuwa na wa kuwaokoeni.
23Anayenipa shukrani kama tambiko yake,
huyo ndiye anayeniheshimu;
yeyote anayedumu katika njia yangu,
huyo ndiye nitakayemwokoa.”



Zaburi50;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: