Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 16 January 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 40...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!
Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kifo chake. Hakuja kwa maji tu, bali kwa maji na kwa damu. Naye Roho anashuhudia kwamba ni kweli, kwani Roho ni ukweli.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....
Basi, wako mashahidi watatu: Roho, maji na damu; na ushahidi wa hawa watatu waafikiana. Ikiwa twaukubali ushahidi wa binadamu, ushahidi wa Mungu una uzito zaidi; na huu ndio ushahidi alioutoa Mungu mwenyewe juu ya Mwanae.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetuBaba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza weweRoho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Anayemwamini Mwana wa Mungu anao ushahidi huo ndani yake; lakini asiyemwamini Mungu, anamfanya yeye kuwa mwongo, maana hakuamini ushahidi alioutoa Mungu juu ya Mwanae. Na, ushahidi wenyewe ndio huu: Mungu alitupatia uhai wa milele, na uhai huo uko kwa Bwana. Yeyote aliye na Mwana wa Mungu anao uhai huo; asiye na Mwana wa Mungu, hana uhai.

Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao

Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mikononi mwako,Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele 
Amina!!
Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake
Nawapenda.

Utenzi wa sifa
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Nilimngojea Mwenyezi-Mungu kwa uvumilivu,
akanielekea na kukisikia kilio changu.
2Aliniondoa katika shimo la hatari,
alinitoa katika matope ya dimbwi,
akanisimamisha salama juu ya mwamba,
na kuziimarisha hatua zangu.
3Alinifundisha wimbo mpya,
wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.
Wengi wataona na kuogopa,
na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.
4Heri mtu anayemtumainia Mwenyezi-Mungu;
mtu asiyejiunga na watu wenye majivuno,
watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.
5Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, umetufanyia mengi ya ajabu,
na mipango yako juu yetu haihesabiki;
hakuna yeyote aliye kama wewe.
Kama ningeweza kusimulia hayo yote,
idadi yake ingenishinda.
6 Taz Ebr 10:5-7 Wewe hutaki tambiko wala sadaka,
tambiko za kuteketeza wala za kuondoa dhambi;
lakini umenipa masikio nikusikie.
7Ndipo niliposema: “Niko tayari;
ninayotakiwa kufanya yameandikwa katika kitabu cha sheria;
8kutimiza matakwa yako, ee Mungu wangu ni furaha yangu,
sheria yako naishika kwa moyo wangu wote!”
9Nimesimulia habari njema za ukombozi,
mbele ya kusanyiko kubwa la watu.
Kama ujuavyo ee Mwenyezi-Mungu,
mimi sikujizuia kuitangaza.
10Sikuuficha moyoni mwangu ukombozi ulionijalia,
nimetangaza daima kuwa wewe ni mwokozi mwaminifu;
sikulificha kusanyiko kubwa la watu
fadhili zako na uaminifu wako.
11Ee Mwenyezi-Mungu, usininyime huruma yako!
Fadhili zako na uaminifu wako vinihifadhi daima.
Sala ya kuomba msaada
(Zaburi 70)
12Maafa yasiyohesabika yanizunguka,
maovu yangu yanikaba hata siwezi kuona;
ni mengi kuliko nywele kichwani mwangu,
nami nimevunjika moyo.
13Upende ee Mwenyezi-Mungu kuniokoa;
ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.
14Wanaonuia kuniangamiza,
na waaibike na kufedheheka!
Hao wanaotamani niumie,
na warudi nyuma na kuaibika!
15Hao wanaonisimanga,
na wapumbazike kwa kushindwa kwao!
16Lakini wote wale wanaokutafuta
wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.
Wapendao wokovu wako,
waseme daima: “Mwenyezi-Mungu ni Mkuu!”
17Mimi ni maskini na fukara, ee Bwana;
lakini ee Bwana wewe wanikumbuka.
Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;
uje, ee Mungu wangu, usikawie!


Zaburi40;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: