Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 3 January 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 31...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, Yona, akiwa tumboni mwa samaki huyo, akawa akimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wake, akisema: “Kwa sababu ya taabu yangu, nilikuomba, ee Mwenyezi-Mungu, nawe ukanisikiliza; toka chini kuzimu, nilikulilia, nawe ukasikiliza kilio changu.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari, gharika ikanizunguka, mawimbi na gharika vikapita juu yangu. Nilidhani kwamba nimetengwa nisiwe mbele yako; nisiweze kuliona tena hekalu lako takatifu. Maji yalinizunguka na kunisonga; kilindi kilinifikia kila upande, majani ya baharini yakanifunika kichwa. Niliteremka hadi kwenye misingi ya milima, katika nchi ambayo milango yake imefungwa milele. Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, umenipandisha hai kutoka humo shimoni.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu,Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na amasikio ya kusikia sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako,Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu
Mungu wetu ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Roho yangu ilipoanza kunitoka, nilikukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu, sala yangu ikakufikia, katika hekalu lako takatifu. Watu wanaoabudu sanamu za miungu batili, huutupilia mbali uaminifu wao kwako. Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea sadaka, na kutimiza nadhiri zangu. Mwenyezi-Mungu, ndiye aokoaye.” Basi, Mwenyezi-Mungu akamwamuru yule samaki, naye akamtapika Yona kwenye nchi kavu.
Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao,Yahweh tunayaweka haya yote mikononi mwako tukiamani Mungu wetu utatenda sawasawa na mapenzi yako
 
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele Amina...!!
Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu
kwakuwanami/kunisoma Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye,Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo wa Mungu Baba ukae nanyi daima....
Nawapenda.

Sala katika shida kubwa
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Kwako, ee Mwenyezi-Mungu, nakimbilia usalama,
usiniache niaibike kamwe;
kwa uadilifu wako uniokoe.
2Unitegee sikio, uniokoe haraka!
Uwe kwangu mwamba wa usalama,
ngome imara ya kuniokoa.
3Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu;
kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.
4Unitoe katika mtego walionitegea mafichoni;
maana wewe ni kimbilio la usalama wangu.
5 Taz Luka 23:46 Mikononi mwako naiweka roho yangu;
umenikomboa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu mwaminifu.
6Wawachukia wanaoabudu sanamu batili;
lakini mimi nakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu.
7Nitashangilia na kufurahia fadhili zako,
maana wewe waiona dhiki yangu,
wajua na taabu ya nafsi yangu.
8Wewe hukuniacha nitiwe mikononi mwa maadui zangu;
umenisimamisha mahali pa usalama.
9Unionee huruma, ee Mwenyezi-Mungu, niko taabuni;
macho yangu yamechoka kwa huzuni,
nimeishiwa nguvu mwilini na rohoni.
10Maisha yangu yamekwisha kwa majonzi;
naam, miaka yangu kwa kulalamika.
Nguvu zangu zimeniishia kwa kutaabika;
hata mifupa yangu imekauka.
11Nimekuwa dharau kwa maadui zangu wote;
kioja kwa majirani zangu.
Rafiki zangu waniona kuwa kitisho;
wanionapo njiani hunikimbia.
12Nimesahaulika kama mtu aliyekufa;
nimekuwa kama chungu kilichovunjikavunjika.
13Nasikia watu wakinongonezana,
vitisho kila upande;
wanakula njama dhidi yangu,
wanafanya mipango ya kuniua.
14Lakini mimi nakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu.
Nasema: “Wewe ni Mungu wangu!”
15Maisha yangu yamo mikononi mwako;
uniokoe na maadui zangu,
niokoe na hao wanaonidhulumu.
16Uniangalie kwa wema mimi mtumishi wako;
uniokoe kwa fadhili zako.
17Usiniache niaibike ee Mwenyezi-Mungu,
maana mimi ninakuomba;
lakini waache waovu waaibike,
waache wapotelee kwa mshangao huko kuzimu.
18Izibe midomo ya hao watu waongo,
watu walio na kiburi na majivuno,
ambao huwadharau watu waadilifu.
19Jinsi gani ulivyo mwingi wema wako,
uliowawekea wale wanaokucha!
Wanaokimbilia usalama kwako
wawapa mema binadamu wote wakiona.
20Wawaficha mahali salama hapo ulipo,
mbali na mipango mibaya ya watu;
wawaweka salama katika ulinzi wako,
mbali na ubishi wa maadui zao.
21Asifiwe Mwenyezi-Mungu,
maana amenionesha fadhili zake kwa namna ya ajabu,
nilipozingirwa kama mji unaoshambuliwa.
22Nami niliogopa na kudhani kwamba ulikuwa umenitupa;
kumbe, ulisikia kilio changu nilipokuita unisaidie.
23Mpendeni Mwenyezi-Mungu, enyi watakatifu wake wote.
Mwenyezi-Mungu huwalinda watu waaminifu;
lakini huwaadhibu kabisa wenye kiburi wanavyostahili.
24Muwe hodari na kupiga moyo konde,
enyi nyote mnaomtumainia Mwenyezi-Mungu.


Zaburi31;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: