Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 26 December 2012

Mfululizo wa Mahojiano ya Wadau wa Filamu na Muziki;147 Critics:John F Kitime (2)!!!


 Muendelezo wa 147 Critics ambapo leo tunamsikiliza mdau muhimu na makini kwenye Muziki wa Dansi na kwa 
upande mwingine kwenye Filamu akielezea kuhusiana na marekebisho ya sheria ya ushuru wa bidhaa Sura 147 
yanayogusa Muziki na Filamu.

Tusikilize 147 Critics:John F Kitime (2)  akiwa ni mtu wa pili kuelezea maoni yake.


Msikilize vyema John F Kitime uweze kufahamu vyema yale anayoyajuwa na anayodhani ni muhimu kuwa sawa katika mabadiliko ya sheria hii!






Mahojiano haya na Ndg John F Kitime yametokana na
-C. Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147
Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato itaanza
kurasimisha biashara ya bidhaa za muziki na filamu kwa
nia ya kuhakikisha kwamba uasili wake unatambulika na
hivyo kuzuia vitendo vya kudurufu kazi za sanaa (piracy of
artists work) hali ambayo inadumaza ukuaji wa sanaa na
vipaji hapa nchini. Aidha, Mamlaka ya Mapato itaweka
stampu kwenye bidhaa hizo ili uuzaji wa kazi hizo uwe
rasmi na kuwawezesha wasanii kupata kipato stahili
kutokana na kazi zao. Vilevile hatua hii itaiingizia serikali
mapato.

kwa Maelezo zaidi ingia;TheImageProfession 

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.

No comments: