Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 26 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora5...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mimi Paulo, Silwano na Timotheo, kwa jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambayo ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Ndugu, tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana. Ndio maana sisi tunajivunia nyinyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake, nyinyi mtastahili ufalme wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Bwana arusi
1Naingia bustanini mwangu,
dada yangu, bi arusi.
Nakusanya manemane na viungo,
nala sega langu la asali,
nanywa divai yangu na maziwa yangu.
Bibi arusi
Kuleni enyi marafiki, kunyweni;
kunyweni sana wapendwa wangu.
Shairi la nne
Bibi arusi
2Nililala, lakini moyo wangu haukulala.
Sauti ya mpenzi wangu anabisha hodi.
Bwana arusi
“Nifungulie, dada yangu mpenzi wangu, bibiarusi wangu,
hua wangu, usiye na kasoro.
Kichwa changu kimelowa umande
na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
Bibi arusi
3Nimekwisha yavua mavazi yangu,
nitayavaaje tena?
Nimekwisha nawa miguu yangu,
niichafueje tena?
4Hapo mpenzi wangu akaugusa mlango,
moyo wangu ukajaa furaha.
5Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu.
Mikono yangu imejaa manemane,
na vidole vyangu vyadondosha manemane,
nilipolishika komeo kufungua mlango.
6Nilimfungulia mlango mpenzi wangu,
lakini kumbe, alikuwa amekwisha toweka.
Moyo wangu ulifurahi alipokuwa akizungumza!
Nilimtafuta, lakini sikumpata;
nilimwita, lakini hakuniitikia.
7Walinzi wa mji waliniona,
walipokuwa wanazunguka mjini;
wakanipiga na kunijeruhi;
nao walinzi wa lango wakaninyanganya shela langu.
8Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,
mkimwona mpenzi wangu,
mwelezeni kwamba naugua kwa mapenzi!
Wanawake
9Ewe upendezaye kuliko wanawake wote!
Kwani huyo mpenzi wako ana nini cha zaidi ya mpenzi mwingine,
hata utusihi kwa moyo kiasi hicho?
Bibi arusi
10Mpenzi wangu ni mzuri na mwenye nguvu,
mashuhuri miongoni mwa wanaume elfu kumi.
11Kichwa chake kizuri kama dhahabu safi,
nywele zake ni za ukoka,
nyeusi ti kama kunguru.
12Macho yake ni kama ya hua kandokando ya kijito,
ni kama njiwa waliooga maziwa kando ya kijito.5:12 kando ya kijito: Kiebrania si dhahiri.
13Mashavu yake ni kama matuta ya rihani
kama bustani iliyojaa manukato na manemane.
Midomo yake ni kama yungiyungi,
imelowa manemane kwa wingi.
14Mikono yake imewekwa bangili za dhahabu,
amevalia johari za Tarshishi.
Kiwiliwili chake ni kama pembe za ndovu
zilizopambwa kwa vito vya johari ya rangi ya samawati.
15Miguu yake ni kama nguzo za alabasta
zilizosimikwa katika misingi ya dhahabu.
Umbo lake ni kama Lebanoni,
ni bora kama miti ya mierezi.
16Kinywa chake kimejaa maneno matamu,
kwa ujumla anapendeza.
Basi, hivyo ndivyo alivyo mpenzi wangu,
naam, ndivyo alivyo rafiki yangu,
enyi wanawake wa Yerusalemu.

Wimbo Ulio Bora5;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: