Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 28 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora 7...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezesheni kustahili maisha aliyowaitia muyaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Bwana arusi
1Nyayo zako katika viatu zapendeza sana!
Ewe mwanamwali wa kifalme.
Mapaja yako ya mviringo ni kama johari,
kazi ya msanii hodari.
2Kitovu chako ni kama bakuli
lisilokosa divai iliyokolezwa.
Tumbo lako ni kama lundo la ngano
lililozungushiwa yungiyungi kandokando.
3Matiti yako ni kama paa mapacha,
ni kama swala wawili.
4Shingo yako ni kama mnara wa pembe za ndovu;
macho yako ni kama vidimbwi mjini Heshboni,
karibu na mlango wa Beth-rabi.
Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,
ambao unauelekea mji wa Damasko.
5Kichwa chako juu yako ni kama mlima Karmeli,
nywele zako za ukoka zangaa kama zambarau;
uzuri7:5 uzuri: Kiebrania si dhahiri. wako waweza kumteka hata mfalme.
6Tazama ulivyo mzuri na wa kuvutia!
Ewe mpenzi, mwali upendezaye!
7Umbo lako lapendeza kama mtende,
matiti yako ni kama shada za tende.
8Nilisema nitaupanda mtende na kuzichuma shada za tende.
Kwangu matiti yako ni kama shada za zabibu,
harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matofaa;
9na kinywa chako ni kama divai tamu.
Bibi arusi
Basi divai na itiririke hadi kwa mpenzi wangu,
ipite juu ya midomo yake na meno yake!8:9 midomo yake na meno yake: Kiebrania: Midomo ya wale walalao.
10Mimi ni wake mpenzi wangu,
naye anionea sana shauku.
11Njoo ewe mpenzi wangu, twende mashambani,
twende zetu tukalale huko vijijini.
12Tutaamka mapema, twende kwenye mashamba ya mizabibu,
tukaone kama imeanza kuchipua,
na kama maua ya zabibu yamekwisha kuchanua,
pia kama mikomamanga imeanza kutoa maua.
Huko ndiko nitakapokupatia pendo langu.
13Harufu nzuri ya tunguja imejaa hewani
karibu na milango yetu kuna kila aina ya matunda bora,
yote mapya na ya siku za nyuma,
ambayo nimekuwekea wewe mpenzi wangu.

Wimbo Ulio Bora7;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: