Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 30 January 2018

Kikombe Cha Asubuhi ; Leo tunaanza kitabu cha -2Samueli1...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Leo tunaanza kitabu cha 2 Samweli Mungu akatubariki na akatupe macho ya rohoni tukapate kuelewa,kukumbuka  na kujifunza zaidi,ikawe faida kwetu na wengine..
Ee Mungu tunaomba ukatuongoze..

Siku moja, Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongamana, wanasikiliza neno la Mungu. Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa. Wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao. Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua. Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, “Endesha mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki.” Simoni akamjibu, “Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu.” Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika. Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama. Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, “Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!” Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile. Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu.” Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.


Tumshukuru Mungu wetu katika yote..
Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu...
Utukuzwe Mungu wetu,Mungu mwenye nguvu,Baba wa Upendo,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote,Alfa na omega,Mungu wa walio hai,Baba wa Yatima,Mume wa Wajane,Mponyaji wetu,Hakuna lilikogumu kwako,Neema yako yatutosha ee Mungu wetu,Hakuna kama wewe Mfalme wa Amani..!!

Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.” Yesu akanyosha mkono, akamgusa na kusema, “Nataka! Takasika!” Mara ule ukoma ukamwacha. Naye Yesu akamwamuru: “Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajioneshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose kuwathibitishia kwamba umepona.” Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.


Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako..
Mungu wetu tunaomba utusamehe makosa yetu yote tuliyoyafanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote walio tukosea..
Jehovah tunaomba utuepushe katika majaribu Yahweh utuoke na yule mwovu na kazi zake zote..
Mfalme wa amani tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..

Siku moja, Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na waalimu wa sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponya wagonjwa. Mara watu wakaja, wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani, wamweke mbele ya Yesu. Lakini, kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya paa, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu. Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, “Rafiki, umesamehewa dhambi zako.” Waalimu wa sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: “Nani huyu anayesema maneno ya kufuru? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!” Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, “Mnawaza nini mioyoni mwenu? Ni lipi lililo rahisi zaidi: Kusema, ‘Umesamehewa dhambi,’ au kusema, ‘Simama utembee?’ Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Simama, chukua kitanda chako, uende zako nyumbani.” Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda nyumbani kwake huku akimtukuza Mungu. Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: “Tumeona maajabu leo.”


Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Yahweh tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Baba wa Mbinguni nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Jehovah tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu Jehovah ukatupe kama inavyokupendeza wewe..

Mungu wetu tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka..
Yahweh tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia..
Baba wa Mbinguni ukabariki tuingiapo/tutokapo Yahweh ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..
Mungu wetu tunaomba utupe neema ya kufuata njia zako Baba wa Mbinguni tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu,Yahweh ukaonekane katika maisha yetu na popote tupitapo Yahweh na ikajulikane kwamba upo Baba wa Mbinguni..
Nuru yako ikaangze katika maisha yetu,Amani ikatawale katika nyumba zetu,Upendo ukadumu kati yetu na tuka nene yaliyo yako Mungu wetu..
Tukawe barua njema Yahweh na tukasomeke kama inavyokupendeza wewe...
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtozaushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, “Nifuate!” Naye akaacha yote akamfuata. Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake. Na kundi kubwa la watozaushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao. Mafarisayo na waalimu wa sheria wakawanungunikia wanafunzi wake wakisema: “Kwa nini mnakula na kunywa pamoja na watozaushuru na wenye dhambi?” Yesu akawajibu, “Wenye afya hawamhitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, wapate kutubu.”

Yahweh tunaomba ukawabariki na kuwatendea wenye shida/tabu
Mungu wetu tunaomba ukawaponye wagonjwa na ukawape uvumilivu na imani wanaowauguza..
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawafungue walio katika vifungo vya yule mwovu,Mungu wetu tazama walio magerezani pasipo na hatia Yahweh tunaomba ukawatendee na haki ikapatikane..
Jehovah tunaomba ukawape chakula wenye njaa Baba wa Mbinguni ukabariki Mashamba na kazi zao za mikono..
Mungu wetu tazama wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali Yahweh tunaomba ukawavushe salama,Baba wa Mbinguni ukawasamehe wale wote walikwenda kinyume nawe na wakaomba na kutubu Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo ziwaweke huru..
Jehovah tunaomba ukawafariji wafiwa,Yahweh ukawe tumaini kwa waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye hofu na mashaka Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako..

Watu wengine wakamwambia, “Wafuasi wa Yohane Mbatizaji hufunga mara kwa mara na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa.” Yesu akawajibu, “Je, wale walioalikwa harusini hutakiwa wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao? La! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.” Yesu akawaambia mfano huu: “Watu hawakati kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama wakifanya hivyo, watakuwa wamelikata hilo vazi jipya, na pia hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu. Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya. Hakuna mtu anayetamani kunywa divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani kwani husema ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Baba wa Mbinguni..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Mielele..
Amina..!!!

Wapendwa katika Bwana asanteni sana kwakuwa nami
Mungu wetu mwenye nguvu akawalinde na kuwabariki
Msipungukiwe katika mahitaji yenu Baba wa Mbinguni akawape kama inavyompendeza yeye..
Nawapenda.



Daudi anahabarishwa juu ya kifo cha Shauli

1Baada ya kifo cha Shauli, Daudi alirudi baada ya kuwashinda Waamaleki, akakaa Siklagi kwa muda wa siku mbili. 2Siku iliyofuata, mtu mmoja kutoka kambi ya Shauli, mavazi yake yakiwa yamechanwa kwa huzuni na akiwa na mavumbi kichwani alimwendea Daudi. Alipomfikia Daudi, alijitupa chini mbele yake akamsujudia. 3Daudi akamwambia, “Unatoka wapi?” Naye akamwambia, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.” 4Daudi akamwambia, “Niambie mambo yalivyokuwa huko.” Yule mtu akamjibu, “Watu wetu wameyakimbia mapigano na wengi wetu wameuawa. Zaidi ya hayo, Shauli na mwanawe Yonathani pia wameuawa.” 5Daudi akamwuliza yule kijana, “Unajuaje kuwa Shauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”
6Yule kijana akamjibu, “Kwa bahati, nilikuwapo mlimani Gilboa. Nilimwona Shauli ameegemea mkuki wake na magari ya wapandafarasi ya adui zake yalikuwa yanamsonga sana. 7Shauli alipotazama nyuma, aliniona, akaniita. Nilipoitika, 8yeye aliniuliza mimi ni nani, nami nikamwambia kuwa mimi ni Mmaleki. 9Hapo, akaniambia, ‘Karibia uniue maana nimejeruhiwa vibaya na maumivu ni makali. Lakini bado ningali hai’. 10Hivyo, nilikwenda karibu naye na kumuua, kwa sababu nilikuwa na uhakika kuwa akianguka chini, hataweza kuishi zaidi. Lakini taji iliyokuwa kichwani pake na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, vyote nimekuletea wewe, bwana wangu.”
11Daudi akayashika mavazi yake na kuyararua kwa huzuni. Hata watu waliokuwa pamoja na Daudi wakafanya vivyo hivyo. 12Wakaomboleza, wakalia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Shauli, Yonathani mwanawe, na nchi ya Waisraeli, watu wa Mwenyezi-Mungu, kwa kuwa wengi wao waliuawa vitani. 13Daudi akamwuliza yule kijana aliyempasha habari, “Unatoka wapi?” Yeye akajibu, “Mimi ni Mmaleki, lakini ninaishi katika nchi yako kama mgeni.” 14Daudi akamwuliza, “Ilikuwaje wewe hukuogopa kuunyosha mkono wako na kumuua mtu aliyeteuliwa na Mwenyezi-Mungu kwa kupakwa mafuta?” 15Kisha, Daudi akamwita mmoja wa vijana wake akamwambia, “Muue mtu huyu!” Yule kijana alimpiga yule Mmaleki, naye akafa. 16Daudi akasema, “Uwajibike wewe mwenyewe kwa kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa mdomo wako ukisema, ‘Nimemuua mtu aliyeteuliwa na Mwenyezi-Mungu kwa kupakwa mafuta.’”

Daudi aomboleza kifo cha Shauli na Yonathani

17Daudi aliimba ombolezo lifuatalo kwa ajili ya Shauli na mwanawe Yonathani. 18Daudi alisema watu wa Yuda wafundishwe ombolezo1:18 ombolezo: Kiebrania: Upinde. hilo, nalo limeandikwa katika kitabu cha Yashari.1:18 Yashari: Au Mnyofu. Daudi aliimba,
19“Walio fahari yako, ee Israeli,
wameuawa milimani pako.
Jinsi gani mashujaa walivyoanguka!
20Jambo hilo msiuambie mji wa Gathi
wala katika mitaa ya Ashkeloni.
La sivyo, wanawake Wafilisti watashangilia,
binti za wasiotahiriwa, watafurahi.
21“Enyi milima ya Gilboa,
msiwe na umande au mvua juu yenu.
Wala mashamba yenu1:21 mashamba yenu: Kiebrania: Mashamba ya dhabihu. daima yasitoe chochote.
Maana huko ngao za shujaa zilitiwa najisi,
ngao ya Shauli haikupakwa mafuta.
22“Upinde wa Yonathani kamwe haukurudi nyuma,
upanga wa Shauli kamwe haukurudi bure,
daima ziliua wengi.
Naam, ziliua mashujaa.
23“Shauli na Yonathani,
watu wa ajabu na wakupendeza.
Maishani na kifoni hawakutengana.
Walikuwa wepesi kuliko tai,
naam, wenye nguvu kuliko simba.
24“Wanawake wa Israeli, mlilieni Shauli!
Aliwavika mavazi mekundu ya fahari,
aliyatarizi mavazi yenu kwa dhahabu.
25“Jinsi gani mashujaa walivyoanguka!
Wamekufa wakiwa katika mapambano.
Yonathani analala,
akiwa ameuawa milimani.
26Nasikitika kwa ajili yako, ndugu yangu Yonathani.
Umekuwa kwangu daima mtu wa kupendeza,
pendo lako kwangu limekuwa la ajabu,
la ajabu kuliko la mwanamke.
27“Jinsi gani mashujaa wameanguka,
na silaha zao zimeachwa, hazina kazi.”


2Samweli1;1-27


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: