Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 8 May 2017

Neno la Faraja;Mungu atupe uvumilivu Ndugu/Familia yangu kwa kuondokewa na Ndugu yetu Christopher-Hamisi Mbegete na Watanzania kwa kuondokewa na Watoto wetu wanafunzi wa Lucky Vicent..

Pichani ni ndugu yetu,Kaka na Mpendwa wetu Christopher-Hamisi Mbegete
Naungana na Ndugu/ familia yangu huko nyumbani kwa wakati huu mgumu sana kwa kuondokewa na mpenzi ndugu yetu..
Daima tutakukumbuka, Sina Neno zuri  la kuweza kusema zaidi ya kumshukuru Mungu kwa maisha yako na kuwa nasi na sasa umetangulia..Mungu akatupe faraja na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu..Mungu akawasimamie na kuwaongoza  wote wanaoshiriki katika maandalizi ya kuulaza mwili wako.Na akawabariki na kuwaongezea zaidi ya walipojitoa, kwa Muda, Faraja na yote..
Ulale kwa Amani.


Niungane na familia, wanafunzi /walimu  na Watanzania wenzangu huko nyumbani na popote walipo kwa wakati huu mgumu kwenye Taifa letu
kwakuondokewa na watoto wetu,wadogo zetu wapendwa wetu Walimu na Wafanya kazi..
Mungu Baba akawape nguvu na uvumilivu kwa wakati huu mgumu,Poleni sana wazazi/ndugu na Watanzania..
Mungu akawafariji na kuwaongoza katika yote.
Mlale kwa Amani malaika  wetu,watoto wetu wapendwa..
ni kipindi kigumu sana lakini tumshukuru Mungu katika yote..






Shukrani kwa Mungu
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote. 4Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu. 5Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye. 6Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji nyinyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi. 7Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.[2wakorintho 1;3-7]






Bwana anakuja
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini. 14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana, kwamba sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia. 16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza. 17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana. 18Basi, farijianeni kwa maneno haya.[1Wathesalonike 4;13-18]


Wapendwa/Waungwana leo tuungane na wenzetu katika kuombeleza Msiba huu..
Mniwie Radhi kesho kwa Neema ya Mungu tutaendelea.
Muwe na wakati mwema na msisahau kuwaweka katika maombi/sala/dua wote wanaopitia mapito haya.

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

No comments: