Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 28 May 2017

Natumaini Jumapili Ilikuwa Njema/inaendelea Vyema;Burudani-Miriam Lukindo Mauki - Hakuna Wa Kubadili Na Eunice Njeri - Nani Kama Wewe ..!!




Ni Nani kama wewe Nakuinua Mungu wangu Leo Nani kama wewe Nakupendaaa..!!
Miguuni pako Nakuinamia Bwana  Heshima na utukufu Baba nakupa Yesu..!!Nimekuja nikuinue Nimekuja nikupendeeh Miguuni pako Nakupendaaa..!!

Haleluyahh.! Mungu wetu  yu mwema sana. Haijalishi nini unapitia,Haijalishi umejikwaaje..!Inuka na uendelee na safari   hakuna mwingine tena kama Mungu..

Wapendwa/Waungwana Natumaini mlikuwa na Jumapili Njema/mnaendelea vyema na Jumapili hii..
Mungu aendelee kuwabariki na kuwapa sawasawa na mapenzi yake..
Amina ooh Amina oohh Amina Mileleeeh..!!
1Mungu wenu asema:
“Wafarijini watu wangu,
nendeni mkawafariji.

Neno la Leo;Isaya 40:1-31 



Tumaini la kuponywa katika Yerusalemu
1Mungu wenu asema:
“Wafarijini watu wangu,
nendeni mkawafariji.
2Semeni na wenyeji wa Yerusalemu kwa upole,
waambieni kwamba utumwa wao umekwisha,
wamesamehewa uovu wao.
Mwenyezi-Mungu amewaadhibu maradufu
kwa sababu ya dhambi zao zote.”
3 40:3 Taz Mat 3:3; Marko 1:3; Yoh 1:23 Sauti ya mtu anaita jangwani:
“Mtayarishieni Mwenyezi-Mungu njia,
nyosheni barabara kuu kwa ajili ya Mungu wetu. 40:3-5 Taz Luka 3:4-6
4Kila bonde litasawazishwa,
kila mlima na kilima vitashushwa;
ardhi isiyo sawa itafanywa sawa,
mahali pa kuparuza patalainishwa.
5Kisha utukufu wa Mwenyezi-Mungu utafunuliwa,
na watu wote pamoja watauona.
Mwenyezi-Mungu mwenyewe ametamka hayo.”
6 40:6-8 Taz Yak 1:10-11; 1Pet 1:24-25 Sikiliza! Kuna sauti inasema, “Tangaza!”
Nami nikauliza, “Nitangaze nini?”
Naye: “Tangaza: Binadamu wote ni kama majani;
uthabiti wao ni kama ua la shambani.
7Majani hunyauka na ua hufifia,
Mwenyezi-Mungu avumishapo upepo juu yake.
Hakika binadamu ni kama majani.
8Majani hunyauka na ua hufifia,
lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9Nenda juu ya mlima mrefu,
ewe Siyoni, ukatangaze habari njema.
Paza sauti yako kwa nguvu,
ewe Yerusalemu, ukatangaze habari njema.
paza sauti yako bila kuogopa.
Iambie miji ya Yuda:
“Mungu wenu anakuja.”
10 40:10 Taz Isa 62:11; Ufu 22:12 Bwana Mungu anakuja na nguvu,
kwa mkono wake anatawala.
Zawadi yake iko pamoja naye,
na tuzo lake analo.
11 40:11 Taz Eze 34:15; Yoh 10:11 Atalilisha kundi lake kama mchungaji,
atawakusanya wanakondoo mikononi mwake,
atawabeba kifuani pake,
na kondoo wanyonyeshao atawaongoza polepole.

Bwana ameshakubali hakuna wakubadili..!!
 Ameshasema ndiyo Leo hakuna wa kubadili
Yeye ni Bwana wa Ma Bwana Hakuna wakubadili...!
Yeye ni Mwamba wa miamba hakuna wa Kubalidili..!!


Mungu wa Israeli hana kifani
12Nani awezaye kupima maji ya bahari kwa konzi yake,
kuzipima mbingu kwa mikono yake?
Nani awezaye kuutia udongo wa dunia kikombeni;
kuipima milima kwa mizani
au vilima kwa kipimo cha uzani?
13 40:13 Taz Rom 11:34; 1Kor 2:16 Nani awezaye kuiongoza akili ya Mwenyezi-Mungu,
au kuwa mshauri wake na kumfunza?
14Mwenyezi-Mungu alimtaka nani shauri,
ndipo akapata kuwa mwenye ujuzi?
Nani aliyemfunza njia za haki?
Nani aliyemfundisha maarifa,
na kumwonesha namna ya kuwa na akili?
15Kwake mataifa ni kama tone la maji katika ndoo,
ni kama vumbi juu ya mizani.
Kwake visiwa ni vyepesi kama vumbi laini.
16Kuni zote za Lebanoni
na wanyama wake wote
havitoshi kwa sadaka ya kuteketezwa mbele yake.
17Mataifa yote si kitu mbele yake;
kwake ni vitu duni kabisa na batili.
18 40:18-19 Taz Mate 17:29 Mtamlinganisha Mungu na nini basi,
au ni kitu gani cha kumfananisha naye?
19Je, anafanana na kinyago?
Hicho, fundi hukichonga,
mfua dhahabu akakipaka dhahabu,
na kukitengenezea minyororo ya fedha!
20Au ni sanamu ya mti mgumu?
Hiyo ni ukuni mtu anaochagua,
akamtafuta fundi stadi,
naye akamchongea sanamu imara!
21Je, nyinyi bado hamjui?
Je, hamjapata kusikia?
Je, hamkuambiwa tangu mwanzo?
Je, hamjafahamu mwanzo wa dunia?
22Dunia iliumbwa na huyo aketiye juu ya mbingu;
kutoka huko wakazi wa dunia ni kama panzi!
Yeye amezitandaza mbingu kama pazia,
na kuzikunjua kama hema la kuishi.
23Yeye huwaporomosha wakuu wenye nguvu,
watawala wa dunia huwafanya kuwa si kitu.
24Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota,
hata kabla hawajatoa mizizi kama miti udongoni,
Mwenyezi-Mungu akiwapulizia hunyauka,
kimbunga huwapeperusha kama makapi!
25Mungu Mtakatifu auliza hivi:
“Nani basi, mtakayemlinganisha nami?
Je, kuna mtu aliye kama mimi?”
26Inueni macho yenu juu mbinguni!
Je, ni nani aliyeziumba nyota hizo?
Ni yule aziongozaye kama jeshi lake,
anayeijua idadi yake yote,
aziitaye kila moja kwa jina lake.
Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi,
hakuna hata moja inayokosekana.
27Enyi watu wa Israeli wazawa wa Yakobo,
kwa nini mnalalamika na kusema:
“Mwenyezi-Mungu hatujali sisi!
Mungu wetu hajali haki yetu!”
28Je, nyinyi bado hamjui?
Je, hamjapata kusikia?
Mwenyezi-Mungu ndiye Mungu wa milele;
yeye ndiye Muumba wa kila kitu duniani.
Yeye hafifii kamwe wala kuishiwa nguvu.
Maarifa yake hayachunguziki.
29Yeye huwapa uwezo walio hafifu,
wanyonge huwapa nguvu.
30Hata vijana watafifia na kulegea;
naam, wataanguka kwa uchovu.
31Lakini wote wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu,
watapata nguvu mpya.
Watapanda juu kwa mabawa kama tai;
watakimbia bila kuchoka;
watatembea bila kulegea.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

No comments: