Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 6 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 49....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Paulo aliwakodolea macho wale wanabaraza, halafu akaanza kusema, “Ndugu zangu, mpaka hivi leo nimekuwa nikiishi na dhamiri njema mbele ya Mungu.” Hapo kuhani mkuu Anania akaamuru wale waliokuwa wamesimama karibu na Paulo wampige kofi mdomoni. Basi, Paulo akamwambia, “Mungu mwenyewe atakupiga kofi wewe uliye kama ukuta uliopakwa chokaa! Unawezaje kukaa hapo ili unihukumu kisheria na huku wewe mwenyewe unaivunja sheria kwa kuamuru nipigwe?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Watu waliokuwa wamesimama pale wakamwambia Paulo, “Unamtukana kuhani mkuu wa Mungu!” Paulo akajibu, “Ndugu zangu, sikujua kama yeye ni kuhani mkuu. Maana Maandiko yasema hivi: ‘Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako.’”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wakati huo Paulo alikwisha tambua kwamba sehemu moja ya wanabaraza wale ilikuwa ni Masadukayo na nyingine Mafarisayo. Basi, alipaza sauti yake mbele ya Baraza, “Ndugu zangu, mimi ni Mfarisayo, mwana wa Mfarisayo. Mimi nimeletwa mahakamani kwa kuwa ninatumaini kwamba wafu watafufuka.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Israeli: Mwanga wa mataifa
1Nisikilizeni, enyi nchi za mbali,
tegeni sikio, enyi watu wa mbali!
Mwenyezi-Mungu aliniita kabla sijazaliwa,
alitaja jina langu nikiwa tumboni mwa mama yangu.
2Aliyapa ukali maneno yangu kama upanga mkali,
alinificha katika kivuli cha mkono wake;
aliufanya ujumbe wangu mkali kama ncha ya mshale,
akanificha katika podo lake.
3Aliniambia, “Wewe ni mtumishi wangu;
kwako, Israeli, watu watanitukuza.”
4Lakini mimi nikafikiri,
“Nimeshughulika bure,
nimetumia nguvu zangu bure kabisa.”
Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu atanipa haki yangu;
tuzo la kazi yangu liko kwa Mungu.
5Lakini asema sasa Mwenyezi-Mungu,
ambaye aliniita tangu tumboni mwa mama yangu
ili nipate kuwa mtumishi wake;
nilirudishe taifa la Yakobo kwake,
niwakusanye wazawa wa Israeli kwake.
Mwenyezi-Mungu amenijalia heshima mbele yake.
Mungu wangu amekuwa ndiye nguvu yangu.
6Yeye asema: “Haitoshi tu wewe kuwa mtumishi wangu,
uyainue makabila ya Yakobo,
na kurekebisha watu wa Israeli waliobaki.
Nitakufanya uwe mwanga wa mataifa,
niwaletee wokovu watu wote duniani.”49:6 sehemu hii imekaririwa katika Mate 13:47, 26:23. Luka naye anaigusia katika 2:32; Taz pia Isa 42:6.
7Mwenyezi-Mungu, Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli,
amwambia hivi yule anayedharauliwa mno,
yule anayechukiwa na mataifa,
na ambaye ni mtumishi wa watawala:
“Wafalme watakuona nao watasimama kwa heshima,
naam, wakuu watainama na kukusujudia
kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu
ambaye hutimiza ahadi zangu;
kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeli
ambaye nimekuteua wewe.”
Kujengwa upya kwa Yerusalemu
8Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wakati wa kufaa nilikujibu ombi lako;
wakati wa wokovu nilikusaidia.
Nimekuweka na kukufanya
uwe kiungo cha agano langu na mataifa yote:
Kuirekebisha nchi iliyoharibika,
na kuwarudishia wenyewe ardhi hiyo;
9kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni humo gerezani’,
na wale walio gizani, ‘Njoni nje mwangani!’
Kila mahali watakapokwenda watapata chakula
hata kwenye vilima vitupu watapata malisho.
10Hawataona tena njaa wala kuwa na kiu.
Upepo wa hari wala jua havitawachoma,
mimi niliyewahurumia nitawaongoza
na kuwapeleka kwenye chemchemi za maji.
11Milima yote nitaifanya kuwa njia,
na barabara zangu kuu nitazitengeneza.
12Watu wangu watarudi kutoka mbali,
wengine kutoka kaskazini na magharibi,
wengine kutoka upande wa kusini.”49:12 kutoka upande wa kusini: Makala ya Kiebrania Sinimu mji uliokaliwa na Waisraeli kusini mwa Misri.
13Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!
Shangilia ewe dunia.
Pazeni sauti mwimbe enyi milima,
maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,
naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.
14Wewe Siyoni wasema:
“Mwenyezi-Mungu ameniacha;
hakika Bwana wangu amenisahau.”
15Lakini Mwenyezi-Mungu asema:
“Je, mama aweza kumsahau mwanawe anayenyonya,
asimwonee huruma mtoto wa tumbo lake?
Hata kama mama aweza kumsahau mwanawe,
mimi kamwe sitakusahau.
16Nimekuchora katika viganja vyangu;
kuta zako naziona daima mbele yangu.
17Watakaokujenga49:17 Watakaokujenga: Kulingana na makala ya Kiebrania iliyopatikana Kumrani na hati nyingine za kale. Tafsiri za mapokeo: Watoto wako. upya wanakuja haraka,
wale waliokuharibu wanaondoka.
18Inua macho uangalie pande zote;
watu wako wote wanakusanyika na kukujia.
Naapa kwa nafsi yangu mimi Mwenyezi-Mungu,
watu wako watakuwa kwako kama mapambo,
utawafurahia kama afanyavyo bibi arusi na utaji wake.
19“Kweli umekumbana na uharibifu,
makao yako yamekuwa matupu,
na nchi yako imeteketezwa.
Lakini sasa itakuwa ndogo mno kwa wakazi wake;
na wale waliokumaliza watakuwa mbali.
20Wanao waliozaliwa uhamishoni,
watakulalamikia wakisema:
‘Nchi hii ni ndogo mno;
tupatie nafasi zaidi ya kuishi.’
21Hapo ndipo utakapojiuliza mwenyewe:
‘Nani aliyenizalia watoto wote hawa?
Nilifiwa na wanangu bila kupata wengine.
Nilipelekwa uhamishoni na kutupwa mbali;
nani basi aliyewalea watoto hawa?
Mimi niliachwa peke yangu,
sasa, hawa wametoka wapi?’”
22Bwana Mungu asema hivi:
“Nitayapungia mkono mataifa;
naam, nitayapa ishara,
nayo yatawabeba watoto wenu wa kiume,
kadhalika na watoto wenu wa kike
na kuwarudisha kwako.
23Wafalme watakushughulikia,
na malkia watakutengenezea chakula.
Watakusujudia na kukupa heshima,
na kuramba vumbi iliyo miguuni pako.
Hapo utatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu;
wote wanaonitegemea hawataaibika.”
24Watu wa Yerusalemu walalamika:
“Je, shujaa aweza kunyanganywa nyara zake?
Au mateka wa mtu katili waweza kuokolewa?”
25Mwenyezi-Mungu ajibu:
“Naam! Hata nyara za shujaa zitachukuliwa,
mateka wa mtu katili wataokolewa.
Mimi mwenyewe nitawakabili maadui zako,
mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.
26Nitawafanya wanaokukandamiza watafunane;
watalewa damu yao wenyewe kama divai.
Hapo binadamu wote watatambua kwamba
mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mwokozi wako,
mimi ni Mkombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

Isaya49;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 5 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 48....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kila walipokwenda kupigana, mkono wa Mwenyezi-Mungu uliwakabili kuwaletea balaa, kama alivyokuwa amewaonya na kuapa. Nao wakawa katika huzuni kubwa. Ndipo Mwenyezi-Mungu akawapa waamuzi ambao waliwaokoa mikononi mwa watu waliopora mali zao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hata hivyo, Waisraeli hawakuwasikiliza waamuzi wao, maana walifanya kama wazinzi kwa kufuata miungu mingine na kuisujudia. Waliacha upesi nyayo walizofuata babu zao ambao walitii amri za Mwenyezi-Mungu; bali wao hawakufanya hivyo. Kila mara Mwenyezi-Mungu alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa mikononi mwa adui zao muda wote wa uhai wa mwamuzi huyo. Aghalabu, Mwenyezi-Mungu aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na dhuluma walizofanyiwa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Lakini kila mara mwamuzi alipofariki walirudia mienendo yao ya zamani, wakaishi vibaya kuliko babu zao. Waliifuata miungu mingine, wakaitumikia na kuisujudia, wala hawakuyaacha matendo yao wala ukaidi wao. Kwa hiyo Mwenyezi-Mungu akawaka hasira dhidi ya Waisraeli, akasema, “Kwa kuwa watu hawa wamevunja agano nililofanya na babu zao, wakakataa kutii sauti yangu, sitayafukuza tena mataifa ambayo Yoshua aliyabakiza, wakati alipofariki. Nitayatumia mataifa hayo kuwajaribu Waisraeli nione kama watairudia njia yangu kama babu zao au sivyo.” Basi, Mwenyezi-Mungu akayaacha mataifa hayo, wala hakuyafukuza mara moja, wala hakumpa Yoshua ushindi juu ya mataifa hayo!
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu atangaza matukio mapya
1Sikilizeni, enyi watu wa Yakobo,
enyi mnaojulikana kwa jina la Israeli,
nyinyi mlio wa ukoo wa Yuda.
Nyinyi huapa kwa jina la Mwenyezi-Mungu,
na kudai mnamwabudu Mungu wa Israeli;
lakini hayo si ukweli wala sawa.
2Nyinyi mnaona fahari kujiita watu wa mji mtakatifu,
na kujidai kumtegemea Mungu wa Israeli,
ambaye jina lake ni Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
3“Nilitangaza zamani matukio ya awali,
niliyatamka mimi mwenyewe
na kuyafanya yajulikane kwenu.
Mara nikaanza kuyatekeleza,
nayo yakapata kutukia.
4Lakini nilikujua wewe kuwa mkaidi;
kichwa kigumu kama chuma,
uso wako mkavu kama shaba.
5Kwa hiyo nilikutangazia tangu zamani,
kabla hayajatukia mimi nilikutangazia,
usije ukasema, ‘Kinyago changu kiliyatenda hayo,
sanamu zangu za kuchonga na kusubu ziliyafanya.’
6“Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote.
Kwa nini huwezi kuyakiri?
Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya;
mambo yaliyofichika ambayo hukuyajua.
7Mambo hayo yanatukia sasa;
hukupata kuyasikia kabla ya leo,
hivyo huwezi kusema, ‘Aa! Nilikwisha yajua.’
8Hujapata kamwe kuyasikia wala kuyajua;
tangu zamani masikio yako hayakuyasikia.
Nilijua kuwa wewe ni mwenye hila,
na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.
9“Kwa heshima ya jina langu,
ninaiahirisha hasira yangu;
kwa ajili ya heshima yangu,
ninaizuia nisije nikakuangamiza.
10Mimi nitawajaribu lakini si kama fedha katika tanuri.
Nitawajaribu katika tanuri ya taabu.
11Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe.
Kwa nini jina langu lidharauliwe?
Utukufu wangu siwezi kumpa mwingine!
Koreshi, mteule wa Mwenyezi-Mungu
12“Nisikilize ee taifa la Yakobo,
nisikilize ee Israeli niliyekuita.
Mimi ndiye Mungu;
mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
13Kwa mkono wangu niliuweka msingi wa dunia,
mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu.
Nikiziita mbingu na dunia,
zinasimama haraka mbele yangu.
14“Kusanyikeni nyote msikilize!
Nani kati ya miungu yenu aliyetabiri vitu hivi?
Mimi Mwenyezi-Mungu nampenda Koreshi;
yeye atatekeleza lengo langu kuhusu Babuloni,
naam, yeye atawashambulia Wakaldayo.
15Mimi, naam, mimi nimeyasema na kumwita;
nimemleta, naye atafaulu katika mpango wake.
16Njoni karibu nami msikie jambo hili:
Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri,
tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwapo.”
Sasa, Bwana Mungu amenituma,
na kunipa nguvu ya roho yake.48:16 Sasa … roho wake: Maneno haya hayaonyeshi dhahiri ni nani anayesema; Pengine ni rafiki (Koreshi) aliyetajwa katika aya ya 14.
Mpango wa Mungu kwa watu wake
17Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli,
Mkombozi wako, asema hivi:
“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
ninayekufundisha kwa faida yako,
ninayekuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.
18Laiti ungalizitii amri zangu!
Hapo baraka zingekutiririkia kama mto,
ungepata fanaka kwa wingi kama mawimbi ya bahari.
19Wazawa wako wangekuwa wengi kama mchanga,
naam, wangekuwa wengi kama chembe za mchanga.
Jina lao kamwe lisingaliondolewa,
kumbukumbu lao halingalitoweka mbele yangu.”
20 48:20 Taz Ufu 18:4 Sasa, ondokeni Babuloni!
Kimbieni kutoka Kaldayo!
Tangazeni jambo hili kwa sauti za shangwe,
enezeni habari zake kila mahali duniani.
Semeni: “Mwenyezi-Mungu amelikomboa
taifa la mtumishi wake Yakobo.”
21Alipowaongoza jangwani hawakuona kiu,
aliwatiririshia maji kutoka mwambani,
aliupasua mwamba maji yakabubujika.
22Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Watu waovu sitawapa amani.”

Isaya48;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 4 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 47....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mw
ingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Yoshua mwana wa Nuni na mtumishi wa Mwenyezi-Mungu, alifariki akiwa na umri wa miaka 110. Wakamzika katika sehemu aliyogawiwa iwe yake huko Timnath-heresi, katika nchi ya milima ya Efraimu kaskazini ya mlima Gaashi. Kisha watu wote wa kizazi chake walifariki, kikafuata kizazi kingine ambacho hakikumjua Mwenyezi-Mungu wala matendo aliyowatendea watu wa Israeli.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Basi, Waisraeli walitenda uovu mbele ya Mwenyezi-Mungu na kuabudu Mabaali. Walimwacha Mwenyezi-Mungu, Mungu wa wazee wao, ambaye aliwatoa katika nchi ya Misri, wakaifuata miungu mingine, miungu iliyoabudiwa na watu walioishi kandokando yao. Waliisujudia miungu hiyo, wakamkasirisha sana Mwenyezi-Mungu.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Walimwacha Mwenyezi-Mungu, wakatumikia Mabaali na Maashtarothi. Basi, hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwaka dhidi ya Israeli, naye akawaacha wanyanganyi wapore mali zao. Aliwakabidhi kwa adui zao waliowazunguka hata wasiweze tena kuwapinga.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Hukumu dhidi ya Babuloni
1“Teremka uketi mavumbini
ewe Babuloni binti mzuri!
Keti chini pasipo kiti cha enzi
ewe binti wa Wakaldayo!
Tokea sasa hutaitwa tena mwororo wala nadhifu.
2Twaa mawe ya kusagia, usage unga kama mtumwa!
Vua utaji wako, ukavue na mavazi yako!
Pandishia vazi lako miguuni, ukavuke mito.
3Watu watauona uchi wako;
naam, wataiona aibu yako.
Mimi nitalipiza kisasi,
wala sitamhurumia yeyote.”
4Mkombozi wetu ndiye Mtakatifu wa Israeli;
Mwenyezi-Mungu wa majeshi ndilo jina lake.
5Mwenyezi-Mungu asema:
“Ewe taifa la Wakaldayo
lililo kama binti mzuri,
keti kimya na kutokomea gizani.
Maana umepoteza hadhi yako
ya kuwa bimkubwa wa falme.
6Niliwakasirikia watu wangu Israeli,
nikawafanya watu wangu kuwa haramu.
Niliwatia mikononi mwako,
nawe hukuwaonea huruma;
na wazee uliwatwisha nira nzito mno.
7Ulijisemea moyoni: ‘Nitakuwa malkia milele’,
nawe hukuyatafakari mambo yanayotokea,
wala kufikiri mwisho wake.
8 47:8-9 Taz Ufu 18:7-8 “Sasa, basi, sikiliza ewe mpenda anasa,
wewe unayedhani kuwa u salama,
na kujisemea: ‘Ni mimi tu,
na hakuna mwingine isipokuwa mimi.
Kamwe sitakuwa mjane,
wala sitafiwa na wanangu.’
9Haya yote mawili yatakupata,
ghafla, katika siku moja:
Kupoteza watoto wako na kuwa mjane,
ijapokuwa una wingi wa uchawi wako,
na nguvu nyingi za uganga wako.
10“Ulijiona salama katika uovu wako;
ukajisemea, ‘Hakuna mtu anayeniona.’
Hekima na elimu yako vilikupotosha,
ukajisemea moyoni mwako, ‘Mimi ndiye;
hakuna mwingine anayenishinda.’
11Lakini maafa yatakupata
ambayo hutaweza kujiepusha nayo.
Balaa litakukumba
ambalo hutaweza kulipinga;
maangamizi yatakujia ghafla
ambayo hujapata kamwe kuyaona.
12Endelea basi na uganga wako,
tegemea wingi wa uchawi wako.
Wewe uliyapania hayo tangu ujana wako
ukitumainia kwamba utafanikiwa
au kusababisha kitisho kwa watu!
13Wewe umejichosha bure na washauri wako.
Basi, na wajitokeze hao wanajimu wakuokoe!
Wao huzigawa mbingu sehemusehemu,
huzichunguza nyota
na kubashiri kila mwezi yatakayokupata.
14“Kumbuka, wao ni kama mabua makavu:
Moto utayateketezea mbali!
Hawawezi hata kujiokoa wenyewe
mbali na ukali wa moto huo.
Moto huo si wa kujipatia joto,
huo si moto wa kuota!
15Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo,
hao uliojishughulisha nao tangu ujana wako.
Watatangatanga kila mmoja njia yake;
hakuna hata mmoja atakayeweza kukuokoa.”


Isaya47;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 1 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 46....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Malaika wa Mwenyezi-Mungu aliondoka Gilgali, akaenda Bokimu, akawaambia Waisraeli, “Niliwatoa nchini Misri na kuwaleta katika nchi ambayo niliwaahidi kwa kiapo babu zenu. Nilisema kwamba sitalivunja agano langu nanyi kamwe. Na kwa upande wenu niliwaamuru msifanye agano na wenyeji wa nchi hii na kwamba madhabahu zao mtazibomoa. Lakini nyinyi hamkuitii amri yangu. Kwa nini mambo haya?
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwa hiyo sasa nasema: Sitawafukuza tena wakazi wa nchi hii bali watawataabisha, nayo miungu yao itakuwa mtego kwenu.” Malaika wa Mwenyezi-Mungu alipowaambia watu wote wa Israeli maneno haya, walipaza sauti zao na kulia. Wakapaita mahali hapo Bokimu. Hapo wakamtolea sadaka Mwenyezi-Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Baada ya Yoshua kuwaaga Waisraeli, kila mmoja alikwenda kwenye eneo lake alilogawiwa ili kuimiliki nchi. Waisraeli walimtumikia Mwenyezi-Mungu siku zote za maisha ya Yoshua na baada ya kifo chake muda wote walioishi wale wazee waliosalia ambao waliyaona matendo makuu ambayo Mwenyezi-Mungu aliwatendea Waisraeli.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


1“Wewe Beli umeanguka;
Nebo umeporomoka.
Wakati mmoja watu walibeba sanamu zenu.
Sasa wanazibeba mgongoni mwa wanyama,
hao wanyama wachovu wamelemewa.
2Nyinyi mmeanguka na kuvunjika,
hamwezi kuviokoa vinyago vyenu;
nyinyi wenyewe pia mtapelekwa uhamishoni!
3“Sikilizeni enyi wazawa wa Yakobo,
nisikilizeni enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli.
Mimi niliwatunzeni tangu mlipozaliwa;
niliwabebeni tangu tumboni mwa mama yenu.
4Mimi ni yuleyule hata katika uzee wenu;
hata katika uzee wenu mimi nitawabeba.
Nilifanya hivyo kwanza,
nitafanya hivyo tena.
Nitawabeba nyinyi na kuwaokoa.
5“Mtanifananisha na nani, tufanane?
Je, mwaweza kunilinganisha na nani, tulingane?
6Watu humimina dhahabu kutoka mifuko yao,
hupima fedha kwenye mizani zao,
wakamwajiri mfua dhahabu atengeneze sanamu
kisha huisujudu na kuiabudu!
7Hujitwisha sanamu hiyo mabegani, wakaibeba,
kisha huiweka mahali pake, ikakaa papo hapo;
kamwe haiwezi hata kusogea kutoka hapo ilipo.
Mtu akiililia, haiwezi kumwitikia,
wala haiwezi kumwokoa mtu katika taabu zake.
8“Kumbukeni jambo hili na kutafakari,
liwazeni akilini mwenu enyi wakosefu.
9Kumbukeni mambo niliyotenda hapo kale!
Mimi ndimi Mungu na hakuna mwingine;
naam, mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine kama mimi.
10Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo,
tangu kale nilitangaza mambo yatakayotukia.
Lengo langu litatimia;
mimi nitatekeleza nia yangu yote.
11Ninamwita tai wangu kutoka mashariki,
naam, msiri wangu kutoka nchi ya mbali.
Mimi nimenena na nitayafanya;
mimi nimepanga nami nitatekeleza.
12“Nisikilizeni, enyi wenye vichwa vigumu,
nisikilizeni enyi mlio mbali na ukombozi.
13Siku ya kuwakomboa naileta karibu,
haiko mbali tena;
siku ya kuwaokoeni haitachelewa.
Nitauokoa mji wa Siyoni,
kwa ajili ya Israeli, fahari yangu.

Isaya46;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.