Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 12 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 53....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, mkuu wa jeshi aliwaita askari wawili akawaambia, “Wekeni tayari askari 200, wapandafarasi sabini na askari 200 wa mikuki, waende Kaisarea; muwe tayari kuondoka kabla ya saa tatu leo usiku. Wekeni farasi kadhaa kwa ajili ya Paulo; mfikisheni salama kwa Felisi, mkuu wa mkoa.” Halafu mkuu huyo wa jeshi akaandika barua hivi:
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

“Mimi Klaudio Lusia ninakuandikia wewe Mheshimiwa Felisi, mkuu wa mkoa. Salamu! “Wayahudi walimkamata mtu huyu na karibu wangemuua kama nisingalifahamishwa kwamba yeye ni raia wa Roma na hivyo nikaenda pamoja na askari nikamwokoa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nilimpeleka mbele ya Baraza lao kuu nikitaka kujua kisa cha mashtaka yao. Niligundua kwamba mashtaka yenyewe yalihusu ubishi juu ya sehemu kadha wa kadha za sheria yao na hivyo sikuona kwamba amefanya chochote kinachostahili auawe au afungwe gerezani.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Nani aliyeamini mambo tuliyosikia?
Nani aliyetambua kuwa mkono wa Mwenyezi-Mungu ulihusika?
2Maana, mbele yake Mwenyezi-Mungu,
mtumishi wake alikua kama mti mchanga,
kama mzizi katika nchi kavu.
Hakuwa na umbo wala sura ya kutupendeza,
wala hakuwa na uzuri wowote wa kutuvutia.
3Alidharauliwa na kukataliwa na watu,
alikuwa mtu wa uchungu na huzuni.
Alikuwa kama mtu kinyaa kwa watu;
alidharauliwa na tukamwona si kitu.
4 53:4 Taz Mat 8:17 Hata hivyo alivumilia majonzi yetu,
na kubeba huzuni zetu.
Sisi tulifikiri amepata adhabu,
amepigwa na Mungu na kuteswa.
5 53:5 Taz 1Pet 2:24 Lakini alijeruhiwa kwa sababu ya dhambi zetu,
aliumizwa kwa sababu ya maovu yetu.
Kwa kuadhibiwa kwake sisi tumepata uhai;
kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
6 53:6 Taz 1Pet 2:25 Sisi sote tumepotea kama kondoo,
kila mmoja wetu ameelekea njia yake.
Lakini Mwenyezi-Mungu alimtwika adhabu,
ambayo sisi wenyewe tuliistahili.
7 53:7 Taz Ufu 5:6 Alidhulumiwa na kuteswa,
lakini alivumilia kwa unyenyekevu,
bila kutoa sauti hata kidogo.
Alikuwa kama mwanakondoo apelekwaye machinjoni,
kama kondoo akaavyo kimya anapokatwa manyoya.
Hakutoa sauti hata kidogo. 53:7-8 Taz Mate 8:32-33
8Alidhulumiwa, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa;
na hakuna mtu aliyejali yanayompata.
Alifukuzwa kutoka nchi ya walio hai,
kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
9 53:9 Taz 1Pet 2:22 Walimzika pamoja na wahalifu;
katika kifo aliwekwa pamoja na matajiri,
ingawa hakutenda ukatili wowote,
wala hakusema neno lolote la udanganyifu.
10Mwenyezi-Mungu alipenda kumwumiza
na kumweka katika huzuni.
Alijitoa mhanga kwa ajili ya kuondoa dhambi.
Mtumishi wa Mungu atakuwa na wazawa;
ataishi maisha marefu.
Yeye ndiye atakayetimiza mpango wa Mwenyezi-Mungu.
11Mungu asema:
“Baada ya kutaabika sana,
mtumishi wangu atafurahi.
Kwa kuwajibika kwake kikamilifu,
atatosheka na matokeo hayo.
Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwadilifu
atawafanya wengi wawe waadilifu
Yeye atazibeba dhambi zao.53:11 atazibeba dhambi zao: Yaani kwa mateso yake adhabu ya dhambi ambayo watu walistahili imempata yeye nao watu wakasamehewa.
12Kwa hiyo, nitamweka katika cheo cha wakuu,
atagawa nyara pamoja na wenye nguvu;
kwa kuwa alijitolea mwenyewe kufa,
akawekwa katika kundi moja na wakosefu,
alizibeba dhambi za watu wengi,
akawaombea msamaha hao wakosefu.”



Isaya53;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 11 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 52....




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki
Nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Askari akamchukua huyo kijana, akamwongoza mpaka kwa mkuu wa jeshi, akasema, “Yule mfungwa Paulo ameniita akaniomba nimlete kijana huyu kwako kwa maana ana jambo la kukuambia.” Mkuu wa jeshi alimshika huyo kijana mkono, akampeleka mahali pa faragha, akamwuliza, “Una nini cha kuniambia?”
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Yeye akasema, “Wayahudi wamepatana wakuombe umpeleke Paulo Barazani wakijisingizia kwamba Baraza lingependa kupata habari kamili zaidi juu yake. Lakini wewe usikubali kwa maana kuna watu zaidi ya arubaini walio tayari kumvamia. Wameapa kutokula wala kunywa kitu mpaka watakapokuwa wamemuua. Sasa wako tayari, wanangojea tu uamuzi wako.”
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mkuu wa jeshi alimwacha aende zake akimwonya asimwambie mtu yeyote kwamba amemletea habari hizo.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Mungu ataikomboa Yerusalemu
1Amka! Amka!
Jipe nguvu zako ewe mji wa Siyoni!
Jivike mavazi yako mazuri,
ewe Yerusalemu, mji mtakatifu.
Maana hawataingia tena kwako
watu wasiotahiriwa na walio najisi.
2Jikungute mavumbi, uinuke
ewe Yerusalemu uliyetekwa nyara!
Jifungue minyororo yako shingoni,
ewe binti Siyoni uliyechukuliwa mateka.
3Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Nyinyi mliuzwa utumwani bila malipo yoyote, na mtakombolewa bila kulipa hata senti moja. 4Tena mwanzoni nyinyi watu wangu mlikimbilia Misri mkakaa huko. Halafu baadaye Waashuru waliwakandamiza bila sababu yoyote.5Katika hali ya sasa napata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa utumwani? Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu laendelea kudharauliwa kila siku. 6Kwa hiyo watu wangu watajua mimi ni nani; siku hiyo watajua kwamba ni mimi ninayesema: Niko!”
7Tazama inavyopendeza
kumwona mjumbe akitokea mlimani,
ambaye anatangaza amani,
ambaye analeta habari njema,
na kutangaza ukombozi!
Anauambia mji wa Siyoni:
“Mungu wako anatawala!”
8Sikiliza sauti ya walinzi wako;
wanaimba pamoja kwa furaha,
maana wanaona kwa macho yao wenyewe,
kurudi kwa Mwenyezi-Mungu mjini Siyoni.
9Pazeni sauti za shangwe, enyi magofu ya Yerusalemu!
Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,
ameukomboa mji wa Yerusalemu.
10Mwenyezi-Mungu ameonesha nguvu yake tukufu,
mbele ya mataifa yote.
Atawaokoa watu wake,
na ulimwengu wote utashuhudia.
11Ondokeni! Ondokeni! Tokeni hapa;
msiguse kitu chochote najisi!
Ondokeni huku Babuloni!
Jitakaseni enyi mbebao vyombo vya Mwenyezi-Mungu.
12Safari hii hamtatoka kwa haraka,
wala hamtaondoka mbiombio!
Maana Mwenyezi-Mungu atawatangulieni,
Mungu wa Israeli atawalinda kutoka nyuma.
Mtumishi wa Mwenyezi-Mungu
13Mungu asema hivi:
“Mtumishi wangu atafanikiwa;
atatukuzwa na kupewa cheo,
atapata heshima kuu.
14Wengi waliomwona walishtuka,
kwa vile sura yake ilikuwa imeharibiwa;
hakuwa tena na umbo la kibinadamu!
15Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi.
Wafalme wanaduwaa kwa sababu yake,
maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa,
na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.”


Isaya52;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 8 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 51....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kulipokucha, Wayahudi walifanya kikao cha faragha. Wakala kiapo: “Hatutakula wala kunywa mpaka tutakapokuwa tumekwisha muua Paulo.” Watu zaidi ya arubaini ndio waliokula njama kufanya hivyo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, walikwenda kwa makuhani wakuu na wazee, wakasema, “Sisi tumekula kiapo kwamba hatutaonja chochote kwa vinywa vyetu mpaka hapo tutakapokuwa tumemuua Paulo. Sasa basi, nyinyi pamoja na Baraza tumeni ujumbe kwa mkuu wa jeshi ili amlete Paulo kwenu mkijisingizia kwamba mnataka kupata habari kamili zaidi juu yake. Tuko tayari kumwua hata kabla hajafika karibu.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Lakini mtoto wa ndugu yake Paulo alisikia juu ya mpango huo; hivyo akaenda ndani ya ngome, akamjulisha Paulo juu ya njama hiyo. Hapo Paulo akamwita mmoja wa maaskari, akamwambia, “Mchukue kijana huyu kwa mkuu wa jeshi; ana kitu cha kumwambia.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Maneno ya faraja kwa Siyoni
1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nisikilizeni enyi mnaotaka kukombolewa,
nyinyi mnaonitafuta mimi Mwenyezi-Mungu.
Utazameni mwamba mlimochongwa,
chimbo la mawe mlimochimbuliwa.
2Mkumbukeni Abrahamu babu yenu,
na Sara aliyewazaa nyinyi.
Abrahamu alikuwa hana mtoto wakati nilipomwita,
lakini nilimbariki na kumfanya kuwa na wengi.
3“Mimi Mwenyezi-Mungu nitaufariji mji wa Siyoni,
nitaparekebisha mahali pake pote palipoharibika.
Nyika zake nitazifanya kama bustani ya Edeni,
majangwa yake kama bustani ya Mwenyezi-Mungu.
Kwake kutapatikana furaha na shangwe,
na nyimbo za shukrani zitasikika humo.
4“Nisikilizeni enyi watu wangu,
nitegeeni sikio enyi taifa langu.
Sheria na haki zitatoka kwangu mimi;
nazo zitakuwa mwanga wa mataifa.
5Nitaleta ukombozi hima;
wokovu nitakaoleta waanza kutokea.
Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa.
Wakazi wa nchi za mbali wananingojea,
wanaitegemea nguvu yangu.
6Inueni macho mzitazame mbingu,
kisha tazameni dunia huko chini.
Mbingu zitatoweka kama moshi,
dunia itachakaa kama vazi,
na wakazi wake watakufa kama wadudu.
Lakini wokovu niuletao wadumu milele;
ukombozi wangu kamwe hautakoma.
7“Nisikilizeni enyi mjuao mambo ya haki,
ambao sheria zangu zimo mioyoni mwenu.
Msiogope dharau za watu,
wala kufadhaishwa na masimango yao.
8Maana wataliwa na nondo kama vile vazi;
viwavi watawala kama walavyo nguo ya sufu.
Lakini ukombozi niletao mimi utadumu milele;
wokovu wangu hautakuwa na mwisho.”
9Amka! Amka ee Mwenyezi-Mungu!
Jivike nguvu zako utuokoe.
Amka kama ulivyofanya hapo zamani,
nyakati za vizazi vya hapo kale.
Je, si wewe uliyemkatakata Rahabu,
ukalitumbua dude hilo la kutisha?
10Wewe ndiwe uliyeikausha bahari,
ndiwe uliyevikausha vilindi vya maji,
ukafanya njia katika vilindi vya bahari,
ili wale uliowakomboa wavuke humo.
11Watu wako uliowakomboa, ee Mwenyezi-Mungu, watarudi,
watakuja Siyoni wakiimba;
watajaa furaha ya milele,
watapata furaha na shangwe.
Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.
12Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mimi, naam mimi, ndimi ninayekufariji.
Kwa nini wewe unamwogopa mtu ambaye hufa,
binadamu ambaye hutoweka kama nyasi?
13Wewe umenisahau mimi Mwenyezi-Mungu Muumba wako,
niliyezitandaza mbingu,
na kuiweka misingi ya dunia!
Wewe waendelea kuogopa siku zote,
kwa sababu ya ghadhabu ya mdhalimu wako,
kwamba yuko tayari kukuangamiza!
Lakini hasira yake itafika wapi?
14Wanaodhulumiwa watafunguliwa hima,
hawatakufa na kushuka shimoni,
wala hawatatindikiwa chakula.
15Mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;
nivurugaye bahari, mawimbi yake yakanguruma;
Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ndilo jina langu!
16Nimeyaweka maneno yangu mdomoni mwako;
nimekuficha katika kivuli cha mkono wangu.
Mimi nilizitandaza mbingu,
nikaiweka misingi ya dunia.
Mimi nawaambieni enyi watu wa Siyoni:
‘Nyinyi ni watu wangu.’”
Mwisho wa mateso ya Yerusalemu
17Amka ewe Yerusalemu!
Amka usimame wima!
Mwenyezi-Mungu amekunywesha kikombe cha ghadhabu yake,
nawe umeinywa mpaka tone la mwisho,
mpaka ukayumbayumba.
18Kati ya watoto wote uliowazaa
hakuna yeyote wa kukuongoza.
Hakuna hata mmoja wa kukushika mkono
kati ya watoto wote uliowalea.
19Majanga haya mawili yamekupata:
Uharibifu na maangamizi; njaa na mauaji.
Nani atakayekuonea huruma?
Nani atakayekufariji?
20Watoto wako wamezirai,
wamelala pembeni mwa kila barabara,
wako kama paa aliyenaswa wavuni.
Wamepatwa na ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu,
wamepatwa na adhabu ya Mungu wako.
21Basi, sikiliza ewe Yerusalemu unayeteseka;
sikiliza wewe uliyelewa, lakini sio kwa divai.
22Bwana, Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
awateteaye watu wake, asema hivi:
“Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha,
hutakunywa tena kikombe cha ghadhabu yangu.
23Nitawanywesha watesi wako kikombe hicho
waliokuambia ulale chini wapite juu yako;
wakaufanya mgongo wako kama ardhi,
kama barabara yao ya kupitia.”

Isaya51;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 7 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 50....




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Baada ya kusema hivyo, mzozo mkali ulitokea kati ya Mafarisayo na Masadukayo na mkutano ukagawanyika sehemu mbili. Kisa chenyewe kilikuwa hiki, Masadukayo hushikilia kwamba wafu hawafufuki, hakuna malaika, na roho nazo hazipo. Lakini Mafarisayo husadiki hayo yote matatu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kelele ziliongezeka na baadhi ya waalimu wa sheria wa kikundi cha Mafarisayo walisimama na kutoa malalamiko yao kwa nguvu: “Hatuoni chochote kilicho kiovu katika mtu huyu; huenda ikawa kwamba roho au malaika ameongea naye.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mzozo ulizidi kuwa mwingi hata mkuu wa jeshi akaogopa kwamba Paulo angeraruliwa vipandevipande. Kwa hiyo, aliwaamuru askari wake kuingia kati ya lile kundi, wamtoe Paulo na kumrudisha ndani ya ngome. Usiku uliofuata, Bwana alisimama karibu na Paulo, akamwambia, “Jipe moyo! Umenishuhudia hapa Yerusalemu, utafanya vivyo hivyo mjini Roma.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Kama nimempa talaka mama yako Yerusalemu,
hati ya talaka iko wapi?
Au kama niliwauza utumwani,
yuko wapi basi, huyo niliyemwuzia?
Kumbukeni mliuzwa utumwani kwa maovu yenu,
mama yenu alifukuzwa kwa makosa yenu.
2“Nilipokuja kwa nini sikukuta mtu?
Nilipoita mbona hamkuitikia?
Je, mkono wangu ni mfupi nisiweze kuwaokoeni?
Je, sina nguvu ya kuwakomboa?
Tazama! Kwa kuikemea kidogo bahari hukauka,
na mito nikaifanya kuwa jangwa,
samaki wake wakafa na kunuka kwa kukosa maji.
3Mimi hulivika anga giza,
na kulivalisha vazi la kuomboleza.”
Mtumishi wa Mwenyezi-Mungu
4Bwana Mungu amenipa ufasaha wa lugha,
niwatie moyo wale waliochoka.
Kila asubuhi hunipa hamu
ya kusikiliza anayotaka kunifunza.
5Bwana Mungu amenifanya msikivu,
nami sikuwa mkaidi
wala kugeuka mbali naye.
6 50:6 Taz Mat 26:67; Marko 14:65 Mgongo wangu niliwaachia walionipiga,
mashavu yangu waliozingoa ndevu zangu;
walioniaibisha na kunitemea mate,
sikujificha mbali nao.
7Bwana Mungu hunisaidia,
kwa hiyo siwezi kufadhaika.
Uso wangu nimeukaza kama jiwe;
najua kwamba sitaaibishwa.
8Mtetezi wangu yuko karibu.
Ni nani atakayepingana nami?
Na aje tusimame mahakamani.
Adui yangu ni nani?
Na ajitokeze mbele basi.
9Tazama Bwana Mungu hunisaidia.
Ni nani awezaye kusema nina hatia?
Maadui zangu wote watachakaa kama vazi,
nondo watawatafuna.
10Nani kati yenu amchaye Mwenyezi-Mungu?
Nani anayetii maneno ya mtumishi wake?
Kama yupo atembeaye gizani bila taa,
amtumainie Mwenyezi-Mungu,
na kumtegemea Mungu wake.
11Lakini nyinyi mnaowasha moto,
na kujifanyia silaha za mienge,
tembeeni kwa mwanga wa moto huo,
miali ya moto mliowasha nyinyi wenyewe.
Mtakachopata kutoka kwa Mwenyezi-Mungu ni hiki:
Nyinyi mtalala chini na mateso makali.


Isaya50;1-11

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.