Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 1 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 46....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Malaika wa Mwenyezi-Mungu aliondoka Gilgali, akaenda Bokimu, akawaambia Waisraeli, “Niliwatoa nchini Misri na kuwaleta katika nchi ambayo niliwaahidi kwa kiapo babu zenu. Nilisema kwamba sitalivunja agano langu nanyi kamwe. Na kwa upande wenu niliwaamuru msifanye agano na wenyeji wa nchi hii na kwamba madhabahu zao mtazibomoa. Lakini nyinyi hamkuitii amri yangu. Kwa nini mambo haya?
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwa hiyo sasa nasema: Sitawafukuza tena wakazi wa nchi hii bali watawataabisha, nayo miungu yao itakuwa mtego kwenu.” Malaika wa Mwenyezi-Mungu alipowaambia watu wote wa Israeli maneno haya, walipaza sauti zao na kulia. Wakapaita mahali hapo Bokimu. Hapo wakamtolea sadaka Mwenyezi-Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Baada ya Yoshua kuwaaga Waisraeli, kila mmoja alikwenda kwenye eneo lake alilogawiwa ili kuimiliki nchi. Waisraeli walimtumikia Mwenyezi-Mungu siku zote za maisha ya Yoshua na baada ya kifo chake muda wote walioishi wale wazee waliosalia ambao waliyaona matendo makuu ambayo Mwenyezi-Mungu aliwatendea Waisraeli.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


1“Wewe Beli umeanguka;
Nebo umeporomoka.
Wakati mmoja watu walibeba sanamu zenu.
Sasa wanazibeba mgongoni mwa wanyama,
hao wanyama wachovu wamelemewa.
2Nyinyi mmeanguka na kuvunjika,
hamwezi kuviokoa vinyago vyenu;
nyinyi wenyewe pia mtapelekwa uhamishoni!
3“Sikilizeni enyi wazawa wa Yakobo,
nisikilizeni enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli.
Mimi niliwatunzeni tangu mlipozaliwa;
niliwabebeni tangu tumboni mwa mama yenu.
4Mimi ni yuleyule hata katika uzee wenu;
hata katika uzee wenu mimi nitawabeba.
Nilifanya hivyo kwanza,
nitafanya hivyo tena.
Nitawabeba nyinyi na kuwaokoa.
5“Mtanifananisha na nani, tufanane?
Je, mwaweza kunilinganisha na nani, tulingane?
6Watu humimina dhahabu kutoka mifuko yao,
hupima fedha kwenye mizani zao,
wakamwajiri mfua dhahabu atengeneze sanamu
kisha huisujudu na kuiabudu!
7Hujitwisha sanamu hiyo mabegani, wakaibeba,
kisha huiweka mahali pake, ikakaa papo hapo;
kamwe haiwezi hata kusogea kutoka hapo ilipo.
Mtu akiililia, haiwezi kumwitikia,
wala haiwezi kumwokoa mtu katika taabu zake.
8“Kumbukeni jambo hili na kutafakari,
liwazeni akilini mwenu enyi wakosefu.
9Kumbukeni mambo niliyotenda hapo kale!
Mimi ndimi Mungu na hakuna mwingine;
naam, mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine kama mimi.
10Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo,
tangu kale nilitangaza mambo yatakayotukia.
Lengo langu litatimia;
mimi nitatekeleza nia yangu yote.
11Ninamwita tai wangu kutoka mashariki,
naam, msiri wangu kutoka nchi ya mbali.
Mimi nimenena na nitayafanya;
mimi nimepanga nami nitatekeleza.
12“Nisikilizeni, enyi wenye vichwa vigumu,
nisikilizeni enyi mlio mbali na ukombozi.
13Siku ya kuwakomboa naileta karibu,
haiko mbali tena;
siku ya kuwaokoeni haitachelewa.
Nitauokoa mji wa Siyoni,
kwa ajili ya Israeli, fahari yangu.

Isaya46;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 31 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 45....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Nitatafakari juu ya kazi zako, na kuwaza juu ya matendo yako makuu. Kila ufanyacho ee Mungu, ni kitakatifu. Ni mungu gani aliye mkuu kama Mungu wetu? Wewe ni Mungu unayetenda maajabu; wewe umeyaonesha mataifa uwezo wako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwa mkono wako wa nguvu uliwakomboa watu wako; uliwakomboa wazawa wa Yakobo na Yosefu. Maji yalipokuona, ee Mungu, maji yalipokuona, yaliogopa mno; naam, bahari ilitetemeka hata vilindini. Mawingu yalichuruzika maji, ngurumo zikavuma angani, mishale ya umeme ikaangaza kila upande. Kishindo cha ngurumo yako kilitokea katika kimbunga, umeme wako ukauangaza ulimwengu; dunia ikatikisika na kutetemeka.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Wewe uliweka njia yako juu ya bahari; ulitembea juu ya maji yale mengi, lakini nyayo zako hazikuonekana. Uliwaongoza watu wako kama kondoo, chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mwenyezi-Mungu amteua Koreshi
1Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Koreshi:
“Wewe ni mfalme wangu niliyekuteua;
mimi naitegemeza nguvu yako
ili uyashinde mataifa mbele yako,
na kuzivunja nguvu za wafalme.
Mimi nayafungua malango ya mji mbele yako,
na hakuna lango litakalofungwa.
2Mimi nitakutangulia,
na kuisawazisha milima mbele yako.
Nitaivunjavunja milango ya shaba,
na kuvikatakata vizuizi vyake vya chuma.
3Nitakupa hazina zilizofichwa gizani,
na mali iliyo mahali pa siri,
upate kutambua kwamba mimi ndimi Mwenyezi-Mungu,
Mungu wa Israeli, ninayekuita kwa jina lako.
4Kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo,
naam, kwa ajili ya mteule wangu Israeli,
nimekuita kwa jina lako;
nimekupa jina la heshima ingawa wewe hunijui.
5“Mimi ni Mwenyezi-Mungu, wala hakuna mwingine;
hakuna Mungu mwingine ila mimi.
Ninakuimarisha ingawa wewe hunijui,
6ili watu wote, toka mashariki hadi magharibi,
wajue kwamba hakuna Mungu mwingine ila mimi;
mimi ni Mwenyezi-Mungu na hakuna mwingine.
7Mimi hufanya mwanga na kuumba giza;
huleta fanaka na kusababisha balaa.
Mimi Mwenyezi-Mungu hutenda vitu hivi vyote.
8Enyi mbingu, nyesheni kutoka huko juu,
mawingu na yadondoshe uadilifu;
dunia na ifunuke, ichipushe wokovu,
na kuchanusha uadilifu pia!
Mimi, Mwenyezi-Mungu nimefanya hayo.”
Uwezo mkuu wa Mungu
9Ole wake mtu ashindanaye na Muumba wake,
mtu aliye chombo cha udongo
kushindana na mfinyanzi wake!
Je, udongo humwuliza anayeufinyanga:
“Unatengeneza nini hapa?”
Au kumwambia, “Kazi yako si kamili!”
10Ole wake mtoto amwambiaye baba yake,
“Kwa nini umenizaa?”
Au amwambiaye mama yake,
“Ya nini umenileta duniani?”
11Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli,
Mungu, Muumba wa Israeli asema:
“Je, mwathubutu kuniuliza juu ya watoto wangu,
au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?
12Ni mimi niliyeifanya dunia,
na kuumba binadamu aishiye humo.
Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu,
na jeshi lote la nyota liko kwa amri yangu.
13Ni mimi niliyemwamuru Koreshi kuchukua hatua,
atekeleze matakwa yangu.
Nitazifanikisha njia zake zote;
ataujenga upya mji wangu Yerusalemu,
na kuwapa uhuru watu wangu walio uhamishoni,
bila kutaka malipo wala zawadi.”
Mwenyezi-Mungu wa majeshi amesema.
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Utajiri wa Misri na bidhaa za Kushi,
pamoja na za watu wa Seba, majitu marefu,
zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli,
zote zitakuwa mali yako.
Watu hao watakutumikia wamefungwa minyororo;
watakusujudia na kukiri wakisema:
‘Kwako kuna Mungu wa kweli,
wala hakuna Mungu mwingine ila yeye.’”
15Kweli wewe ni Mungu uliyefichika,
Mungu wa Israeli, Mungu Mwokozi.
16Watengenezaji sanamu wataaibika na kufadhaika,
wote kwa pamoja watavurugika.
17Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Mwenyezi-Mungu,
litapata wokovu wa milele.
Halitaaibishwa wala kufadhaishwa milele.
18Mwenyezi-Mungu, Mungu pekee,
ndiye aliyeiumba dunia,
ndiye aliyeiumba na kuitegemeza.
Hakuiumba iwe ghasia na tupu,
ila aliiumba ikaliwe na viumbe vyake.
Yeye asema sasa:
“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu,
wala hakuna mwingine.
19Mimi sikunena kwa siri,
wala katika nchi yenye giza.
Mimi sikuwaambia wazawa wa Yakobo
wanitafute katika ghasia.
Mimi Mwenyezi-Mungu husema ukweli,
maneno yangu ni ya kuaminika.”
20Enyi watu wa mataifa mliosalia,
kusanyikeni pamoja mje!
Nyinyi mmekosa akili:
Nyinyi mwabeba sanamu za miti
na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.
21Semeni wazi na kutoa hoja zenu;
shaurianeni pamoja!
Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa?
Ni nani aliyetamka mambo haya zamani?
Je, haikuwa mimi Mwenyezi-Mungu?
Hakuna Mungu mwingine ila mimi!
Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi;
hakuna mwingine ila mimi.
22Nigeukieni mimi mpate kuokolewa,
popote mlipo duniani.
Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.
23Mimi nimeapa kwa nafsi yangu,
ninachotamka ni ukweli,
neno langu halitarudi nyuma:
Kila binadamu atanipigia magoti,
kila mtu ataapa uaminifu.
24“Watasema juu yangu,
‘Haki na nguvu viko kwa Mwenyezi-Mungu peke yake.’”
Wote waliomwakia hasira Mwenyezi-Mungu
watamjia yeye na kuaibishwa.
25Lakini wazawa wa Israeli
watapata ushindi kwake Mwenyezi-Mungu na kufurahi.


Isaya45;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 30 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 44....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Namlilia Mungu kwa sauti, kwa sauti namlilia Mungu anisikie. Wakati wa taabu namwomba Bwana; namnyoshea mikono yangu usiku bila kuchoka, lakini sipati faraja yoyote kwa mtu. Ninamfikiria Mungu na kusononeka; ninatafakari na kufa moyo. Wanizuia hata kupata lepe la usingizi, nina mahangaiko hata kusema siwezi.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nafikiria siku za zamani; nakumbuka miaka ya hapo kale. Usiku nawaza na kuwazua moyoni; natafakari na kujiuliza rohoni: “Je, Bwana ametuacha kabisa? Je, hatatuonesha tena hisani yake? Je fadhili zake zimekoma kabisa? Je, hatatimiza tena ahadi zake? Je, Mungu amesahau kuwa na huruma? Je, hasira yake imeuondoa upole wake?”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kisha nikasema, “Kinachonichoma zaidi ni kwamba, Mungu Mkuu hatendi tena kitu kwa ajili yetu!” Nitayakumbuka matendo yako, ee Mwenyezi-Mungu, naam, nitayafikiria maajabu yako ya hapo kale.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mwenyezi-Mungu ndiye Mungu pekee
1“Sikiliza ewe taifa Israeli mtumishi wangu;
sikiliza ewe kizazi cha Yakobo mteule wangu.
2Mimi, Mwenyezi-Mungu Muumba wako,
niliyekufanya tangu tumboni mwa mama yako,
nimekuja kukusaidia wewe.
Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:
Usiogope, ewe taifa la Yakobo, mtumishi wangu,
naam, usiogope ewe Yeshuruni mteule wangu.
3“Nitaimwagilia maji nchi iliyokauka,
na kutiririsha mto katika nchi kame.
Nitawamiminia roho yangu wazawa wako,
nitawamwagia watoto wako baraka yangu.
4Watachipua kama nyasi penye maji mengi,
kama majani kandokando ya vijito.
5“Mmoja atasema: ‘Mimi ni wa Mwenyezi-Mungu’,
mwingine atajiita kwa jina la Yakobo,
mwingine ataandika mkononi mwake, ‘Wa Mwenyezi-Mungu’,
na kujitambulisha kwa jina la Israeli.”
6Mwenyezi-Mungu, Mfalme na Mkombozi wa Israeli,
naam, Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Mimi ni wa kwanza na wa mwisho;
hakuna Mungu mwingine ila mimi.
7Ni nani Mungu aliye kama mimi?
Mwache atangaze na kusema wazi mbele yangu.
Nani alitangaza hapo kale mambo ambayo yatatukia?
Na watuambie yale ambayo bado kutokea.44:7 aya ya 7 Kiebrania si dhahiri.
8Enyi watu wangu, msiogope wala msiwe na hofu,
Je, sikuwaambia tangu zamani mambo yatakayotokea?
Nyinyi ni mashahidi wangu.
Je, yuko Mungu mwingine ila mimi?
Je, kuna mwenye nguvu mwingine?
Huyo simjui!”
Upumbavu wa kuabudu sanamu
9Watu wote wanaotengeneza sanamu za miungu ni bure kabisa; na vitu hivyo wanavyovifurahia haviwafai chochote. Wanaoshuhudia hiyo miungu ya uongo ni vipofu na wajinga. Kwa hiyo hao wataaibishwa! 10Ajabu ya mtu kutengeneza sanamu au kinyago cha mungu ambaye hawezi kumsaidia chochote! 11Hakika wote wanaomheshimu wataaibishwa, tena hao mafundi wa sanamu ni binadamu tu. Basi, wakutane wote, wajitokeze, nao watatishika na kuaibishwa.
12Mfuachuma huchukua madini, akayayeyusha motoni na kufua sanamu. Huigongagonga kwa nyundo ili kuipa umbo kwa mikono yake yenye nguvu. Wakati wote huo yeye huona njaa na kuchoka; huona kiu na nguvu kumwishia. 13Kadhalika naye seremala hupima kipande cha mbao, akakitia alama kwa kalamu yake, kisha kwa vifaa vyake hukichonga na kukipa umbo la binadamu na sura ya kupendeza; kisha akaiweka sanamu hiyo ya mungu mahali pake pa pekee. 14Mtu hukata mti wa mwerezi ili autumie, au huchagua mberoshi au mwaloni. Huuacha ukue kati ya miti ya msituni. Au hupanda mwerezi na mvua huustawisha. 15Sehemu ya mti huo itatumiwa kama kuni; mtu huota moto wake na kuoka mikate yake juu yake. Sehemu nyingine ya mti huohuo, mtu hujichongea sanamu ya mungu, akainakshi, halafu akaiabudu. 16Kisha huchukua kuni zake akaoka nazo moto, akachoma nyama juu yake, akala, akashiba. Halafu hukaa hapo akiota moto na kusema, “Naam! Ama kweli nimepata joto! Huo ndio moto!” 17Sehemu iliyobaki ya mti huohuo, hujichongea sanamu ya mungu, kinyago chake, kisha huisujudia na kuiabudu. Huiomba akisema, “Wewe ni mungu wangu, niokoe!”
18Watu hao hawajui wala hawaelewi kitu chochote. Wamefumbwa macho wasiweze kuona; kadhalika na akili zao wasiweze kufahamu. 19Hakuna awezaye kutafakari; au kuwa na akili na kufikiri na kusema: “Nusu ya mti huo niliwashia moto; tena nikaoka mikate juu ya makaa yake, nikachoma nyama, nikala. Je, sehemu iliyobaki nitatengeneza sanamu ambayo ni chukizo na kukisujudia hicho kipande cha mti?”
20La! Fikira zake zimeambatana na hicho ambacho ni majivu tu! Mtu huyo amepotoka hata hawezi kujiokoa mwenyewe na kusema: “Kweli ninachoshika mkononi ni udanganyifu mtupu!”
Mwenyezi-Mungu, hatawasahau Waisraeli
21Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Ewe taifa la Yakobo kumbuka;
naam, kumbuka ewe Israeli:
Wewe ni mtumishi wangu.
Nilikuumba ili uwe mtumishi wangu,
nami kamwe sitakusahau.
22Nimeyafagilia mbali makosa yako kama wingu,
nimezifanya dhambi zako zitoweke kama ukungu.
Rudi kwangu maana mimi nimekukomboa.”
23Imbeni kwa furaha enyi mbingu,
kwa sababu ya hayo aliyotenda Mwenyezi-Mungu.
Pazeni sauti enyi vilindi vya dunia!
Imbeni kwa furaha enyi milima!
Enyi misitu na miti yote iliyomo, imbeni.
Maana Mwenyezi-Mungu amewakomboa wazawa wa Yakobo,
naye atatukuka katika nchi ya Israeli.
24Mwenyezi-Mungu, Mkombozi wako,
aliyekuumba tangu tumboni mwa mama yako, asema:
“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu niliyeumba vitu vyote.
Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu,
niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!
25 44:25 Taz 1Kor 1:20 Mimi huzivuruga ishara za watabiri waongo
na kuwapumbaza waaguzi.
Mimi huyakanusha maneno ya wenye hekima
na kufanya ujuzi wao kuwa upumbavu.
26Lakini huuthibitisha ujumbe wa mtumishi wangu,
na kukamilisha maaguzi ya wajumbe wangu.
Mimi ndimi niuambiaye mji wa Yerusalemu:
Wewe Yerusalemu, utakaliwa tena na watu.
Na miji ya Yuda:
Nyinyi mtajengeka tena:
Magofu yenu nitayarekebisha tena.
27Mimi ndimi ninayeviamuru vilindi:
Kaukeni.
28Ndimi nimwambiaye Koreshi:
Wewe utawachunga watu kwa niaba yangu.
Wewe utatekeleza mipango yangu yote.
Ndimi ninayesema kuhusu Yerusalemu:
Wewe Yerusalemu utajengwa tena upya;
na juu ya hekalu: Msingi wako utawekwa tena.”

Isaya44;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 29 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 43....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili. Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hakuna anayeweza kukana mambo hayo. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari. Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko. Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali. Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.” Baada ya kusema hayo, aliuvunja mkutano.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu aahidi kuwaokoa watu wake
1Mwenyezi-Mungu aliyewaumba enyi watu wa Yakobo,
yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, asema:
“Msiogope, maana mimi nimewakomboa;
nimewaita kwa jina nanyi ni wangu.
2Mkipita katika mafuriko,
mimi nitakuwa pamoja nanyi;
mkipita katika mito,
haitawashinda nguvu.
Mkitembea katika moto,
hamtaunguzwa;
mwali wa moto hautawaunguza.
3Maana mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,
Mungu Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu.
Nitaitoa nchi ya Misri iwe fidia yenu,
nitaitoa Kushi na Seba ili mwachwe huru.
4Kwa vile mna thamani mbele yangu,
kwa kuwa nimewapa hadhi na kuwapenda,
mimi nawaacha watu kusudi niwapate nyinyi,
nayaachilia mataifa badala ya maisha yenu.
5Msiogope maana mimi nipo pamoja nanyi.
“Nitawarudisha wazawa wenu toka mashariki,
nitawakusanyeni kutoka magharibi.
6Nitaiambia kaskazini, ‘Waache waondoke’,
na kusini, ‘Usiwazuie’!
Warudisheni watu kutoka mbali,
kutoka kila mahali duniani.
7Kila mmoja hujulikana kwa jina langu,
niliwaumba wote na kuwafanya
kwa ajili ya utukufu wangu.”
Israeli ni ushahidi wa Mwenyezi-Mungu
8Waleteni mbele watu hao,
ambao wana macho lakini hawaoni
wana masikio lakini hawasikii!
9Mataifa yote na yakusanyike,
watu wote na wakutane pamoja.
Nani kati ya miungu yao awezaye kutangaza yatakayotukia?
Nani awezaye kutuonesha yanayotukia sasa?
Wawalete mashahidi wao
kuthibitisha kwamba walifanya hivyo.
Waache wasikilize na kusema, “Ilikuwa kweli.”
10Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nyinyi Waisraeli ni mashahidi wangu;
niliwachagua muwe watumishi wangu,
mpate kunijua na kuniamini,
kwamba ndimi peke yangu Mungu.
Kabla yangu hajapata kuwapo mungu mwingine,
wala hatakuwapo mungu mwingine.
11“Mimi peke yangu ndimi Mwenyezi-Mungu,
hakuna mkombozi mwingine ila mimi.
12Nilitangaza yale ambayo yangetukia,
kisha nikaja na kuwakomboa.
Hakuna mungu mwingine aliyewahi kufanya hivyo,
nanyi ni mashahidi wangu.
13Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu daima.
Hakuna awezaye kuiepa nguvu yangu;
hakuna awezaye kupinga ninayofanya.”
Kukombolewa kutoka Babuloni
14Mwenyezi-Mungu, Mkombozi wenu,
Mtakatifu wa Israeli, asema hivi:
“Kwa ajili yenu nitatuma jeshi Babuloni.
Nitayavunjilia mbali malango ya mji wake,
na kelele za hao Wakaldayo zitageuka maombolezo.
15Mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wenu;
Mimi ndimi Muumba wa Israeli, Mfalme wenu.”
16Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wakati mmoja nilifanya barabara baharini
nikaweka njia kati ya mawimbi makubwa.
17Nililipiga jeshi lenye nguvu,
jeshi la magari na farasi wa vita,
askari na mashujaa wa vita.
Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena,
niliwakomesha na kuwazima kama utambi wa taa.
Sasa nasema:
18‘Msiyanganganie mambo yaliyopita,
wala msifikirie vitu vya zamani.
19Tazameni, mimi ninafanya kitu kipya.
Kinafanyika sasa hivi,
nanyi mtaweza kukiona.
Nitafanya njia nyikani,
na kububujisha mito jangwani.
20Wanyama wa porini wataniheshimu,
kina mbweha na kina mbuni,
maana nitaweka maji nyikani,
na kububujisha mito jangwani,
ili kuwanywesha watu wangu wateule,
21watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe,
ili wazitangaze sifa zangu!’
Dhambi ya Israeli
22“Lakini ewe taifa la Yakobo, hukuniabudu mimi;
enyi watu wa Israeli, mlinichoka mimi!
23Hamjaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa,
wala kuniheshimu kwa tambiko zenu.
Nami sikuwalemeza kwa kutaka sadaka,
wala sikuwachosha kwa kuwadai ubani.
24Hamkuninunulia manukato kwa faida yenu,
wala kuniridhisha kwa nyama nono za tambiko.
Badala yake dhambi zenu zimekuwa mzigo kwangu,
mmenichosha kabisa kwa makosa yenu.
25Walakini mimi ndimi niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu,
ndimi niyafutaye makosa kwa ajili yangu mwenyewe,
na wala sitazikumbuka dhambi zenu.
26“Niambie kama mna kisa nami,
njoo tukahojiane;
toeni mashtaka yenu ili tuuone ukweli wenu!
27Babu yenu wa kwanza alitenda dhambi,
wapatanishi wenu waliniasi.
28Kwa hiyo niliwafanya haramu wakuu wa mahali patakatifu
nikawaacha watu wa Yakobo waangamizwe,
naam, nikawaacha Waisraeli watukanwe.”

Isaya43;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.