Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 29 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 43....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili. Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hakuna anayeweza kukana mambo hayo. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari. Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko. Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali. Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.” Baada ya kusema hayo, aliuvunja mkutano.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu aahidi kuwaokoa watu wake
1Mwenyezi-Mungu aliyewaumba enyi watu wa Yakobo,
yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, asema:
“Msiogope, maana mimi nimewakomboa;
nimewaita kwa jina nanyi ni wangu.
2Mkipita katika mafuriko,
mimi nitakuwa pamoja nanyi;
mkipita katika mito,
haitawashinda nguvu.
Mkitembea katika moto,
hamtaunguzwa;
mwali wa moto hautawaunguza.
3Maana mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,
Mungu Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu.
Nitaitoa nchi ya Misri iwe fidia yenu,
nitaitoa Kushi na Seba ili mwachwe huru.
4Kwa vile mna thamani mbele yangu,
kwa kuwa nimewapa hadhi na kuwapenda,
mimi nawaacha watu kusudi niwapate nyinyi,
nayaachilia mataifa badala ya maisha yenu.
5Msiogope maana mimi nipo pamoja nanyi.
“Nitawarudisha wazawa wenu toka mashariki,
nitawakusanyeni kutoka magharibi.
6Nitaiambia kaskazini, ‘Waache waondoke’,
na kusini, ‘Usiwazuie’!
Warudisheni watu kutoka mbali,
kutoka kila mahali duniani.
7Kila mmoja hujulikana kwa jina langu,
niliwaumba wote na kuwafanya
kwa ajili ya utukufu wangu.”
Israeli ni ushahidi wa Mwenyezi-Mungu
8Waleteni mbele watu hao,
ambao wana macho lakini hawaoni
wana masikio lakini hawasikii!
9Mataifa yote na yakusanyike,
watu wote na wakutane pamoja.
Nani kati ya miungu yao awezaye kutangaza yatakayotukia?
Nani awezaye kutuonesha yanayotukia sasa?
Wawalete mashahidi wao
kuthibitisha kwamba walifanya hivyo.
Waache wasikilize na kusema, “Ilikuwa kweli.”
10Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nyinyi Waisraeli ni mashahidi wangu;
niliwachagua muwe watumishi wangu,
mpate kunijua na kuniamini,
kwamba ndimi peke yangu Mungu.
Kabla yangu hajapata kuwapo mungu mwingine,
wala hatakuwapo mungu mwingine.
11“Mimi peke yangu ndimi Mwenyezi-Mungu,
hakuna mkombozi mwingine ila mimi.
12Nilitangaza yale ambayo yangetukia,
kisha nikaja na kuwakomboa.
Hakuna mungu mwingine aliyewahi kufanya hivyo,
nanyi ni mashahidi wangu.
13Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu daima.
Hakuna awezaye kuiepa nguvu yangu;
hakuna awezaye kupinga ninayofanya.”
Kukombolewa kutoka Babuloni
14Mwenyezi-Mungu, Mkombozi wenu,
Mtakatifu wa Israeli, asema hivi:
“Kwa ajili yenu nitatuma jeshi Babuloni.
Nitayavunjilia mbali malango ya mji wake,
na kelele za hao Wakaldayo zitageuka maombolezo.
15Mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wenu;
Mimi ndimi Muumba wa Israeli, Mfalme wenu.”
16Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wakati mmoja nilifanya barabara baharini
nikaweka njia kati ya mawimbi makubwa.
17Nililipiga jeshi lenye nguvu,
jeshi la magari na farasi wa vita,
askari na mashujaa wa vita.
Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena,
niliwakomesha na kuwazima kama utambi wa taa.
Sasa nasema:
18‘Msiyanganganie mambo yaliyopita,
wala msifikirie vitu vya zamani.
19Tazameni, mimi ninafanya kitu kipya.
Kinafanyika sasa hivi,
nanyi mtaweza kukiona.
Nitafanya njia nyikani,
na kububujisha mito jangwani.
20Wanyama wa porini wataniheshimu,
kina mbweha na kina mbuni,
maana nitaweka maji nyikani,
na kububujisha mito jangwani,
ili kuwanywesha watu wangu wateule,
21watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe,
ili wazitangaze sifa zangu!’
Dhambi ya Israeli
22“Lakini ewe taifa la Yakobo, hukuniabudu mimi;
enyi watu wa Israeli, mlinichoka mimi!
23Hamjaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa,
wala kuniheshimu kwa tambiko zenu.
Nami sikuwalemeza kwa kutaka sadaka,
wala sikuwachosha kwa kuwadai ubani.
24Hamkuninunulia manukato kwa faida yenu,
wala kuniridhisha kwa nyama nono za tambiko.
Badala yake dhambi zenu zimekuwa mzigo kwangu,
mmenichosha kabisa kwa makosa yenu.
25Walakini mimi ndimi niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu,
ndimi niyafutaye makosa kwa ajili yangu mwenyewe,
na wala sitazikumbuka dhambi zenu.
26“Niambie kama mna kisa nami,
njoo tukahojiane;
toeni mashtaka yenu ili tuuone ukweli wenu!
27Babu yenu wa kwanza alitenda dhambi,
wapatanishi wenu waliniasi.
28Kwa hiyo niliwafanya haramu wakuu wa mahali patakatifu
nikawaacha watu wa Yakobo waangamizwe,
naam, nikawaacha Waisraeli watukanwe.”

Isaya43;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 28 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 42....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia. Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimpelekea Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao. Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Mtumishi wa Mungu
1“Tazameni mtumishi wangu ninayemtegemeza;
mteule wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye.
Nimeiweka roho yangu juu yake,
naye atayaletea mataifa haki.
2Hatalia wala hatapiga kelele,
wala hatapaza sauti yake barabarani.
3Mwanzi uliochubuka hatauvunja,
utambi ufukao moshi hatauzima;
ataleta haki kwa uaminifu.
4Yeye hatafifia wala kufa moyo,
hata atakapoimarisha haki duniani.
Watu wa mbali wanangojea mwongozo wake.”
Mwanga wa mataifa
5Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungu
aliyeziumba mbingu, akazitandaza kama hema,
yeye aliyeiunda nchi na vyote vilivyomo,
yeye awapaye watu waliomo pumzi,
na kuwajalia uhai wote waishio humo:
6“Mimi Mwenyezi-Mungu nimekuita kutenda haki,
nimekushika mkono na kukulinda.
Kwa njia yako nitaweka ahadi na watu wote,
wewe utakuwa mwanga wa mataifa.
7Utayafumbua macho ya vipofu,
utawatoa wafungwa gerezani,
waliokaa gizani utawaletea uhuru.
8Jina langu mimi ni Mwenyezi-Mungu;
utukufu wangu sitampa mwingine,
wala sifa zangu sanamu za miungu.
9Tazama, mambo niliyotabiri yametukia;
na sasa natangaza mambo mapya,
nakueleza hayo kabla hayajatukia.”
Wimbo wa sifa
10Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya!
Dunia yote iimbe sifa zake:
Bahari na vyote vilivyomo,
nchi za mbali na wakazi wake;
11jangwa na miji yake yote ipaaze sauti,
vijiji vya wakazi wa Kedari vimsifu,
wakazi wa Sela waimbe kwa shangwe;
wapaaze sauti kutoka mlimani juu.
12Wote wakaao nchi za mbali,
na wamtukuze na kumsifu Mwenyezi-Mungu.
13Mwenyezi-Mungu ajitokeza kama shujaa;
kama askari vitani ajikakamua kupigana.
Anapaza sauti kubwa ya vita,
na kujionesha mwenye nguvu dhidi ya maadui zake.
Mungu aahidi kuwasaidia watu wake
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Kwa muda mrefu sasa nimenyamaza,
nimekaa kimya na kujizuia;
lakini sasa nitalia kama mama anayejifungua,
anayetweta pamoja na kuhema.
15Nitaharibu milima na vilima,
na majani yote nitayakausha.
Mito ya maji nitaigeuza kuwa nchi kavu,
na mabwawa ya maji nitayakausha.
16“Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu,
nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui.
Mbele yao giza nitaligeuza kuwa mwanga,
na mahali pa kuparuza patakuwa laini.
Huo ndio mpango wangu wa kufanya,
nami nitautekeleza.
17Wote wanaotegemea sanamu za miungu,
wote wanaoziambia: Nyinyi ni miungu yetu;
watakomeshwa na kuaibishwa.
Waisraeli ni viziwi na vipofu
18“Sikilizeni enyi viziwi!
Tazameni enyi vipofu, mpate kuona!
19Nani aliye kipofu ila mtumishi wangu?
Nani aliye kiziwi kama mjumbe ninayemtuma?
Ni nani aliye kipofu kama huyu niliyemweka wakfu,
au kipofu kama mtumishi wa Mwenyezi-Mungu?
20Nyinyi mmeona mambo mengi,
lakini hamwelewi kitu.
Masikio yenu yako wazi,
lakini hamsikii kitu!”
21Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya uaminifu wake,
alipenda kukuza mwongozo wake na kuutukuza.
22Lakini hawa ni watu walioibiwa mali na kuporwa!
Wote wamenaswa mashimoni,
wamefungwa gerezani.
Wamekuwa kama mawindo bila mtu wa kuwaokoa,
wamekuwa nyara na hakuna asemaye, “Waokolewe!”
23Je, mtatega sikio kusikia kitu hiki?
Nani kati yenu atakayesikiliza vizuri yatakayotukia?
24Ni nani aliyewatia Waisraeli mikononi mwa adui zao?
Nani aliyewaacha wanyanganywe mali zao?
Ni Mwenyezi-Mungu ambaye tumemkosea!
Wazee wetu walikataa kuzifuata njia zake,
wala hawakuzitii amri zake.
25Kwa hiyo aliwamwagia hasira yake kali,
akawaacha wakumbane na vita vikali.
Hasira yake iliwawakia kila upande,
lakini wao hawakuelewa chochote;
iliwachoma, lakini hawakutilia jambo hilo maanani.

Isaya42;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 25 October 2019

Chaguo la Mswahili Leo-Nyimbo za Tenzi





Shukrani;Dinu Zeno


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.


Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 41....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.” Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo njia ya Bwana. Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi wake faida kubwa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii. Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si hapa Efeso tu, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo. Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mungu anaahidi kuisaidia Israeli
1Mungu asema hivi:
“Enyi wakazi wa mbali nyamazeni mnisikilize!
Enyi mataifa jipeni nguvu;
jitokezeni mkatoe hoja zenu,
na tuje pamoja kwa hukumu.
2“Nani, ila mimi, aliyemwita shujaa toka mashariki,
mtu ambaye hupata ushindi popote aendako?
Mimi huyatia mataifa makuchani mwake,
naye huwaponda wafalme chini ya miguu yake!
Upanga wake huwafanya kuwa kama vumbi,
kwa upinde wake huwapeperusha kama makapi.
3Yeye huwafuatia na kupita salama;
huenda kasi kana kwamba hagusi chini.
4Nani aliyefanya yote haya yatendeke?
Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio?
Mimi Mwenyezi-Mungu nipo tangu mwanzo,
mimi nitakuwapo hata milele.
5“Wakazi wa mbali wameona niliyotenda, wakaogopa;
dunia yote inatetemeka kwa hofu.
Watu wote wamekusanyika, wakaja.
6Kila mmoja anamhimiza mwenzake akisema,
‘Haya! Jipe moyo!’
7Fundi anamhimiza mfua dhahabu,
naye alainishaye sanamu kwa nyundo,
anamhimiza anayeiunga kwa misumari.
Wote wanasema, ‘Imeungika vizuri sana!’
Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.
8Sikiliza ewe Israeli, mtumishi wangu,
wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua,
wewe mzawa wa Abrahamu, rafiki yangu;
9wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia,
wewe niliyekuambia: ‘Wewe u mtumishi wangu;
mimi sikukutupa, bali nilikuchagua.’
10Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe.
Usifadhaike, mimi ni Mungu wako.
Nitakuimarisha na kukusaidia;
nitakulinda kwa mkono wangu wa ushindi.
11“Naam! Wote waliokuwakia hasira,
wataaibishwa na kupata fedheha.
Wote wanaopingana nawe,
watakuwa si kitu na kuangamia.
12Utawatafuta hao wanaopingana nawe,
lakini watakuwa wameangamia.
13Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
ndimi ninayetegemeza mkono wako.
Mimi ndimi ninayekuambia:
‘Usiogope, nitakusaidia.’”
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Enyi watu wa Yakobo dhaifu kama mdudu,
enyi Waisraeli, msiogope!
Mimi Mwenyezi-Mungu nasema nitawasaidia.
Mimi ni Mkombozi wenu,
Mtakatifu wa Israeli.
15Nitawafanya muwe kama chombo cha kupuria,
chenye meno mapya na makali.
Mtaipura milima na kuipondaponda;
vilima mtavisagasaga kama makapi.
16Mtaipepeta milima hiyo,
nao upepo utaipeperushia mbali,
naam, dhoruba itaitawanya huko na huko.
Nanyi mtafurahi kwa sababu yangu Mwenyezi-Mungu;
mtaona fahari kwa sababu yangu
Mungu Mtakatifu wa Israeli.
17“Maskini na fukara wakitafuta maji wasipate,
wakiwa wamekauka koo kwa kiu,
mimi Mwenyezi-Mungu nitawajibu;
mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.
18Nitabubujisha mito kwenye milima mikavu,
na chemchemi katika mabonde.
Nitaigeuza nyika kuwa bwawa la maji,
na nchi kame kuwa chemchemi za maji.
19Nitapanda miti huko nyikani:
Mierezi, mikakaya, mijohoro, na mizeituni;
nitaweka huko jangwani:
Miberoshi, mivinje na misonobari.
20Watu wataona jambo hilo,
nao watatambua na kuelewa kwamba
mimi Mwenyezi-Mungu nimetenda hayo,
mimi Mtakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.”
Mwenyezi-Mungu aipuuza miungu ya uongo
21Mwenyezi-Mungu, Mfalme wa Yakobo, asema:
“Enyi miungu ya mataifa,
njoni mtoe hoja zenu!
22Leteni hoja zenu, mtuambie yatakayotukia.
Tuambieni matukio ya kwanza yalikuwa yapi
nasi tutayatafakari moyoni.
Au tutangazieni yajayo,
tujue yatakayokuja.
23Tuambieni yatakayotokea baadaye,
nasi tujue basi kama nyinyi ni miungu.
Fanyeni kitu chochote, chema au kibaya,
ili tutishike na kuogopa.
24Hakika, nyinyi si kitu kabisa.
hamwezi kufanya chochote kile.
Anayechagua kuwaabudu nyinyi ni chukizo.
25“Nimechochea mtu toka kaskazini,
naye amekuja;
naam, nimemchagua mtu toka mashariki,
naye atalitamka jina langu.
Yeye atawakanyaga wafalme kama tope,
kama vile mfinyanzi apondavyo udongo wake.
26Nani aliyebashiri haya tangu mwanzo,
hata sisi tupate kuyatambua?
Nani aliyetangulia kuyatangaza,
ili sasa tuseme, alisema ukweli?
Hakuna hata mmoja wenu aliyeyataja,
wala hakuna aliyesikia maneno yenu.
27Mimi ni yule wa kwanza, niliyetangaza kwa Siyoni,
nikapeleka Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
28Nimeangalia kwa makini sana,
lakini simwoni yeyote yule;
hamna yeyote kati ya hao miungu awezaye kushauri;
nikiuliza hakuna awezaye kunijibu.
29La! Miungu hiyo yote ni udanganyifu,
haiwezi kufanya chochote;
sanamu zao za kusubu ni upuuzi.


Isaya41;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 24 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 40....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu. Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande 50,000 vya fedha. Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Tumaini la kuponywa katika Yerusalemu
1Mungu wenu asema:
“Wafarijini watu wangu,
nendeni mkawafariji.
2Semeni na wenyeji wa Yerusalemu kwa upole,
waambieni kwamba utumwa wao umekwisha,
wamesamehewa uovu wao.
Mwenyezi-Mungu amewaadhibu maradufu
kwa sababu ya dhambi zao zote.”
3Sauti ya mtu anaita jangwani:
“Mtayarishieni Mwenyezi-Mungu njia,
nyosheni barabara kuu kwa ajili ya Mungu wetu.
4Kila bonde litasawazishwa,
kila mlima na kilima vitashushwa;
ardhi isiyo sawa itafanywa sawa,
mahali pa kuparuza patalainishwa.
5Kisha utukufu wa Mwenyezi-Mungu utafunuliwa,
na watu wote pamoja watauona.
Mwenyezi-Mungu mwenyewe ametamka hayo.”
6Sikiliza! Kuna sauti inasema, “Tangaza!”
Nami nikauliza, “Nitangaze nini?”
Naye: “Tangaza: Binadamu wote ni kama majani;
uthabiti wao ni kama ua la shambani.
7Majani hunyauka na ua hufifia,
Mwenyezi-Mungu avumishapo upepo juu yake.
Hakika binadamu ni kama majani.
8Majani hunyauka na ua hufifia,
lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9Nenda juu ya mlima mrefu,
ewe Siyoni, ukatangaze habari njema.
Paza sauti yako kwa nguvu,
ewe Yerusalemu, ukatangaze habari njema.
paza sauti yako bila kuogopa.
Iambie miji ya Yuda:
“Mungu wenu anakuja.”
10Bwana Mungu anakuja na nguvu,
kwa mkono wake anatawala.
Zawadi yake iko pamoja naye,
na tuzo lake analo.
11Atalilisha kundi lake kama mchungaji,
atawakusanya wanakondoo mikononi mwake,
atawabeba kifuani pake,
na kondoo wanyonyeshao atawaongoza polepole.
Mungu wa Israeli hana kifani
12Nani awezaye kupima maji ya bahari kwa konzi yake,
kuzipima mbingu kwa mikono yake?
Nani awezaye kuutia udongo wa dunia kikombeni;
kuipima milima kwa mizani
au vilima kwa kipimo cha uzani?
13 Nani awezaye kuiongoza akili ya Mwenyezi-Mungu,
au kuwa mshauri wake na kumfunza?
14Mwenyezi-Mungu alimtaka nani shauri,
ndipo akapata kuwa mwenye ujuzi?
Nani aliyemfunza njia za haki?
Nani aliyemfundisha maarifa,
na kumwonesha namna ya kuwa na akili?
15Kwake mataifa ni kama tone la maji katika ndoo,
ni kama vumbi juu ya mizani.
Kwake visiwa ni vyepesi kama vumbi laini.
16Kuni zote za Lebanoni
na wanyama wake wote
havitoshi kwa sadaka ya kuteketezwa mbele yake.
17Mataifa yote si kitu mbele yake;
kwake ni vitu duni kabisa na batili.
18Mtamlinganisha Mungu na nini basi,
au ni kitu gani cha kumfananisha naye?
19Je, anafanana na kinyago?
Hicho, fundi hukichonga,
mfua dhahabu akakipaka dhahabu,
na kukitengenezea minyororo ya fedha!
20Au ni sanamu ya mti mgumu?
Hiyo ni ukuni mtu anaochagua,
akamtafuta fundi stadi,
naye akamchongea sanamu imara!
21Je, nyinyi bado hamjui?
Je, hamjapata kusikia?
Je, hamkuambiwa tangu mwanzo?
Je, hamjafahamu mwanzo wa dunia?
22Dunia iliumbwa na huyo aketiye juu ya mbingu;
kutoka huko wakazi wa dunia ni kama panzi!
Yeye amezitandaza mbingu kama pazia,
na kuzikunjua kama hema la kuishi.
23Yeye huwaporomosha wakuu wenye nguvu,
watawala wa dunia huwafanya kuwa si kitu.
24Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota,
hata kabla hawajatoa mizizi kama miti udongoni,
Mwenyezi-Mungu akiwapulizia hunyauka,
kimbunga huwapeperusha kama makapi!
25Mungu Mtakatifu auliza hivi:
“Nani basi, mtakayemlinganisha nami?
Je, kuna mtu aliye kama mimi?”
26Inueni macho yenu juu mbinguni!
Je, ni nani aliyeziumba nyota hizo?
Ni yule aziongozaye kama jeshi lake,
anayeijua idadi yake yote,
aziitaye kila moja kwa jina lake.
Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi,
hakuna hata moja inayokosekana.
27Enyi watu wa Israeli wazawa wa Yakobo,
kwa nini mnalalamika na kusema:
“Mwenyezi-Mungu hatujali sisi!
Mungu wetu hajali haki yetu!”
28Je, nyinyi bado hamjui?
Je, hamjapata kusikia?
Mwenyezi-Mungu ndiye Mungu wa milele;
yeye ndiye Muumba wa kila kitu duniani.
Yeye hafifii kamwe wala kuishiwa nguvu.
Maarifa yake hayachunguziki.
29Yeye huwapa uwezo walio hafifu,
wanyonge huwapa nguvu.
30Hata vijana watafifia na kulegea;
naam, wataanguka kwa uchovu.
31Lakini wote wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu,
watapata nguvu mpya.
Watapanda juu kwa mabawa kama tai;
watakimbia bila kuchoka;
watatembea bila kulegea.


Isaya40;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.