Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 27 September 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 3....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?


Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe ee Mungu wetu....!!




Mose alikusanya jumuiya yote ya Waisraeli, akawaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Mwenyezi-Mungu amewaamuru muyafanye: Kwa siku sita mtafanya kazi zenu; lakini siku ya saba ni Sabato siku ya mapumziko ambayo ni wakfu kwa Mwenyezi-Mungu. Yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima auawe. Msiwashe hata moto katika makao yenu siku ya Sabato.”


Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti 

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....




Mose aliiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo jambo ambalo Mwenyezi-Mungu amewaamuru mlifanye: Mtatoa katika mali zenu mchango wa kumpa Mwenyezi-Mungu. Kila mtu mwenye moyo mwema atamletea Mwenyezi-Mungu mchango: Dhahabu, fedha, shaba; sufu ya buluu, ya zambarau na nyekundu; kitani safi iliyosokotwa; manyoya ya mbuzi; ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi; mbao za mjohoro, mafuta kwa ajili ya taa, viungo kwa ajili ya mafuta ya kupaka na kwa ajili ya ubani wenye harufu nzuri; vito vya sardoniki na vito vingine kwa ajili ya mapambo ya kizibao na kifuko cha kifuani.



Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...




“Kila mtu mwenye ujuzi wa kazi fulani miongoni mwenu atakuja kufanya vitu vyote alivyoamuru Mwenyezi-Mungu: Kutengeneza hema takatifu, kifuniko chake na pazia lake, kulabu zake, pau zake, vikalio vyake; sanduku la agano pamoja na mipiko yake, kiti cha rehema, pazia la mahali patakatifu sana; meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate iliyowekwa mbele ya Mwenyezi-Mungu; vinara vya taa pamoja na vyombo vyake vyote, taa zake na mafuta yake; madhabahu ya ubani na mipiko yake, mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri, pazia la mlango wa hema takatifu; madhabahu ya sadaka za kuteketezwa pamoja na wavu wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, birika na tako lake; vyandarua vya ua, nguzo zake na vikalio vyake, pazia la mlango wa ua; vigingi vya hema takatifu na vya ua pamoja na kamba zake; mavazi yaliyofumwa vizuri kabisa kwa ajili ya huduma ya mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na ya wanawe, kwa ajili ya huduma yao ya ukuhani.”


Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


MAJADILIANO YA YOBU NA RAFIKI ZAKE

Yobu analalamika

1 Taz Yer 20:14-18 Hatimaye Yobu aliamua kuongea, akailaani siku aliyozaliwa. 2Yobu akasema:
3 Taz Sir 23:14 “Ilaaniwe siku ile niliyozaliwa;
usiku ule iliposemwa, ‘Mwana amechukuliwa mimba’
4Siku hiyo na iwe giza!
Mungu juu asijishughulishe nayo!
Wala nuru yoyote isiiangaze!
5Mauzauza na giza nene yaikumbe,
mawingu mazito yaifunike.
Giza la mchana liitishe!
6Usiku huo giza nene liukumbe!
Usihesabiwe katika siku za mwaka,
wala usitiwe katika idadi ya siku za mwezi.
7Naam, usiku huo uwe tasa,
sauti ya furaha isiingie humo.
8Walozi wa siku waulaani,
watu stadi wa kuligutua dude Lewiyathani waulaani!
9Nyota zake za pambazuko zififie,
utamani kupata mwanga, lakini usipate,
wala usione nuru ya pambazuko.
10Maana usiku huo haukulifunga tumbo la mama,
wala kuficha taabu nisizione.
11Mbona sikufa nilipozaliwa,
nikatoka tumboni na kutoweka?
12Kwa nini mama yangu alinizaa?
Kwa nini nikapata kunyonya?
13Maana ningekuwa nimezikwa, kimya;
ningekuwa nimelazwa na kupumzika,
14pamoja na wafalme na watawala wa dunia,
waliojijengea upya magofu yao;
15ningekuwa pamoja na wakuu waliokuwa na dhahabu,
waliojaza nyumba zao fedha tele.
16Au, mbona sikuwa kama mimba iliyoharibika,
naam, kama mtoto aliyezaliwa mfu?
17Huko kwa wafu waovu hawamsumbui mtu,
huko wachovu hupumzika.
18Huko wafungwa hustarehe pamoja,
hawaisikii kamwe sauti ya mnyapara.
19Wakubwa na wadogo wako huko,
nao watumwa wamepata uhuru mbali na bwana zao.
20Ya nini kumjalia nuru yule aliye taabuni;
na uhai yule aliye na huzuni moyoni?
21Mtu atamaniye kifo lakini hafi;
hutafuta kifo kuliko hazina iliyofichika.
22Mtu kama huyo atashangilia mno na kufurahi,
atafurahi atakapokufa na kuzikwa!
23Ya nini kumjalia uhai mtu ambaye njia zake zimefungwa,
mtu ambaye Mungu amemwekea kizuizi?
24Kwa maana kusononeka ndio mkate wangu,
kupiga kite kwangu kunatiririka mithili ya maji.
25Kile ninachokiogopa kimenipata,
ninachokihofia ndicho kilichonikumba.
26Sina amani wala utulivu;
sipumziki, taabu imenijia.”



Yobu3;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

1 comment:

Anonymous said...

Thanks for sharing such a good thinking, post is good, thats why
i have read it entirely