Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 31 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 16...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tusalimiane na kukumbushana wema wa Mungu na fadhili zake..

Jee unamkumbuka Ndugu yako katika Kristo katika lipi?
kwa wema wake?kujitoa katika kazi ya Mungu /kanisa?
kujitoa kwa wapendwa wengine ndani na nje ya kanisa?
Hekima,Busara,uvumilivu,upatanishi,uongozi bora,Upendo,ucheshi,
unyenyekevu,amani,ukweli,uimbaji wake? na vingine vingi unaweza kusema ambavyo mimi sikuviweka...

Jee asipokuwepo kunakuwa na pengo,upweke,kupwaya na kuhisi
kunaupungufu kidogo?

Au unamkumbuka Ndugu yako katika Kristo kwa baya lipi?
Makwazo,ugombanishi,uongo,uzushi,ukorofi,kisirani,unafiki?na vingine
vingi unavyoona vibaya ambavyo mimi sikuviweka wewe unaviju..

Jee umechukua hatua gani? Umemsifia kwa mema/mazuri
 anayoyafanya na kumuombea aendelee kusimamia hayo na
Mungu aendelee kumuongoza katika yote yampendezayo?

Jee kwa mabaya pia umechukua hatua gani?
Au unaendeleza nawe ubaya na kusengenya pembeni?
Umejaribu kumshauri hiyo njia siyo?na kumuonya/kumuelisha
kwa upendo,hekima na busara?

Jee unampenda?au unamdanganya na unajidanganya mwenyewe
kwa sababu upendo wa kweli ni kumwambia ukweli naye anaweza
kujirudi hata kama kwa wakati ule alihamaki lakini atajifikiria
na kuchukua hatua....

Ebu tujaribu leo kwa watu 2 wa karibu yako iwe kwa mazuri yao
au mabaya yao,unaweza kufikiri kwamba alikuwa anatenda
vibaya kwa jambo unaloliona wewe lakini kumbe anasababu na anaweza
kukupa sababu ya kufanya hivyo..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote tunayoenda kufanya/kutenda,
kunena na tukanene yaliyo yake..
Mungu ni pendo apenda watu...
Nakupenda..
Tuendelee...

Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea. Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia. Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu. Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine. Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni wa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo. Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu. Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi. Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana. Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku. Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo. Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana. Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana. Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia. Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao. Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao. Salimianeni nyinyi kwa nyinyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
Tumshukuru Mungu wetu kwa wema na fadhili zake kwetu..
Asante Baba wa Mbinguni kwa ulinzi wako wakati wote..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea
kuina leo hii..Si kwamba sisi tumetenda mema sana,wala si kwa
nguvu/utashi wetu sisi kuwa hivi tulivyo ni kwa neema/rehema
zako Mungu wetu ni kwa mapenzi yako...

Ukuu ni wako, ee Mwenyezi-Mungu, una nguvu, utukufu, ushindi na enzi. Vyote vilivyoko mbinguni na duniani ni vyako. Ee Mwenyezi-Mungu, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, u mkuu juu ya vitu vyote. Utajiri na heshima hutoka kwako, vyote wavitawala. Uwezo na nguvu vimo mkononi mwako, nawe wawakuza uwapendao, na huwaimarisha wote. Sasa ee Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu jina lako tukufu.

Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachlia mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Yahweh tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea..
Jehovah tunaomba utuepushe katika majaribu Baba utuokoe
na yule mwovu na kazi zake zote..
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Jehovah 
utufunikekwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Ndugu zangu, nawasihi mwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao, maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu. Kila mtu amesikia juu ya utii wenu katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya. Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipateri, wananchi wenzangu, wanawasalimu. Nami Tertio, ninayeandika barua hii, nawasalimuni kwa jina la Bwana. Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu. [ Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.]
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
vyote tunavyoenda kufanya/kutenda Yahweh tukatende
kama inavyo kupendeza wewe..
Jehovah tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji..
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu Mungu wetu ukatupe
sawasawa na mapenzi yako..

Mfalme wa Amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na
wote wanaotuzunguka Yahweh tunaomba ulinzi wako,
Baba tunaomba ukatamalaki na kutuatamia,ukatubariki,
Baba wa Mbinguni tukawe na kiu/shauku ya kujua/kufuata njia zako,
 kusoma Neno lako na likawe taa na Nuru kwenye maisha yetu
Ukatupe neema ya kusimamia Neno lako amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu..
Tukawe barua njema na tukasomeke kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote tukawe na kiasi...
Ee Baba ukasikie kuomba kwetu na ukapokee maombi/sala zetu..

Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita. Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirishwa kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii. Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina.

Tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wenye njaa,walio
katika vifungo mbalimbali,wanaopitia magumu/majaribu,
waliokata tamaa Baba wa Mbinguni ukawape tumaini
Yahweh ukawape neema ya kujiombea,kusimamia njia zako
ukawaguse na mkono wako wenye nguvu Yahweh wakapate
kupona kimwili na kiroho pia,ukawape ubunifu katika kazi,kilimo,
biashara na ukawatendee sawasawa na mapenzi yako..
Sifa na utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!

Wapendwa katika Bwana asanteni kwakuwa pamoja nami
Mungu wa Upendo akadumu katika maisha yenu...
aendelee kuwabariki nanyi mkawe baraka kwa wengine..
Nawapenda.

Nchi ya Efraimu na ya Manase

1Sehemu waliyogawiwa wazawa wa Yosefu kwa kura ilianzia karibu na mto Yordani, mashariki ya chemchemi ya Yeriko, na kupitia jangwani, hadi kwenye sehemu za milima mpaka Betheli. 2Kutoka Betheli mpaka ulielekea Luzu ukapita Atarothi ambako waliishi Waarki. 3Kisha ukashuka magharibi katika nchi ya Wayafleti hadi Beth-horoni ya Chini na Gezeri na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. 4Wazawa wa Yosefu, yaani kabila la Manase na kabila la Efraimu, walipewa nchi hiyo kuwa milki yao.

Nchi ya kabila la Efraimu

5Watu wa kabila la Efraimu kulingana na jamaa zao walipata sehemu yao ambayo mpaka wake upande wa mashariki ulipita Ataroth-adari hadi Beth-horoni ya Juu, 6na kuishia bahari ya Mediteranea. Kwa upande wa kaskazini mpaka ulipita Mikmethathi na kwa mashariki yake ulizunguka na kuelekea Taanath-shilo ambako ulipita upande wa mashariki hadi Yanoa. 7Kutoka Yanoa ulikwenda hadi Atarothi na Naara, hata kufika Yeriko, ambako uliishia katika mto Yordani. 8Kutoka Tapua, mpaka ulikwenda magharibi hadi kijito cha Kana na kuishia bahari ya Mediteranea. Hii ndiyo nchi waliyopewa watu wa kabila la Efraimu kulingana na jamaa zao, 9pamoja na miji na vijiji ambavyo waliongezewa kutoka kwenye nchi ya kabila la Manase. 10Taz Amu 1:29 Waefraimu hawakuwafukuza Wakanaani walioishi Gezeri. Wakanaani hao waliendelea kukaa miongoni mwa watu wa Efraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.


Yoshua 16;1-10

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: