Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 30 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 15...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Ni wiki/siku nyingine tena Mungu wetu ametuchagua na
ametupa kibali chakuendelea kuona leo hii..
Tumshukuru Mungu wetu kwa wema na fadhili zake kwetu..

Asante Mungu wetu kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kutuamsha salama na tukiwa
tayari kwa majukumu yetu..

Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu,Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu juu
ya Mbinguni,Utukufu  wako uenee duniani kote..
Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu utufundishe masharti yako..
Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu kwasababu ya nguvu yako!
Tutaimba na kuusifu uwezo wako..
Sio sisi, ee Mwenyezi-Mungu ,Sio sisi, bali wewe peke yako Utukuzwe,
Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako..
Utukuzwe milele na milele ee Mwenyezi-Mungu Mungu wa Abrahamu,
Isaka na Yakobo,Baba yetu,Muumba wetu,Unatosha Baba wa Mbinguni..


Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, tangazeni ukuu wake; yajulisheni mataifa mambo aliyotenda! Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa; simulieni matendo yake ya ajabu! Jisifieni jina lake takatifu; wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi. Tafuteni msaada kwa Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu; mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima. Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda, miujiza yake na hukumu alizotoa, enyi wazawa wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake; Yeye ndiye Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu; hukumu zake zina nguvu duniani kote. Yeye hulishika agano lake milele, hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu. Hushika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka. Alimthibitishia Yakobo ahadi yake, alimhakikishia Israeli agano hilo la milele. Alisema: “Nitawapeni nchi ya Kanaani, nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”
Sifa na utukufu tunakurudishia wewe ee Mungu wetu..

Tazama jana imepita Mungu wetu Leo ni siku mpya Jehovah na
 kesho ni siku nyingine Yahweh..!
Tunakuja mbele zako tukijinyeyekeza,tukijishusha na kujiachilia
mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Yahweh tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Jehovah nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wote
waliotukosea..
Baba wa Mbimnguni tunaomba utuepushe katika majaribu Yahweh
utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..

Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali.” Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko. Hapo akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.” Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe.” Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Ndio kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho inataka lakini mwili ni dhaifu.” Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kipite bila mimi kukinywa, basi, utakalo lifanyike.” Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale. Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi. Amkeni; twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”

Mungu wetu tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Jehovah
tunaomba utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na
 Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu na vyote
tunavyoenda kufanya kutenda Mungu wetu tukatende kama inavyokupendeza wewe..
BABA tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo Yahweh
nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Jehovah tunaomba tusipungukiwe katika mahitaji yetu,Yahweh
ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Mungu wetu tuyaweka maisha yetu mikononi mwako..
Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba/ndoa zetu, watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote
wanaotuzunguka...
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia,Baba tunamba ulinzi wako
Yahweh tunaomba utupe neema ya hekima,busara,utu wema na fadhili..
Jehovah utupe neema ya kusimamia Neno lako Amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu..
Ukatufanye chombo chema Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..

Ee Bwana, tangu vizazi vyote, wewe umekuwa usalama wetu. Kabla ya kuwapo milima, kabla hujauumba ulimwengu; wewe ndiwe Mungu, milele na milele. Wamwambia binadamu, “Rudi mavumbini!” Naye binadamu hurudi mavumbini alimotoka! Kwako miaka elfu ni kama siku moja tu, ni kama jana ambayo imekwisha pita; kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku! Wawafutilia mbali watu kama ndoto! Binadamu ni kama nyasi zinazochipua asubuhi: Asubuhi huchipua na kuchanua, jioni zimekwisha nyauka na kukauka. Hasira yako inatuangamiza; tunatishwa na ghadhabu yako. Maovu yetu umeyaweka mbele yako; dhambi zetu za siri ziko wazi mbele yako. Kwa hasira yako maisha yetu yatoweka, yanaisha kama pumzi. Miaka ya kuishi ni sabini, au tukiwa wenye afya, themanini; lakini yote ni shida na taabu! Siku zapita mbio, nasi twatoweka mara! Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayejali matokeo ya ghadhabu yako? Utufundishe ufupi wa maisha yetu ili tuweze kuwa na hekima. Urudi, ee Mwenyezi-Mungu! Utakasirika hata lini? Utuonee huruma sisi watumishi wako. Utushibishe fadhili zako asubuhi, tushangilie na kufurahi maisha yetu yote. Utujalie sasa miaka mingi ya furaha, kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu. Utuoneshe matendo yako sisi watumishi wako; uwaoneshe wazawa wetu uwezo wako mtukufu. Utufadhili ee Bwana, Mungu wetu; uzitegemeze kazi zetu, uzifanikishe shughuli zetu.
Baba tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
na ukawape uponyaji wa mwili na roho wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,wagonjwa,walio katika
vifungo vya yule mwovu Yahweh tunaomba ukawafungue na wakawe
huru,Baba tazama wenye njaa tunaomba ukawatendee katika
mapito yao,ukabariki mashamba yao,kazi zao,biashara na ukawape
ubunifu katika utendaji wao..Baba ukawape neema ya kujiombea
na kufuata njia zako,Nuru yako ikaangaze katika maisha yao..
Baba ukapokee sala/maombi ya watoto wako wote wanaokuomba
na kukutafuta kwa bidii,Imani/kuamini Mungu wetu mwenye huruma
tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!

Wapendwa/waungwana asanteni sana kwakuwa nami
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea sawasawa
na mapenzi yake..
sina neno zuri la kusema zaidi yakusema..
Nawapenda.

Eneo walilopewa watu wa Yuda

1Eneo la nchi waliyopewa kwa kura watu wa kabila la Yuda kulingana na jamaa zake lilienea tangu kusini-mashariki hadi mpakani mwa Edomu. Sehemu ya kusini kabisa ilikuwa jangwa la Sini. 2Mpaka wao upande wa kusini ulianza pembe ya kusini ya Bahari ya Chumvi, 3ukaendelea kusini hadi mwinuko wa Akrabimu, ukapitia kando ya Sini, na kusini ya Kadesh-barnea, ukipitia Hesroni hadi Adari na kisha ukageuka kuelekea Karka. 4Kutoka hapo ulipita karibu na Asmoni na kufuata kijito cha Misri hadi kufikia kwenye bahari ya Mediteranea. Hapo ndipo ulipopita mpaka wa kusini wa Yuda. 5Mpaka wao wa upande wa mashariki ni Bahari ya Chumvi hadi pale mto Yordani unapoingilia baharini. Na mpaka wao upande wa kaskazini ulipita kutoka pembe ya Bahari ya Chumvi mahali ambapo mto Yordani unaingilia baharini. 6Mpaka huo ukapita Bethi-hogla na kaskazini ya Beth-araba hadi kwenye jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 7Kutoka hapo, uliendelea hadi Debiri kwenye bonde la Akori na kaskazini kuelekea Gilgali, ulio karibu na mwinuko wa Adumimu ambao uko kusini mwa kijito, kisha ukaelekea kwenye chemchemi za En-shemeshi na kuishia En-rogeli. 8Kisha, mpaka huo ulipitia kwenye Bonde la Hinomu, upande wa kusini mwa kilima cha Wayebusi, yaani Yerusalemu, kuelekea kilele cha mlima ulio magharibi ya bonde la Hinomu na kufika mwishoni mwa bonde la Refaimu. 9Kutoka hapo, ulielekea mlimani hadi chemchemi za Neftoa, mpaka kwenye miji ya mlima wa Efroni. Hapo mpaka uligeuka na kuelekea Baala, yaani Kiriath-yearimu, 10ambako ulipinda magharibi kuelekea Mlima Seiri; ukapita kaskazini ya mlima wa Yerimu, yaani Kesaloni, na kuteremka hadi Beth-shemeshi ambapo ulipita karibu na Timna. 11Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekroni, ukazunguka kuelekea Shikroni ambapo ulipita karibu na mlima Baala hadi Yabneeli ukaishia katika bahari ya Mediteranea. 12Mpaka wa magharibi ulikuwa bahari ya Mediteranea. Ndivyo ilivyokuwa mipaka ya eneo walilopewa watu wa kabila la Yuda kulingana na koo zao.

Watu wa Kalebu wanamiliki eneo la Hebroni

13 Taz Amu 1:20 Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya nchi ya Yuda kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriath-arba au mji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Mji huo sasa unaitwa Hebroni. 14Kalebu alizifukuza kutoka mji huo koo tatu za Anaki yaani ukoo wa Sheshai, ukoo wa Ahimani na ukoo wa Talmai. 15Kutoka Hebroni alikwenda kuwashambulia wakazi wa Debiri, mji ambao hapo awali uliitwa Kiriath-seferi. 16Kalebu akatangaza kwamba atamwoza binti yake Aksa kwa mwanamume yeyote atakayeuteka mji wa Kiriath-seferi. 17Basi, Othnieli, mwana wa Kenazi, nduguye Kalebu, akauteka mji huo, naye Kalebu akamwoza bintiye. 18Katika siku yao ya harusi, Aksa alimwambia Othnieli amwombe Kalebu shamba. Aksa alikuwa amepanda punda, na alipokuwa anashuka chini, Kalebu akamwuliza, “Unataka nikupe nini?” 19Aksa akamjibu, “Nipe zawadi; nipe sehemu yenye maji kwa kuwa huko Negebu ulikonipa ni kukavu.” Basi, Kalebu akampa chemchemi za maji zilizokuwa kwenye nyanda za juu na za chini.
20Hii ndiyo nchi waliyopewa watu wa kabila la Yuda kulingana na koo zake. 21Miji iliyokuwa upande wa kusini kabisa wa nchi ya Yuda kuelekea mpaka wa Edomu ilikuwa: Kabseeli, Ederi, Yaguri, 22Kina, Dimona, Adada, 23Kedeshi, Hazori, Ithnani, 24Zifu, Telemu, Bealothi, 25Hazor-hadata, Kerioth-hezroni (yaani Hazori), 26Amamu, Shema, Molada, 27Hasar-gada, Heshmoni, Beth-peleti, 28Hasar-shuali, Beer-sheba, Biziothia, 29Baala, Iyimu, Ezemu, 30Eltoladi, Kesili, Horma, 31Siklagi, Madmana, Sansana, 32Lebaothi, Shilhimu, Aini na Rimoni. Jumla ya miji waliyopewa ni ishirini na tisa pamoja na vijiji vyake.
33Miji iliyokuwa kwenye tambarare ilikuwa: Eshtaoli, Sora, Ashna, 34Zanoa, Enganimu, Tapua, Enamu, 35Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka, 36Shaaraimu, Adithaimu, Gedera na Gederothaimu. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na minne pamoja na vijiji vyake.
37Walipewa pia miji ya Senani, Hadasha, Migdal-gadi, 38Dileani, Mizpa, Yoktheeli, 39Lakishi, Boskathi, Egloni, 40Kaboni, Lahmamu, Kithlishi, 41Gederothi, Beth-dagoni, Naama na Makeda. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake. 42Tena walipewa miji ya Libna, Etheri, Ashani, 43Yifta, Ashna, Nezibu, 44Keila, Akzibu na Maresha. Jumla ya miji waliyopewa ni tisa pamoja na vijiji vyake. 45Vilevile walipewa Ekroni pamoja na miji yake midogo na vijiji, 46miji yote na vijiji vilivyokuwa karibu na Ashdodi kati ya Ekroni na bahari, 47Ashdodi na Gaza pamoja na miji na vijiji vyake, mpaka kijito cha Misri hadi pwani ya bahari ya Mediteranea.
48Miji iliyokuwa kwenye eneo la milimani ni Shamiri, Yatiri, Soko, 49Dana, Kiriath-sana (yaani Debiri), 50Anabu, Eshtemoa, Animu, 51Gosheni, Holoni na Gilo. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na mmoja pamoja na vijiji vyake. 52Walipewa pia miji ya Arabu, Duma, Eshani, 53Yanimu, Beth-tapua, Afeka, 54Humta, Kiriath-arba (yaani Hebroni) na Siori. Jumla ya miji waliyopewa ni tisa pamoja na vijiji vyake. 55Pia walipewa miji ya Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta, 56Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa, 57Kaini, Gibea na Timna. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi pamoja na vijiji vyake. 58Vilevile miji ya Halhuli, Beth-suri, Gedori, 59Maarathi, Beth-anothi na Eltekoni. Jumla ya miji waliyopewa ni sita pamoja na vijiji vyake. 60Kadhalika walipewa Kiriath-baali, uitwao pia Kiriath-yearimu, na Raba. Jumla ya miji waliyopewa ni miwili pamoja na vijiji vyake.
61Miji ya nyikani ilikuwa Beth-araba, Midini, Sekaka, 62Nibshani, Mji wa Chumvi na Engedi. Jumla ya miji waliyopewa ni sita pamoja na vijiji vyake.
63 Taz Amu 1:21; 2Sam 5:6; 1Nya 11:4 Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalemu, na mpaka leo Wayebusi bado wanaishi mjini humo pamoja na watu wa Yuda.


Yoshua 15;1-63

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: