Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 27 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 14...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Asante Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu,Muumba wa Nchi na Mbingu
Asante Mwokozi wetu,Mlinzi wetu,Tunakusifu Mungu wetu,
Tunakuabudu Mungu wetu Mtakatifu,Wewe ni Mungu wetu Milele utakuwa kiongozi wetu,Tukutumikie Mungu wetu na kukutii Mungu wetu,Twakili hakuna mwingine kama wewe Mungu wetu..
Nani aliye Mungu ispokuwa Mungu wetu ?Nani aliye mwamba wa usalama isipokuwa Mungu wetu?
Mungu wetu ndiye Mungu wakutuokoa,Kila ufanyacho ee Mungu nikitakatifu Ni Mungu gani aliye mkuu kama Mungu wetu?
Mwenyezi -Mungu amejaa wema na uaminifu Mungu wetu ni mwenye huruma,Matendeo yako ni makuu sana,Matendo yako ni ya ajabu..
Unatosha Baba wa Mbinguni..!!


“Tazameni mtumishi wangu ninayemtegemeza; mteule wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye atayaletea mataifa haki. Hatalia wala hatapiga kelele, wala hatapaza sauti yake barabarani. Mwanzi uliochubuka hatauvunja, utambi ufukao moshi hatauzima; ataleta haki kwa uaminifu. Yeye hatafifia wala kufa moyo, hata atakapoimarisha haki duniani. Watu wa mbali wanangojea mwongozo wake.”
Asante kwa wema na Fadhili zako wetu..
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea
kuiona leo hii Mungu wetu..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari katika majukumu yetu

Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungu aliyeziumba mbingu, akazitandaza kama hema, yeye aliyeiunda nchi na vyote vilivyomo, yeye awapaye watu waliomo pumzi, na kuwajalia uhai wote waishio humo: “Mimi Mwenyezi-Mungu nimekuita kutenda haki, nimekushika mkono na kukulinda. Kwa njia yako nitaweka ahadi na watu wote, wewe utakuwa mwanga wa mataifa. Utayafumbua macho ya vipofu, utawatoa wafungwa gerezani, waliokaa gizani utawaletea uhuru. Jina langu mimi ni Mwenyezi-Mungu; utukufu wangu sitampa mwingine, wala sifa zangu sanamu za miungu. Tazama, mambo niliyotabiri yametukia; na sasa natangaza mambo mapya, nakueleza hayo kabla hayajatukia.”
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako Yahweh..
Baba wa Mbinguni tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
 tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Jehovah nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea..
Baba wa Mbinguni tunaomba utuepushe katika majaribu na utuokoe
na yule mwovu na kazi zake zote..
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Jehovah
utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..



Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya! Dunia yote iimbe sifa zake: Bahari na vyote vilivyomo, nchi za mbali na wakazi wake; jangwa na miji yake yote ipaaze sauti, vijiji vya wakazi wa Kedari vimsifu, wakazi wa Sela waimbe kwa shangwe; wapaaze sauti kutoka mlimani juu. Wote wakaao nchi za mbali, na wamtukuze na kumsifu Mwenyezi-Mungu. Mwenyezi-Mungu ajitokeza kama shujaa; kama askari vitani ajikakamua kupigana. Anapaza sauti kubwa ya vita, na kujionesha mwenye nguvu dhidi ya maadui zake.
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
vyote tunavyoenda kufanya/kutenda Yahweh tukatende sawasawa na mapezni yako..
Mungu wetu tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Yahweh nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Jehova tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
ukatupe kama inavyokupendeza wewe..

Jehovah tuyakabidhi maisha yetu mikononi mwako,tunaomba
ukabariki nyumba/ndoa zetu watoto,wazazi wetu,familia/ndugu
na wote wanaotuzunguka Mungu wetu tunaomba ulinzi wako
Baba tunaomba amani yako ikatawale,Yahweh tunaomba utupe
neema ya kusimamia Neno lako Amri na sheria zako siku zote
za maisha yetu...
Baba ukatufanye chombo chema nasi tukatumike
kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..




Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Kwa muda mrefu sasa nimenyamaza, nimekaa kimya na kujizuia; lakini sasa nitalia kama mama anayejifungua, anayetweta pamoja na kuhema. Nitaharibu milima na vilima, na majani yote nitayakausha. Mito ya maji nitaigeuza kuwa nchi kavu, na mabwawa ya maji nitayakausha. “Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao giza nitaligeuza kuwa mwanga, na mahali pa kuparuza patakuwa laini. Huo ndio mpango wangu wa kufanya, nami nitautekeleza. Wote wanaotegemea sanamu za miungu, wote wanaoziambia: Nyinyi ni miungu yetu; watakomeshwa na kuaibishwa.
Baba wa Mbinguni tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wenye njaa
wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokatika vifungo vya
yule mwovu na waliokata tamaa na wote walio katika mapito
mbalimbali,Mungu wetu ukawaguse kwa mkono wako wenye
nguvu,ukawape uponyaji wa mwili na roho pia,ukawape neema
ya kukujua wewe,kukutafuta wewe,kufuata njia zako na
wakaweze kujiombea....
  Mungu wetu tunaomba ukapokee sala/maombi
ya watoto wako wanaokutafuta kwa bidii,imani/kuamini..
ee Baba uwainue na kuwapa mwanga kwenye maisha yao..
Asante Baba wa Mbinguni,sifa na utukufu tunakurudishia wewe
Kwakuwa Ufalme ni wako,Nguvu na utukufu hata Milele..
Amina..!
Wapendwa katika Bwana nawatakia kila lililo la kheri
Baraka,Amani na Mungu aendelee kuonekana katika maisha yenu
Nawapenda.



Kugawanywa kwa nchi ya Kanaani

1Yafuatayo ni maeneo ya nchi ambayo walipewa Waisraeli katika nchi ya Kanaani. Kuhani Eleazari na Yoshua, mwana wa Nuni, pamoja na wakuu wa koo za makabila ya Waisraeli waliwagawia Waisraeli. 2Taz Hes 26:52-56; 34:13 Sehemu yao hiyo waligawiwa kwa kura kama vile Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose awape yale makabila tisa na nusu. 3Taz Hes 32:33; 34:14-15; Kumb 3:12-17 Mose alikuwa ameyapa yale makabila mawili na nusu sehemu yao mashariki ya Yordani, lakini Walawi hawakuwa wamepewa sehemu yao pamoja nao. 4Wazawa wa Yosefu walikuwa makabila mawili: Manase na Efraimu. Kabila la Lawi halikupewa sehemu yoyote ya nchi, ila miji tu ya kuishi na sehemu za malisho kwa ajili ya wanyama wao na riziki zao. 5Basi, Waisraeli wakaigawanya nchi kama vile Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose.

Kalebu anapewa mji wa Hebroni

6 Taz Hes 14:30 Siku moja watu wa kabila la Yuda walimwendea Yoshua huko Gilgali. Kalebu mwana wa Yefune, ambaye alikuwa Mkenizi, akamwambia Yoshua, “Bila shaka unakumbuka jinsi Mwenyezi-Mungu alivyomwambia Mose, mtu wa Mungu, juu yangu na wewe tulipokuwa Kadesh-barnea: 7Taz Hes 13:1-30 Nilipokuwa na umri wa miaka arubaini, Mose mtumishi wa Mungu, alinituma kutoka Kadesh-barnea, kwenda kuipeleleza nchi. Niliporudi nilimletea habari za mambo ya huko kadiri nilivyoamini moyoni mwangu, 8hali wale wenzangu waliokwenda pamoja nami waliwavunja watu moyo, lakini mimi nilimfuata Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, kwa uaminifu. 9Taz Hes 14:24 Siku hiyo Mose aliniapia, ‘Hakika sehemu ya nchi ile ambayo ulipita itakuwa yako wewe na wazawa wako milele. Kwa sababu ya uaminifu wako kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wako’. 10Lakini sasa tazama! Ni muda wa miaka arubaini na mitano tangu Mwenyezi-Mungu alipoongea na Mose, wakati Waisraeli walipokuwa wanapitia jangwani. Tangu wakati huo Mwenyezi-Mungu, kama alivyoahidi, amenihifadhi hai mpaka leo, na sasa mimi nina umri wa miaka themanini na mitano. 11Lakini bado nina nguvu kama nilivyokuwa wakati ule Mose aliponituma. Hata sasa nina nguvu za kuweza kupigana vita au kufanya kazi nyingine yoyote. 12Sasa naomba unipe nchi hii ya milima ambayo Mwenyezi-Mungu aliniahidi siku ile. Wewe ulisikia siku ile kwamba Waanaki waliishi humo katika miji yenye ngome; huenda Mwenyezi-Mungu atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza kama Mwenyezi-Mungu alivyosema.”
13Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune na kumpa mji wa Hebroni kuwa sehemu yake. 14Kwa hiyo, mji wa Hebroni ni sehemu yao wazawa wa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi mpaka hivi leo, kwa sababu Kalebu alikuwa mwaminifu kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli. 15Mji wa Hebroni hapo awali uliitwa Kiriath-arba.14:15 Kiriath-arba: Maana yake mji wa Arba. Arba alikuwa mtu maarufu kuliko wote kati ya Waanaki. Nchi nzima ikawa tulivu bila vita.


Yoshua 14;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.


No comments: