Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 11 August 2014

CITE SUMMER CONFERENCE 2014 COVENTRY WEST MIDLANDS UK WITH MWL.MWAKASEGE.[Tujikumbushe Picha za Mkutano na Mchungaji Daniel Kulola,Uliofanyika Coventry]



Picha hizi za chini ni mkutano wa zamani kidogo na Mchungaji Daniel Kulola,Ulifanyika Coventry UK.
Si vibaya tukijikumbusha.....



























Picha kutoka Maktaba ya Swahili Na Waswahili

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 10 August 2014

Muendelee na JumaPili hii kwa Amani na Upendo;Burudani-Franck Mulaja,Alleluya,Nzambe malamu..!!!!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu Jumapili inaendelea vyema;Iwe yenye Imani,Kuomba pasipo kukoma,Uponyaji,Shukrani na kujitoa kwa wenye kuhitaji.

14.Hata walipowafikia wanafunzi, waliona mkutano mkuu wakiwazunguka, na waandishi wakijadiliana nao,15. Mara mkutano wote walipomuona walishangaa, Wakamwendea mbio,wakamsalimu.16.Akawauliza, Mnajadiliana nini nao?

Neno La Leo;Marko Mtakatifu:9:1-50

17.Mtu mmoja katika mkutano akaijibu,Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako,ana pepo bubu;18. Na kila  ampagaapo,humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda;Nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze.19.Akawajibu,akasema,Enyi kizazi kisichoamini,nikae nanyi hata lini?Nichukuliane nanyi hata lini?Mleteni kwangu.20.Wakamleta kwake;hata alipomwona,mara yule pepo alimtia kifafa;naye akaanguka chini,akagaagaa,akitokwa na povu.

21.Akamuuliza babaye,Amepatwa na haya tangu lini?Akasema tangu utoto.22.Na mara nyingi amemtupa katika moto,na katika maji,amwangamize;Lakini ukiweza neno lolote, utuhurumie, na kutusaidia.

23.Yesu akamwambia, Ukiweza!Yote yawezekana kwake aaminie.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Saturday 9 August 2014

Chaguo La Mswahili Leo;Mary Mary - Shackles,Get Up,In The Morning,Shackles,Haven,Go Get It...!!!!!!!!

Waungwana;Chaguo La Mswahili Leo; ni Mary Mary..kitambo kidogo na sasa..zipi zinakubamba/kuzipenda..zamani au sasa au zooote?
Nisikuchoshe..Twende Sote sasa......









>


"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima

Thursday 7 August 2014

Hotuba ya Mhe Rais Uhuru Kenyatta kwa waKenya Washington DC. Aug 6, 2014‏


Mhe. Rais Uhuru Kenyatta akihutubia waKenya jijini Washington Aug 6, 2014
Karibu kusikiliza hotuba ya Mhe. Uhuru Kenyatta alipozungumza na waKenya usiku wa Agosti 6, 2014 kwenye hotel ya Marriott Wardman Park Hotel, jijini Washington DC nchini Marekani.

Mahojiano na mgombea urais wa jumuia DMV, Liberatus Mwang'ombe‏


Karibu katika mahojiano kati ya Kwanza Production na Liberatus Mwang'ombe.
Mgombea uRais wa Jumuiya ya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia
Uchaguzi unategemewa kufanyika Agosti 9, 2014

Wednesday 6 August 2014

Kipindi cha Maswali na Majibu kati ya Rais Kikwete na waTanzania, Washington DC‏


Mhe. Rais Dk Jakaya Kikwete akijibu maswali ya waTanzania
Usiku wa Agosti 2, 2014, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk Jakaya Mrisho Kikwete alikutana na waTanzania katika hoteli ya Marriot jijini Washington DC

Baada ya hotuba yake, Mhe. Rais aliruhusu maswali kutoka kwa waTanzania hao

Na haya, ndiyo yaliyoulizwa kwake.

Karibu


Tuesday 5 August 2014

Hotuba Ya Mhe Rais Jakaya Kikwete Kwa WaTanzania Washington DC. Aug 2, 2014‏




Karibu kusikiliza hotuba ya Mhe. Dk Jakaya M Kikwete alipozungumza na waTanzania usiku wa Agosti 2, 2014 kwenye hotel ya Marriot, jijini Washington DC nchini Marekani.




Monday 4 August 2014

Ujumbe wa Leo; kutoka kwa kaka Boniface Ole Precious "Msakatonge"


MWANANGU MPENDWA, NAOMBA UNISIKILIZE KWA UZURII KABLA HUJAOA..


1. Mwanangu, mwanamke anaweza kuwa mkeo, mwingine anaweza kuwa mama wa watoto wako, lakini ukipata mwanamke ambae atakuwa kama mama kwako, mama kwa wanao na mama kwa familia, tafadhari mwanangu usimuache huyo!

2. Mwanangu, usimfanye mwanamke wako kuwa ndio wa kupika na kufanya kazi zote za jikoni peke yake, tabia hiyo sio nzuri Kwani hata nyakati zetu, mashamba yetu yalijulikana kwa majina yetu wanaume lakini tulifanya kazi pamoja!

3. Mwanangu, nikikwambia wewe ni kichwa cha familia, simaanishi kutuna kwa pochi lako, usiangalie kabisa pochi yako, angalia kama utaona tabasamu usoni kwa mke wako. Pesa sio kila kitu katika ndoa na haileti ukuu wa familia!

4. Mwanangu, ukitaka kuwa na maisha marefu na ukapunguza misongo ya mawazo, ongea na mkeo pangeni bajeti ya mahitaji yenu, kisha mwache mkeo awe na jukumu la kuratibu mahitaji ya kila siku ya familia kwa kumkabidhi fungu husika hata kama limetokana na michango yenu wawili. wanawake wanajua sana kupanga bajeti na hii haitakuwa rahisi kwa yeye kutumia hela hovyo wakati akijua kuwa nyumbani kuna mahitaji ya msingi, lakini hela zikiwa mikono mwako ataendelea kuomba hata kama utakuwa umeishiwa!

5. Mwanangu, Usithubutu kumpiga mkeo, maumivu ya kipigo hukaa ndani ya moyo wake kwa muda mrefu sana na huacha kidonda ambacho hukawia sana kupona. Ni hatari sana kuishi na mwanamke mwenye majeraha moyoni!

6. Mwanangu, sasa unaamua kuoa,kama bado utaendelea kuishi maisha kama ya ubachela na mke wako, sio muda mrefu utakuwa bachela tena. ukioa Badilika anza kuishi maisha ya mke na mume!

7. Mwanangu, zamani,tulikuwa na wake wengi na watoto wengi kwa sababu tulikuwa na mashamba makubwa na mavuno yalikuwa makubwa, lakini kwa sasa maisha yamebadilika, kwa hiyo mkumbatie mwanamke wako peke yake kwani hakuna ardhi tena na mahitaji ya watoto ni makubwa sana. Angalia ukubwa wa familia yako!

8. Mwanangu, chini ya mwembe ambao nilikuwa nikikutana na mama yako inaweza kuwa ni hoteli kubwa kwa nyakati zenu,lakini kumbuka, kitu pekee tulichoweza kufanya chini ya mwembe ilikuwa ni kukumbatiana pekee.nakushauri ukikutana na marafiki wa kike kikubwa unachoweza kufanya nao ni kupeana mikono na ikizidi ni kukumbatiana hadharani sio vinginevyo!

9. Mwanangu, usibadilike mara utakapoanza kupata mafanikio Zaidi, kuliko kuwahudumia hao viruka njia wa mtaani ambao hawajui mmetoka wapi na mkeo, nakushauri utumie na kufurahia mafanikio yako na mkeo ambae aliweza kusimama imara wakati wote wa mapito yenu magumu.

10. Mwanangu, kumbuka unapoanza kusema au kuona mke wako kabadilika, ujue kuwa kuna kitu ambacho ulikuwa ukikifanya umeacha kukifanya. Jitathmini na anza kufanya au kutimiza wajibu wako.

11. Mwanangu, usijaribu kumfananisha au kumlinganisha mke wako na mwanamke mwingine wa nje, kwani hata yeye anakuvumilia sana na hajakufafanisha na mwanaume mwingine yoyote huko nje na ndio maana aliamua kuwa na wewe.

12. Mwanangu, sasa hivi kuna hiki kitu kinaitwa haki za wanawake, sawa,kama mwanamke anasema ana haki sawa na wewe katika nyumba, basi gawanya mahitaji yote ya ndani kwenu katika sehemu mbili zilizo sawa,halafu timiza nusu yako na mwambie atimize nusu iliyobaki.

13. Mwanangu, nilimuoa mama yako akiwa bado kigoli (bikra) na nilikuwa naenda sana kwao kabla sijamuoa, lakini kutomkuta mkeo bikra kusikufanye umlaumu kuwa alikuwa muhuni, kumbuka wanawake wa enzi zetu na wasasa ni tofauti, ulimchagua mwenyewe na ukigoli wake hukuujua kabisa. Usiingize mambo ya kabla ya ndoa kwenye ndoa yenu.

14. Mwanangu, sikuwapeleka dada zako shule kwa kuwa nilikuwa mjinga kama wazee wengi wa hapa kijiji wasemavyo, tafadhari usifanye ujinga huu, kwani kiwango cha mafanikio ya wanawake sasa kimefanya wanaume waonekane ni watu wa kawaida sana na sio muhimu kama enzi zetu. Ukijaliwa watoto wape elimu.

15. Mwanangu, zamani enzi za ujana wetu, wanawake walikuwa na urembo wa asili, ingawa siwezi kukudanganya, wengine waliongeza urembo kwa kujichora hina na hata kutoboa pua na masikio lakini usisahau hawakuonyesha maumbile yao nyeti hadharani kama sasa. Hakikisha mkeo analijua hili!

16. Mwanangu, mama yako na mimi hatuna hisa katika kila kitu kinachoendelea kwenye maisha yenu, jaribuni kutatua changamoto zenu wenyewe bila kila mara kuja kwetu kuomba usuluhishi. Ndoa ni pamoja na ukomavu wa kutatua changamoto zenu bila kuziuza kama gazeti kwa kila mtu.

17. Mwanangu, nilimnunulia mama yako kifaa cha kupikia vitumbua ili aanzishe mradi wa kuuza vitumbua, pia nilimsaidia kununua cherehani yake ya kwanza, tafadhari msaidie mke wako kutimiza ndoto zake kulingana na uwezo wako kama ambavyo unahangaika kutimiza ndoto zako.

18. Mwanangu, usiache kutusaidia mimi na mama yako, utu uzima una changamoto nyingi sana na Mungu akikujalia utaziona muda ukifika. Pamoja na kutimiza majukumu yako kama baba wa familia kumbuka pia bado tunaishi na wewe ni mtoto wetu.

19. Mwanangu, kila upatapo muda wa kusali, Sali na familia yako, kuna kesho ambayo huijui, ongea na MUNGU wako ambae anajua kila kitu kila siku!

20. NAKUTAKIA MAISHA MEMA YA NDOA MWANANGU. NAKUPENDA!

Ujumbe huu umeandaliwa na Boniface Ole Precious "Msakatonge" Ametoa ruhusa ya ku-share na marafiki.

Shukrani;https://www.facebook.com/SautiYaMwanamke/timeline

Sunday 3 August 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani-Living Water Worship Team Yesu U Mwema,Sifa ni kwako,Yehova Mwenye Nguvu Zote..!!!!!!!!


Wapendwa;Nawatakia Jumapili Njema Yenye Kusifu,Kuabudu,Kutukuza,Kushukuru,Kuwa na Matumaini na Kupendana......
5.Naam, na kwa sababu hiyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,6.Na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, 7. Na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.....


Neno La Leo;Waraka Wa Pili Wa Petro;1:1-21

19.Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing'aayo mahali penye giza, mwafanya vema, mpaka kutakapo pambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu.20.Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu furani tu.21.Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu;bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa MUNGU,Wakiongozwa na roho mtakatifu.






"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima

Friday 1 August 2014

Siku Kama Ya Leo da'Rachelsiwa Alizaliwa;[Happy birthday]Namshukuru MUNGU kwa kila Jambo!!!!!!!

Wapendwa/Waungwana,Siku Kama Ya Leo mimi "Rachel siwa"Nilizaliwa.Namshukuru sana MUNGU wangu kwa yote aliyonitendea/anayonitendea...Yeye ni mwingi wa Rehema,Neema,Baraka,Upendo.Yeye ni kila kitu maishani mwangu..
Nawashukuru Sana Wazazi/Walezi wangu kwa malezi na yote mliyonitendea kulingana na uwezo wenu,Nathamini sana mchango wenu,Kwani malezi yenu hayana mwisho kwangu.
Namshukuru sana Mume wangu katika yote,Tangu pale tulipokutana/tulipotoka mpaka sasa tulipo na tunapoelekea ni kwa Uwezo wa MUNGU tutafika salama.
Niwashukuru sana Watoto wangu wote,wale wa kuwazaa na wakurithi , kwa Faraja,Heshima,Upendo na mengineyo..Najivunia kuwa MAMA.
Nawashukuru sana Dada,Kaka,Mawifi,Mashemeji,Ndugu,Jamaa,Marafiki na Watu wote wanaonifahamu kwa namnamoja au nyingine..Nawapenda Wote.MUNGU azidi kuwabariki na kuwaongezea kila lililo jema.
Asante sana kwa wote walioniletea zawadi,wanaoniombea,walionitumia ujumbe na mnaondelea kuniombea...MUNGUazidi kuwa Bariki na kuwatendea....



Asanteni Sana kwa kunisoma  na MUNGU awabariki Sana.

"Swahili Na Swahili" Pamoja Sana.

Tuesday 29 July 2014

Eid Mubarak Waungwana!!!!!

Nawatakia Eid Njema[Eid Mubarak]Ndugu,Jamaa,Marafiki na Wote .....
Muendelee/Muwe na Wakati Mwema,Amani,Upendo na Furaha.
"Swahili Na Waswahili"Pamoj Sana.

Sunday 27 July 2014

Muendelee na Jumapili Vyema;Burudani-Angela Chibalonza - Yahwe Uhimidiwe na Nyingine...Na Siku Kama Ya Leo Bibi na Bwana Isaac Walifunga Ndoa [Happy Anniversary]


Siku kama ya Leo, Bibi na Bwana Isaac,[Isaacrachel]Tuliungana na kuwa mwili mmoja[Tulifunga Ndoa].
Tuna Mshukuru sana MUNGU katika yote na   tunazidi kujiachilia mikononi mwake.Si kwa uwezo wetu  wala akili zetu.ni Mapenzi yake/Kwa Neema tuu
.


Wapendwa; Natumaini Jumapili inandelea/ilikuwa njema,MUNGU azidi kuwabariki,Kuwainua,Kuwalinda,Kuwaponya,Kuwatendea,Kuwafariji,Kuwapa amani,Kuwapa Furaha,kuwaunganisha na Kuwafunulia.......

Ndipo Samweli akatwaa jiwe,na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri,akisema, Hata sasa BWANA ametusaidia.

Neno La Leo;1Swamweli:7:1-17
Hivyo wafilisti walishindwa,wasiingie tena  ndani ya mipaka ya Israeli; na mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Wafiristi siku zote za Samweli..........








"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Wote.

Sunday 20 July 2014

Natumaini JumaPili inaendelea Vyema;Burudani-Swahilli Worship Songs!!!!!

Wapendwa;Natumaini Jumapili  inaendelea vyema,Iwe Yenye Imani,Tumaini,Baraka,Furaha na Amani....

Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani,wakamkuta yule mtumwa ni mzima.

Neno La Leo;Luka Mtakatifu:7:1-10

Alipokwisha kuyamaliza maneno yake yote masikioni mwa watu,aliingia Kapernaumu.......



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Tuesday 15 July 2014

Siku Kama Ya Leo da'Sandra-Neema Alizaliwa







 Wapendwa/Waungwana;Siku kama ya Leo ,1998.
 Familia ya Isaac,MUNGU alitubariki/Kutujaalia mtoto wa kike.
Sandra-Neema.Umekuwa na Endelea kuwa Baraka kwetu.

Tunamshukuru sana MUNGU kwa baraka hii na Tunazidi kumtukuza katika yote.
Tunayaweka Maisha ya Sandra-Neema mikononi mwake Mungu.

Azidi kukua Kiroho/Kiimani,Kimaadili,Kimo,Kimaarifa.
Azidi kuwa Baraka Kwetu sisi Wazazi naWalezi,Ndugu,Jamaa,Marafiki,Majirani,Wakubwa Kwa Watoto na Jamii Nzima.
Shukrani sana Kwa wote tunaoshirikiana katika Malezi,Maombi/Sala/Dua na Katika yote yanayochangia Maisha ya binti yetu.
Mungu Baba azidi kuwabariki na Kuwaonngezea kila lililo jema.


Hongera sana da'Sandra-Neema katika siku yako hii  Muhimu.
Hongera kwa kumaliza vyema GCSE's Na tunakitakia kila la heri katika A-Levels[Sixth Form].
Ukawe kichwa na si Mkia.
Tunakupenda Sana na Tunakuunga mkono katika Safari yako njema ya Maisha.
MUNGU ndiyo kila kitu katika Maisha yako.Ubarikiwe Mno!!!!

Happy birthday Sandra[se-Ndondole].Wako;Mama,Baba,Mdogo wako-Tracey-Sarah.[Isaac Family]
MUNGU wetu ni Mwema Sana.



"Swahili Na Waswahili" Rachel siwa, ninawapenda Wote.

Monday 14 July 2014

Mahojiano na washiriki wa maonyesho ya Utamaduni wa Kenya hapa Washington DC


Kati ya Juni 25 na Julai 6, jiji la Washington DC lilikuwa mwenyeji wa maonyesho ya kila mwaka ya yanayohusu maisha a watu na jamii mbalimbali.

Mwaka huu, nchi ya Kenya ilishirikishwa, wakionyesha utamaduni wao na changamoto za kuzidumisha katika zama hizi za sayansi na teknolojia.

Kwanza Production ilipata fursa ya kutembelea maonyesho hayo na kuzungumza na baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo ambapo walieleza mengi ya kufurahisha.

KARIBU UUNGANE NASI


Zaidi ya washiriki 100 kutoka nchini Kenya waLIkuja hapa jijini kuonyesha mambo mbalimbali kama kutengeneza vyungu kwa ufinyanzi, uchongaji vinyago, mapambo ya shanga, useremala, nakshi za majengo, ujenzi wa majahazi, mapishi , muziki na mengine yanayotunza utamaduni wa nchi hiyo


Maelezo ya ujenzi na sehemu za JAHAZI (DHOW) toka kwa Ali Skanda aliyetoka Lamu Kenya
Na mtangazaji mkongwe abdushakur Aboud mbele ya Jahazi lililoletwa kwenye makumbusho ya hapa Washington DC kutoka Lamu nchini Kenya
Mtaalamu wa mapambo yatokanayo na shanga na usimamizi wa filamu nchini Kenya Emmah Irungu
Mwandishi wa habari kutoka Kenya BMJ Mureithi

Sunday 13 July 2014

Tumalizie JumaPili hii na Pastor Donis and Nnunu Nkone- SINGING WITH THEIR CHILDREN

Wapendwa;Natumaini MUNGU anazidi kuwabariki na Mnaendelea Vyema na Jumapili hii..
Iwe Njema,Yenye Heri,Baraka,Neema,Tumaini,Utuwema,Fadhili,Shukrani na Amani.

Neno La Leo;Tumsikilize, Pastor Donis na Familia Yake ......




Shukrani Sana na MUNGU azidi kuwabariki;Donis-andNnunu Nkone

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 11 July 2014

Jikoni Leo;How to Make Mbaazi,Viazi Vya Tamu Vya Nazi na Mswahili Sheikha Agil

Waungwana;"Jikoni Leo"  Mapishi haya yatasaidia sana wanaofunga Mwezi huu[Futari]....
Mengi sina nawatakia Mapishi mema.






Shukrani;Sheikha Agil

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Sunday 6 July 2014

Tuendelee Na JumaPili hii Vyema;Burudani-Furaha Choir London - Tuimbe Wimbo (Muda Tutakwenda Nyumbani)na Nyingine...!!!

Wapendwa; natumaini Jumapili hii inaendelea Vyema,Iwe yenye Amani,Baraka,Furaha,Upendo,Fadhili, Shukran,Utukufu tumrudishie MUNGU.......

Mkimshukuru Baba,aliyewastahilisha kupokea  sehemu ya Urithi wa watakatifu katika nuru.

Neno La Leo;Wakolosai:1:1-29


Nae alituokoa katika nguvu za giza,akatuhamisha na kutuingiza katika uflame wa Mwana wa pendo Lale.




"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima

Saturday 5 July 2014

Mahojiano ya Kwanza Production na Diamond Platnumz baada ya tuzo za BET‏


Diamond Platnumz na DMK kwenye utoaji tuzo za BET Los Angeles
Photo Credits: DMK Global Promotions' facebook page
Karibu katika mahojiano ya Kwanza Production na Damond Platnumz. Msanii mwenye mafanikio makubwa kutoka nchini Tanzania
Amejiunga nasi kwa njia ya simu punde baada ya kuhudhuria utoaji tuzo za BET ambako yeye alikuwa mmoja wa waliokuwa wakiwania tuzo hizo.
Kazungumza mengi kuhusu TUZO HIZO.
Alipopokea na alivyopokea uteuzi wake, aliloliona kwenye tuzo hizo, ulinganishaji wake katika utoaji tuzo hizi na za Tanzania / Afika, alichojifunza, faida ya kuja kushiriki hili na hata mikakati yake ijayo kuhakikisha kuwa muziki wa Tanzania unafika mbali zaidi.
SWALI jingine alilojibu ni kuwa....ni kweli kuwa ili muziki wa Tanzania ushinde tuzo ni lazima uwe na mahadhi ya Afrika Magharibi (kama muziki wake wa Number One) ama Afrika Kusini 
Amejiunga nasi kwa msaada wa promota Dickson Mkama almaarufu DMK ambaye pia ndiye meneja wa msanii huyo hapa nchini.
KARIBU





Thursday 3 July 2014

Chaguo La Mswahili Leo;Michelle Williams - Say Yes ft. Beyoncé, Kelly Rowland.!!!!!

Waungwana Chaguo La Mswahili Leo.Say Yes.....
Mmmhhh Maneno mengi sina..Twende sote sasaaaaa.....
.



Mimi umenishikaaa..wewe je?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana
.

Wednesday 2 July 2014

Mahojiano na Kwanza Production na NURU THE LIGHT‏


Photo Credits: Bongo Celebrity 
Karibu katika mahojiano kamini kati ya Kwanza Production na NURU THE LIGHT.
Msanii, Mjasiriamali, Mtangazaji, Blogger na Mwanaharakati ambaye amekuwa mkarimu sana kujiunga nasi moja kwa moja kutoka Stockholm Sweden
Kazungumza mengi ikiwa ni pamoja na alivyoanza muziki
Kisha akagusia kuhusu onyesho lake la kwanza kabisa jukwaani.
Na kama nilivyokuja kumtambua, ni mtu mwenye misimamo na anayejitambua, utamsikia msimamo wake awapo studio
Nikataka kujua pia, nini anaona kama tatizo kubwa kwenye muziki wetu?
Haya ni machache kati ya mengi aliyozungumza nami
JIUNGE NASI



Sunday 29 June 2014

Tumalize JumaPili hii Kwa Amani Na Shukrani;Burudani,Solomon Mukubwa - Mungu Mwenye Nguvu,Ni Kwa Neema Na Rehema - Edson Mwasabwite. Na Siku Kama Ya Leo,Kaka Lusungu Ndondole Alizaliwa!!!

Wapendwa,Tumalizie/Tuendelee na JumaPili Hii kwa,Amani Shukrani,Furaha,Upendo na Matumaini.....
Basi, tuseme nini juu ya hayo?MUNGU akiwa upande wetu,ni nani aliye juu yetu?

Neno La Leo;Warumi:8:31-39
Wala yaliyo juu,Wala yaliyo chini,Wala kiumbe kingine chochote hakitaweza kututenga na upendo wa MUNGU ulio katika Kristo YESU BWANA wetu.

Siku Kama Ya Leo;Bibi Na Bwana I.Ndondole Walipata Mtoto wa Kiume.
Hongera Sana kwa Kutimiza Miaka Kadhaa, Mwl. Lusungu Ndondole
MUNGU azidi kukubariki kila iitwapo Leo,Uendelee kuwa Baraka kwa Wazazi,Familia na Jamii pia.
MUNGU akupe Miaka Mingi na Ufanikishe Ndoto zako.


Mhhhhh Ni Kwa Neema Na Rehema.......




"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 27 June 2014

JESCA KIPLAGAT ELECTRIFYS THE HALL WINNING FACE OF KENYA UK 2014


Jesca won because of her unique story. She was educated by charity, Educated in University using HELB loans and is now in UK on a sponsorship program. In her own words, she says she has received so much its time to give back. Jesca raised £560 for her charity of choice Kapchaselewes childrens home in Marakwet district.

Other contestants had a beautiful English ascent but Jesca proudly pulled a Kalenjin English accent and just really portrayed the pride of Kenya. During the talents, most contestants choose to sing and dance but Jesca chose to have a motivational speech as her talent, this was unique, moving and melting the hall away, she won the audiences hearts
"I must say this was a worthy course to have participated in. I had a wonderful experience, enjoyed myself and as well it has given me a platform to give back to my community. I have attended photo shoots, fundraisers, networking dinner among other initiatives that I have thoroughly enjoyed. I am honoured and humbled by this wonderful experience, It has inculcated in me a sense of nationalism-proud Kenyan and yes giving back to the community which is the ultimate thing that have really made it a worthy course and I promise to lead other youths in the national building exercise as The Face of Kenya UK 2014 BRAND AMBASSODOR".


FUNDS: £ 560 KAPSCHELEWES CHILDREN HOME MARAKWET.




Kwa picha zaidi;http://www.ukentv.com/faceofkenyauk.html
 Video; Africanacts


congratulations sister Janet, great job!

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Wednesday 25 June 2014

Katika "HUYU NA YULE" ya NJE-NDANI wiki hii......‏


Photo Credits: Bongo Celebrity 
Katika NJE NDANI wiki hii, mbali na habari kutoka Afrika, utasikia mahojiano yangu na NURU THE LIGHT.

Msanii, Mjasiriamali, Mtangazaji, Blogger na Mwanaharakati ambaye amekuwa mkarimu sana kujiunga nami kutoka Stockholm Sweden

Kazungumza mengi mema

Jiunge nami, MUBELWA BANDIO Jumamosi (June 28) katika NJE NDANI ya Kwanza Production na Border Radio kuanzia saa sita mpaka saa nane mchana kwa saa za Marekani ya mashariki kupitia www.kwanzaproduction.com ama www.bordermediagroup.com