Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 10 August 2014

Muendelee na JumaPili hii kwa Amani na Upendo;Burudani-Franck Mulaja,Alleluya,Nzambe malamu..!!!!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu Jumapili inaendelea vyema;Iwe yenye Imani,Kuomba pasipo kukoma,Uponyaji,Shukrani na kujitoa kwa wenye kuhitaji.

14.Hata walipowafikia wanafunzi, waliona mkutano mkuu wakiwazunguka, na waandishi wakijadiliana nao,15. Mara mkutano wote walipomuona walishangaa, Wakamwendea mbio,wakamsalimu.16.Akawauliza, Mnajadiliana nini nao?

Neno La Leo;Marko Mtakatifu:9:1-50

17.Mtu mmoja katika mkutano akaijibu,Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako,ana pepo bubu;18. Na kila  ampagaapo,humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda;Nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze.19.Akawajibu,akasema,Enyi kizazi kisichoamini,nikae nanyi hata lini?Nichukuliane nanyi hata lini?Mleteni kwangu.20.Wakamleta kwake;hata alipomwona,mara yule pepo alimtia kifafa;naye akaanguka chini,akagaagaa,akitokwa na povu.

21.Akamuuliza babaye,Amepatwa na haya tangu lini?Akasema tangu utoto.22.Na mara nyingi amemtupa katika moto,na katika maji,amwangamize;Lakini ukiweza neno lolote, utuhurumie, na kutusaidia.

23.Yesu akamwambia, Ukiweza!Yote yawezekana kwake aaminie.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Kwangu ilikuwa yenye amani na furaha pua upendo...naamini ndivyo ilikuwa kwa wengi...ahsante Kachiki.