Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 19 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 107...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Nyinyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana. Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu, tunawaombeni mfanye hata zaidi. Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali. Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini. Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana, kwamba sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia. Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana. Basi, farijianeni kwa maneno haya.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

KITABU CHA TANO
(Zaburi 107–150)
Sifa kwa Mungu mwema
1 Taz Zab 100:5; 106:1; 118:1; 136:1 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!
2Semeni hivyo, enyi mliokombolewa na Mwenyezi-Mungu,
watu ambao aliwaokoa katika taabu,
3akawakusanyeni kutoka nchi za kigeni:
Kutoka mashariki na magharibi,
kutoka kaskazini na kusini.107:3 kusini: Kiebrania: Bahari; yaani magharibi.
4Baadhi walitangatanga katika jangwa tupu,
wasiweze kufikia mji wa kukaa.
5Waliona njaa na kiu;
wakavunjika moyo kabisa.
6Ndipo katika taabu yao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso yao.
7Aliwaongoza katika njia iliyonyoka,
mpaka wakaufikia mji wa kukaa.
8Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
9Yeye huwatosheleza walio na kiu;
na wenye njaa huwashibisha mema.
10Baadhi waliishi katika giza na ukiwa,
wafungwa katika mateso na minyororo,
11kwa sababu waliasi maagizo ya Mungu,
na kuyapuuza mashauri yake Mungu Mkuu.
12Walikuwa hoi kwa kazi ngumu,
wakaanguka chini, pasiwe na wa kuwasaidia.
13Ndipo katika taabu yao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso yao.
14Aliwatoa katika giza na ukiwa,
na minyororo yao akaivunjavunja.
15Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
16Yeye huvunja na kufungua milango ya shaba,
na kukatakata fito za chuma.
17Baadhi walipumbaa kwa sababu ya dhambi zao,
waliteseka kwa sababu ya uovu wao;
18chakula kikawa kinyaa kwao,
wakawa nusura wafe.
19Ndipo katika taabu yao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso yao.
20Kwa neno lake aliwaponya,
akawaokoa wasiangamie.
21Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
22Wamtolee tambiko za shukrani;
wasimulie matendo yake kwa nyimbo za shangwe.
23Baadhi walisafiri baharini kwa meli,
na kufanya shughuli zao humo baharini.
24Waliyaona matendo ya Mwenyezi-Mungu,
mambo ya ajabu aliyotenda huko.
25Aliamuru, akazusha dhoruba kali,
ikarusha juu mawimbi ya bahari.
26Walitupwa juu angani, kisha chini vilindini;
uhodari wao ukawaishia katika mkasa huo.
27Waliyumbayumba na kupepesuka kama walevi;
maarifa yao ya uanamaji yakawaishia.
28Ndipo katika taabu zao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso zao.
29Aliifanya ile dhoruba kali itulie,
nayo mawimbi yakanyamaza.
30Hapo wakafurahi kwa kupata utulivu;
akawafikisha kwenye bandari waliyoiendea.
31Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
32Mtukuzeni katika kusanyiko la watu,
na kumsifu katika baraza la wazee.
33Mungu aliigeuza mito kuwa jangwa,
chemchemi akazikausha kabisa.
34Ardhi yenye rutuba akaifanya udongo wa chumvi,
kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.
35Aligeuza majangwa kuwa mabwawa ya maji,
na nchi kame kuwa chemchemi za maji.
36Akawahamishia huko wenye njaa,
nao wakajenga mji wa kukalika.
37Walilima mashamba na kupanda mizabibu,
wakavuna mazao kwa wingi.
38Aliwabariki watu wake, wakaongezeka;
na idadi ya wanyama wao akaizidisha.
39Kisha walipopungua na kuwa wanyonge,
kwa kukandamizwa, kuteswa na huzuni,
40aliwadharau wakuu waliowatesa,
akawazungusha jangwani kusiko na njia.
41Lakini aliwaokoa wahitaji katika taabu zao,
akaongeza jamaa zao kama kundi la kondoo.
42Waadilifu waonapo jambo hilo wanafurahi,
lakini waovu wote wananyamazishwa.
43Wenye hekima na wayafikirie mambo haya,
wazitambue fadhili zake Mwenyezi-Mungu.



Zaburi107;1-43

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 18 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 106...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu. Mungu anataka nyinyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa. Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima, na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....
Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo. Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu. Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali anamdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Jehovah ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu kila mmoja na mahitaji yake...
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao....
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele....
Amina..!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Wema wa Mungu kwa watu wake
1 Taz Zab 11:5; 107:1; 118:1; 136:1 Haleluya! Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!
2Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu?
Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?
3Heri wale wanaotekeleza haki,
wanaotenda daima mambo yaliyo sawa.
4Unikumbuke ee Mwenyezi-Mungu unapowafadhili watu wako;
unisaidie wakati unapowaokoa;
5ili niweze kuona fanaka ya wateule wako,
nipate kufurahia furaha ya taifa lako,
na kuona fahari pamoja na watu wako.
6Tumetenda dhambi sisi na wazee wetu;
tumetenda maovu, tumefanya mabaya.
7Wazee wetu walipokuwa Misri,
hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu;
hawakukumbuka wingi wa fadhili zake,
bali walimwasi kando ya bahari ya Shamu.
8Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi,
ili aoneshe nguvu yake kuu.
9Aliikemea bahari ya Shamu ikakauka;
akawapitisha humo kama katika nchi kavu.
10Aliwaokoa mikononi mwa waliowachukia;
aliwaokoa kutoka kwa nguvu za maadui zao.
11Maji ya bahari yaliwafunika maadui zao;
wala hakusalia hata mmoja wao.
12Hapo watu wake wakaamini maneno yake,
wakamwimbia tenzi za sifa yake.
13Lakini mara walisahau matendo yake,
wakaacha kutegemea shauri lake.
14Walijawa na tamaa kubwa kule jangwani,
wakamjaribu Mungu kule nyikani.
15Naye akawapa kile walichoomba,
lakini akapeleka maradhi mabaya kati yao.
16Kule kambini walimwonea wivu Mose,
na Aroni mtumishi mtakatifu wa Mwenyezi-Mungu.
17Ndipo ardhi ikafunguka ikammeza Dathani,
na kumzika Abiramu na kundi lake lote;
18moto ukawatokea wafuasi wao,
ukawateketeza watu hao waovu.
19Walitengeneza ndama wa dhahabu kule Horebu,
wakaiabudu sanamu hiyo ya kusubu;
20waliubadilisha utukufu wa Mungu,
kwa sanamu ya mnyama ambaye hula nyasi.
21Walimsahau Mungu aliyewaokoa,
aliyetenda mambo makuu nchini Misri,
22maajabu katika nchi hiyo ya Hamu,
na mambo ya kutisha katika bahari ya Shamu.
23Mungu alisema atawaangamiza watu wake,
ila tu Mose mteule wake aliingilia kati,
akaizuia hasira yake isiwaangamize.
24Kisha wakaidharau nchi ile ya kupendeza,
kwa sababu hawakuwa na imani na ahadi ya Mungu.
25Walinungunika mahemani mwao,
wala hawakumsikiliza Mwenyezi-Mungu.
26Hivyo Mungu akainua mkono akaapa
kwamba atawaangamizia jangwani;
27atawatawanya wazawa wao kati ya watu,
na kuwasambaza duniani kote.
28Kisha wakajiunga kumwabudu Baali kule Peori,
wakala tambiko zilizotambikiwa mizimu.
29Waliichochea hasira ya Mwenyezi-Mungu kwa matendo yao,
maradhi mabaya yakazuka kati yao.
30Lakini Finehasi akasimama kufanya malipizi,
na yale maradhi yakakoma.
31Jambo hilo lakumbukwa kwa heshima yake,
tangu wakati huo na nyakati zote.
32Walimkasirisha Mungu penye maji ya Meriba,
Mose akapata taabu kwa ajili yao.
33Walimtia Mose uchungu rohoni,
hata akasema maneno bila kufikiri.
34Hawakuwaua watu wa mataifa mengine
kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru.
35Bali walijumuika na watu wa mataifa,
wakajifunza kutenda mambo yao.
36Waliabudu sanamu za miungu yao,
nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza.
37Waliwaua watoto wao wa kiume na wa kike,
wakawatoa tambiko kwa pepo.
38Walimwaga damu ya wasio na hatia,
damu ya watoto wao wa kiume na wa kike
ambao waliwatoa tambiko kwa sanamu za Kanaani,
nayo nchi ikatiwa unajisi kwa mauaji hayo.
39Hivyo wakafanywa najisi kwa matendo yao,
2wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazinzi.
40Hasira ya Mwenyezi-Mungu ikawawakia watu wake,
akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.
41Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa,
hao wenye kuwachukia wakawatawala.
42Maadui zao waliwakandamiza,
wakawatumikisha kwa nguvu.
43Mara nyingi Mungu aliwaokoa watu wake,
lakini wao wakachagua kumwasi,
wakazidi kuzama katika uovu wao.
44Hata hivyo Mungu alizijali taabu zao,
wakati aliposikia kilio chao;
45kwa ajili yao alilikumbuka agano lake,
akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.
46Aliwafanya waliowakandamiza wawaonee huruma.
47Utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa,
tupate kulisifu jina lako takatifu,
na kuona fahari juu ya sifa zako.
48Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele!
Na watu wote waseme: “Amina!”
Asifiwe Mwenyezi-Mungu!


Zaburi106;1-48

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 17 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 105...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: “Kama mkisikia sauti yake leo, msiwe wakaidi kama wakati ule waliponiasi kama wakati ule wa majaribio kule jangwani. Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, ingawa walishuhudia matendo yangu kwa miaka arubaini! Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, ‘Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu’. Basi, nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai. Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi. Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti yake leo, msiwe wakaidi kama wakati ule waliponiasi.” Ni akina nani waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri. Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arubaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani. Mungu alipoapa: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi. Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....Nawapenda.

Mungu na watu wake
(1Nya 16:8-22)
1Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, tangazeni ukuu wake;
yajulisheni mataifa mambo aliyotenda!
2Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;
simulieni matendo yake ya ajabu!
3Jisifieni jina lake takatifu;
wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.
4Tafuteni msaada kwa Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;
mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.
5Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda,
miujiza yake na hukumu alizotoa,
6enyi wazawa wa Abrahamu mtumishi wake,
enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake;
7Yeye ndiye Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;
hukumu zake zina nguvu duniani kote.
8Yeye hulishika agano lake milele,
hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.
9Hushika agano alilofanya na Abrahamu,
na ahadi aliyomwapia Isaka.
10Alimthibitishia Yakobo ahadi yake,
alimhakikishia Israeli agano hilo la milele.
11Alisema: “Nitawapeni nchi ya Kanaani,
nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”
12Watu wa Mungu walikuwa wachache; hawakuwa maarufu,
tena walikuwa wageni nchini Kanaani.
13Walitangatanga kutoka taifa hadi taifa;
kutoka nchi moja hadi nchi nyingine.
14Lakini Mungu hakuruhusu mtu awadhulumu;
kwa ajili yao aliwaonya wafalme:
15“Msiwaguse wateule wangu;
msiwadhuru manabii wangu!”
16Mungu alizusha njaa nchini mwao,
akaharibu chakula chao chote.
17Lakini aliwatangulizia mtu mmoja,
Yosefu aliyekuwa ameuzwa utumwani.
18Walimfunga miguu kwa minyororo,
na shingoni kwa nira ya chuma,
19Muda si muda alichotabiri kilitimia.
neno la Mwenyezi-Mungu lilimdhibiti.
20Mfalme wa Misri akaamuru afunguliwe;
mtawala wa mataifa akamwachilia huru.
21Alimweka kuwa mkurugenzi wa serikali yake,
na mkuu wa mali yake yote;
22awaongoze maofisa wake apendavyo,
na kuwafundisha wazee wake hekima.
23Ndipo Israeli akaingia nchini Misri;
Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu.
24Mwenyezi-Mungu akawafanya watu wake wazae sana;
akawajalia nguvu kuliko maadui zao.
25Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake,
wakawatendea hila watumishi wake.
26Kisha akamtuma Mose mtumishi wake,
akamtuma na Aroni mteule wake.
27Wakafanya ishara za Mungu kati ya Wamisri,
na miujiza katika nchi hiyo ya Hamu.
28Mungu akaleta giza juu ya nchi;
lakini Wamisri wakakataa kutii amri zake.105:28 wakakataa kutii amri zake: Hivyo katika hati kadha za kale. Kiebrania: Wakatii.
29Akageuza mito yao kuwa damu,
akawaua samaki wao wote.
30Vyura wakaivamia nchi yao,
hata jumba la mfalme likajawa nao.
31Mungu akanena, kukazuka makundi ya nzi,
na viroboto katika nchi yote.
32Badala ya mvua akawapa mvua ya mawe,
na umeme uliomulika nchi yao yote;
33akaharibu mizabibu na mitini yao,
akaivunja pia miti ya nchi yao.
34Mungu akanena, kukazuka nzige,
na panzi maelfu yasiyohesabika;
35wakaitafuna mimea yote katika nchi,
wakayala mazao yao yote.
36Aliwaua wazaliwa wa kwanza nchini mwao,
chipukizi wa kwanza wa jamaa za Wamisri.
37Kisha akawatoa watu wa Israeli nchini,
wakiwa na fedha na dhahabu;
wala hakuna hata mmoja wao aliyejikwaa.
38Wamisri walifurahia kuondoka kwao,
kwani hofu iliwashika kwa sababu yao.
39Mungu alitandaza wingu juu ya watu wake,
na moto ili kuwaangazia usiku.
40Waliomba105:40 Waliomba: Makala nyingine za kale; Aliomba. naye akawaletea kware,
akawapa mkate kutoka mbinguni kwa wingi.
41Alipasua mwamba maji yakabubujika;
yakatiririka jangwani kama mto.
42Aliikumbuka ahadi yake takatifu,
aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43Basi akawatoa watu wake nchini,
wateule wake wakaimba na kushangilia.
44Aliwapa nchi za mataifa mengine
na kuwakabidhi mashamba ya wenyeji;
45kusudi watu wake watii masharti yake,
na kufuata sheria zake.
Asifiwe Mwenyezi-Mungu!

Zaburi105;1-45

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 16 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 104...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Ndugu zangu, watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu Mtume na Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama. Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Lakini Yesu anastahili heshima kubwa kuliko Mose maana mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye. Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi wenyewe ni nyumba yake kama tukiendelea kuwa hodari na thabiti katika kile tunachotumainia.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Kumsifu Muumba
1 Taz Ebr 1:7 Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu!
Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, wewe ni mkuu mno!
Umejivika utukufu na fahari.
2Umejizungushia mwanga kama vazi,
umezitandaza mbingu kama hema;
3umejenga makao yako juu ya maji ya mbingu.
Umeyafanya mawingu kuwa gari lako;
waruka juu ya mabawa ya upepo,
4waufanya upepo kuwa mjumbe wako,
moto na miali yake kuwa watumishi wako.
5Dunia umeiweka imara juu ya misingi yake,
ili isitikisike milele.
6Uliifunika dunia kwa bahari kama vazi,
na maji yakaimeza milima mirefu.
7Ulipoyakaripia, maji yalikimbia,
yaliposikia ngurumo yako yalitimka mbio.
8Yaliporomoka toka milimani hadi mabondeni,
mpaka pale mahali ulipoyatengenezea.
9Uliyawekea hayo maji mipaka,
yasije yakaifunika tena dunia.
10Umetokeza chemchemi mabondeni,
na mikondo yake ipite kati ya vilima.
11Hizo zawapatia maji wanyama wote porini.
Humo pundamwitu huzima kiu zao.
12Ndege hujenga viota vyao katika miti ya hapo,
hutua katika matawi yake na kuimba.
13Toka juu angani wainyeshea milima mvua,
nayo dunia waitosheleza kwa baraka yako.
14Waotesha nyasi kwa ajili ya mifugo,
na mimea kwa matumizi ya binadamu
ili naye ajipatie chakula chake ardhini:
15Divai ya kumchangamsha,
mafuta ya zeituni ya kumfurahisha,
na mkate wa kumpa nguvu.
16Miti mikubwa ya Mwenyezi-Mungu yapata maji ya kutosha;
naam, mierezi ya Lebanoni aliyoiotesha.
17Humo, ndege hujenga viota vyao;
korongo hufanya maskani yao katika misonobari.
18Milima mirefu ni makao ya mbuzimwitu;
na pelele hupata maficho yao miambani.
19Umeuumba mwezi utupimie majira;
jua nalo lajua wakati wa kutua.
20Waleta giza, usiku waingia;
nao wanyama wote wa porini wanatoka:
21Wanasimba hunguruma wapate mawindo,
humngojea Mungu awape chakula chao.
22Jua lichomozapo hurudi makwao,
na kujipumzisha mapangoni mwao.
23Hapo naye binadamu huenda kwenye shughuli zake;
na kufanya kazi zake mpaka jioni.
24Ee Mwenyezi-Mungu, umetenda mambo mengi mno!
Yote umeyafanya kwa hekima!
Dunia imejaa viumbe vyako!
25Mbali kule iko bahari - kubwa na pana,
ambamo kumejaa viumbe visivyohesabika,
viumbe hai, vikubwa na vidogo.
26 Taz Zab 74:14 Ndimo zinamosafiri meli,
na lile dude Lewiyathani uliloliumba licheze humo.
27Wote wanakungojea wewe,
uwapatie chakula chao kwa wakati wake.
28Wanaokota chochote kile unachowapa;
ukifumbua mkono wako wanashiba vinono.
29Ukiwapa kisogo, wanaogopa;
ukiondoa pumzi yao, wanakufa,
na kurudi mavumbini walimotoka.
30Ukiwapulizia pumzi yako, wanaishi tena;
wewe waipa dunia sura mpya.
31Utukufu wa Mwenyezi-Mungu udumu milele;
Mwenyezi-Mungu apendezwe na matendo yake mwenyewe.
32Huitazama dunia nayo hutetemeka,
huigusa milima nayo hutoa moshi!
33Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu maisha yangu yote;
nitamsifu Mungu wangu muda wote niishipo.
34Upendezwe, ee Mwenyezi-Mungu, na mawazo yangu haya;
maana furaha yangu naipata kwako.
35Wenye dhambi waondolewe duniani,
pasiwe na waovu wowote tena!
Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Zaburi104;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.