Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 23 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 109...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu, enyi msikiao neno lake mkatetemeka: “Ndugu zenu ambao wanawachukia, na kuwapiga marufuku kwa sababu yangu, wamesema kwa dharau ‘Mungu na aoneshe utukufu wake, nasi tuwaone nyinyi mkishinda!’ Lakini wao wenyewe ndio watakaoaibishwa!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Sikilizeni, ghasia kutoka mjini, sauti kutoka hekaluni! Hiyo ni sauti ya Mwenyezi-Mungu akiwaadhibu maadui zake!
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

“Mji wangu mtakatifu, ni kama mama ajifunguaye bila kuona uchungu; kabla uchungu kuanza, amekwisha zaa mtoto. Ni nani aliyepata kusikia jambo kama hilo? Ni nani aliyewahi kuona jambo kama hilo? Je, nchi nzima yaweza kuzaliwa siku moja? Je, taifa zima laweza kuzaliwa mara moja? Maana Siyoni, mara tu alipoanza kuona uchungu, alijifungua watoto wake.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Lalamiko la mtu taabuni
(Kwa Mwimbishaji. Wimbo wa Daudi)
1Usinyamaze, ee Mungu ninayekusifu!
2Watu waovu na wadanganyifu wanishambulia,
wanasema uongo dhidi yangu.
3Wanasema maovu juu yangu,
na kunishambulia bila kisa.
4Ingawa niliwapenda, walinishtaki,
hata hivyo niliwaombea dua.
5Wananilipa uovu kwa wema wangu,
na chuki kwa mapendo yangu.
6Umweke hakimu mbaya dhidi ya adui yangu;
na mshtaki wake ampeleke mahakamani.
7Anapohukumiwa apatikane na hatia;
lalamiko lake lihesabiwe kuwa kosa jingine.
8 Taz Mate 1:20 Siku za maisha yake ziwe chache,
mtu mwingine na achukue kazi yake!
9Watoto wake wawe yatima,
na mke wake awe mjane!
10Watoto wake watangetange na kuombaomba;
wafukuzwe katika magofu ya nyumba zao!
11Anayemdai kitu amnyanganye mali yake yote;
na wageni wanyakue mapato ya jasho lake!
12Pasiwe na mtu wa kumwonea huruma,
au Kuwatunza watoto wake yatima!
13Wazawa wake wote wafe;
jina lake lisahauliwe katika kizazi kijacho!
14Mwenyezi-Mungu aukumbuke uovu wa wazee wake,
dhambi za mama yake zisifutwe kamwe!
15Mwenyezi-Mungu azikumbuke dhambi zao daima;
lakini wao wenyewe wasahauliwe duniani.
16Mwovu huyo hakujali kabisa kuwa na huruma,
ila aliwadhulumu maskini na fukara,
kadhalika na watu wanyonge mpaka kifo.
17Yeye alipenda kulaani watu,
laana na impate yeye mwenyewe.
Hakuwatakia wengine baraka,
basi, asipate baraka yeye mwenyewe.
18Kwake kulaani ni kama kuvaa nguo,
basi, laana hizo zimloweshe kama maji,
zimwingie mifupani mwake kama mafuta.
19Laana zimfunike kama nguo,
zimzunguke daima kama ukanda.
20Mwenyezi-Mungu awalipe hayo hao watu wanaonishtaki,
naam hao wanaosema mabaya dhidi yangu.
21Lakini ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wangu,
unitendee kadiri ya hisani yako;
uniokoe, kwa sababu ya wema wa fadhili zako!
22Mimi ni maskini na fukara;
nimejeruhiwa mpaka moyoni mwangu.
23Natoweka kama kivuli cha jioni;
nimepeperushwa kama nzige.
24Magoti yangu yamenyongonyea kwa mfungo;
nimebaki mifupa na ngozi.
25 Taz Mat 27:39; Marko 15:29 Nimekuwa dhihaka tupu kwa watu;
wanionapo hutikisa vichwa vyao kwa dharau.
26Unisaidie, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu;
uniokoe kadiri ya fadhili zako.
27Waoneshe watu kuwa ndiwe uliyetenda hayo,
wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe uliyefanya hivyo.
28Waache walaani, lakini wewe unibariki;
wanaonishambulia waaibike, nami mtumishi wako nifurahi.
29Maadui zangu na wavishwe fedheha;
wajifunike aibu yao kama blanketi.
30Nitamshukuru sana Mwenyezi-Mungu kwa sauti;
nitamsifu kati ya kundi kubwa la watu,
31kwa maana yeye humtetea maskini,
humwokoa wakati anapohukumiwa.

Zaburi109;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 22 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 108...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Mbingu ni kiti changu cha enzi, dunia ni kiti cha kuwekea miguu yangu. Mtanijengea nyumba ya namna gani basi, Mahali nitakapoweza kupumzika?
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi ni mtu mnyenyekevu na mwenye majuto, mtu anayetetemeka asikiapo neno langu.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

“Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: Wananitolea tambiko ya ng'ombe na mara wanaua watu kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwanakondoo na pia wanamvunja mbwa shingo. Wananitolea tambiko ya nafaka na pia kupeleka damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe. Basi, nitawaletea taabu; yatawapata yaleyale wanayoyahofia; maana nilipoita hakuna aliyeitika, niliponena hawakusikiliza. Bali walifanya yaliyo maovu mbele yangu, walichagua yale ambayo hayanipendezi.”
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Sala ya kujikinga na maadui
(Zaburi ya Daudi: Wimbo)
1Niko thabiti moyoni, ee Mungu,
naam, niko thabiti moyoni;
nitaimba na kukushangilia!
Amka, ee nafsi yangu!
2Amkeni enyi kinubi na zeze!
Nitayaamsha mapambazuko!
3Ee Mwenyezi-Mungu, nitakushukuru kati ya mataifa;
nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
4Fadhili zako ni kubwa kuliko mbingu;
uaminifu wako waenea hata mawinguni.
5Utukuzwe, ee Mungu juu ya mbingu!
Utukufu wako uenee duniani kote!
6Watu hao uwapendao na wasalimishwe;
utusaidie kwa mkono wako na kutusikiliza.
7Mungu amesema kutoka patakatifu pake:108:7 kutoka … pake: Au katika utakatifu wake.
“Sasa nitaigawa Shekemu kwa shangwe,
bonde la Sukothi nitalipima sehemusehemu.
8Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu;
Efraimu ni kofia yangu ya chuma,
na Yuda ni fimbo yangu ya enzi.
9Moabu ni kama bakuli langu la kunawia;
kiatu changu nitaitupia Edomu kuimiliki.
Nitapiga kelele ya ushindi juu ya Filistia!”
10Ni nani, atakayenipeleka kwenye mji wa ngome?
Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?
11Je, umetuacha kabisa, ee Mungu?
Wewe huendi tena na majeshi yetu!
12Utupatie msaada dhidi ya maadui zetu,
maana msaada wa binadamu haufai kitu.
13Mungu akiwa upande wetu tutashinda,
yeye atawaponda maadui zetu.


Zaburi108;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 19 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 107...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Nyinyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana. Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu, tunawaombeni mfanye hata zaidi. Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali. Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini. Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana, kwamba sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia. Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana. Basi, farijianeni kwa maneno haya.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

KITABU CHA TANO
(Zaburi 107–150)
Sifa kwa Mungu mwema
1 Taz Zab 100:5; 106:1; 118:1; 136:1 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!
2Semeni hivyo, enyi mliokombolewa na Mwenyezi-Mungu,
watu ambao aliwaokoa katika taabu,
3akawakusanyeni kutoka nchi za kigeni:
Kutoka mashariki na magharibi,
kutoka kaskazini na kusini.107:3 kusini: Kiebrania: Bahari; yaani magharibi.
4Baadhi walitangatanga katika jangwa tupu,
wasiweze kufikia mji wa kukaa.
5Waliona njaa na kiu;
wakavunjika moyo kabisa.
6Ndipo katika taabu yao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso yao.
7Aliwaongoza katika njia iliyonyoka,
mpaka wakaufikia mji wa kukaa.
8Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
9Yeye huwatosheleza walio na kiu;
na wenye njaa huwashibisha mema.
10Baadhi waliishi katika giza na ukiwa,
wafungwa katika mateso na minyororo,
11kwa sababu waliasi maagizo ya Mungu,
na kuyapuuza mashauri yake Mungu Mkuu.
12Walikuwa hoi kwa kazi ngumu,
wakaanguka chini, pasiwe na wa kuwasaidia.
13Ndipo katika taabu yao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso yao.
14Aliwatoa katika giza na ukiwa,
na minyororo yao akaivunjavunja.
15Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
16Yeye huvunja na kufungua milango ya shaba,
na kukatakata fito za chuma.
17Baadhi walipumbaa kwa sababu ya dhambi zao,
waliteseka kwa sababu ya uovu wao;
18chakula kikawa kinyaa kwao,
wakawa nusura wafe.
19Ndipo katika taabu yao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso yao.
20Kwa neno lake aliwaponya,
akawaokoa wasiangamie.
21Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
22Wamtolee tambiko za shukrani;
wasimulie matendo yake kwa nyimbo za shangwe.
23Baadhi walisafiri baharini kwa meli,
na kufanya shughuli zao humo baharini.
24Waliyaona matendo ya Mwenyezi-Mungu,
mambo ya ajabu aliyotenda huko.
25Aliamuru, akazusha dhoruba kali,
ikarusha juu mawimbi ya bahari.
26Walitupwa juu angani, kisha chini vilindini;
uhodari wao ukawaishia katika mkasa huo.
27Waliyumbayumba na kupepesuka kama walevi;
maarifa yao ya uanamaji yakawaishia.
28Ndipo katika taabu zao wakamlilia Mwenyezi-Mungu,
naye akawaokoa katika mateso zao.
29Aliifanya ile dhoruba kali itulie,
nayo mawimbi yakanyamaza.
30Hapo wakafurahi kwa kupata utulivu;
akawafikisha kwenye bandari waliyoiendea.
31Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa fadhili zake;
kwa sababu ya maajabu aliyowatendea binadamu.
32Mtukuzeni katika kusanyiko la watu,
na kumsifu katika baraza la wazee.
33Mungu aliigeuza mito kuwa jangwa,
chemchemi akazikausha kabisa.
34Ardhi yenye rutuba akaifanya udongo wa chumvi,
kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.
35Aligeuza majangwa kuwa mabwawa ya maji,
na nchi kame kuwa chemchemi za maji.
36Akawahamishia huko wenye njaa,
nao wakajenga mji wa kukalika.
37Walilima mashamba na kupanda mizabibu,
wakavuna mazao kwa wingi.
38Aliwabariki watu wake, wakaongezeka;
na idadi ya wanyama wao akaizidisha.
39Kisha walipopungua na kuwa wanyonge,
kwa kukandamizwa, kuteswa na huzuni,
40aliwadharau wakuu waliowatesa,
akawazungusha jangwani kusiko na njia.
41Lakini aliwaokoa wahitaji katika taabu zao,
akaongeza jamaa zao kama kundi la kondoo.
42Waadilifu waonapo jambo hilo wanafurahi,
lakini waovu wote wananyamazishwa.
43Wenye hekima na wayafikirie mambo haya,
wazitambue fadhili zake Mwenyezi-Mungu.



Zaburi107;1-43

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 18 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 106...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu. Mungu anataka nyinyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa. Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima, na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....
Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo. Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu. Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali anamdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Jehovah ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu kila mmoja na mahitaji yake...
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao....
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele....
Amina..!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Wema wa Mungu kwa watu wake
1 Taz Zab 11:5; 107:1; 118:1; 136:1 Haleluya! Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!
2Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu?
Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?
3Heri wale wanaotekeleza haki,
wanaotenda daima mambo yaliyo sawa.
4Unikumbuke ee Mwenyezi-Mungu unapowafadhili watu wako;
unisaidie wakati unapowaokoa;
5ili niweze kuona fanaka ya wateule wako,
nipate kufurahia furaha ya taifa lako,
na kuona fahari pamoja na watu wako.
6Tumetenda dhambi sisi na wazee wetu;
tumetenda maovu, tumefanya mabaya.
7Wazee wetu walipokuwa Misri,
hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu;
hawakukumbuka wingi wa fadhili zake,
bali walimwasi kando ya bahari ya Shamu.
8Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi,
ili aoneshe nguvu yake kuu.
9Aliikemea bahari ya Shamu ikakauka;
akawapitisha humo kama katika nchi kavu.
10Aliwaokoa mikononi mwa waliowachukia;
aliwaokoa kutoka kwa nguvu za maadui zao.
11Maji ya bahari yaliwafunika maadui zao;
wala hakusalia hata mmoja wao.
12Hapo watu wake wakaamini maneno yake,
wakamwimbia tenzi za sifa yake.
13Lakini mara walisahau matendo yake,
wakaacha kutegemea shauri lake.
14Walijawa na tamaa kubwa kule jangwani,
wakamjaribu Mungu kule nyikani.
15Naye akawapa kile walichoomba,
lakini akapeleka maradhi mabaya kati yao.
16Kule kambini walimwonea wivu Mose,
na Aroni mtumishi mtakatifu wa Mwenyezi-Mungu.
17Ndipo ardhi ikafunguka ikammeza Dathani,
na kumzika Abiramu na kundi lake lote;
18moto ukawatokea wafuasi wao,
ukawateketeza watu hao waovu.
19Walitengeneza ndama wa dhahabu kule Horebu,
wakaiabudu sanamu hiyo ya kusubu;
20waliubadilisha utukufu wa Mungu,
kwa sanamu ya mnyama ambaye hula nyasi.
21Walimsahau Mungu aliyewaokoa,
aliyetenda mambo makuu nchini Misri,
22maajabu katika nchi hiyo ya Hamu,
na mambo ya kutisha katika bahari ya Shamu.
23Mungu alisema atawaangamiza watu wake,
ila tu Mose mteule wake aliingilia kati,
akaizuia hasira yake isiwaangamize.
24Kisha wakaidharau nchi ile ya kupendeza,
kwa sababu hawakuwa na imani na ahadi ya Mungu.
25Walinungunika mahemani mwao,
wala hawakumsikiliza Mwenyezi-Mungu.
26Hivyo Mungu akainua mkono akaapa
kwamba atawaangamizia jangwani;
27atawatawanya wazawa wao kati ya watu,
na kuwasambaza duniani kote.
28Kisha wakajiunga kumwabudu Baali kule Peori,
wakala tambiko zilizotambikiwa mizimu.
29Waliichochea hasira ya Mwenyezi-Mungu kwa matendo yao,
maradhi mabaya yakazuka kati yao.
30Lakini Finehasi akasimama kufanya malipizi,
na yale maradhi yakakoma.
31Jambo hilo lakumbukwa kwa heshima yake,
tangu wakati huo na nyakati zote.
32Walimkasirisha Mungu penye maji ya Meriba,
Mose akapata taabu kwa ajili yao.
33Walimtia Mose uchungu rohoni,
hata akasema maneno bila kufikiri.
34Hawakuwaua watu wa mataifa mengine
kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru.
35Bali walijumuika na watu wa mataifa,
wakajifunza kutenda mambo yao.
36Waliabudu sanamu za miungu yao,
nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza.
37Waliwaua watoto wao wa kiume na wa kike,
wakawatoa tambiko kwa pepo.
38Walimwaga damu ya wasio na hatia,
damu ya watoto wao wa kiume na wa kike
ambao waliwatoa tambiko kwa sanamu za Kanaani,
nayo nchi ikatiwa unajisi kwa mauaji hayo.
39Hivyo wakafanywa najisi kwa matendo yao,
2wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazinzi.
40Hasira ya Mwenyezi-Mungu ikawawakia watu wake,
akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.
41Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa,
hao wenye kuwachukia wakawatawala.
42Maadui zao waliwakandamiza,
wakawatumikisha kwa nguvu.
43Mara nyingi Mungu aliwaokoa watu wake,
lakini wao wakachagua kumwasi,
wakazidi kuzama katika uovu wao.
44Hata hivyo Mungu alizijali taabu zao,
wakati aliposikia kilio chao;
45kwa ajili yao alilikumbuka agano lake,
akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.
46Aliwafanya waliowakandamiza wawaonee huruma.
47Utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa,
tupate kulisifu jina lako takatifu,
na kuona fahari juu ya sifa zako.
48Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele!
Na watu wote waseme: “Amina!”
Asifiwe Mwenyezi-Mungu!


Zaburi106;1-48

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.