Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 17 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 105...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: “Kama mkisikia sauti yake leo, msiwe wakaidi kama wakati ule waliponiasi kama wakati ule wa majaribio kule jangwani. Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, ingawa walishuhudia matendo yangu kwa miaka arubaini! Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, ‘Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu’. Basi, nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai. Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi. Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti yake leo, msiwe wakaidi kama wakati ule waliponiasi.” Ni akina nani waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri. Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arubaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani. Mungu alipoapa: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi. Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....Nawapenda.

Mungu na watu wake
(1Nya 16:8-22)
1Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, tangazeni ukuu wake;
yajulisheni mataifa mambo aliyotenda!
2Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;
simulieni matendo yake ya ajabu!
3Jisifieni jina lake takatifu;
wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.
4Tafuteni msaada kwa Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;
mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.
5Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda,
miujiza yake na hukumu alizotoa,
6enyi wazawa wa Abrahamu mtumishi wake,
enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake;
7Yeye ndiye Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;
hukumu zake zina nguvu duniani kote.
8Yeye hulishika agano lake milele,
hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.
9Hushika agano alilofanya na Abrahamu,
na ahadi aliyomwapia Isaka.
10Alimthibitishia Yakobo ahadi yake,
alimhakikishia Israeli agano hilo la milele.
11Alisema: “Nitawapeni nchi ya Kanaani,
nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”
12Watu wa Mungu walikuwa wachache; hawakuwa maarufu,
tena walikuwa wageni nchini Kanaani.
13Walitangatanga kutoka taifa hadi taifa;
kutoka nchi moja hadi nchi nyingine.
14Lakini Mungu hakuruhusu mtu awadhulumu;
kwa ajili yao aliwaonya wafalme:
15“Msiwaguse wateule wangu;
msiwadhuru manabii wangu!”
16Mungu alizusha njaa nchini mwao,
akaharibu chakula chao chote.
17Lakini aliwatangulizia mtu mmoja,
Yosefu aliyekuwa ameuzwa utumwani.
18Walimfunga miguu kwa minyororo,
na shingoni kwa nira ya chuma,
19Muda si muda alichotabiri kilitimia.
neno la Mwenyezi-Mungu lilimdhibiti.
20Mfalme wa Misri akaamuru afunguliwe;
mtawala wa mataifa akamwachilia huru.
21Alimweka kuwa mkurugenzi wa serikali yake,
na mkuu wa mali yake yote;
22awaongoze maofisa wake apendavyo,
na kuwafundisha wazee wake hekima.
23Ndipo Israeli akaingia nchini Misri;
Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu.
24Mwenyezi-Mungu akawafanya watu wake wazae sana;
akawajalia nguvu kuliko maadui zao.
25Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake,
wakawatendea hila watumishi wake.
26Kisha akamtuma Mose mtumishi wake,
akamtuma na Aroni mteule wake.
27Wakafanya ishara za Mungu kati ya Wamisri,
na miujiza katika nchi hiyo ya Hamu.
28Mungu akaleta giza juu ya nchi;
lakini Wamisri wakakataa kutii amri zake.105:28 wakakataa kutii amri zake: Hivyo katika hati kadha za kale. Kiebrania: Wakatii.
29Akageuza mito yao kuwa damu,
akawaua samaki wao wote.
30Vyura wakaivamia nchi yao,
hata jumba la mfalme likajawa nao.
31Mungu akanena, kukazuka makundi ya nzi,
na viroboto katika nchi yote.
32Badala ya mvua akawapa mvua ya mawe,
na umeme uliomulika nchi yao yote;
33akaharibu mizabibu na mitini yao,
akaivunja pia miti ya nchi yao.
34Mungu akanena, kukazuka nzige,
na panzi maelfu yasiyohesabika;
35wakaitafuna mimea yote katika nchi,
wakayala mazao yao yote.
36Aliwaua wazaliwa wa kwanza nchini mwao,
chipukizi wa kwanza wa jamaa za Wamisri.
37Kisha akawatoa watu wa Israeli nchini,
wakiwa na fedha na dhahabu;
wala hakuna hata mmoja wao aliyejikwaa.
38Wamisri walifurahia kuondoka kwao,
kwani hofu iliwashika kwa sababu yao.
39Mungu alitandaza wingu juu ya watu wake,
na moto ili kuwaangazia usiku.
40Waliomba105:40 Waliomba: Makala nyingine za kale; Aliomba. naye akawaletea kware,
akawapa mkate kutoka mbinguni kwa wingi.
41Alipasua mwamba maji yakabubujika;
yakatiririka jangwani kama mto.
42Aliikumbuka ahadi yake takatifu,
aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43Basi akawatoa watu wake nchini,
wateule wake wakaimba na kushangilia.
44Aliwapa nchi za mataifa mengine
na kuwakabidhi mashamba ya wenyeji;
45kusudi watu wake watii masharti yake,
na kufuata sheria zake.
Asifiwe Mwenyezi-Mungu!

Zaburi105;1-45

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 16 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 104...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Ndugu zangu, watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu Mtume na Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama. Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Lakini Yesu anastahili heshima kubwa kuliko Mose maana mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye. Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi wenyewe ni nyumba yake kama tukiendelea kuwa hodari na thabiti katika kile tunachotumainia.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Kumsifu Muumba
1 Taz Ebr 1:7 Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu!
Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, wewe ni mkuu mno!
Umejivika utukufu na fahari.
2Umejizungushia mwanga kama vazi,
umezitandaza mbingu kama hema;
3umejenga makao yako juu ya maji ya mbingu.
Umeyafanya mawingu kuwa gari lako;
waruka juu ya mabawa ya upepo,
4waufanya upepo kuwa mjumbe wako,
moto na miali yake kuwa watumishi wako.
5Dunia umeiweka imara juu ya misingi yake,
ili isitikisike milele.
6Uliifunika dunia kwa bahari kama vazi,
na maji yakaimeza milima mirefu.
7Ulipoyakaripia, maji yalikimbia,
yaliposikia ngurumo yako yalitimka mbio.
8Yaliporomoka toka milimani hadi mabondeni,
mpaka pale mahali ulipoyatengenezea.
9Uliyawekea hayo maji mipaka,
yasije yakaifunika tena dunia.
10Umetokeza chemchemi mabondeni,
na mikondo yake ipite kati ya vilima.
11Hizo zawapatia maji wanyama wote porini.
Humo pundamwitu huzima kiu zao.
12Ndege hujenga viota vyao katika miti ya hapo,
hutua katika matawi yake na kuimba.
13Toka juu angani wainyeshea milima mvua,
nayo dunia waitosheleza kwa baraka yako.
14Waotesha nyasi kwa ajili ya mifugo,
na mimea kwa matumizi ya binadamu
ili naye ajipatie chakula chake ardhini:
15Divai ya kumchangamsha,
mafuta ya zeituni ya kumfurahisha,
na mkate wa kumpa nguvu.
16Miti mikubwa ya Mwenyezi-Mungu yapata maji ya kutosha;
naam, mierezi ya Lebanoni aliyoiotesha.
17Humo, ndege hujenga viota vyao;
korongo hufanya maskani yao katika misonobari.
18Milima mirefu ni makao ya mbuzimwitu;
na pelele hupata maficho yao miambani.
19Umeuumba mwezi utupimie majira;
jua nalo lajua wakati wa kutua.
20Waleta giza, usiku waingia;
nao wanyama wote wa porini wanatoka:
21Wanasimba hunguruma wapate mawindo,
humngojea Mungu awape chakula chao.
22Jua lichomozapo hurudi makwao,
na kujipumzisha mapangoni mwao.
23Hapo naye binadamu huenda kwenye shughuli zake;
na kufanya kazi zake mpaka jioni.
24Ee Mwenyezi-Mungu, umetenda mambo mengi mno!
Yote umeyafanya kwa hekima!
Dunia imejaa viumbe vyako!
25Mbali kule iko bahari - kubwa na pana,
ambamo kumejaa viumbe visivyohesabika,
viumbe hai, vikubwa na vidogo.
26 Taz Zab 74:14 Ndimo zinamosafiri meli,
na lile dude Lewiyathani uliloliumba licheze humo.
27Wote wanakungojea wewe,
uwapatie chakula chao kwa wakati wake.
28Wanaokota chochote kile unachowapa;
ukifumbua mkono wako wanashiba vinono.
29Ukiwapa kisogo, wanaogopa;
ukiondoa pumzi yao, wanakufa,
na kurudi mavumbini walimotoka.
30Ukiwapulizia pumzi yako, wanaishi tena;
wewe waipa dunia sura mpya.
31Utukufu wa Mwenyezi-Mungu udumu milele;
Mwenyezi-Mungu apendezwe na matendo yake mwenyewe.
32Huitazama dunia nayo hutetemeka,
huigusa milima nayo hutoa moshi!
33Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu maisha yangu yote;
nitamsifu Mungu wangu muda wote niishipo.
34Upendezwe, ee Mwenyezi-Mungu, na mawazo yangu haya;
maana furaha yangu naipata kwako.
35Wenye dhambi waondolewe duniani,
pasiwe na waovu wowote tena!
Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Zaburi104;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 15 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 103...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme, aliwahutubia watu. Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, “Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu.” Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa. Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza huduma yao, walitoka tena Yerusalemu, wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Sala kuu ya shukrani
(Zaburi ya Daudi)
1Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu;
nafsi yangu yote ilisifu jina lake takatifu!
2Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu!
Usisahau kamwe wema wake wote.
3Ndiye anayenisamehe uovu wangu wote,
na kuniponya magonjwa yote.
4Ndiye aniokoaye kutoka kifoni,
na kunijalia rehema na fadhili zake.
5Ndiye anayeniridhisha mema maisha yangu yote,
hata nabaki kijana mwenye nguvu kama tai.
6Mwenyezi-Mungu huhukumu kwa haki;
huwajalia wanaodhulumiwa haki zao.
7Alimjulisha Mose mwongozo wake,
aliwaonesha watu wa Israeli matendo yake.
8Mwenyezi-Mungu ni mwenye rehema na huruma;
ni mvumilivu na mwingi wa fadhili.
9Hatukemeikemei daima,
wala hasira yake haidumu milele.
10Yeye hatuadhibu kama tunavyostahili;
hatulipizi kadiri ya uovu wetu.
11Kama vile anga lilivyo juu mbali na dunia,
ndivyo ulivyo mwingi wema wake kwa watu wanaomcha.
12Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi,
ndivyo azitengavyo dhambi zetu mbali nasi.
13Kama vile baba amhurumiavyo mwanawe,
ndivyo Mwenyezi-Mungu awahurumiavyo wote wamchao.
14Mungu ajua mfumo wa nafsi zetu;
ajua kwamba sisi ni mavumbi.
15Walakini binadamu, maisha yake ni kama nyasi tu;
huchanua kama ua shambani:
16Upepo huvuma juu yake nalo latoweka;
na mahali lilipokuwa hapaonekani tena.
17Lakini fadhili za Mwenyezi-Mungu hudumu milele,
kwa wale wote wanaomheshimu;
na wema wake wadumu vizazi vyote,
18kwa wote wanaozingatia agano lake,
wanaokumbuka kutii amri zake.
19Mwenyezi-Mungu ameweka kiti chake cha enzi mbinguni;
yeye anatawala juu ya vitu vyote.
20Enyi malaika wakuu, msifuni Mwenyezi-Mungu;
mnaotimiza amri zake na kutekeleza neno lake!
21Enyi jeshi lote la mbinguni, msifuni Mwenyezi-Mungu;
enyi watumishi wake mnaotekeleza matakwa yake!
22Msifuni Mwenyezi-Mungu enyi viumbe vyake vyote;
msifuni popote mlipo katika milki yake.
Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu!


Zaburi103;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 12 April 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 102...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni. Wakamwambia yule msichana, “Una wazimu!” Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, “Huyo ni malaika wake.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa. Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro. Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea, akaenda Kaisarea ambako alikaa.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

Sala katika taabu
(Sala ya mtu aliye katika shida na ambaye anamwekea Mwenyezi-Mungu malalamiko yake)
1Usikie sala yangu, ee Mwenyezi-Mungu,
na kilio changu kikufikie.
2Usijifiche mbali nami wakati wa taabu!
Unitegee sikio lako,
unijibu upesi wakati ninapokuomba!
3Siku zangu zapita kama moshi;
mifupa yangu yaungua kama katika tanuri.
4Nimepondwa moyoni kama nyasi na kunyauka;
sina hata hamu ya chakula.
5Kutokana na kusononeka kwangu,
nimebaki mifupa na ngozi.
6Nimekuwa kama ndege wa jangwani;
kama bundi kwenye mahame.
7Ninalala macho wazi,
kama ndege mkiwa juu ya paa.
8Mchana kutwa maadui zangu wananisimanga,
wanaonidhihaki hutumia jina langu kulaania.
9Majivu yamekuwa chakula changu,
machozi nayachanganya na kinywaji changu,
10kwa sababu ya ghadhabu na hasira yako,
maana umeniokota na kunitupilia mbali.
11Maisha yangu ni kama kivuli cha jioni;
ninanyauka kama nyasi.
12Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, watawala milele;
jina lako lakumbukwa vizazi vyote.
13Wewe utainuka na kuurehemu mji wa Siyoni;
maana wakati umefika wa kuutendea mema;
wakati wake uliopangwa umefika.
14Watumishi wako wanauthamini sana,
ujapokuwa magofu sasa;
wanauonea huruma,
ingawa umeharibika kabisa.
15Mataifa yataliheshimu jina la Mwenyezi-Mungu;
wafalme wote duniani wataogopa utukufu wake.
16Mwenyezi-Mungu ataijenga upya Siyoni,
na kuonekana alivyo mtukufu.
17Ataikubali sala ya fukara;
wala hatayakataa maombi yao.
18Andika jambo hili kwa ajili ya vizazi vijavyo;
watakaozaliwa baadaye wamsifu Mwenyezi-Mungu.
19Kwamba aliangalia chini kutoka patakatifu pake juu,
Mwenyezi-Mungu aliangalia dunia kutoka mbinguni,
20akasikia lalamiko la wafungwa;
akawaachilia huru waliohukumiwa kuuawa.
21Hivyo watu watatangaza jina la Mwenyezi-Mungu huko Siyoni;
sifa zake zitatangazwa huko Yerusalemu,
22wakati mataifa yatakapokusanyika pamoja
na falme zitakutana kumwabudu Mwenyezi-Mungu.
23Mungu amenipunguzia nguvu ningali kijana;
ameyafupisha maisha yangu.
24Ee Mungu wangu, usinichukue sasa
wakati ningali bado kijana.
Ee Mwenyezi-Mungu wewe wadumu milele.
25 Taz Ebr 1:10-12 Wewe uliiumba dunia zamani za kale,
mbingu ni kazi ya mikono yako.
26Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki;
hizo zitachakaa kama vazi.
Utazitupilia mbali kama nguo,
nazo zitapotelea mbali.
27Lakini wewe ni yuleyule daima,
na maisha yako hayana mwisho.
28Watoto wa watumishi wako watakaa salama;
wazawa wao wataimarishwa mbele yako.


Zaburi102;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.