Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 10 July 2016

Jumapili iendelee vyema;Burudani-Glory Come Down,My God is Awesome,BreakEvery Chain





                  Wapendwa /Waungwana nawatakia jumapili njema
                   yenye,Afya Njema,Amani,Upendo,Kweli,Uvumilivu,

                   Hekima,Busara,Tumaini,Furaha,Upolekiasi.
               
                   Mungu aendelee kuwabariki.  




Neno La Leo;Mwanzo 37:4-36



Yosefu na ndugu zake
1Yakobo aliendelea kukaa katika nchi ya Kanaani, alimoishi baba yake kama mgeni. 2Hizi ndizo habari za ukoo wa Yakobo.
Yosefu, akiwa kijana wa umri wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake, wana wa Bilha na Zilpa, wake za baba yake. Yosefu akawa anamjulisha baba yake juu ya tabia mbaya za ndugu zake.
3Israeli alimpenda Yosefu kuliko watoto wake wote kwa sababu alikuwa amezaliwa wakati wa uzee wake. Alimshonea Yosefu kanzu ndefu. 4Lakini ndugu zake walipoona kwamba baba yao alimpenda Yosefu kuliko wao, wakamchukia hata hawakuzungumza naye kwa amani.


Ndoto za Yosefu
5Usiku mmoja, Yosefu aliota ndoto, lakini alipowasimulia ndugu zake, wao wakazidi kumchukia. 6Aliwaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota: 7Niliota kuwa sote tulikuwa shambani tukifunga miganda na ghafla mganda wangu ukainuka na kusimama wima. Miganda yenu ikakusanyika kuuzunguka na kuuinamia mganda wangu.” 8Ndugu zake wakamwuliza, “Je, unataka kutuambia kwamba utatutawala? Au utakuwa na mamlaka juu yetu?” Basi, wakazidi kumchukia kwa sababu ya ndoto na maneno yake.
9Kisha Yosefu akaota ndoto nyingine, akawasimulia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine; nimeona jua, mwezi na nyota kumi na moja vinaniinamia.” 10Lakini alipomsimulia baba yake na ndugu zake ndoto hiyo, baba yake alimkemea akisema, “Ni ndoto gani hiyo uliyoota? Je, itatulazimu mimi, mama yako na ndugu zako kuja kuinama chini kwa heshima mbele yako?” 11Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akawa analifikiria jambo hilo.



Yosefu anauzwa
12Siku moja, ndugu zake Yosefu walikwenda kuchunga wanyama wa baba yao karibu na Shekemu. 13Basi, Israeli akamwambia Yosefu, “Unajua ndugu zako wanachunga wanyama kule Shekemu. Kwa hiyo nataka nikutume kwao.” Yosefu akajibu, “Niko tayari.” 14Baba yake akamwambia, “Nenda ukawaangalie ndugu zako na wanyama kama wako salama, kisha uniletee habari.” Basi, Yakobo akamtuma Yosefu kutoka bonde la Hebroni. Yosefu alipokaribia Shekemu 15mtu mmoja akamkuta akitangatanga mbugani, akamwuliza, “Unatafuta nini?” 16Yosefu akamjibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Tafadhali, niambie mahali wanakochunga wanyama.” 17Yule mtu akamwambia, “Bila shaka wamekwisha ondoka, kwa sababu niliwasikia wakisema kwamba wanakwenda Dothani.” Basi, Yosefu akawafuata ndugu zake, akawakuta huko Dothani. 18Ndugu zake walipomwona akiwa mbali na kabla hajafika karibu, wakafanya mpango wa kumuua. 19Waliambiana, “Tazameni! Yule mwota ndoto anakuja. 20Haya, tumuue na kumtupa ndani ya shimo mojawapo. Baadaye tutasema kwamba ameuawa na mnyama wa porini. Halafu tutaona hizo ndoto zake zitakuwaje.” 21Lakini Reubeni aliposikia maneno hayo, akataka kumwokoa mikononi mwao; basi akawaambia ndugu zake, “Tafadhali, tusimuue. 22Msimwage damu. Ila mtumbukizeni katika shimo hili hapa mbugani, lakini msimdhuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu mikononi mwao, na baadaye amrudishe kwa baba yake. 23Yosefu alipowafikia ndugu zake, wao wakamvua kanzu yake. 24Kisha wakamshika na kumtupa shimoni. Lakini shimo hilo halikuwa na maji.
25Walipoketi kula, wakaona msafara wa Waishmaeli wakisafiri kutoka Gileadi kwenda Misri. Ngamia wao walikuwa wamebeba ubani, zeri na manemane. 26Hapo Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutapata faida gani tukimuua ndugu yetu na kuficha mauaji yake? 27Afadhali tumwuze kwa hawa Waishmaeli, lakini tusiguse maisha yake, kwani yeye ni ndugu yetu; yeye ni damu moja nasi.” Ndugu zake wakakubaliana naye.28Wafanyabiashara Wamidiani walipofika mahali hapo, hao ndugu wakamtoa Yosefu katika shimo, wakamwuza kwa Waishmaeli kwa bei ya vipande ishirini vya fedha; nao wakamchukua Yosefu hadi Misri.
29Basi, Reubeni aliporudi kwenye lile shimo, na asimwone Yosefu tena, akazirarua nguo zake kwa huzuni, 30akawaendea ndugu zake, akawaambia, “Kijana hayupo nami niende wapi?” 31Basi, wakachinja mbuzi, wakaichukua kanzu ya Yosefu na kuichovya katika damu ya huyo mbuzi. 32Kisha wakampelekea baba yao ile kanzu, wakamwambia, “Tumeiokota kanzu hii. Hebu iangalie kama ni ya mwanao, au siyo.”33Baba yao akaitambua hiyo kanzu, akasema, “Ndiyo hasa! Bila shaka mnyama wa porini amemshambulia na kumla. Hakika Yosefu ameraruliwa vipandevipande.” 34Hapo Yakobo akayararua mavazi yake kwa huzuni, akavaa vazi la gunia kiunoni. Akamlilia mwanawe kwa muda wa siku nyingi. 35Watoto wake wa kiume na wa kike wakamjia ili kumfariji, lakini akakataa kufarijiwa, akisema, “Niacheni; nitaendelea kuomboleza kwa ajili ya mwanangu, mpaka nitakaposhuka kuzimu alipo.” Ndivyo baba yake alivyomlilia.
36Wakati huo, kule Misri, wale Wamidiani walimwuza Yosefu kwa mtu aitwaye Potifa, mmoja wa maofisa wa Farao, ambaye alikuwa mkuu wa kikosi cha ulinzi.Biblia Habari Njema



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.



Tuesday 21 June 2016

Hotuba ya Maalim Seif Shariff Hamad + maswali na majibu....Washington DC


Photo Credits: Swahilivilla Blog
June 18, 2016, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Maalim
Seif Sharif HamaD alifanya mkutano kuzungumza na waTanzania waishio nje
ya nchi kupitia wale waishio jijini Washington DC.

Hii ilikuwa sehemu ya shughuli zake alipokuwa katika ziara yake ya siku 14 nchini Marekani na Canada.

Ameeleza
mengi kuhusu uchaguzi wa Zanziba, kilichotokea, kilivyotokea na namna
wanavyotafuta suluhisho la mgogoro wa kisiasa, kikatiba na kisheria
uliopo nchini Zanzibar

Karibu umsikilize

Baada ta hapo, wahudhuriaji walipata nafasi ya kuuliza maswali
Karibu uwasikilize

Mahojiano na Makala Jasper kuhusu Tuzo ya National Geographic Society for Leadership



Makala Jasper ni Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika lisilo la kiserikali la Mpingo Conservation & Development Initiative (MCDI).

Juni 16, 2016, alitunukiwa tuzo ya National Geographic Society/Buffett Award for Leadership in African Conservation, akiwa ni mshindi miongoni ma washiriki 30 kutoka barani Afrika.

Tuzo hiyo imetokana na kazi anayofanya pamoja na wananchi katika Vijiji mbalimbali mkoani Lindi.
MCDI huwezesha wanakijiji kutumia rasilimali za misitu kujenga uchumi na kutunza mazingira.

Katika miradi inayofanyika chini ya MCDI, wananchi wameweza kujiendeleza na kujenga shule, hospitali, kununua chakula cha dharura na kutoa misaada kwa vijiji vingine.

Tuzo ya National Geographic Society/Buffet Award ni ya pili kupokelewa na Bw. Jasper.

Ya kwanza ilikuwa Whitley Fund for Nature Award aliyopokea nchini Uingiereza tarehe 27 Aprili, 2016.

Karibu umsikilize

Sunday 19 June 2016

Jumapili iendelee vyema Na Happy Father's Day;Burudani-Sarah K-Liseme,Nasema Asante Na Ambassadors Of Christ Choir - Moyoni Mwangu,Nimekupata Yesu,




Wapendwa/Waungwana;Natumaini Jumapi ilikuwa/inaendelea vyema,
Mungu azidi kuwalinda na kuwabariki kila iitwapo leo,msipungukiwe na Amani ya moyo,
Upendo,Furaha na Upendo....

"Happy Father's Day" kwa BABA yangu mpendwa Ulale kwa Amani[R.I.P]
Kwa BABA wa watoto wangu na wa BABA wote wanaojua makujukumu yao kama baba
Mungu azidi kuwapa Hekima,Busara,Upendo na utunzaji/Ulezi mwema...

Mungu akawabariki na kuwajaalia wananume wote wanaohitaji watoto
Mungu awape sawa sawa na amapenzi yake....
 Ameeen....










Neno La Leo;waefeso 3:14-21

Upendo wa Kristo
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba, 15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni. 16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu, 17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo 18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina. 19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.

Biblia Habari Njema














"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe wote.

Tuesday 14 June 2016

Msemaji wa serikali azungumza na Diaspora.......Jukwaa Langu Juni 13 2016


Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga
Photo Credits: Wavuti.com
Katika kipindi hiki, tumezungumza na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga ambaye ameeleza kuhusu nafasi na wajibu wa serikali kwa waTanzania waishio Diaspora.
Pia amegusia wajibu wa waTanzania hao kwa nchi yao na kujibu maswali mbalimbali
Karibu


Sunday 12 June 2016

Nawatakia Jumapili iliyo njema;Burudani-William Yilima-Yesu Nitie NguvuNimalize Salama,Ee MUNGU,Uko Wapi,Subiri Muujiza Wako,UmulunguMwinza....



Habari za Jumapili wapendwa/wangwana..
nawatakia jumapili yenye baraka tele...




Neno La Leo;Ufunuo 2:1-29
Ujumbe kwa Efeso







Ujumbe kwa Smurna






Ujumbe kwa Pergamumu








Ujumbe kwa Thuatira





































"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 7 June 2016

Mahojiano na Chef Issa Kapande toka Sweden


Chef Issa ma ma-Chef
 wa timu ya Stockholm, Sweden, waliposhiriki na kushika nafasi ya
kwanza katika kipengele cha timu za kanda kwenye mashindano ya Kombe la
Dunia la Mapishi  2014 yajulikanayo kama  
Villeroy & Boch Culinary World Cup 2014  yaliyofanyika nchini Luxemborg.
Chef Issa Kapande ni mpishi maarufu na mmiliki wa mgahawa mkubwa unaotoa
huduma za chakula cha Kitanzania nchini Sweden, unaojulikana kama
Tanzania Restaurant
Alikuwa mkarimu sana kujiunga na Mubelwa Bandio kuzungumzia safari yake katika fani ya upishi na mpaka alipofikia.
Karibu ujiunge nasi kusikiliza






Tuesday 31 May 2016

Kama umeguswa msaidie huyu bibi..






"Nimetumiwa na Rafiki"
~
Haya wapendwa  nataka ku share hii video na nyinyi na yoyote atakae pata imani please inbox Facebook[Nana O Al Wakuvuruga ]msaada wako. Miezi kadhaa nyuma niliwaho share hii video na baadhi ya groups ili atakae weza amsaidie huyu bibi kuna ambao wamejitolea alhamdulillah lakini kwa ufupi pesa itamtosha kwa miezi miwili mitatu kununulia kula yake halafu baada ya hapo atarudi to square one. Inawezekana mnajiuliza huyu bibi ni nani? Huyu bibi sihusiani nae na wala sijawahi kutana nae ila inshaAllah mwaka huu nitamtafuta nimjue kwa ukaribu. Mimi nilipewa video hii na mwenzangu ambae nae pia alipata kumjua mwaka jana alipoenda matembezi Tanzania. Akapewa habari ya bibi huyu ili kama anaweza amsaidie chochote. Kubwa alienipa hii taarifa kajua hawezi lifanya hili jambo peke yake ndio akanijulisha na mimi. Sasa kwa ufupi huyu bibi hakujaaliwa mtoto, amefadhiliwa na watu hicho chumba mnacho kiona kwenye video na picha nitawatumia mpate kuona vizuri mazingira anayo ishi. Hajui kula yake ataitolea wapi wala tiba, kabaki anapita akiomba ndio siku inaenda. Hicho chumba mnacho kiona kukinyesha mvua ya nguvu maji yanajaa huko chumbani kwake anashinda juu ya kitanda mpaka maji yakauke. Nahitaji watu wajitolee kwa hali na mali apate kukarabatiwa chumba chake na at least japo ajijue anapata japo mlo mmoja kwa siku. Wazee wetu kweli wana shida lakini naamini hawajafikia hali hii, kumbuka bibi huyu hakujaaliwa kuzaa kwahiyo hana matumaini zaid ya kuomba vijumbani. Please find it in your heart and inshaAllah donate whatever you can. I joke a lot this is not one of those jokes; its real for this elderly lady and ahe doesn't even know I'm doing this




"Swahili Na Waswahili"Kutoa ni Moyo.

Monday 30 May 2016

MISS TANZANIA USA PAGEANT AEESHA KAMARA TEMBELEA, KUONGEA NA KUTOA MSAADA KENTON HIGH SCHOOL


Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara akiongea na wanafunzi wa Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam siku alipotembelea shuleni hapo katika moja ya majukumu yake ya kuhudumia jumuiya. Miss Kamara anadhamini wanafunzi wawili shuleni hapo
Miss Tanzania USA Pageant Aeesha Kamara akimkabidhi msaada mwalimu mipira siku alipotembela shule ya Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania USA Aesha Kamara akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wawili anaowadhamini kwa kuwasomesha shuleni hapo.
Picha ya pamoja

TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI


TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI

MAREHEMU JACKLINE OSWALD KAPINGA

Familia ya Marehemu Mzee Oswald Kapinga ya Sinza - Dar e salaam (karibu na  white inn) inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Jacqueline kilichotokea jana tarehe 29/05/2016 katika hospitali ya muhimbili jijini Dar es salaam. 

Familia inapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki ya kuwa, msiba utakuwa nyumbani kwa wazazi wake hapo sinza. 

Taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika, taarifa ya awali kutoka kwa familia, Marehemu wanategemea kumuhifadhi kwenye nyumba yake ya milele siku ya kesho (Jumanne) ya Tarehe 31/05/2016 katika makaburi ya sinza karibu na Ukumbi wa mwika kuanzia saa 8.00 Mchana. 

Kwa taarifa zaidi na maelekezo mbali mbali unaweza kuwasiliana na makaka wa marehemu hapo chini: 

JOSEPH O. KAPINGA (Mwananchi communication)  - 0788617654

GOSBERT O. KAPINGA - 0754286301

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, 
JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMEN.