Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Mahojiano/Waswahili. Show all posts
Showing posts with label Mahojiano/Waswahili. Show all posts

Friday 4 August 2017

Mahojiano ya Mubelwa Bandio na Maduhu Emmanuel ndani ya Kilimanjaro Studios



Emmanuel Maduhu ni mtangazaji wa Morning Star Radio na Televisheni jijini Dar Es Salaam
Mwezi Julai 2017 alifanya ziara ya kikazi nchini Marekani, ambapo alitembelea majimbo kadhaa.
Mwishoni mwa ziara yake, alipata fursa kuketi na Mubelwa Bandio wa Kwanza Production ndani ya Kilimanjaro Studios na kujadili mambo mbalimbali kuhusu kazi, ziara, maisha nk
Karibu ujiunge nasi


Tuesday 7 June 2016

Mahojiano na Chef Issa Kapande toka Sweden


Chef Issa ma ma-Chef
 wa timu ya Stockholm, Sweden, waliposhiriki na kushika nafasi ya
kwanza katika kipengele cha timu za kanda kwenye mashindano ya Kombe la
Dunia la Mapishi  2014 yajulikanayo kama  
Villeroy & Boch Culinary World Cup 2014  yaliyofanyika nchini Luxemborg.
Chef Issa Kapande ni mpishi maarufu na mmiliki wa mgahawa mkubwa unaotoa
huduma za chakula cha Kitanzania nchini Sweden, unaojulikana kama
Tanzania Restaurant
Alikuwa mkarimu sana kujiunga na Mubelwa Bandio kuzungumzia safari yake katika fani ya upishi na mpaka alipofikia.
Karibu ujiunge nasi kusikiliza






Tuesday 26 April 2016

Kipindi cha Jukwaa Langu. Mjadala wa DICOTA Convention 2016 April 25


Kongamano la kila mwaka la waTanzania waishio Marekani (DICOTA) litafanyika mwishoni mwa juma hili jijini Dallas Texas.
Katika kipindi cha Jukwaa Langu jumatatu hii, tulipata fursa ya kuzungumza na viongozi waandamizi wa DICOTA, Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini Lunda Asmani na Mwenyekiti wa DICOTA Dr Ndaga Mwakabuta.

Pia wachangiaji mbalimbali

KARIBU


Wednesday 29 July 2015

Mazungumzo na mtangazaji Rose Chitallah kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU


Mubelwa Bandio na Rose Chitallah studioni
Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania

Katika kipindi cha wiki hii tumebahatika kuungana na mtangazaji Rose Chitallah

Karibu

Mahojiano na Balozi Amina Salum Ali kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU


Mhe. Balozi Amina Salum Ali akifafanua jambo ndani ya Kilimanjaro Studio
Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania

Katika kipindi cha wiki hii tumebahatika kuungana na Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali

Karibu

Sunday 26 July 2015

Mahojiano na Charles Magali ndani ya Washington DMV


Charles Magali akiwa ndani ya Kilimanjaro Studio zinazomilikiwa na Vijimambo Radio, Kwanza Production na NesiWangu Media
Ijumaa ya Julai 24, 2015, mwigizaji na mwimbaji wa muziki nchini
Tanzania Charles Magali alipata fursa ya kutembelea studio zetu zilizopo
Beltsville Maryland. Hapo akazungumza nasi kwa ufupi

Karibu umsikilize akihojiwa na Mbunifu na Mtayarishaji wa kipindi hiki Dj Luke Joe na Mubelwa Bandio

Monday 27 April 2015

Mahojiano na mbunifu mavazi Linda Bezuidenhout (LB) Pt II


Karibu katika sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano na mbunifu wa kimataifa wa mitindo mwenye asili ya Tanzania, Linda Bezuidenhout

 Ameeleza mengi kuhusu kazi yake na familia kwa ujumla.

Anavyokabiliana na kazi zake, changamoto za afanyalo, tuzo alizopata nk

Na pia, kaeleza kuhusu mtazamo wake juu ya waTanzania (hasa wa Diaspora) na ushauri kwa kinamama wote

KARIBU

Monday 23 February 2015

Mazungumzo na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi....Sehemu ya mwisho


Karibu sana na asante kwa kujiunga nasi katika kipindi hiki cha HUYU NA YULE

Tumepata fursa ya kuongea na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi

Tumefanya mazungumzo naye ya sehemu nne, kueleza safari yake kimaisha

Na katika sehemu hii ya nne na ya mwisho ya mazungumzo yetu, Mhe Balozi Nyang'anyi anaanza kuelezea

1:Tukio la ugaidi la Septemba 11, 2001  - walivyopata taarifa (kama wanadiplomasia), na kilichofuata

2: Jukumu la kukuza mwanya wa biashara kati ya Marekani na Afrika, ambalo lilisababisha kupitishwa kwa muswada wa sheria wa AGOA

3: Siku yake ya kawaida kama Balozi inavyokuwa na alizimudu vipi?

4: Kituo chake kipya cha kazi huko Abu Dhabi Julai 2002

5: Utata juu ya wajibu wa ofisi za ubalozi kwa wananchi wake

6: Maisha baada ya kustaafu

7: Kazi yake kama Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Ndege Tanzania (ATC)

8: Nani alioshirikiana  na kuhusiana nao kwa urahisi zaidi

9: Maisha yake ya kisiasa na BUSARA ZAKE

KARIBU

Kama ulikosa sehemu za awali, unaweza kuangalia Sehemu ya kwanza hapa, sehemu ya pili hapa na sehemu ya tatu hapa

Wednesday 4 February 2015

Mazungumzo na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi (Pt 1)


Karibu sana na asante kwa kujiunga nasi katika kipindi hiki cha HUYU NA YULE

Tumepata fursa ya kuongea na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi ambaye ametueleza mengi juu ya safari yake kimaisha

Katika sehemu hii ya kwanza, Mhe. Balozi Nyang'anyi anaelezea

1: Historia yake.

 2: Aliposoma na alivyosoma.

 3: Namna alivyofika / kupata kazi Shirika la Utangazaji Tanganyika (TBC)

 4: Alivyoingia kwenye masuala ya diplomasia na kisha.....alivyoiona nafasi ya ubunge kwa mara ya kwanza 1970. Hii ni safari ndeefu ambayo kwa hakika utapenda kuisikia.

 KARIBU

Wednesday 1 October 2014

Mahojiano na waandaaji wa SWAHILI FESTIVAL Marekani

Patric Kajale. Mmoja wa waandaaji wa Tamasha hilo.

PHOTO CREDITS DMK Blog 
Karibu katika mahojiano kati ya Mubelwa Bandio na waandaaji wa SWAHILI FESTIVAL iliyofanyika Sept 21 jijini Bladensburg, jimbo la Maryland nchini Marekani
Karibu