Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 28 May 2014

Amina's Baby Shower,Coventry,UK.!!!!!!

Mapokezi/Twasubiri Mgeni...

Michezo......
Mawilimatatu,Kutakiana kheri,kucheka/Furaha.....


Kucheza tulicheza....

Baadhi ya wanakamati ikiongozwa na Zayana[Mwasu]



Ilkuwa  Shughuli ndogo ya[Suprise] Baby Shower ya Amina[Emmy].
Iliandaliwa na Dada yake Zayana[Mwasu] mwenye nguo Nyekundu,Akishirikiana na Baadhi ya Ndugu,Jamaa na Marafiki.
Ilifanyika Coventry,UK.
Pia wageni mbalimbali kutoka Birmingham na Vitongoji vingine walijumuika pamoja.

Da'Zayana[Mwasu] Anawashukuru sana Wote kwa,Zawadi,kutoa Muda,Upendo na Mengineyo.
MUNGU awabariki na Kuwaongezea pale mlipopunguza na zaidii.
Anawapenda Wote.

Burudani/Muziki na kaka Paul....
Muongozaji wa Shughuli/MC;Da'Rachel siwa[Kachiki]
Picha na Mpiga Picha wetu wa Swahili Na Waswahili;Da'Neema[Nyanyile]



"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 27 May 2014

Mjadala na Hussein Kauzela, Shamis Khatry, Liberatus Mwang'ombe na Solomon Christopher‏




Karibu katika mjadala na Hussein Kauzela, Shamis Khatry, Liberatus Mwang'ombe na Solomon Christopher uliojikita zaidi katika mwenendo wa kusaka katiba mpya nchini Tanzania.

Huu ni mfululizo wa mazungumzo na watu mbalimbali kuhusu suala hili muhimu kwa mustakabali wa nchi ya Tanzania.
Karibu

Kwa maoni, tafadhali wasiliana nasi kwa barua pepe kwanzaproduction at gmail dot com

Monday 26 May 2014

Mahojiano ya Idd Ligongo (Bicco) na Kwanza Production‏



Idd
Photo Credits: Idd's Facebook Page 
Karibu katika mahojiano ya Kwanza Production na Idd Ligongo
Msanii na mwanahabari makini ambaye amezungumza mengi mema kuhusu Sanaa na Habari ya Tanzania.
Amezungumzia historia yake katika fani hizi, ilipo na anapoiona ikielekea

Ni kati ya mazungumzo ninayoamini utapata mengi ya kujifunza.
KARIBU UNGANE NASI


Kwa maoni, tafadhali wasiliana nasi kwa barua pepe kwanzaproduction at gmail dot com

Sunday 25 May 2014

Natumaini JumaPili hii Inaendelea Vyema;Burudani-Emmy Kosgei-Asiyalasun,Jerusalem!!!!!!!



Wapendwa;Natumaini JumaPili inaendelea Vyema,Iwe Yenye Amani,Baraka,Upendo,Rehema na Furaha..
Ndugu zangu,wengi wenu msiwe waalimu.Kama mjuavyo,sisi waalimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine.
Neno La Leo;Yakobo:3:1-18

Je,ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu?Basi,aoneshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na Hekima.

Ulimi;1-12
Hekima itakayo juu mbinguni;13-18






"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 22 May 2014

Siku Kama Ya Leo Da'Tracey-Sarah Alizaliwa[13]!!!!!!!





Wapendwa/Waungwana;Siku kama ya Leo Binti Yetu Mpendwa,Da'Tracey-Sarah,Alizaliwa.
 Leo ametimiza miaka 13.Tunamshukuru sana MUNGU kwa Zawadi hii,Tunamtakia Masomo/Maisha Mema yenye Baraka,Amani,Upendo,Hekima.
Awe Baraka kwetu na Jamii pia.
Awe Kichwa na si Mkia.
MUNGU akumpe miaka mingi ,Akupe Maono/Njozi na Ukapate Kufanikisha Ndoto zako.
MUNGU azidi kumsimamia kila iitwapo Leo.


Mungu Ukawajaalie na wale wanaotafuta Watoto.

Shukrani kwa Wote Mnaoungana/Mlioungana/Mnaoendelea kuungana nasi Katika Malezi,MUNGU azidi kuwatendea kila lililo Jema.


Pia tunawatakia kheri na Baraka Watoto/Watu  wote waliozaliwa siku kama ya leo.


Familia ya Isaac tunawapenda Wote na Asanteni kwa yoooote!!



"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Monday 19 May 2014

Mahojiano ya Maggid Mjengwa na Kwanza Production‏


Maggid Mjengwa


Karibu katika mahojiano mwanahabari makini na wa muda mrefu ambaye pia ni mmiliki wa Kwanza Jamii, Maggid Mjengwa na Mubelwa Bandio wa Kwanza Production.
Amegusia mambo mbalimbali kama masuala ya uandishi, siasa (kama mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba) na mwenendo mzima wa nchi ya Tanzania.

Huu ni mfululizo wa mazungumzo na watu mbalimbali kuhusu masuala tofauti yaliyo muhimu kwa mustakabali wa nchi za Afrika Mashariki
Karibu

Kwa maoni, tafadhali wasiliana nasi kwa barua pepe kwanzaproduction at gmail dot com

Friday 16 May 2014

Matembezi ya Mswahili Vijijini;Burudani-Nuta Jazz Band (Tanzania) - Pongezi Wakulima (60's Tanzanian Rumba!)

Waungwana;Nipatapo muda huwa napenda kuzunguka/Kutembea na kujifunza/kujione mambo yakoje...
Basi Leo niwapeleke Shamba /Vijijini kidogo.

Swali.....
Wakulima wa Ng'ambo wapi wanapatia na Wakulima wa Afrika wapi wanakosea?
Jee Mkulima ni Mtu Masikini/Fukara,Mnyonge,Kaishiwa na........?

Jee unapenda kuwa Mkulima?








Nuta....Pongezi kwa Wakulima...


"Swahili Na Waswahili" Muwe na Wakati Mwema.

Monday 12 May 2014

Boko Haram: Waonyesha wasichana waliotekwa


Wasichana ambao kundi la Boko Haram liliwateka nyara


Kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekahu amesema kuwa atawaachilia huru wasichana waliotekwa nyara iwapo tu wapiganaji wa kundi hilo wanaozuiliwa na serikali ya Nigeria wataachiliwa huru.
Katika kanda mpya iliyotolewa na kundi hilo, kiongozi huyo, amesema kuwa wasichana hao waliweza kusilimu katika kipindi cha wiki nne zilizopita tangu watekwe nyara.
Kanda hiyo inaonyesha zaidi ya wanawake miamoja wakiwa wamevalia hijabu na kuswali. Abubaka Shekau anasema kuwa wanawake hao ni wasichana waliotekwa nyara na kundi hilo.
Walitekwa nyara kutoka katika shule yao mjini Chibok, Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo
Rais wa Ufaransa amejitolea kuwa mwenyeji wa mkutano utakaotafuta njia za kupambana na Boko Haram.

Habari zaidi;http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Shukrani.

Sunday 11 May 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani-Umoja One SDA Church choir Volume 3 DVD



Wapendwa;Nawatakia JumaPili Njema,Amani,Baraka,Upendo,Utuwema,Kweli,Shukrani,Tumaini,Imani,Upole kiasi na Utukufu Turudishe kwa BWANA......


Sisi twatokana na MUNGU.Yeye amjuaye MUNGU atusikia;yeye asiyetokana na MUNGU hatusikii.Katika hili twamjua Roho wa kweli,na roho ya upotevu.........

Neno La Leo;Waraka wa Kwanza wa Yohana:4;1-21
Kuzipima Roho;1-6
MUNGU ni Pendo;7-21


Na amri hii tumepewa na yeye,ya kwamba yeye ampendaye MUNGU,Ampende na ndugu yake.


Mhhhhhh.......
 Asante/Shukrani;Umoja SDA

"Swahili Na Waswahili"MUNGU Atubariki Sote.

Sunday 4 May 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani,Kijitonyama-Twaokolewa kwa Neema Na Nyingine!!!!!!!!

Wapendwa nawatakia JumaPili Njema na Yenye Baraka,Amani,Upendo na Utukufu Turudishe kwake BWANA....

Mimi nitasimama katika zamu yangu,nitajiweka juu ya mnara,nitaangalia ili nione atakalo niambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwanngu.
Neno La Leo;Hababkuki;2:1-5.


BWANA akanijibu akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji.





"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Monday 28 April 2014

Mhe Mwigulu Nchemba akizungumzia suala la uraia pacha Washington DC‏

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba akihojiana na Mubelwa Bandio wa Kwanza Production Washington DC.

Photo Credits: Habari Kwanza blog
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa anajivunia kiasi cha UZALENDO walichonacho waTanzania hapa nchini, jambo linalompa moyo kuendeleza harakati zake za kusaidia kupatikana kwa uraia pacha, ombi lililo kuu kwa waTanzania waishio nje ya nchi katika mabadiliko ya katiba mpya.

Mhe Nchemba, ambaye alikuwa mmoja wa wageni waalikwa kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika jijini Washington DC nchini Marekani, amesema kuwa ushiriki wa waTanzania na rafiki zao katika maadhimisho haya, umemdhihirishia nia na mapenzi yao kwa nchi yao, na hilo limemsukuma zaidi kusaidia kupitishwa kwa suala la uraia pacha kwenye katiba mpya.

Hii ni ripoti katika kipindi cha Morning Jam

Hotuba Ya Mhe. Mwigulu Nchemba katika sherehe za Muungano Washington DC‏


Mhe. Mwigulu Nchemba akizungumza katika moja ya hafla hapa Washington DC
Picha kwa hisani ya Vijimambo Blog
Ifuatayo ni hotuba ya Mhe Mwigulu Nchemba.

Naibu Waziri wa Fedha na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (Tanzania Bara) aliyoitoa katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano hapa Washington DC.

Audio hii ni kwa hisani ya Vijimambo Blog


Sunday 27 April 2014

Muendelee Vyema na Jumapili Hii Iwe Yenye Maono Na Imani;Burudani-Upendo Group Kijitonyama - Mungu Anakupenda,Sifa na Zivume!!!!

Wapendwa,Natumaini J'Pili hii inaendelea vyema,Na iwe Yenye Imani,Maono/Ndoto,Shukrani na Hekima.
Mithali:29:18;Pasipo Maono,watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.


Neno La Leo;Waebrania:11:1-40.[Maana Ya Imani]
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo,ni bayana ya mambo yasiyoonekana.






"Swahili Na Waswahili"MUNGU Atubariki Sote.

Friday 25 April 2014

Maandalizi ya sherehe za Muungano Washington DC‏





Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Liberata Mulamula akizungumzia maandalizi ya sherehe za miaka 50 ya muungano ofisini kwake Washington Dc Jumatano, Aprili 23, 2014.
Photo: Sunday Shomari

Thursday 24 April 2014

Mswahili wetu Leo;Da'Faiza wa Fabuloustaa!!!!!!!

Mswahili wetu Leo ni  da'Faiza Omar.
Binti huyu ni Blogger na ana mambo meengi mazuri
Kumjua zaidi Karibu sana kwenye Blog yake.

Mtembelee hapa;http://fabulousfaa.blogspot.co.uk

Tuesday 22 April 2014

Mazungumzo na Dr Patrick Nhigula kuhusu Bunge maalum la Katiba‏





Karibu katika mazungumzo na Dr Patrick Nhigula kuhusu mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba na mwenendo mzima wa nchi ya Tanzania.
Huu ni mfululizo wa mazungumzo na watu mbalimbali kuhusu suala hili muhimu kwa mustakabali wa nchi ya Tanzania.
Karibu

Kwa maoni, tafadhali wasiliana nasi kwa barua pepe kwanzaproduction at gmail dot com

Saturday 19 April 2014

Shukrani/Asanteni Wote na MUNGU awabariki Sana!!!!


Salaam Waungwana;

Tunamshukuru MUNGU mwenyeezi kwa yote.
Tunamshukuru MUNGU kwa maisha ya Mama/Bibi yetu mpendwa Khadija Mgaya Chuma[bibi Mwalimu].
Tunamshukuru MUNGU kwa kufanikisha vyema,Mazishi ya Mpendwa wetu.
Bi Khadija alifariki usiku wa Jumanne na Kuzikwa siku Alhamisi katika Makaburi ya Ilala Mchikichini.Dar.
Mama Kiwinga na Familia yake,Wanawashukuru sana Ndugu,Jamaa,Marafiki,Majirani na Wote walioshiriki kwa Michango,Muda,Upendo,Faraja, Sala/Dua na Mengineyo.
MUNGU azidi kuwabariki na kuwaongezea kila lililo jema kwenu.

Wenu Mama Kiwinga
Wa Ilala Sharifu/Shamba.

Asante Sana.


"Swahili Na Waswahili" Tunawashukuru wote katika yote.

Sunday 13 April 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani-Molimo na Nzambe yaka/Nitakushukuru,Mungu ni mwema/Kombo nayo ekumama ,Kutoka kwa- Feza Shamamba Hosseya

Wapendwa;Nawatakia JumaPili yenye Unyenyekevu,Upole,Uvumilivu,Upendo na Umoja....

Kwahiyo nawasihi,mimi niliye mfungwa katika BWANA,Mwenende kama  inavyoustahili wito wenu mlioitiwa;
Kwa unyenyekevu wote na upole,kwa uvumilivu,mkichukuliana katika upendo.

Neno La Leo;Waefeso:4:1-16
3.Na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4.Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5.BWANA mmoja,imani moja,ubatizo mmoja.
6.MUNGU mmoja,naye ni BABA wa wote,aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.
7.Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. 






"Swahili Na Waswahili"MUNGU Atubariki Sote.

Saturday 12 April 2014

[AUDIO]. DAKIKA 90 ZA DUNIA: Maadhimisho ya Kwibuka20, Washington DC‏


 Wiki
kama hii, miaka 20 iliyopita, nchi ya Rwanda ilishuhudia kuanza kwa
mauaji ambayo kwa siku 99 zilizofuata, yaliacha historia mbaya na ambayo
itaendelea kukumbukwa na vizazi vijavyo.
Ndani ya siku 100, watu wanaokadiriwa kufika milioni 1 waliuawa katika mauaji ya kimbari.
Miaka
20 baadaye (mwaka huu), dunia nzima imeungana na Rwanda kukumbuka kile
ambacho wengi wanaona kuwa kilitokea na kuachwa kuendelea kutokana na
Jumuiya ya kimataifa kutoingilia kati na kutoa msaada muafaka kwa wakati
muafaka.
Kumekuwa na matukio mbalimbali kukumbuka mauaji ya kimbari
ya Rwanda ambayo yamefanyika duniani kote, Kutoka Kigali Rwanda mpaka
hapa Dar-Es Salaam na hata huko Washington DC.



Hii ni sehemu ya
ripoti ya Kwanza Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA
kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Friday 11 April 2014

Jikoni Leo;Kitchen Boss- Date Night Dessert,Buddy and wife Lisa..!!!!!

Waungwana;"Jikoni Leo" mimi huwanafuatilia/Mpenzi Sana wa  vipindi vya huyu Bwana..Basi leo nikaona vyema nikusogezee hapa, kama wewe hujapata kuviona Au ulipitwa na hiki au kingine basi upate uhondo kidooogo....

Mwanaume Jiko au?

Mwanaume akipenda jiko/kupika  wengi wao wanakuwa wapishi wakubwa na kuwa kazi na yenye kumuingizia Pesa.Lakini Wanawake wengi ,wapishi wanaishia kupikia familia, mitaani/mama Ntilie.... ni wachache sana inakuwa kazi ya Maana/kumuingizia pesa. Hivi ni kwanini?


"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Tuesday 8 April 2014

Maangalizi ya afya Washington DMV...bure‏



Wataalam wa afya DMV (HCP Metro DC) wanatuleta huduma ya afya kwa wale wasiokuwa na bima ya afya. Huduma hii itatolewa kwa usawa bila kujali dini,rangi,umri,uraia au uchumi.



Kama una rafiki, ndugu au  mzazi asiyekuwa na bima ya afya tunaomba mshiriki ili tuwe na jamii inayoshamiri na yenye afya njema. Zoezi hili litachukuwa hatua ya kuwaona wale watakaokuwa na hali pungufu ya afya njema mara moja kwa mwezi.




Tarehe: 04/12/2014   (Jumamosi)
Saa 3:00 asubuhi hadi mchana 7:00 (waweza kuja hata kwa saa moja)  
MAHALA
3621 Campus Drive, 
College Park, MD 20740

Leo hii wadau wetu tunaomba tujitolee kufanikisha huduma hii ya maangalizi ya afya ya bure kwa wadau wa DMV. 

Unaweza kujitolea kwa namna mbalimbali


  • Iwe ni kumsadia mtu usafiri,
  • kuandikisha majina ya wanaokuja
  • kubeba na kupanga meza kabla na baada ya maangalizi
  • au kushiriki katika timu ya kitaalam
Tafadhali wasiliana nasi kupitia barua pepe nesiwangublog@gmail.com ili tuweze kupata idadi na uhakika wa msaada wako.

Monday 7 April 2014

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA. Mauaji kwenye kambi ya jeshi Fort Hood‏

Jenerali Mark Milley, Kamanda wa Fort Hood akizungumza na waandishi wa habari  
Wiki iliyopita, nchi ya Marekani ilikumbwa na mauaji mengine yaliyotokea kwenye kambi ya jeshi huko Fort Hood, Texas.

Jumatano Aprili 2, askari mmoja wa Jeshi la nchi hiyo, Ivan Lopez ambaye
inasemekana alikuwa na matatizo ya msongo wa mawazo, aliwafyatulia
risasi na kuwaua wanajeshi wenzake 3, kujeruhi 16 kabla hajajigeuzia
bastola na kujiua

Mauaji haya, yanarejesha kumbukumbu ya mauaji
makubwa kabisa kutokea kwenye kambi za jeshi nchini humo, yaliyotokea
kwenye kambi hiyohiyo takriban miaka 5 iliyopita.



Hii ni sehemu ya
ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA
kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Sunday 6 April 2014

Tumalizie JumaPili hii kwa Amani;Burudani-PASTOR ANTHONY MUSEMBI - Unastahili na ni Wewe,Mataifa Yote,Unaweza,natamani Wamebarikiwa,Nakuabudu Na Angalia.!!!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu JumaPili hii Imeenda/inaendelea Vyema...Muwe na Amani,Baraka,Rehema, na Upendo

Mwanangu,usiisahau sheria yangu,Bali moyo wako uzishike amri zangu.


Neno La Leo;Mithali:3:1-10
Rehema na kweli zisifarakane nawe;Zifunge shingoni mwako;Ziandike juu ya kibao cha moyo wako
.




Mmmmhhhhh..MUNGU ni MWEMA SAANA.


"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Wote Mliopita Hapa.

Wednesday 2 April 2014

Wa Afrika Na Sherehe zao Leo Tupo ;RWANDA: TWIN BROTHERS MARRY TWIN SISTERS!!!!!!




Mwenzangu umeonaje hii Arusi?
Mimi nimeona kama hawana Furaha..sijui wamelazimishwa au Utiifu/Heshima...
Tunawatakia kila la kheri na Baraka.

Mengi sina karibu kwa Maoni Yako.

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Monday 31 March 2014

Jikoni Leo; Nyama Choma - How to Eat Your Meat the East African Way,Tanzanian Mishkaki - Beef and Chicken Kebabs

Waungwana;"Jikoni Leo" Mmmmmmhhh mambo ya mitaani Bongo Tanzania....
Lakini wa Ughaibuni/Ng'ambo..hasa U.K. Hali ya hewa kwa sasa si mbaya saaana..unaweza kufanya mambo haya.





Shukrani;Mark Wiens

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Sunday 30 March 2014

Nawatakia JumaPili Njema na Happy Mother's Day;Burudani kutoka -African Gospel.....[Mchanganyiko]!!!!!!!!


Happy Mother's Day to all mothers, may GOD bless you.
Natumaini Jumapili hii inaendelea vyema..

Lakini  yanenaje?Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.

Neno La Leo;Warumi:10:5-15

Tena wahubirije, wasipopelekwa?kama ilivyoandikwa,Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema. 




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana

Saturday 29 March 2014

Jikoni Leo;Afya na Jamii-How to be slim _ BBC DOCUMENTARY_health documentary!!!!!

Waungwana ni "Jikoni Leo"; Tuangalie Afya zetu na Vyakula,Vinaweza kuwa Sumu au Dawa......


Sina mengi twende Pamoja...


"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Tuesday 25 March 2014

Monday 24 March 2014

[AUDIO]: Mdau Boniface Makulilo akijadili suala la Scholarship katika kipindi cha NJE-NDANI‏

Mdau Ernest Makulilo ambaye huandika kuhusu masuala ya Scolarship HAPA na pia kutoa video za suala hili HAPA
UNATAKA SCOLARSHIP?
Unajua pa kuzipata?
Unajua namna ya kuzipata?
Masharti yake je?
Makosa yanayofanywa na wengi?
Tofauti ya Scholarships za Undergraduate na Graduates wazijua?
Yapi ya kuchunga wakati wa kutafuta scholarships?
Boniface Makulilo ambaye amenufaika na scholarship hizi na kuandika kuzihusu kwa miaka ipatayo sita anaungana na Mubelwa Bandio wa Jamii Production kujadili hili.
Kuna mengi mema ya kujifunza.
KARIBU

NJE-NDANI ni kipindi kutoka Jamii Production Washington DC kinachokujia moja kwa moja (LIVE) kila Jumamosi kuanzia saa 6 mpaka 8 mchana (saa za Marekani mashariki) ambacho kinaleta Habari na Taarifa kuhusu yale yanayotokea na kuwagusa waAfrika walio NJE na NDANI ya Afrika.

Sunday 23 March 2014

Nawatakia JumaPili yenye Furaha Na Shukrani;Burudani Kutoka- African Mega Praise....!!!!!!

GOD can do Anything, Anytime, Anywhere in His time!!!!!!
Nawatakia JumaPili Yenye,Furaha,Shukrani,Matumaini,Amani na Baraka....

Nitamhimidi BWANA kila wakati,Sifa zake zi kinywani mwangu daima...

Neno La Leo;Zaburi:34:1-12

Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima,Apendaye siku nyingi apate kuona mema?




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 22 March 2014

[AUDIO]: DAKIKA 90: Kupotea kwa Air Malaysia na takwimu za usalama wa anga duniani‏

Ndege aina ya Boeing 777 ya Malaysia Airlines ikiruka kutoka Roissy-Charles de Gaulle Airport nchini Ufaransa mwaka 2011.
Photo Credits: PressTv
Wakati harakati za
kutafuta ndege ya Shirika la ndege la Malaysia iliyopotea zikizidi kushika kasi
na kuvunja rekodi ya kushirikisha mataifa mengi duniani, baadhi ya takwimu
kuhusu hali ya usalama wa safari za anga duniani zimezidi kuibuka na kufungua
macho ya wengi waliokuwa wakiamini kuwa tukio hili ni la kwanza na / ama
miongoni mwa machache kupata kutokea duniani.


Mtandao wa Usalama wa safari za Anga ama Aviation Safety Network
ilitoa orodha ya ndege zilizopotea tangu kumalizika kwa vita kuu ya pili ya
dunia.



Kwa mujibu wa takwimu hizo, ndege 88 zimepotea
tangu mwaka 1948, hivyo kufanya wastani wa ndege zinazopotea na kutopatikana
wala miili ya abiria kuwa 1.33 kwa mwaka.


Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90
ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es
Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30
AM).

Tuesday 18 March 2014

IskaJojo Studios; Ilimuhoji Miriam Kinunda Author of Taste of Tanzania Cookbook‏


IskaJojo Studios; Ilimuhoji "Miriam Kinunda" Mwandishi wa kitabu cha mapishi a Taste of Tanzania: Modern Swahili Recipes for the West.
Akieleza historia yake fupi ya kazi na mapishi na mengineo yanayoweza mnufaisha yoyote anayetaka kuandika kitabu na kufanikisha.



Miriam Kinunda - Taste of Tanzania  Na  IskaJoJo Studios 


"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Monday 17 March 2014

Boniface Makulilo azungumzia maisha katika jeshi la Marekani kwenye kipindi cha NJE-NDANI‏

Boniface Makulilo alipokuwa katika Jeshi la Maji la Marekani (Navy)
Mtanzania Boniface Makulilo ametumikia Jeshi la Maji (NAVY) hapa
Marekani kwa miaka miwili na sasa ni mwanajeshi mstaafu (Veteran)

Amezungumza
na Mubelwa Bandio wa Jamii Production kuhusu maisha yake ya jeshini na
namna ambavyo watu toka nje ya nchi wanaweza kunufaika na mafao yaliyopo
jeshini.

Ameeleza mengi ya manufaa ambayo wengi hatuyajui kuhusu maisha katika jeshi hilo.

Karibu uungane nasi

NJE-NDANI ni kipindi kutoka Jamii Production Washington DC kinachokujia moja kwa moja (LIVE) kila Jumamosi kuanzia saa 6 mpaka 8 mchana (saa za Marekani mashariki) ambacho kinaleta Habari na Taarifa kuhusu yale yanayotokea na kuwagusa waAfrika walio NJE na NDANI ya Afrika.

Sunday 16 March 2014

Nawatakia JumaPili Njema na Furaha;Burudani kutoka kwa Beatrice Kitauli-YESU Unipendaye[TENZI],Imbombo Inunu mwa JESU na Nyingine!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu Jumapili inaendelea vyema..

Heri kila mtu amchaye BWANA,Aendaye katika njia yake.


Neno La Leo;Zaburi:128:1-6

Tazama,atabarikiwa hivyo,yule amchaye BWANA......





"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Saturday 15 March 2014

[AUDIO]: DAKIKA 90 ZA DUNIA: Mfungwa aliyekuwa akisubiria KIFO aachiwa huru‏


Picha iliyopigwa na mwanasheria wake, ikimuonyesha Bwn Ford, siku ya kwanza kama mtu huru baada ya miaka 30 jela kwa kosa ambalo hakufanya. Photo Credits: theatlantic.com
Wiki hii, mmoja wa wafungwa nchini Marekani, ambaye alikuwa kwenye orodha ya wanaosubiri kunyongwa kutokana na kuhukumiwa kifo kwa mauaji  aliyotuhumiwa kufanya mwaka 1984 aliachiwa huru baada ya Jaji kukubali kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa ni yeye aliyeshiriki mauaji hayo.

Sasa, mfungwa huyu atalipwa dola 25,000 kwa kila mwaka aliotumikia kifungo hicho, lakini, kwa mujibu wa sheria ya Louisiana, kiwango cha juu anachoweza kulipwa ni dola 250,000

Ina maana, atalipwa kwa miaka 10 tu kati ya 30 aliyokaa gerezani

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Tuesday 11 March 2014

[AUDIO]: Kipindi cha FAMILIA. Siku ya wanawake duniani‏

Karibu katika kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production.
Kipindi hiki kilirushwa moja kwa moja (live) Jumamosi Machi 8, 2014

Katika kipindi cha wiki hii, mjadala ulijikita zaidi katika SIKU YA WANAWAKE DUNIANI ambapo wageni Mary Ndaro akiwa Wichita Kansas na Mch. Tumaini Mwanyonga  walijadili kwa mapana suala hili.

Wamegusa mengi mema ambayo ni muhimu kuyasikiliza.





Photo Credits: happyholidays2014.com

Monday 10 March 2014

Jikoni Leo; Njoo Tupike Na Chef Kile-Kuchoma Ndizi Mzuzu kwa Oven na Mengine!!!!!

Waungwana;"Jikoni Leo" Tupo na Njoo Tupike Na Chef Kile.

Vijiwe/Vibaraza vya Mapishi kwa sasa Vinakuwa Kwa Kaaasi.
Sasa kama wewe ni Mpishi/Unapenda Kujifunza ,Mpenzi wa mapishi mbalimbali Wakati ndiyo huu.
Nisiwachoshe na Maneno Meengi...
Twende Sote sasa;"Jikoni Leo" Na....





Jee kuna faida/umejifunza kitu hapa?

Mimi hii ya Ndizi  Mzuzu kwa Oveni nimeondoka nayo/Nimejifunza!!!!

Zaidi ingia;youtube.Njoo Tupike /http://www.njootupike.com/

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 9 March 2014

JumaPili hii Tusifu Na Kuabudu;Burudani-Mr&Mrs Goodluck Sandy-Alipo BWANA,Viumbe Vyote,Hakuna mwingine Tena,MUNGU U Mwema,Hakuna wa Kufanana na YESU!!!!!

Hatuja chelewa saana,Wapendwa Waungwana..WANAWAKE JUU!!



Wapendwa; Nawatakia JumaPili Njema, Yenye Kusifu na Kuabudu,Imani,Furaha,Amani,Tumaini,Subira,Uvumilivu,Hekima,Busara na UPENDO!!!!


Wanafunzi waliposikia,walishangaa mno,wakisema,Ninani basi awezaye kuokoka?



Neno La Leo;Mathayo Mtakatifu:19:23-30


YESU akawakazia macho,akawaambia,kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa MUNGU yote yanawezekana.


Lakini wengi walio wa  kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.